Judgment Day: May 21, 2011 (Really?)

lets read and understand our holy books rather than relying on the translation given by our spiritual leaders
 
Kama wahusika wanatumia Biblia, basi siyo lazima itakuwa siyo biblia hii tunayoijua wote. Kwa sababu biblia ninayoijua hata mimi inasema "Walakini, habari za siku ile na saa ile hakuna ajuaye, HATA MALAIKAWALIO MBINGUNI wala Mwana ila BABA PEKE YAKE"! [Mathayo 24:36]

Sasa hawa jama zangu habari za mwisho wa dunia wa tarehe 21 mei 2011 wanazipata wapi? Yesu anayeuwakilisha uKristo ndiyo aliyeyasema haya, sasa hawa jamaa zangu habari za Mungu wanawakilishwa na nani? Au wanadhani Mungu anaweza kufanyiwa utafiti kama mambo ya kisayansi tu?

Ninaamini kuwa tarehe 21 itapita na hakuna lolote litakalotokea, kitakachotekea ni aibu tu kwa hao walioleta unabii huo na pia watajulikana kuwa ni manabii wa uwongo kama biblia yenyewe inenavyo katika Mathayo 24:4-5; Yesu akajibu akawaambia, [yale waliyotaka kuyajua wanafunzi wake kuhusiana na mwisho wa dunia]Angalieni, mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watawadanganya wengi. Unaona!

Kwa ujumla hizi ni nyakati za mwisho, na hizo habari za akina 21 mei ni dalili mojawapo. Msingi wa uhakika wa habari hizi ni Mathayo 24:36 zaidi ya hapo ni uwongo!

Asante, nimeingia bila hodi; naomba mnikubali nyumbani mwenu, huko nje kuna watu wanakera wanasema habari za kuwatisha watu, nimekasirika nimejikuta nimeingia mpaka ndani bila hodi ili niwajuvya uwongo huo wa mchana kweupe.

Bwana awe nawe,hakika biblia unaijua.Hata mimi nasadiki kuwa,hakuna ajuae siku wala saa.Bwana akubariki na kukulinda.
 
Hata Nostradamus alichemsha kutabiri mwisho wa dunia alioneshwa matukio yanayoashiria mwisho wa dunia lakini siyo siku wala saa,huyu aliweza kutabiri mambo mengi ambayo yametokea na kuwa kweli mfano ni pale alipotabiri watu watakaofukua kaburi lake kutafuta kurithi busara zake kwa kutoa wosia kuwa atakapofariki awekewe kibao kinachoonesha namba 17... juu ya jeneza na kumbe ndiyo mwaka wale watafiti walipokuja kufukua kaburi lake miaka zaidi ya 200 baadae.sasa hawa wanaotabiri na kunoa ni vipi,kwani wametabiri 1994 haikutokea sasa 21 May 2011,hiyo biblia imetayarishwa kwa ajili yao tu?.Wanatakiwa kuelewa kuwa hilo la mwisho wa dunia ni fumbo lililofungwa na Mwenyenzi Mungu na siri hiyo anaijua mwenyewe tu.hata wasaidizi wake yaani malaika hawaijui,laiti wangeijua hiyo siri ingevuja,kwani siri nyingi za mbinguni zimevuja kupitia Malaika.mifano mingi ipo sina haja ya kuirudia.HAWA WANAJITAFUTIA UMAARUFU BILA KUVUJA JASHO KWA KUOGOPESHA WANADAMU.
 
Mwanzoni nilikua na taarifa kuhusu mwisho wa dunia ni December 21,2012 na leo tena nimeona 2012 sio tena na sasa bado siku 2 yani ni may 21, 2011--Jama wataalamu wa sayansi munatuambiaje kwa hili?---Mimi imani yangu ipo pale pale (Only Allah(S.W) know end of the day).

Angalieni hii habari: Family Radio Swahili - Kiswahili
 
Hivi huu uzushi wa kujua siku ya mwisho umezibuka katika dini gani?--maana hizo ni siri za muumbaji!!!-basi na siku zao za kufa wanazijua-
------------------
22/05/2011-WE WILL BACK IN JF.
 
Crazy church peoples who still believe Jesus is the Son of God. Nonesense

naona ww unavamia wala huji maandiko yanasemaje. yesu ni mwana wa Mungu biblia inaandika hivo na pia yesu ni Mungu.Soma Injili ya Yohana 1:1 au soma Isaya nk sitaki kungia deep kuanza kukufundisha biblia hapa we baki na imani yako na ujue unashangaza sana kwa ulichoandika.Jina lako haliendani na mawazo yako.
 
naona ww unavamia wala huji maandiko yanasemaje. yesu ni mwana wa Mungu biblia inaandika hivo na pia yesu ni Mungu.Soma Injili ya Yohana 1:1 au soma Isaya nk sitaki kungia deep kuanza kukufundisha biblia hapa we baki na imani yako na ujue unashangaza sana kwa ulichoandika.Jina lako haliendani na mawazo yako.
Achana naye huyo. Unapoteza muda wako bure. Yeye anaamini Muhamadi ndiye mtume wa mwisho.
 
Mwanzoni nilikua na taarifa kuhusu mwisho wa dunia ni December 21,2012 na leo tena nimeona 2012 sio tena na sasa bado siku 2 yani ni may 21, 2011--Jama wataalamu wa sayansi munatuambiaje kwa hili?---Mimi imani yangu ipo pale pale (Only Allah(S.W) know end of the day).

Angalieni hii habari: Family Radio Swahili - Kiswahili

Hapo kwenye RED huyo ndio nani? maana sio wote waarabu humu.
 
Mwanzoni nilikua na taarifa kuhusu mwisho wa dunia ni December 21,2012 na leo tena nimeona 2012 sio tena na sasa bado siku 2 yani ni may 21, 2011--Jama wataalamu wa sayansi munatuambiaje kwa hili?---Mimi imani yangu ipo pale pale (Only Allah(S.W) know end of the day).

Angalieni hii habari: Family Radio Swahili - Kiswahili

Hizo ni idiology mbili tofautti, kuna wanaosema ni 2012 na wengine wanasema 2011; usiwe mvivu wa kusoma bana! Ila ya 2012 ndy ina nguvu sana!
Will the world end on December 21, 2012? The worrying evidence behind ancient astrologers' claim and the film they inspired | Mail Online
2012 phenomenon - Wikipedia, the free encyclopedia

Hizo zote ni posibilities; dont ignore them!
 
Mwanzoni nilikua na taarifa kuhusu mwisho wa dunia ni December 21,2012 na leo tena nimeona 2012 sio tena na sasa bado siku 2 yani ni may 21, 2011--Jama wataalamu wa sayansi munatuambiaje kwa hili?---Mimi imani yangu ipo pale pale (Only Allah(S.W) know end of the day).

Angalieni hii habari: Family Radio Swahili - Kiswahili

its true only Allah S.W who knows the day and the tyme of the end of the world
 
Back
Top Bottom