Joe Biden: China Iko Taabani Kiuchumi

Joe Biden: China Iko Taabani Kiuchumi

Huu ndio ukweli ila wale wafuasi wake Watapinga.

Idadi ya Watu wanaozaliwa China imepungua kuliko vifo.

Idadi ya Wazee inazidi kuongezeka

Ukuaji wa Uchumi wake Umepungua sana.

Shida ya Kisiasa za ndani zimenza,sera ya zero covid iliwaahinda Hadi watu wakaandamana dhidi ya Utawala.

Kampuni zake za nyumba zimeanza kupata shida na Baadhi mbioni kufilisika eg Garden

Gharama za Uwekezaji wa viwandani zimeanza kuongezeka.

Mwisho China imeanza Utapeli wa Mali na ukoloni mamboleoa Kwa Nchi za Kiafrika Kwa njia ya Mikopo nk.


My Take
China haiaminiki, siku yaja Yuan yake itaporomoka sana.

Wee kweli ndio funza tu wa hao kina biden. Sasa hapo ndio uchina iko taaban kiuchumi?
 
Russia, China na India zote zinapinga utawala wa kiislam wa Kigaidi wa ISIS, so sio USA pekee....
Zingatia hindi magaidi wa ISIS walivyobamizwa na Russia miaka michahche iliyopita kutokea Syria na taliban

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuuliza kitu kingine umejibu kitu kingine kabisa! Unaonekana wewe ni wale wamarekani wa Nzega wenye mahaba niue na US.
 
Dikteta Xi jinpin anawaponza sana watu wa China.

Anawapeleka shimoni kila siku mi nasemaga hapa.

Alileta sera yake ya "return forest to farmland" akihamasisha kilimo kwa kukata miti kila pahala hata mahali pasipofaa matokeo yake juzi beijin na maeneo mbalimbali yamepigwa na mafuriko yaliyotokana na tufani balaa, watu wameripotiwa Kufa cha ajabu CCP haionekani kujali chochote.

Sera za Dikteta Xi zote yaani zote zimegoma na zimekuwa zikiwagharimu watu wachina wasiokuwa na hatia.

Bado sera yake ya "One china" ambayo imelenga kuirudisha Taiwan chini ya utawala wa CCP. Hii sera ndio itaiua kabisa CCP.... yani akijichanganya tu kuivamia Taiwan na CCP ndo inakuwa imekufa. Yaan CCP na Jeshi lake la PLA watapigika kila upande ndani na nje ya China tupo hapa mtakuja kuniambia.

Kuna baadhi ya wachina ni kwa vile hawana silaha lakini ukiwapa silaha wako radhi kupambana na ÇCP na jeshi lake, jambo hili Xi Jinping bado hajalifikiria..

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuhusu China ulishasema sana humu ndani ila watu wakawa wanakupinga.

Heshima yako mkuu
 
Viwanda vingi vya mabeberu vipo china sababu ya cheap labor so hata ukienda nunua mzigo china basi Kuna faida pia unampatia beberu.
Na siku mabeberu wasitoe tu uwekezeji hapo China, wakija kuutoa China watatafutana.
 
Mkuu nafatilia kwa karibu sana Geopolitics issues migogoro yote ya Asia na Pacific.

China ndio anaeongoza kwa ukorofi kwa mataifa jirani.

Juzi katoka kumuharass Philippine kwa kuipulizia maji yenye presha meli ya kifilipino iliyokuwa inaelekea kwenye eneo lililoko kwenye EEZ yao kisheria ambalo ni eneo Leo.

Bado ana ugomvi na Vietnam, Indonesia, India, Japan Taiwan , at the same time unataka uvutie uwekezaji uchumi wako ukue vitu non sense kabisa.

Wasipochukua hatua ya kumwondoa xi Jinping madarakani uchumi wa China utakufa serious.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa hao majirani zake wakiungana si hatari mkuu? Vipi kwanza hao majiran wana long ranges za kutosha?
 
Sasa lini US alikuwa mzalishaji wa yeboyebo na malonyalonya haya mnayoenda kuagiza China.
Uliwahi enda ofisi za Silent Ocean ukalinganisha tofauti ya wanaoenda kuagiza mizigo China, India, Uturuki, Dubai na Marekani walivyo? Wanaoenda China wana maneno balaa mzigo unachelewa siku moja wanalia kama wamekula mtaji.
Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha

Nimecheka sana mkuu! Mkuu mizigo ikichelewa kutoka China hizo kelele ni balaa.
 
Viwanda vingi vya mabeberu vipo china sababu ya cheap labor so hata ukienda nunua mzigo china basi Kuna faida pia unampatia beberu.
Ila China inalia kutokana na gharama za uendeshaji kupanda, unemployment kubwa kutokana na automation na robotics
 
Back
Top Bottom