Joe Biden: China Iko Taabani Kiuchumi

Joe Biden: China Iko Taabani Kiuchumi

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
82,489
Reaction score
88,633
Huu ndio ukweli ila wale wafuasi wake Watapinga.

Idadi ya Watu wanaozaliwa China imepungua kuliko vifo.

Idadi ya Wazee inazidi kuongezeka

Ukuaji wa Uchumi wake Umepungua sana.

Shida ya Kisiasa za ndani zimenza,sera ya zero covid iliwaahinda Hadi watu wakaandamana dhidi ya Utawala.

Kampuni zake za nyumba zimeanza kupata shida na Baadhi mbioni kufilisika eg Garden

Gharama za Uwekezaji wa viwandani zimeanza kuongezeka.

Mwisho China imeanza Utapeli wa Mali na ukoloni mamboleoa Kwa Nchi za Kiafrika Kwa njia ya Mikopo nk.


My Take
China haiaminiki, siku yaja Yuan yake itaporomoka sana.
 
Mkuu hayo yote yalitamkwa ndio yanayoendelea China. Uhalisia ndio huo

Sent using Jamii Forums mobile app
Una ushahidi wa kitaalamu juu iko alichosema Biden?? Wewe ni mchumi?

Or kwasababu kaongea Biden na wewe unaamini ?? Hujui USA ndio mpinzani mkubwa wa China kiuchumi??, Sasa unategemea USA waisifu china?

Watu weusi sjui tunashida gani,yaani kitu akiongea Marekani basi nasisi tunaamini
 
Nia ya Marekani haikuwa kuigeuza China nchi ya kidikteta Bali kuwafanya wazidi kubadilika na kuwa nchi ya kidemokrasia iliyostaarabika.

Amekuja Dikteta xi na tamaa zake amebadilisha uelekeo wote na kuivuruga China yote.

Wachina wengi hawampendi ni vile basi tu hawana cha kufanya

Sent using Jamii Forums mobile app
Who is USA ??? Mpaka afundishe watu demokrasia??
 
Sijawahi sikia naenda USA kuchukua mzigo
Utasikia naenda china Dubai kuchukua mizigo
Pyeee Biden kumbukumbu huna
Sasa lini US alikuwa mzalishaji wa yeboyebo na malonyalonya haya mnayoenda kuagiza China.
Uliwahi enda ofisi za Silent Ocean ukalinganisha tofauti ya wanaoenda kuagiza mizigo China, India, Uturuki, Dubai na Marekani walivyo? Wanaoenda China wana maneno balaa mzigo unachelewa siku moja wanalia kama wamekula mtaji.
 
Huu ndio ukweli ila wale wafuasi wake Watapinga.

Idadi ya Watu wanaozaliwa China imepungua kuliko vifo.

Idadi ya Wazee inazidi kuongezeka

Ukuaji wa Uchumi wake Umepungua sana.

Shida ya Kisiasa za ndani zimenza,sera ya zero covid iliwaahinda Hadi watu wakaandamana dhidi ya Utawala.

Kampuni zake za nyumba zimeanza kupata shida na Baadhi mbioni kufilisika eg Garden

Gharama za Uwekezaji wa viwandani zimeanza kuongezeka.

Mwisho China imeanza Utapeli wa Mali na ukoloni mamboleoa Kwa Nchi za Kiafrika Kwa njia ya Mikopo nk.


My Take
China haiaminiki ,siku yaja Yuan yake itaporomoka sana.

China imetangaza kupata deflation mwezi huu nadhani ilikuwa kama 0.3%. Na ajira hazipatikani.
Hayo ndiyo matatizo makubwa nayaona kwake, mengine ya wazee kuongezeka, uchumi kupungua na gharama za uwekezaji kuongezeka yalitarajiwa huwezi kuyakwepa kutokana na sera zao na structure yao ya kiuchumi.

Nchi nyingi duniani zina uchumi wa kusuasua sasa hivi
 
Facts za uchumi zinaenda na research,

Sasa wewe unabwabwanya tu hutoi ushahidi wowote kuhusu uchumi wa China kuanguka, kisa Biden ndio kasema.

Nenad Kwenye tovuti ya World bank na IMF kasome then rudi hapa!

Hujatoa facts yoyote ya kiuchumi unapiga siasa tu kama Biden!

Watu weusi tunashida gani? Yaani kitu akiongea USA basi nasisi tunalipokea tu
 
Unatia kinyaa,..

Unapochangia mada kama huna uelewa na hilo jambo ni Bora ukae kimya upate ufahamu,

Kuna makampuni kibao ya uchumi yanayofanya uchunguzi kwaajili ya wateja wao ambao ni makampuni ya kimataifa na kila wakifanya uchunguzi wa kiuchumi wanatangàza matokeo yao.

Achilia hilo, IMF na china yentewe imekiri kuzorota kwa uchumi wao, halafu ww unakuja kupinga kitu ambacho huna ujuzi navyo

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakin pia nenda kasome pia ripoti ya nusu mwaka ya mwaka huu kuhusu uchumi ya USA na China then njoo hapa useme ,Je!! USA ananafuu ya kumcheka China???

Acha kuongozwa nahisia
 
Hata ukigoogle marekani ndio iko hoi kimadeni kidunia.
Screenshot_20230811_192601_Chrome.jpg
 
Kuna baadhi ya wachina ni kwa vile hawana silaha lakini ukiwapa silaha wako radhi kupambana na ÇCP na jeshi lake, jambo hili Xi Jinping bado hajalifikiria....
Unazungumzia Wachina wa Tibet na Xinjiang bila shaka.....Ila hao huenda ni sehemu ndogo tu ya walio tayari kufanya hilo.

Bado ana ugomvi na Vietnam, Indonesia, India, Japan Taiwan , at the same time unataka uvutie uwekezaji uchumi wako ukue vitu non sense kabisa.
Hiyo mivutano ya kimipaka imeanza kitambo sana Ila tukubali tu kwa sasa China pia ni 'regional power' na hao mahasimu hasa India na Japan wanahofia sana hilo...

.hivyo migogoro hiyo kuna muda hukuzwa makusudi au hutumika kuhalalisha kujijenga kijeshi kwa hao mahasimu mfano Japan na Marekani.
Amekuja Dikteta xi na tamaa zake amebadilisha uelekeo wote na kuivuruga China yote.

Wachina wengi hawampendi ni vile basi tu hawana cha kufanya
Hizi takwimu za Xi kutopendwa na Wachina wengi ni nadharia tu zisizoweza kuthibitishwa, Ccp walimpa Urasi kwa kishindo.

Baada ya kusambaratika kwa Ussr kwenye karne ya 20, China ndio mshindani mkubwa ajaye wa ulimwengu wa magharibi kwenye Vita baridi mpya ya karne ya 21.

T14 Armata
 
Research źinafanywa na nani?

Why China inetangaza kuwa na unemployment rate ya 21.3% kwa 16 to 24 years old people na inasemekana inazidi kukuwa? Na inasemekana ni zaidi ya 46% ukujumuisha watu wa rika zote

Kwann wana tatizo la real estate boom? Hii inaashiria nn? Na kwann wao wamenyewe wanakiri sekta yao ya real estate inashida?
Unaweza kunieleza sekta ya real estate China inachangia GDP kwa asilimia ngapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hako kazee nako ni kajinga sana mbona hakaongelei nchi kanayo iongoza ambapo maelfu ya mabenki yamefirisika.
 
Back
Top Bottom