Joseph Mbilinyi anavochemka!

Kwa faida ya wale ambao hawawezi ku-download hilo tangazo, naomba ni-post neno kwa neno barua yenyewe (main body only). Dah! hizi lugha jamani. Ningekuwa mimi ninge-resign leo leo:

TO
THE ALL RESIDENCE AND
RENTER AT APARTMENT, HOTEL
AND OTHERS

REF: CENSER COUNTING PEOPLE 26 AUG 2012

Refer the above mentioned Subject

Remember the Government of Republic Union of Tanzania announce on 26.08.2012 is the day of counting people [censer] for all living visitors in Tanzania. This is legal order for Bureau Statistics No: 1 of 2002.

Because of this day any people who sleep at your House, Hotel, or residence apartment on 26.08.2012 he or she must be accountable in this censer. Also all people must answer this Question from the Censer Officer.

ORDER
If your refuse to be countable or stop censer Officer to do the job of counting people from 26.08.2012and 7 days more its is criminal case, then you will be charged in the court and fine with sentenced in prison for 6 month. The please give all assistance Censer Officer what he or she need
 
...mwee! zisi izi ze inglishi kwa kweli...mie sio kipanga katika lugha husika ila hii imezidi!!
 
Huyo Mchaga atakuwa kasoma St. Kayumba, mkiambiwa MoU hazisaidii kusomesha watu, mnakataa, matokeo ndio hayo.

ndugu yangu zoba utaacha lini udini au kutuma post zisizo na harufu ya udini udini mpaka lini?
 
This is outcome of ignoring professionalism. How does one dare to write such a hotchpotch of words and have it presented to the public. Even competent writers seek 'proof reading' from others. Simfagilii Sugu, ila katika hili sioni kuhusika kwake.
 
Badala ya kujadili hoja, kuna wenzangu na mimi wanaleta udini. Hii meli ya udini waliyopanda inazama muda sio mrefu....tujiandae kuokoa wahanga wa meli hiyo maana imepoteza mvuto.
 
Hahaha! Yaani this made this countable day of mine. Duh! Kwani offical language ya nji hii si kiswahili?
 
sasa badala ya kuwakomalia walioko madarakani mnataka kuwabana walio nje ya madaraka. Sasa imagine kuwa Mbilinyi kasema na kakemea then what? Utakuwa umeridhika na kujisikia vizuri!

Yeye kama waziri kivuli ni kazi yake kukosoa pale anapoona hapajakaa sawa.. atimize wajibu.. hao walio madarakani wasipushughulikia hayo ni mengine ... Ndio umuhimu wa upunzani bungeni kutoa maoni yao pale wanapoona pana hitilafu .. sasa wakiwa wanakaa kimya ati si kazi yao... Nini itakuwa umuhimu wa upinzani.. ?
 
Nadhani tatizo si kukemea au kutokumea bali kuwa na serikali iliyoko madarakani ikiundwa na watu wasio na maadili. Siku hizi Tanzania imekuwa dampo la kila uchafu hasa miigizo. Tuna vituo vya TV vyenye kutoa huduma chafu kwa wateja. Tuna vipindi vya kisagaji kama Mikasi na utitiri wa magazeti ya udaku. Kenya hawana magazeti ya udaku, matangazo machafu wala vipindi vya hovyo kama Tzania. Nadhani tatizo ni jamii ya kitanzania kupenda vitu vya hovyo na kuchukia vitu muhimu. Iwapo rais mwenyewe hana maadili hadi kuwaambiwa wanafunzi wanaopata mimba eti ni kutokana na kiherehere chake huku wabunge wake wengi wakiwa wavuta bangi na walevi unategemea nini? Hili si tatizo la upinzani bali CCM.

Umesema vema kabisa
 
Ujumbe uliwafikia walengwa? Kama hakuelewa bado wanayo nafasi ya kumuuliza mhusika; muhimu ni ujumbe uliifika?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Huyo Mchaga atakuwa kasoma St. Kayumba, mkiambiwa MoU hazisaidii kusomesha watu, mnakataa, matokeo ndio hayo.
Ingekuwa ajabu sana kama ungechangia mjadala huu bila kuitaja MoU (sijui kwa nini waisilamu wengi wakisikia MoU wanajua ni makubaliano ya kanisa na serikali, hawajui kama mbali ya kanisa na serikali, kuna MoU nyingine nyingi tu!). Kwa kuwa MoU si mjadala hapa, turudi kwenye barua ya sensa!
 
nani anabisha kuwa hiyo sio product ya morogoro m university?

hujajua tatizo hili ni zaidi ya mliloliona kwa huyu ndugu.tena huyu kajitahidi. niliwahi kukutana na barua moja imeandikwa na mtu mkubwa na madaraka makubwa hicho kimombo chake balaa. ili uelewe alikuwa anakusudia kusema nini inabidi kwanza ushushe mambi kwa MUNGU akupe msaada.sasa hivi ni kutoka vyuo vingi tu mastery ya lugha ni questionable.
 
waliopo ndani ni viziwi

huyu yuko nje alitakiwa apiganie na ikibidi apewe taarifa na a go public na maelezo toka kwa jamaa wa wizara ya sheria na TAMISEMI lakini wapi

kilichobaki ni kuja kusemea humu labda atasoma asubuhi hiii

Ndo matatizo yetu watanzania haya,mara nyingi tunaacha kushughulikia tatizo hasa tunang'ang'ana kufanya projection wakati tunajua kabisa kwa kufanya hivyo hatutatui tatizo. Je umemwambia waziri husika mwenye mamlaka zote na wizara hiyo hadi umlaumu waziri kivuli!!??? This is pure naive consciousness!
 
Back
Top Bottom