Kwenye picha ya Meza Kuu katika mkutano wa Baraza Kuu la Uongozi wa chama cha CUF kilichoketi huko Zanzibar, anaonekana kada na mwanachama wa CHADEMA na mgombea mwenza wa Urais wa Tanzania kupitia UKAWA Babu Duni Haji akiwa kiti cha mbele kabisa.
Baraza hilo la Uongozi wa CUF limekutana ili kujadili hali ya kisiasa katika Visiwa vya Zanzibar, lakini nimeshangaa kumuona kada wa CHADEMA Babu Duni Haji akiwa "High table" kwenye meza ya viongozi wa CUF, Je, alipata mwaliko au ndio karudi kwenye chama chake cha zamani kimya kimya?
View attachment 304690View attachment 304691