Ndalama
JF-Expert Member
- Nov 22, 2011
- 8,787
- 6,542
umezama wapi? mwili lazima upumue joto kali sana
Umezama mwilini
umezama wapi? mwili lazima upumue joto kali sana
Haah haaaaa...vipi kwenye kingo za mto??.
Haah haaaaa...vipi kwenye kingo za mto??.
Huwezi Amini ndio zinaongezeka ukali Kama mbolea ya samadi Aisee.Hivi na hili joto mbegu zetu hazipungui ubora kweli?
Dar es Salaam. Magonjwa ya ngozi, kupungukiwa maji mwilini na maumivu ya kichwa ni kadhia zitakazowakumba baadhi ya wakazi wa Dar es Salaam kutokana na joto kali linalolikumba jiji hilo.
Tayari Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa hali ya hewa katika jiji hilo hadi jana lilikuwa limefikia nyuzi joto 35.
Meneja wa Huduma za Utabiri wa TMA, Samwel Mbuya jana alisema joto la mwaka huu limevunja rekodi kwani kwa kawaida, kipindi cha Januari linatakiwa liwe nyuzi joto 32.
Mbuya alisema joto hilo pia limeongezeka hata kwa upande wa Zanzibar ambako limefikia nyuzi joto 35 ikiwa ni ongezeko la asilimia mbili.
Alisema sababu kubwa ni kuongezeka kwa joto katika ukanda wa Bahari ya Hindi ambalo pia linatishia kuwapo kwa mvua za El-nino.
Alisema kadiri mvua zinavyochelewa, ndivyo joto la bahari linavyozidi kuongezeka na kusababisha hali iliyopo.
Madhara ya joto kiafya
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya ndani ya mwili, Meshack Shimwela alisema kwa sasa wanapokea kesi nyingi za magonjwa ya ngozi kama upele, fangasi, kupungua maji mwilini na kuumwa kichwa.
Alisema joto kali linamfanya mtu apoteze wastani wa lita tatu za maji kwa siku. “Kwa watu wasiokunywa maji katika kipindi hiki wanaweza kukaukiwa maji, kwa sababu hawanywi vimiminika vya kutosha kujazia kiwango kile kilichopotea,” alisema.
Chanzo: Mwananchi
Hope utatoka lakinUmezama mwilini
MmhHuwezi Amini ndio zinaongezeka ukali Kama mbolea ya samadi Aisee.
nasikia kuna mji huko oman kitu kinafikia 60 degree Celsius
cc GENTAMYCINE bila shaka anajua kuhusu hili.Hivi na hili joto mbegu zetu hazipungui ubora kweli?
Tofauti ya wale jamaa na sisi ni kwamba Qatar mpaka kwenye vituo vya mabasi kuna Air condition na karibia kila sehemu Ina ACs. Hapa kwetu Joto linatutesa sana hasa sisi walala hoi tusioweza gharama za Air Cons.Kuna documentary moja nilikuwa naangalia sasa hivi wanasema Qatar mwezi june na july joto linafika hadi nyuzi joto 50. Nimeogopa.
Hapo ndio nazidi kupata hasira na huenda labda nisije kukunyaga jiji la dar maisha yangu yote
Haiwezekani jiji lenyewe chafu,
Folene kila sehemu
Joto na hapo bado sijakutana na vibaka
Mbona watu wa dar mnahangaika sana na maisha
Jiji lenyewe limejengwa kama mchwa
Tumia dawa ya Gentrisone Cream, made in Korea, utaleta mrejesho, inapatikana kwenye maduka yote ya dawa.Kweli joto limezidi. Daaa chini ya manyonyo kumechubuka, mapajani kumechubuka hali ni hovyo.
Vipele vipo sehemu gani? sema nikupe dawa.Nimetokwa vipele kama mtoto mdogo. Naulizwa umepaka nini!! Au maji ya chumvi? Walaa... Kumbe joto....
Inyeshege tu hio mvua kha!