Joseph Mbilinyi anavochemka!

Joseph Mbilinyi anavochemka!

Ahaa ujumbe umeeleweka asiyeeelewa na aombe ufafanuzi!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
waliopo ndani ni viziwi

huyu yuko nje alitakiwa apiganie na ikibidi apewe taarifa na a go public na maelezo toka kwa jamaa wa wizara ya sheria na TAMISEMI lakini wapi

kilichobaki ni kuja kusemea humu labda atasoma asubuhi hiii

Oh! kumbe unajua waliopo ndani ni viziwi kwa hiyo hata sugu akipiga kelele hawatamsikia,so you was joking enh!!!!!
 
Hii ndio manifestation ya aina gani ya viongozi tulio nao Tanzania. Seriously, we need a dictator to turn this shit upside-down, tunatia aibu.mwanzisha uzi inaonekana na wewe ni kilaza kama aliyendika huo upuuzi, ndio maana umeamua kumtwisha mzigo wa lawama Sugu asiye usika. Unataka Sugu aanzishe darasa la kuwafundisha kiingereza?... Hujui kama English pia ni official language Tanzania?.
 
Huyu ni waziri kivuli wa Utamaduni lakini cha ajabu hakemei wala hasemi neno juu ya matumizi ya lugha za kigeni kwenye majarida, miswada ya sheria na kwingineko

hiivi maana ya kukaa kimya ni nini?

Freeman kama huyu jamaa kashindwa kazi tuwekee mchapa kazi ambaye anaweza kusimamia mambo haya

sensa+%281%29.jpg

SUGU anahusikaje na hili tangazo? Si umbane mhusika bwana Peter Mushi!
 
Sijui ni kwa nini napata taabu kuiamini kama hiyo barua ni ya kweli! Kama ni ya kweli basi kuna tatizo kubwa sana nchi hii kuliko tunavyodhani.
 
Katika suala la wizara ya habari na utamaduni hakuna jambo linalonikera kama hivi vigazeti vya udaku.Yanamomonyoa maadili kwa kasi huku wahusika wametulia maofisini.Dada zetu wamekuwa wagonjwa wakubwa bora asile lakini ajue nani kafumaniwa,fulani siku hizi mpenziwe nani,na hizo picha ndio hazitazamiki.Serikali iko bize kujenga kizazi cha wanaudaku na upuuzi wake lengo kuzalilisha mbumbumbu wakutosha ili waweze kukomba vema.Huitaji ushaidi hapa,wamiliki wake ni makada wazuri wa CCM,hivyo huo ni mchango mzuri kwa chama chao.Usishangae kumkuta mbunge naye kashikilia gazeti la udaku likiwa na picha za uchi mpango umefanikiwa kwa kiasi kikubwa.Viongozi wa dinh wanajitahidi kuwarudisha watu mstari huku serikali ya CCM ikijitahidi kuwapotosha,sitashangaa siku TBC ikianza kurusha vipindi vya pilau au blue movie kama zinavyojulikana.Hii serikali ni janga!
 
Nashauri siku nyingine ukiamka uwe unasugua kinywa na kunawa uso kisha si vibaya ukichamba koo kwa kikombe cha kahawa au chai ya rangi kabla hujakaa kwa kutumia kiungo cha kukalia kisha ufikiri na kuandika humu. Huu ni ushauri unaoweza pia kuupata kwa mtaalam yeyote wa saikolojia ya vichaa.
 
Jamaa amemwaga uzungu wa kiwango cha juu""""

Kidumu Chama Letu la CDM, no ulimi pana mfupa ......CCM
 
Nashauri siku nyingine ukiamka uwe unasugua kinywa na kunawa uso kisha si vibaya ukichamba koo kwa kikombe cha kahawa au chai ya rangi kabla hujakaa kwa kutumia kiungo cha kukalia kisha ufikiri na kuandika humu. Huu ni ushauri unaoweza pia kuupata kwa mtaalam yeyote wa saikolojia ya vichaa.

mkuu punguza ukali wa maneno,hauendani nayo hasa ukizingatia unatumia jina halisi!!
 
Magamba kwa kuvuta hisia za watu! Sasa hapa Mbilinyi afanye nini? Au unashindwa kuandika Dr Fenela?
 
kwani kaandika Mr. 2 Sugu hilo,
si mmeandika nyie wenyewe.

tena una chuki binafsi unavyoonekana,
kwani zanzibar huru na mr 2 sugu mnagombea nini hasa.
 
Kwa faida ya wale ambao hawawezi ku-download hilo tangazo, naomba ni-post neno kwa neno barua yenyewe (main body only). Dah! hizi lugha jamani. Ningekuwa mimi ninge-resign leo leo:

TO
THE ALL RESIDENCE AND
RENTER AT APARTMENT, HOTEL
AND OTHERS

REF: CENSER COUNTING PEOPLE 26 AUG 2012

Refer the above mentioned Subject

Remember the Government of Republic Union of Tanzania announce on 26.08.2012 is the day of counting people [censer] for all living visitors in Tanzania. This is legal order for Bureau Statistics No: 1 of 2002.

Because of this day any people who sleep at your House, Hotel, or residence apartment on 26.08.2012 he or she must be accountable in this censer. Also all people must answer this Question from the Censer Officer.

ORDER
If your refuse to be countable or stop censer Officer to do the job of counting people from 26.08.2012and 7 days more its is criminal case, then you will be charged in the court and fine with sentenced in prison for 6 month. The please give all assistance Censer Officer what he or she need

I was countable and i give all assistance Censer Officer and i did not stop Cencer officer to do job of counting people..............teh
 
Sasa badala ya kumsema mwenye dola unakimbilia Waziri kivuli. Laumu serikali yako we unafikiri sugu hata akisema watafanya nini? Mangapi yamesemwa lakini hatuna lolote? Amka shtuka.
 
Tanzania tuna tatizo kubwa sana, nadhani alichotaka kusema mtoa uzi sio hicho kinachojadiliwa, yeye alitaka watu waone usahihi wa lugha ilivyotumika. Suala sio kiingereza bali sio kiingereza sanifu.

Kwa maana hiyo, tatizo ninaloliongelea hapa ni uwezo wetu mdogo wa kuandika lugha kwa usahihi. Na tatizo sio la kiingereza au lugha yeyote ya kigeni ila hata lugha yetu adhimu, ya kiswahili. Tunafanya makosa mengi ya kiuandishi na hata wakati wa kuzungumza.

Nadhani hii ni fursa ya kiuchumi, wajitokeze wataalam wa lugha( fasihi andishi na fasihi simulizi) soko la ndani bado ni kubwa na wanaweza hata kuwasaidia watoto wetu.
 
Back
Top Bottom