Just in: UDSM wafukuzwa



NB:

Napenda kuwatangazia mapema kuwa endapo uongozi utawapa viongozi wa DARUSO masharti ya kujinyonga ili warudi chuoni, msiwe na shaka HAWATATUABISHA!
 
Tanzanianjema,
Unafikiri hivyo?..
Labda hunifahamu vizuri ndugu yangu lakini mtu kama mimi siwezi kupendekezwa wala kupewa nafasi ktk kundi la washindi kwa sababu nitakuwa mzigo mkubwa sana.. eeeeh bwana wee mimi baba ubishi sii rahisi kubebeka hata kidogo. Tatizo kubwa ni kwamba nina Imani ya dini namuogopa Mungu na pia imani ya nchi kuiogopa sheria.
Kujiunga na hao jamaa inawezekana kabisa ikiwa watanipa nafasi kwa sababu haikatazwi kuingia msikitini/kanisani kuomba dua.
Na pengine JK anahitaji vichwa kama vyetu kuupata ushindi kwa njia halali na hilo fagio la chuma kuwa kwa viongozi wabaya!..
Nyerere kawahi kusafisha baraza zima la mawaziri!...nasikia kutokana na kichwa kimoja tu kilichomshauri!...
 
This has made my day, nauona moto wa activism kwa hawa vijana. Hapa walipofikia ningewaomba ndugu zangu wa vyama vya siasa wakae kimya, wasitie neno-wanaweza kuchafua hewa. Huyu dada Bernadetta ni kiongozi shupavu mpaka hapo!
 
FFU watanda Chuo Kikuu kusubiri amri



SOURCE: Nipashe

Serikali inatumia sana vyombo vya dola kunyanyasa wananchi wake?
 
Kitila hapa leo naona nikupinge unaposema wanasiasa wakae pembeni ni kosa kwani bila prtesha za wanasiasa chuo kisingelifunguliwa na hapo keshokutwa jumamosi watakuwa na mkutano mwingine kule tanga kuwaamsha watanzania ili kujua maana ya asilimia 40.

Kumbuka kule Morogoro walifanikiwa kuamsha hisia za watanzania nami nawapa go ahead kuwani huwa hii serikali ya jk kazi yake ni kusikilizia tuu wakiona watu wnaelewa ukweli wanatafuta pa kutokea. Kumbuka ishu za richmond hadi wanawatuma pcb,ishu nza malima vs mengi, nssf ona limekufa kwani hakuna wanasiasa waliolivalia njuga.

Wanasiasa tieni timu nchi imeuzwa hii.
 
Prof unakumbuka hapa?
 
enzi hizi alikuwa hajarukwa na akili.
 
Is it my eyes?
Huyu anayetumia jina la mgombea ubunge Ubungo ni yeye mwenyewe au mtu mwingine?
 
Huyu si ni CCM damu.

Anazungumziaje uchaguzi wa mwaka huu ambao wapinzani wote wamefutwa ili wasalie madarakani bila RAIDHAA AYA WANANCHI
 
Yupo CCM sahivi na anafanya kazi kwa maelekezo ya msoga gang.
Alikua na mawazo chanya sana huyu mwamba. Yaani alikua akiongea unapata ile ladha tamu ya wahadhiri mahiri na wabobezi wa chuo kikuu baba, chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Sasa hivi anaweza kukuangalia machoni na bila soni akakuambia "mwaka huu kutakua na uchaguzi wa haki"
Kanisa la Gwajima limefungwa na serikali, liko jimboni kwake, mwamba sijui kama anajua hilo. Kimara Mbezi walivunjiwa nyumba zao kwa kuonewa, mwamba anaona sawa tu. Kimara kwa sasa kuna tabu ya usafiri wa kwenda mjini, mwamba hajaliona hilo, yuko Mikocheni au Masaki anapata breeze.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…