JK Rais Bora kuliko wote Tanzania

JK Rais Bora kuliko wote Tanzania

Tatizo tulilonalo watanzania wengi ni ushabiki wa kisiasa,unavyofikili wewe ni tofauti na ninavyofikili,we kataa haya nisemayo ila ukweli utabaki kuwa hivyo.
Huwezi linganisha Uongozi wa JK na Marais waliopita JK ameface challenges nyingi sana katika kipindi chake na hili linatokana na watendaji wake kuwa wabovu.na tumeshuhudia watu wakiwajibishwa siwez kukupa mifano ya waliowajibishwa ila natumaini unajua

Naomba nisaidie kitu kimoja. Hao wasaidizi wake wabovu wanawekwa hapo walipo na nani???????????????
 
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

Namtakia kila la heri na kazi yake

Yah I can testfy
1 Tanzania isthe world’s third largest recipient of bilateral and multilateral assistance.Only Iraq and Afghanistanare receiving more aid
2 At least 38% of children under five in Tanzaniaare chronically malnourished
3 More than 50% of children suffer stunted growth in over30% of all regions in the country
4 Tanzania ranksfirst for having the fewest number ofcars per 1,000 people
5 Tanzania’s grossdomestic product (GDP) is the fifth most dependent on agriculture—about 45%. Atleast 76% of the population works in the agricultural sector6 More than 40% of Tanzania’s population lives inchronic food-deficit regions.
 
We unatafuta matatizo na hiyo thread yako. Hata kama unamsanifu kuwa makini... Utaona reaction humu ndani
 
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

Namtakia kila la heri na kazi yake
Jitahidi kujipendekeza, akipata hizo sifa unazommiminia anaweza akakupa ukuu flan wa idara flan au hata ubunge, sababu kikatiba yeye ndiye mwajri mkuu
 
wapuuzi ndivyo mlivyo......mnaangalia hizo flana za njano na kijani mnazoletewa na c maendeleo.
 
yawezekana Riz1 anakucameroon.ndo maana wakati anakucamerooon akakpa laptop utupie uzi hn jf
 
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

Namtakia kila la heri na kazi yake

Mkuu umepoteza muda wako mwingi kujaza maji kwenye gunia tupu. Ushauri wa bure huu hapa- tafadhali kamwoone dr. Akupe dawa ya kurudisha kumbukumbu zako. Juzi tu hata mwezi haujaisha umeshasahau kwamba Lowassa alitangaza live kuwa richmond ilikuwa ni ya JK. Usipenda kudandia hoja kama hizi sinakuumbua mkuu!!!
 
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

Namtakia kila la heri na kazi yake

Matope kweli uhuru wa kuongea anatoa rais na sio KATIBA.Umesoma shule gani wewe?
 
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

Namtakia kila la heri na kazi yake

Ala! Kila mtu na akili yake. Hivi ni kweli?
 
Ya kwanza ni Tanzania, wakati tunakubali masharti ya IMF na World Bank, hii nchi ilikuwa nyang'anyang'a, hicho ni kipindi cha Mwinyi alipokea hii nchi kutoka kwa nyerere. Hatuna fedha za kigeni, watu wote ukiwaona taabani hata kandambili hakuna madukani watu tunavaa makata mbuga. Hatuna mafuta, gari hazitembei Jumamosi na Jumapili mpaka kwa vibali, unakwenda vituo vya mafuta unakumbana na foleni, vigari vyenyewe vilikuwa kidoogo na hivyo hivyo vimechakaa kuliko Watanzania wenyewe. Hatuna chakula, kila kaya mnapewa kilo moja ya unga wa manjano kwa wiki, sukari kilo kwa wiki. Nchi imejaa rushwa na vyakula vya magendo vinavyoibiwa NMC, ukionekana umebeba mfuko tu, mgambo hao tayari wamesha kusimamisha. Hata sokoni ukienda nyanya zimesinyaa, zitatoka wapi? hakuna magari ya kuleta kutoka mashamba, mashamba hawalimi, ulime upeleke wapi mazao ukauze?

Nakumbuka hotuba ya Mwinyi alipowaita wazee wa Dar pale Diamond kuwaelezea alivyoipokea hii nchi mara tu baada ya kukabidhiwa, watu walilia machozi na nnakumbuka alipowaita tena baada ya mwaka kuwaelezea kwanini alikubali kukubaliana na IMF, hii ni hotuba inayoitwa "mikuki miwili" nayo ililiza watu, huko ndiko tulikowachiwa na Nyerere. Mengi sana, mengi sana, nikikumbuka nalia.

Leo unauliza ni nchi gani imefanikiwa kwa IMF na WB wakati mfano hai unao? au hukuwepo wakati Mwinyi anakabidhiwa hii nchi? kama hukuwepo ni bora utuulize tukueleze kiutaratibu lakini usikurupuke.

Hayo unayasema wewe, tubandikie hapa "quotations" zao kiukamilifu ili tujionee wenye walichokisema, tukuamini wewe kama nani? wakati unashindwa kuja na hata kimoja ambacho Kikwete hajakifanya unakuja na fulani kasema hivi, fulani kasema vile. Unanini? nchi inaendeshwa kwa maneno ya Warioba? nchi inaendeshwa kwa kuonesha vitendo na si porojo, hapa barabara hii, mkataba huu, na inajengwa kuanzia sehemu hii kwenda hii siyo nani kasema hiki nani kasema kile, huo ni ujinga. Mtu makini haoneshi maendeleo ya nchi kwa kusema nani kasema. Hao wote unaowataja ni vijiba vya roho kwani wao si ndiyo walikuwa viongozi wa zamani wamekiwacha nini cha kujivunia? foleni za unga wa uji na ugali?

Hayo ya mshule ndiyo usiseme kabisa, Kikwete kawachiwa hii nchi ina shule za Sekondari hazifiki 2000 na hizo ni Mkoloni, nyerere, mkapa, mwinyi wote changanya pamoja. Kwa wakati wake tu, zaidi ya shule 5000. hao waliomtangulia walikuwa wapi? leo statistics za shule zinasema 97% ya watoto wa umri wa kwenda shule wana uwezo wa kwenda shule, labda wawe na matatizo mengine, na isitoshe vyuo vikuu 11 kwa wakati wa miaka 6 tu, chuo kimoja tu cha Dodoma kinachukuwa wanafunzi zaidi ya vyuo vyote walivyoacha nyerere, mwinyi, mkapa ukichanganya pamoja, au yote hayo huyaoni?

Hao unaosema watoto wa vingunge, si wakati huu toka mkoloni mpaka leo, kila mzazi aliye na uwezo alipeleka mwanawe shule aipendayo, sema kabla ya mwinyi watu walibanwa na umasikini alioujaza Nyerere, watu wakawa hawana uwezo, baada ya Mwinyi tu tukaanza kuona mashule yaliyotaifishwa mengine yanarudishwa, watu kujenga mashule mapya "ruksa", watu kusomesha watoto zao nje "ruksa", sasa wangoje nini? na Nyerere aliwacha shule nyang'anyag'a hazitamaniki, hata zilizokuwa za mkoloni nzuri na za kupendeza yeye akaziuwa hakuna yenye afadhali, na watu wameshafunguliwa kwa "ruksa" na Al Haj Ali Hassan Mwinyi, wafanye nini> wenye uwezo wakapeleka watoto zao, Ulaya, wengine India, wengine Malaysia, wengine Kenya, wengine USA, wengine Canada, wengine Uganda, almuradi kila mmoja yuko huru, na hao unaowaona wewe walalahoi, huo ndiyo urithi wa Nyerere, alifanya nini miaka zaidi ya 20 aliyotawala kawawacha watu hohehahe.

Hebu sema kweli kuhusu hili, ATC Kikwete kaikuta hoi bin taabani, TRC kaikuta hoi bina taabani tunaona yeye ndiye anaejitahidi kuzifufuwa sasa hivi, hao walioziacha hoi wakina nani, jiulize? si ndio haohao kina Warioba? haohao waliyoiuwa hii nchi, haohao ndiyo waliyoziuwa hizo. Leo wakati wa Kikwete tunaona Mataka anapandishwa kizimbani, wako wapi wa kabla ya Mataka? ni nani aliyeonesha hata kukemea? kwa hili huna na bado utayaona mengi ya haya madudu yanafichuliwa na Kikwete, kuanzia kina mramba, yona, mahalu na sasa kina mataka na bado anaendelea hajamaliza. Tartiibu, lakini "action speaks louder than words".

Umeshajiuliza kwanini hali ikafikia hivyo? au waalimu wanaota juu ya miti? hao wa kabla ya Kikwete walifanya nini kuhusu hilo? hawakufanya kitu ndiyi maana unauona huo uozo, leo tunana Kikwete anajenga vyuo vya walimu kila Mkoa na kwa muda huu mfupi tu wa Kikwete anatowa Waalimu zaidi ya 20,000 ya aliyetowa yeyote wa kabla yake kwa mwaka, haya ni mafanikio makubwa sana, Jee walikuwa wapi wa kabla yake?

Hao unaosema wewe wachache tuambie kabla ya Kikwete walikuwa wengi zaidi au walikuwa wachache zaidi? nnakuhakikishia wakati huu mfupi wa Kikwete anatowa wanafunzi wengi wa chuo Kikuu kuliko wakati mwengine wowote ule, na bado vyuo vinajengwa, hebu kuwa mkweli japo kidogo. Kuhusu ajira na fursa za kujiwezesha zilizopo leo Tanzania huna haja hata ya kusema, tunaona watu wa nchi mbali mali wakizikimbilia hizo fursa, sasa mtu unataka uwezeshwe vipi zaidi ya hivyo, mpaka wageni wanaziona fursa ziliopo, hao waliopo humu ndani hawazioni? Au unataka mtu akae na mfuko wa fedha anawajaza mifukoni ndiyo ujuwe kuna fursa? hilo sahau, hakuna nchi duniani inafanya hivyo, jitume na jitume kwa kasi zaidi. nguvu zaidi na ari zaidi.

Hizo kauli zako tu hapo juu zinaonesha ni chuki binafsi, alikufanyia usanii upi? Kikwete ni kiongozi tena mzuri sana na kila utapogusa katika uongozi wake utakuta kafanya zaidi ya yoyote wa kabla yake. kwa kuwa huna la kuonesha kuwa hajafanya vyema ndiyo kwa chuki zako tu binafsi unaanza kumuita majina asiyokuwa nayo, mimi nataka unioneshe kimoja tu, ambacho hajakifanya vyema zaidi ya Rais yeyote usinletee hadithi fulani kasema fulani kasema vile.

Leta hoja hapa usilete chuki zako binafsi, Nnakuhakikishia huna.
ka
One man's meat is another man's poison. Mtu akiwa anafikiria kama wewe FF yote unayosema yanaweza kuwa ni mafanikio lakini ambayo yako yako too utopian. Wingi wa shule sio ubora wa shule. Sitaki kuweka exaggeration lakini ubora wa shule zetu ni questionable beyond doubt na tafiti zinaoneysha hili ila kama kawaida ya walio wengi mnakataa tafiti mnataka kujenga hoja zisizokuwa na mashiko. Na lazima tusume ukweli swala la shule za sekondari japo kwa majina lakini ki ukweli hazina hadhi ya sekondari ni mchakato toka serikali ya awamu ya tatu. Na FF ukikataa kuwa kuna strategies ambazo zinakuwepo na Rais ajaye anatakiwa kuziendeleza basi useme nchi yetu inaongozwa kiajabuajabu kawa kwavumba haina strategies endelevu. Hivyo tunatakiwa labda kusifia kuendeleza IMF funded education strategy though very fragile maana ingekuwa ni sera yetu na sio shinikizo afadhali tungejenga vyuo vya ufundi kila Wilaya ili wahitimu wapate kujitegema. Tuwe wakweli wahtimu wa shule za kata ni bomu litakalolipuka na wote tutalipa gharama. Wenye uwezo wanapeleka watoto wao nje.

Vyuo vikuu kusema ni mafanikio ya Kikwete mimi naona hapa you aren trying to argue on limited circles. Kwanza haikuwa agenda ya CCM wala JK kuongeza idadi ya vyuo. Na vyuo vikuu sio kitu cha siku moja ni mpango wa muda mrefu unaofanywa na tasisi za elimu za ndani na nje kuona kama kinachotaka kufanywa chuo kikuu kina vigezo. ARHI University imekuwa na mchakato wa muda mrefu wa kutaka kuwa chuo kikuu mpaka ilipotimiza vigezo mwisho ikawa chuo kinachojitegemea. Chuo chenye ni matuda ya Nyerere toka majengo mapka academic disciplines. Sasa Kikiwte anakujaje hapa. St.Augustine ni juhudi za Kanisa kama ilivyokuwa Tumaini University na St.John's na Muslim University ni juhudi za Waislamu. Vingine tunavihesabu lakini hakuna contribution ya JK hapa ni matunda ya process kuanzia kwenye academic cdiscipline, content na mengineyo lakini kama tunaangalia kuwa vimeruhisiwa kuwa vyuo vikuu kipindi cha utawala wake na kukataa kuwapa sifa wale waliozaa watoto, kuwalea mpaka wakakakua na kuwaka falsafa halafu tukasifia wengine.

Kuhusu miundo mbinu ya barabara ni ya kitwakwimu kuliko ukweli na ubora na zaidi ukisema TZ sasa ina miradi kmingi kuliko nchi yoyote ni kichekesho. Kila nchi ina viapaumbele vyake.Sasa kama nchi ina miundo mbinu tayari ya barabara kwanini iwe na miradi kulingana na Tanzania? Nchi baadaya ya barabara inafanya kingine kutegenmea na mipango endelevu. Hili la barabara na miradi mingi limekaa kiumbea na sio scientific msana hatupimi maendeleo kwa wingi wa miradi wakati tayari wengine walishamaliza hilo. Unakejeli serikali zilizopita wakati ziliendeleza reli kujenga mpya na nchi zote duniani zimeedelea kwa kutumia reli.Mimi ningesikia tuna mradi wa kujenga reli au kuboresha zilizopo ningefurahi maana tumezungukwa na land rocked countries amabzo zingetumia bandari zetu na reli zetu kuwafikishia bidhaa zao kwao.

Mbona hamsemi airports na airport terminals ambazo ziko kwenye pathetic conditions. Tuwape watu credit Nyerere na Mwinyi waliziacha pazuri lakini Mkapa na Kikwete wameziacha zikiwa ICU. Kamwacha Mataka akaiharibu ATC leo i=unakuja usanii wa kumshtaki.Very disgusting.Prevention always is better than cure.

Halafu kama unataka kumpa JK sifabasi panua wigo wako mlinganishe na marais wengine ndani ya miaka sita wamefanya nini na hasa nchi zilituzunguka hasa kwenye uchumi utaona tulivyoacchwa nyuma kama koti
 
Ndiyo maana Rais Mkapa amewahi kusema kuwa Watanzania ni wavivu wa kufikiri.
Mimi nataka tuwe wakweli miradi ya barabara ilianzwa enzi za Mkapa anachofanya Kikwete ni kukamilisha kazi ambazo Mkapa alizianza
Ujenzi wa shule na Zahanati pia zilianza wakati wa Mkapa, yeye amemalizia.
Kwa ujumla kwangu kitu pekee alichofanya Kikwete ni kuanzisha UDOM na labda kumleta Maximo kuwa kocha wa Taifa stars.
Labda ukiniambia amefanikiwa kukuinza mfumko wa bei kutoka 4.5 alizoacha Mkapa hadi kufikia 25 za sasa hapo nakubaliana na wewe.
 
Dr. Slaa!
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani
Kuzidisha Barabara
Kuzidisha Shule
Kuzidisha afya
Kuzidisha Uchumi
Kuzidisha Demokrasia
Kuzidisha Maji
Kuzidisha Kazi
Kuzidisha Viwanda
Utalii
Kupigana na Rushwa
Kwa haraka haraka hayo hapo juu kafanya kuliko Rais yoyote wa kabla yake!
 
Acha niseme ukweli ulio wazi mimi siyo mfuasi na sijawahi na sitakuja kuwa mfuasi wa mh.JAKAYA ila napenda kuzungumza ukweli ulio wazi ya kwamba pamoja na udhaifu wake woote huyu jamaa amesemwa sana ameandikwa sana ya ukweli na yenye uwongo ndani yake amekuwa m2 mwenyewe uvumilivu mkubwa kuhusu habari nyingi hususani kwenye mitandao ya kijamii,magazeti na stori za kawaida mitaani na sehemu za kazi.Binafsi ningekuwa mimi nisingeweza nadhani hata kamanda wa mafisadi aka mh. 6 asingeweza rejea alipowaambia wabunge msiwe wepesi wa kulalamika mnabidi muwe na ngozi ngumu kama ya KENGE lakini mwenyewe baadae alikuja kulalamika kama vyombo vya habari vinamwandama
 
Nyanya mbichi,

Nakuunga mkono. Nawiwa kupendekeza JF iwe ya kwanza kumtunuku nishani ya Uvumilivu Kwa vyombo vya habari ila nina hakika nitatukanwa hadi matusi ya sirini. Lakini ukweli unaki kuwa ukweli kuwa JK is exceptional kwenye issues za uvumilivu. Labda kwa sababu ni mtoto wa Pwani na huko wamezoea matusi tena ya nguoni kama utani?! Anatukanwa Twitter, anatusiwa Facebook, anachorwa katuni Afrika Mashariki nzima, anavuliwa nguo JF, watu wanamfotoshop bila mipaka wala ukomo kimaadili lakini JK wapi hana time na mtu....


Watakao bisha sasa, watakuwa wa kwanza kusema "Bora JK" hata kabla ya June, 2016. Tuombe Mungu atupe uzima na azilinde server za JF ili zije kuwa mashahidi.
 
Hakuna rais aliyekuwa akiandikwa na kuchorwa vibaya katika media za tanzania kama Ally Hassan Mwinyi. Kumbuka enzi zake za urais namna magazeti kama Motomoto, Tazama, Heko, Family Mirror na mengineyo jinsi yalivyokuwa yakiandika ovyo na kumsema hovyo huyo mzee na jinsi alivyovumilia yote. Huyu JK hajaandikwa hovyo hata kidogo na wala sioni why unamsifia kwa uvumilivu. UPI????
 
sure Jk balaa.
jamaa akitoka tutajibeba....ila kwenye uchumi jamaa kachemka mbayaaaaaaaa
 
Hakuna rais aliyekuwa akiandikwa na kuchorwa vibaya katika media za tanzania kama Ally Hassan Mwinyi. Kumbuka enzi zake za urais namna magazeti kama Motomoto, Tazama, Heko, Family Mirror na mengineyo jinsi yalivyokuwa yakiandika ovyo na kumsema hovyo huyo mzee na jinsi alivyovumilia yote. Huyu JK hajaandikwa hovyo hata kidogo na wala sioni why unamsifia kwa uvumilivu. UPI????

Have you also considered the evolution of electronic media? Was there Facebook, Twitter, JF, Wanabidii, etc to make the situation similar?
 
sure Jk balaa.
jamaa akitoka tutajibeba....ila kwenye uchumi jamaa kachemka mbayaaaaaaaa

Hivi ndivyo Great Thinker anapaswa kuamua mambo. Penye sifa mpe mtu sifa yake. Na alipoboronga vilevile kandia
 
Back
Top Bottom