Daudi1
JF-Expert Member
- Dec 14, 2013
- 8,799
- 8,706
JOTO LA MAPENZI-1
Kutokana na maji kuingia kwa kasi katika shimo alilokuwemo kijana ambe yalimzindua kutokana na kuteleza na kudondokea humo wakati wakiwakimbia askari magereza na kupoteza fahamu. Ilikuwa katika jaribio la kutoroka kwa bahati mbaya aliangukia kwenye shimo. Rafiki yake Aloys Mabina hakutaka kumwacha alijitahidi kumwamsha ili amtoe shimoni, lakini aligundua amepoteza fahamu hivyo asingeweza kuendelea kuwepo eneo lile kwa kuhofia askari wanaowatafuta kumkuta eneo lile. Aliona kama angeendelea kuwepo pale lazima askari wanaowakimbiza wangefika eneo lile na kumkamata. Hivyo aliendelea na safari kuwakimbia na kumwacha rafiki yake ndani ya shimo.
Ambe baada ya kuzinduka taratibu alijitoa kwenye shimo huku mvua ikiendelea kupiga kwa kasi, shimo halikuwa refu sana hiyo ilimsaidia kutoka nje kwa urahisi. Alijikuta akiwa njia panda na kushindwa afanye nini arudi gerezani au aendelee kukimbia. Wazo la kurudi lilimtisha kidogo kutokana na kuogopa kuulizwa juu ya mwenzake Mabina aliyekuwa swahiba wake mkubwa gerezani. Walikuwa wamefanya tukio baya la kutoroka na silaha baada ya kumkaba askari magereza na kukimbia na bunduki ambayo ilikuwa inakwenda kutimiza azma ya rafiki yake Mabina ya kuua ili kutimiza kisasi.
Ambe na Mabina walikuwa na matukio ya kufanana yaliyowafanya waingie gerezani na kila mmoja kufungwa miaka saba. Lakini kila mmoja alikuwa na njia yake iliyomwingiza gerezani. Mabina aliapa akitoka lazima alipe kisasi kwa kuwaua wabaya wake na ndiyo sababu ya kutoroka na silaha. Lakini ilikuwa tofauti kwa Ambe, pamoja na kufanyiwa unyama mkubwa lakini aliapa hatalipiza zaidi ya kumuachia Mungu. Mabina hakuwa hivyo hakutaka kabisa kusikia eti mtu anakutendea unyama unamshtakia Mungu wakati una uwezo wa kulipa kisasi.
Baada ya kumweleza rafiki yake sababu iliyomwingiza gerezani ambayo ilikuwa ni uonevu aliapa akitoka lazima aue tena kwa risasi. Ambe pamoja na kumsihi rafiki yake asilipe kisasi hakusikilizwa. Mabina alisema toka alipofanyiwa unyama ule na mwisho wa yote kufungwa bila kosa miaka saba. Asingemsamehe mtu aliapa lazima atalipa kisasi tena cha damu. Ambe akiwa anatoka kwenye shimo huku mvua ikiendelea kumnyeshea, moyoni alijikuta akijilaumu maamuzi ya rafiki yake ya kumpiga askari na kuichukua bunduki ambayo alimwambia ndiyo silaha aliyoitafuta kwa muda mrefu.
Katika muda wote waliokuwa gerezani Mabina aliapa akitoka gerezani lazima aue ili anyongwe na kuamini kile ndicho kitakuwa kifungo cha kweli kwake. Matatizo ya rafiki yake hayakuwa na tofauti na yake ya kutendewa unyama na familia ya rafiki yake wa kike na mwisho wa yote kufungwa gerezani miaka saba bila kosa lolote kisa mapenzi.Tofauti ya kuingia gerezani kwa Ambe na Mabina ilitofautiana, Mabina alitangulia kuingia kwa mwezi mmoja hivyo hata muda wao wa kutoka ungepishana kwa mwezi mmoja.Ambe akiwa bado yupo njia panda aelekee wapi kwa vile pori lile lilikuwa geni kwake japokuwa hakutaka kurudi gerezani.
Alikumbuka kauli za rafiki yake baada ya kumsimulia mkasa uliomwingiza gerezani: "Ambe nakuhakikishia siwezi kuwasamehe wote walionifanyia unyama, hawezi kutudhulumu mali yetu, wamuue baba yangu na mimi kufungwa miaka saba bila kosa kisa tu nilikuwa nikijua mengi juu ya ugomvi wa baba na jirani yake juu ya mpaka wa nyumba.
"Najua sina uwezo wa kipesa, lakini lazima nimuue kwa risasi kama alivyomuua baba yangu."
"Utapata wapi bunduki?" Ambe alimuuliza rafiki yake.
"Hapahapa gerezani." Mabina alijibu kwa kujiamini.
"Hapahapa gerezani! Utaipata vipi?" Ambe alishtuka.
"Utaona tu."
Siku ilipofika walikuwa kwenye kazi za nje kutokana na kubakiza muda mchache wa kuwepo gerezani. Wafungwa wengi walipewa kazi za nje, yeye akiwa amebakiza miezi miwili na Mabina mwezi mmoja wa kutoka gerezani. Wakiwa eneo lililojificha walilopangiwa Ambe na Mabina kukata miti huku askari magereza akiwa mbali kidogo.Mabina alimwambia Ambe amwite askari kwa sauti ya juu, naye alifanya hivyo kwa kupaza sauti kumwita askari.
Askari alifika haraka eneo aliloitiwa alipofika alishangaa kumuona Mabina akigaragara chini kama mtu aliyekuwa akiumwa kitu. alipomuuliza Ambe ambaye hakuwa na jibu. Alipomwinamia ili kutaka kujua anaumwa nini, Mabina alinyanyuka na kumkaba askari huku Ambe akishangaa. Baada ya kumkaba mpaka kupoteza fahamu alichukua bunduki na kumlazimisha Ambe waondoke."Twende wapi?" Ambe aliuliza.
"Ukibaki shauri yako utaulizwa nimekwenda wapi, najua hautakuwa na jibu kwa vile sisi ni marafiki wakubwa watajua nawe unahusika hivyo utaozea gerezani."Ambe alijikuta akimfuata Mabina aliyeanza kukimbia kuingia porini, kwa vile hakuwa amejiandaa baada ya mwendo wa saa tatu bila kupumzika, pumzi ilikata na kujikuta akianza kuona kizunguzungu kwa bahati mbaya pembeni na sehemu aliyokuwa amesimama kulikuwa na shimo aliangukia ndani.
Habari ya siku nyingi wanajamvi, poleni na majukumu ya kujenga taifa, baada ya kupotea muda mrefu nimerudi tena, Kwa hisani ya GLOBAL PUBLISHER kwa wale wapenzi wa mikasa ya mapenzi tupate uhondo huu, kuna mafundisho mengi ndani ya mkasa huu ungana nami muongojazi wako mpaka mwisho wa safari karibuni
Kutokana na maji kuingia kwa kasi katika shimo alilokuwemo kijana ambe yalimzindua kutokana na kuteleza na kudondokea humo wakati wakiwakimbia askari magereza na kupoteza fahamu. Ilikuwa katika jaribio la kutoroka kwa bahati mbaya aliangukia kwenye shimo. Rafiki yake Aloys Mabina hakutaka kumwacha alijitahidi kumwamsha ili amtoe shimoni, lakini aligundua amepoteza fahamu hivyo asingeweza kuendelea kuwepo eneo lile kwa kuhofia askari wanaowatafuta kumkuta eneo lile. Aliona kama angeendelea kuwepo pale lazima askari wanaowakimbiza wangefika eneo lile na kumkamata. Hivyo aliendelea na safari kuwakimbia na kumwacha rafiki yake ndani ya shimo.
Ambe baada ya kuzinduka taratibu alijitoa kwenye shimo huku mvua ikiendelea kupiga kwa kasi, shimo halikuwa refu sana hiyo ilimsaidia kutoka nje kwa urahisi. Alijikuta akiwa njia panda na kushindwa afanye nini arudi gerezani au aendelee kukimbia. Wazo la kurudi lilimtisha kidogo kutokana na kuogopa kuulizwa juu ya mwenzake Mabina aliyekuwa swahiba wake mkubwa gerezani. Walikuwa wamefanya tukio baya la kutoroka na silaha baada ya kumkaba askari magereza na kukimbia na bunduki ambayo ilikuwa inakwenda kutimiza azma ya rafiki yake Mabina ya kuua ili kutimiza kisasi.
Ambe na Mabina walikuwa na matukio ya kufanana yaliyowafanya waingie gerezani na kila mmoja kufungwa miaka saba. Lakini kila mmoja alikuwa na njia yake iliyomwingiza gerezani. Mabina aliapa akitoka lazima alipe kisasi kwa kuwaua wabaya wake na ndiyo sababu ya kutoroka na silaha. Lakini ilikuwa tofauti kwa Ambe, pamoja na kufanyiwa unyama mkubwa lakini aliapa hatalipiza zaidi ya kumuachia Mungu. Mabina hakuwa hivyo hakutaka kabisa kusikia eti mtu anakutendea unyama unamshtakia Mungu wakati una uwezo wa kulipa kisasi.
Baada ya kumweleza rafiki yake sababu iliyomwingiza gerezani ambayo ilikuwa ni uonevu aliapa akitoka lazima aue tena kwa risasi. Ambe pamoja na kumsihi rafiki yake asilipe kisasi hakusikilizwa. Mabina alisema toka alipofanyiwa unyama ule na mwisho wa yote kufungwa bila kosa miaka saba. Asingemsamehe mtu aliapa lazima atalipa kisasi tena cha damu. Ambe akiwa anatoka kwenye shimo huku mvua ikiendelea kumnyeshea, moyoni alijikuta akijilaumu maamuzi ya rafiki yake ya kumpiga askari na kuichukua bunduki ambayo alimwambia ndiyo silaha aliyoitafuta kwa muda mrefu.
Katika muda wote waliokuwa gerezani Mabina aliapa akitoka gerezani lazima aue ili anyongwe na kuamini kile ndicho kitakuwa kifungo cha kweli kwake. Matatizo ya rafiki yake hayakuwa na tofauti na yake ya kutendewa unyama na familia ya rafiki yake wa kike na mwisho wa yote kufungwa gerezani miaka saba bila kosa lolote kisa mapenzi.Tofauti ya kuingia gerezani kwa Ambe na Mabina ilitofautiana, Mabina alitangulia kuingia kwa mwezi mmoja hivyo hata muda wao wa kutoka ungepishana kwa mwezi mmoja.Ambe akiwa bado yupo njia panda aelekee wapi kwa vile pori lile lilikuwa geni kwake japokuwa hakutaka kurudi gerezani.
Alikumbuka kauli za rafiki yake baada ya kumsimulia mkasa uliomwingiza gerezani: "Ambe nakuhakikishia siwezi kuwasamehe wote walionifanyia unyama, hawezi kutudhulumu mali yetu, wamuue baba yangu na mimi kufungwa miaka saba bila kosa kisa tu nilikuwa nikijua mengi juu ya ugomvi wa baba na jirani yake juu ya mpaka wa nyumba.
"Najua sina uwezo wa kipesa, lakini lazima nimuue kwa risasi kama alivyomuua baba yangu."
"Utapata wapi bunduki?" Ambe alimuuliza rafiki yake.
"Hapahapa gerezani." Mabina alijibu kwa kujiamini.
"Hapahapa gerezani! Utaipata vipi?" Ambe alishtuka.
"Utaona tu."
Siku ilipofika walikuwa kwenye kazi za nje kutokana na kubakiza muda mchache wa kuwepo gerezani. Wafungwa wengi walipewa kazi za nje, yeye akiwa amebakiza miezi miwili na Mabina mwezi mmoja wa kutoka gerezani. Wakiwa eneo lililojificha walilopangiwa Ambe na Mabina kukata miti huku askari magereza akiwa mbali kidogo.Mabina alimwambia Ambe amwite askari kwa sauti ya juu, naye alifanya hivyo kwa kupaza sauti kumwita askari.
Askari alifika haraka eneo aliloitiwa alipofika alishangaa kumuona Mabina akigaragara chini kama mtu aliyekuwa akiumwa kitu. alipomuuliza Ambe ambaye hakuwa na jibu. Alipomwinamia ili kutaka kujua anaumwa nini, Mabina alinyanyuka na kumkaba askari huku Ambe akishangaa. Baada ya kumkaba mpaka kupoteza fahamu alichukua bunduki na kumlazimisha Ambe waondoke."Twende wapi?" Ambe aliuliza.
"Ukibaki shauri yako utaulizwa nimekwenda wapi, najua hautakuwa na jibu kwa vile sisi ni marafiki wakubwa watajua nawe unahusika hivyo utaozea gerezani."Ambe alijikuta akimfuata Mabina aliyeanza kukimbia kuingia porini, kwa vile hakuwa amejiandaa baada ya mwendo wa saa tatu bila kupumzika, pumzi ilikata na kujikuta akianza kuona kizunguzungu kwa bahati mbaya pembeni na sehemu aliyokuwa amesimama kulikuwa na shimo aliangukia ndani.
Habari ya siku nyingi wanajamvi, poleni na majukumu ya kujenga taifa, baada ya kupotea muda mrefu nimerudi tena, Kwa hisani ya GLOBAL PUBLISHER kwa wale wapenzi wa mikasa ya mapenzi tupate uhondo huu, kuna mafundisho mengi ndani ya mkasa huu ungana nami muongojazi wako mpaka mwisho wa safari karibuni