Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,053
Kwa Mod:
Si sahihi hata kidogo kuiunganisha thread ya "Uvumilivu wa JAKAYA ni noooooma" kuwa moja na ya "JK Rais Bora kuliko wote Tanzania" na kisha kukiacha kichwa cha habari cha pili hai.
Binafsi, nimekubaliana na kichwa cha habari na hoja iliyojengwa chini ya "Uvumilivu wa JAKAYA ni noooooma". Kitendo chako cha kuziunganisha hizi topiki mbili kuwa mmoja na kuacha kichwa kimoja hai ni sawa na kuniweka/kutuweka (sisi tuliokubaliana na hoja ya kichwa cha habari ulicho-ua) kwenye mabano, ukatuzidisha na sifuri!
Sikubali J.K kuwa Rais bora, nakubali J.K ni Rais mvumilivu kwa vyombo vya habari. Japo vyote ni sifa lakini sifa ninayompa ni ndogo katka seti kubwa ya ubovu na udhaifu wake unaomfanuya asiwe Rais bora kuliko wote.
Si sahihi hata kidogo kuiunganisha thread ya "Uvumilivu wa JAKAYA ni noooooma" kuwa moja na ya "JK Rais Bora kuliko wote Tanzania" na kisha kukiacha kichwa cha habari cha pili hai.
Binafsi, nimekubaliana na kichwa cha habari na hoja iliyojengwa chini ya "Uvumilivu wa JAKAYA ni noooooma". Kitendo chako cha kuziunganisha hizi topiki mbili kuwa mmoja na kuacha kichwa kimoja hai ni sawa na kuniweka/kutuweka (sisi tuliokubaliana na hoja ya kichwa cha habari ulicho-ua) kwenye mabano, ukatuzidisha na sifuri!
Sikubali J.K kuwa Rais bora, nakubali J.K ni Rais mvumilivu kwa vyombo vya habari. Japo vyote ni sifa lakini sifa ninayompa ni ndogo katka seti kubwa ya ubovu na udhaifu wake unaomfanuya asiwe Rais bora kuliko wote.
Nyanya mbichi,
Nakuunga mkono. Nawiwa kupendekeza JF iwe ya kwanza kumtunuku nishani ya Uvumilivu Kwa vyombo vya habari ila nina hakika nitatukanwa hadi matusi ya sirini. Lakini ukweli unaki kuwa ukweli kuwa JK is exceptional kwenye issues za uvumilivu. Labda kwa sababu ni mtoto wa Pwani na huko wamezoea matusi tena ya nguoni kama utani?! Anatukanwa Twitter, anatusiwa Facebook, anachorwa katuni Afrika Mashariki nzima, anavuliwa nguo JF, watu wanamfotoshop bila mipaka wala ukomo kimaadili lakini JK wapi hana time na mtu....
Watakao bisha sasa, watakuwa wa kwanza kusema "Bora JK" hata kabla ya June, 2016. Tuombe Mungu atupe uzima na azilinde server za JF ili zije kuwa mashahidi.
Hivi ndivyo Great Thinker anapaswa kuamua mambo. Penye sifa mpe mtu sifa yake. Na alipoboronga vilevile kandia
