John Magufuli: Ninautamani urais!

John Magufuli: Ninautamani urais!

By mavumbi Hana haiba, uwezo, msimamo, ujasiri, wala IQ ya kutosha

toa tafsiri ya hayo uliyotoa hapo juu,uliyosema hayo yote magufuli anayo tena zaidi ya yote.

1. Haiba: Mvuto, bashasha
2. Uwezo: Uthabiti, Ufanisi
3. Ujasiri: Uthubutu, Bila woga
4. I.Q. : Uwezo wa kutambua / kuchambua mambo

Mifano Hai:

Samahani nitumie lugha yetu na ya kigeni:
1. Lacks fluency and application of proper speech iwe Swahili au Kiingereza (yawezekana ni suala la kabila)
2. Wizara anayoiongoza imejaa ufisadi na rushwa ya ajabu (uliza wanaoendesha magari makubwa wakifika vituo vya weigh-bridges)lakini anachofanya ni kukimbizana na miradi ya barabara .
3. Alitumwa na nanin kwenda Kenya kutoa salamu kwenye campaign ya Raila Odinga? Huyu ametuweka mahali pagumu sana na Wakenya ...Kama angekuwa jasiri angemwambia aliyemtuma kule kwamba hakikuwa kitendo muafaka. Haya ..yako wapi?
4. Ameuza nyumba za serikali halafu serikali hiyo hiyo inaingia gharama ya mamailioni ya shilingi kuwaweka watumishi waandamizi nkwenye mahoteli... tena ya kifahari? Hiyo sio questionable IQ?

SEMA... NIONGEZE NYINGINE?
 
Magufuli siyo tu hana nguvu ndani ya Chama , bali pia Hana sifa za kuwa Rais. Rais lazima awe mtu mwenye uwezo aw kujenga Hoja , siyo wa kukariri kilometer au idadadi ya Samaritan haharini. Anatakiwa mtu mwenye uadilifu usiotiliwa shaka. Magufuli si madilifu, licha ya kupiga makelele, ni mpokeaji mkubwa we rushwa kutoka kwa makandarasi. Vile vitisho anayo toa kwa makandarasi ndiyo mbinu yake ya kujizolea milungula kutoka Kwao. Ni mtu asiyesikiliza ushauri wowote kutoka kwa watalaamu wake, kwa vile anadhani anajua kila kitu. Ndiyo maana Aliza nyumba zote za serikali mpaka za hospitali na Vito vya polisi na kuuza nyumba za serikali kwa hawala na nudge zake walikuwa watumishi aw serikali. Mbali na hayo wizard yake inashindwa kueleza ziliko shs 260 bn zilizotengwa kulipa madeni ya makandarasi ambayo haya kulipwa na fedha hazijulikani zilipo. Kama hayo yote anayafanya akiwa waziri je akiwa itakuwaje. Hafar Hafai Hafai.
 
Ccm wanapenda sifa za kijinga
Source NIPASHE 05/07/2013

Katika hali inayoonyesha kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli,
anautamani urais, amesema anaweza kutangaza nia hiyo kama atakidhi
masharti yatakayowekwa kwenye Katiba mpya.

Alisema iwapo Katiba ijayo itakuja na sifa ambazo atakidhi vigezo kuna
uwezekano mkubwa wa kuwania nafasi hiyo na kwamba iwapo atapungukiwa
sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba hataingia kwenye kinyang’anyiro
hicho.

Dk. Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato alitoa kauli hiyo wakati
akizungumza na wazee wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa ‘Mshikamano
Saccos’, muda mfupi baada ya mzee Paschal Nyambibo (87) kumsihi agombee
nafasi hiyo mwaka 2015 kutokana na sifa zake za uchapakazi ndani ya
serikali.

Nyambibo alisema kutokana na uwajibikaji mzuri aliouonyesha Dk. Magufuli
tangu mwaka 2000 akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na katika wizara
mbalimbali, Watanzania wamekuwa na imani kubwa na uwajibikaji wake na
kwamba anastahili kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
ifikapo mwaka 2015.

Licha ya kauli hiyo kusababisha minong’ono mingi kwa wazee waliohudhuria
kikao hicho, Dk. Magufuli alionekana kutuliza hali hiyo kwa kusema
isubiriwe Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano iwapo itakuwa na masharti
ambayo yatamfanya kujitathimini iwapo ana sifa za kugombea au
vinginevyo.

Hata hivyo, Dk. Magufuli hakusita kuonyesha hisia zake za kukerwa na
baadhi ya wananchi wanaobeza maendeleo aliyotekeleza katika jimbo lake
tangu alipochaguliwa kuwa Mbunge.

Alimshutumu hadharani aliyekuwa Katibu wa CCM wilaya ya Chato kabla ya
kuhamishiwa wilayani Mbogwe, Gervas Stephano, kuwa hana shukrani.

Dk. Magufuli alimwelezea katibu huyo kuwa hana fadhila kutokana na mambo
mengi aliyomtendea tangu akiwa katibu wa ofisi yake ya jimbo ambapo
alimsaidia kupanda ngazi na kuwa Katibu wa CCM wilaya Chato, Kwimba,
Kasulu, Kilosa na kurejea tena Chato kabla ya kuhamishiwa wilaya ya
Mbogwe mkoani Geita kuendelea na wadhifa huo.

“Tatizo lenu watu wa Chato hamna shukrani…mambo mengi nimefanya hapa
Chato, lakini yote mnaona ziro…hata niliowasaidia kama Gervas naye sasa
hivi ananiponda…lakini nawashukuru sana wazee wangu kwa kunikumbusha
niliyoyafanya kwenye jimbo letu kupitia risala yenu nzuri,” alisema Dk.
Magufuli.

“Kutokana na hali hiyo ninawazawadia Sh. 1,000,000 mfanye sherehe ya
kujipongeza kwa kuwa natambua mmejitesa sana mpaka kufanikisha kikao
hiki cha leo…na kwa kuwa hamna mradi wowote wa kuwaingizia kipato kama
wazee, ninaahidi kuwapa Sh. 3,000,000 kutoka mfuko wa jimbo, ili
muanzishe walau saccos ya kukopeshana,” alisema.

Baadhi ya viongozi na wananchi wamekuwa wakilitaja mara kwa mara jina la
Waziri Magufuli miongoni mwa watu wanaodhaniwa kutaka kugombea nafasi
ya urais wa Tanzania mwaka 2015, ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha
uvumi huo.

Mbali na Dk. Magufuli, wengine ndani ya CCM wanaotajwa ni pamoja na
aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa;
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye anajiita
mtaji wa urais; Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Katibu wa
Halmashauri Kuu ya Taifa Ushirikiano wa Kimataifa –CCM, Dk. Asha-Rose
Migiro na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Mambo ya Nje, Bernard
Membe, ambaye alipata kusema anasubiri kuiteshwa na Mungu kuwania
nafasi hiyo.
 
Urais hautafutwi na mtu binafsi, inampasa asubiri kuombwa na chama chake cha ccm baada ya mchujo.Hata hivyo inampasa ajipime kama anastahili kuiongoza nchi hii.Kazi ya kusimsmia ujenzi wa barabara hapana shaka ni tofauti kabisa na kuongoza nchi ya watu 45 milioni wenye hisia tofauti.This time tumpate Rais mwenye angalau asilimia 30 ya sifa za hayati baba wa Taifa bila kujali anatoka chama gani
 
Atapigiwa kura na wanyamwezi/wasukuma + watani zao wazaramo,wakwere,wandengereko,wagogo,wangoni,wahehe,wazigua,wabondei,wamwera,wadigo na wasambaa wote! Sasa hapo unabisha? Magufuli ni hazina ya urais 2015,hata asipopiga kampeni ni lazima ashinde tu,hilo halina ubishi na ujiandae kuhamia burundi bundi wewe
 
...huyu bwanamdogo akiweza kubomoa jengo la ubungo kama alivyoapa mara kadhaa,basi nitaamini anaweza kujisimamia mwenyewe,vinginevyo ni mtu anayehitaji kuwa chini ya mtu inapokuja suala la utendaji...
 
..hana staha, hana busara, na hana uadilifu, kuweza kuhimili changamoto za Uraisi.
 
hongera watakatifu.
akili zilizoganda wapumbavu msiojua kesho yenu.
subirini,mtaisoma number msifikiri uwoga huu wa watanzania utadumu milele.

ameiba wake za watu,unaumia nini,amemuiba mama yako?
wewe ni wakili wake?stupid mind.
vinywa vyenu like public toilet,jifunzeni kuweka akiba ya maneno,kesho itawagharimu.

haya hapa.
 
Mtu akitamani kazi ya Uraisi amefanya vema, basi imempasa raisi kuwa mtu wa aina hii;

1. Asiwe mlevi
2. Asiwe fisadi
3. Asiwe CCM/CDM, Bali Mtanzania halisi
4. Asiwe Mkabila
5. Awe na dini safi na isiyo na mawaa/ Anaye mpenda Mungu na kumwogopa
6. Awe na msimamo dhabiti juu ya wezi na mtandao wa wezi wa mali za umma
7. Asiwe kinyonga/ awe na rangi halisi inayo julikana
8. Awe na ujasiri wa kurekebisha makosa yote yaliyo fanyika bila kumumunya maneno
9. Asiwe na kinyongo kwa jinsi ya kujilipizia kisasi
10. Awe na uwezo wa kusimamia rasilimali za nchi kwa faida ya mtanzania kwanza

Hizi ni sifa za mtu yeyote anaye utaka uraisi mwaka 2015, Magufuli unakaribishwa kujipima na kwa kuwa muda bado upo,basi unaweza kujijenga kwa sifa ambazo kwa sasa zinapungua

Asante
 
Magufuli ni mzuri kiutendaji na anaweza kufanya wonders akiwa Rais ila ujinga wake ni kumsifia mno mtu dhaifu aliyeshindwa kuiongoza nchi. Pia akiwa Rais atawalinda waliofisadi nchi kwa sababu atalishwa kiapo cha kisirisiri na mafisadi ya CCm.


Duru zinasema Magufuli akisimama basi uchaguzi umeisha! Atashinda kwa kishindo
 
Mtu akitamani kazi ya Uraisi amefanya vema, basi imempasa raisi kuwa mtu wa aina hii;

1. Asiwe mlevi
2. Asiwe fisadi
3. Asiwe CCM/CDM, Bali Mtanzania halisi
4. Asiwe Mkabila
5. Awe na dini safi na isiyo na mawaa/ Anaye mpenda Mungu na kumwogopa
6. Awe na msimamo dhabiti juu ya wezi na mtandao wa wezi wa mali za umma
7. Asiwe kinyonga/ awe na rangi halisi inayo julikana
8. Awe na ujasiri wa kurekebisha makosa yote yaliyo fanyika bila kumumunya maneno
9. Asiwe na kinyongo kwa jinsi ya kujilipizia kisasi
10. Awe na uwezo wa kusimamia rasilimali za nchi kwa faida ya mtanzania kwanza

Hizi ni sifa za mtu yeyote anaye utaka uraisi mwaka 2015, Magufuli unakaribishwa kujipima na kwa kuwa muda bado upo,basi unaweza kujijenga kwa sifa ambazo kwa sasa zinapungua

Asante

Katika woooote wanaosemwa huwezi kumpata huwezi kumpata mwenye sifa hizo.
 
twende twende twendeeeeeeeeeeeeeeeee Magufuli........... hofu yangu ni kama mafisadi watakupitisha. CCM umebaki wewe tu.
 
ni jana tu nimeona ilani ya mtu mmoja ikiandaliwa kwa ajili ya mwaka 2015 nae akiutaka huo huo urais!!... jamaa ana imani kubwa kweli ya kuukwaa urais
 
Hamuwezi jembe EDDO

Sent from my BlackBerry 9700 using Jamii Forums

...Ni kweli, Magufuli hamuwezi Eddo kwenye nyanja ya "ukosefu wa uadilifu na ufungamano na makundi ya kifisadi"....

...Kwenye hilo Eddo yupo kwenye ligi ya peke yake, hakuna mwanasiasa nchi hii anayeweza kushindana na Eddo kwa mafungamano na ufisadi...
 
CCM wampe Pombe URAISI hawajipendi
Itakuwa kama SATA Zambia atawaweka ndani zaidi ya nusu ya vigogo wa SASA.
Kama anataka inabidi aaze jivika ngozi ya kondoo kuanzia sasa ili wakimpa URAISI tuu anajivika ya SIMBA
 
Magufuli kusema ukweli jamaa ni NOMA, anawazidi WOTE CCM hakuna ubishi.
 
Akigombea then CCM wasipitishe kwa hila, akigeuka MWANAWANE ina kula kwao 95%
 
By mavumbi Hana haiba, uwezo, msimamo, ujasiri, wala IQ ya kutosha



1. Haiba: Mvuto, bashasha
2. Uwezo: Uthabiti, Ufanisi
3. Ujasiri: Uthubutu, Bila woga
4. I.Q. : Uwezo wa kutambua / kuchambua mambo

Mifano Hai:

Samahani nitumie lugha yetu na ya kigeni:
1. Lacks fluency and application of proper speech iwe Swahili au Kiingereza (yawezekana ni suala la kabila)
2. Wizara anayoiongoza imejaa ufisadi na rushwa ya ajabu (uliza wanaoendesha magari makubwa wakifika vituo vya weigh-bridges)lakini anachofanya ni kukimbizana na miradi ya barabara .
3. Alitumwa na nanin kwenda Kenya kutoa salamu kwenye campaign ya Raila Odinga? Huyu ametuweka mahali pagumu sana na Wakenya ...Kama angekuwa jasiri angemwambia aliyemtuma kule kwamba hakikuwa kitendo muafaka. Haya ..yako wapi?
4. Ameuza nyumba za serikali halafu serikali hiyo hiyo inaingia gharama ya mamailioni ya shilingi kuwaweka watumishi waandamizi nkwenye mahoteli... tena ya kifahari? Hiyo sio questionable IQ?

SEMA... NIONGEZE NYINGINE?

ni kweli anaongoza wizara iliyojaa ufisadi mkubwa kuanzia ma inginia mpaka technicians,juzi kwenye bunge la budget alihojiwa matumizi ya bill 300 ya kulipia madeni!!!!kimya mpaka leo!!!
 
Back
Top Bottom