John Mnyika: Nakiona Kitanzi cha Bima ya Afya kwa wote kabla hata hatujafika Mbali

Heparin

Senior Member
Sep 24, 2021
127
420
Screen-Shot-2019-12-20-at-09.50.46.png
Nitashukuru Rais Samia na Waziri Ummy Mwalimu mkatoa maelezo kwa umma ni kwa vipi wakati pricing list ya 2016 (NHIF) inatolewa bei ya petroli ilikuwa shilingi chini ya 1700 kwa lita dola moja ilikuwa chini ya 2100 halafu pricing list mpya ya NHIF inayoanza kutumika kesho Machi Mosi Petroli ikiwa zaidi ya 3000 kwa lita dola moja ya Marekani ikiwa zaidi ya 2600 ikiwa chini ya 2016? Nani anayefidia hilo pengo na kubeba mzigo?

Kupunguza bei ya bidhaa muhimu ikiwemo madawa na vifaa tiba kunahitaji Mkakati wa Dharura, haraka na makusudi utakaokuwa mtambuka na kutazama picha pana kwenye sekta kuu za kiuchumi kwa umma na kwa binafsi. Mkakati wa kisera, kikodi, kiutendaji na kimatumizi. Rais pitia ripoti iliyoko mezani kwako ya ufisadi na matumizi mabaya NHIF itakuongoza kufanya maamuzi sahihi. Nakiona kitanzi kwa bima ya afya kwa wote kabla hata hatujafika mbali. Narudia rai yetu ya kutaka mjadala juu ya huduma bora na nafuu za afya kwa wote.

John Mnyika
Mtandao wa X
 
Baada ya kukanusha kwingiii mwishowe ukweli umesimama.

Kifuatacho ITV ni kuwawekea vikwazo hao waliogoma kama case ya KM wa CWT.
 
Back
Top Bottom