Jinsi ya kulala usingizi mtamu kila siku

fazili

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
13,819
18,555
Usingizi mrefu na usio katikakatika ni muhimu sana kwa afya ya mwili, akili na roho. Mtu mzima anapaswa kulala si chini ya saa 8 kwa siku. Zingatia yafuatayo ulale usingizi mrefu na mtamu.

1. Oga kabla ya kulala

2. Kula chakula chepesi na kidogo walau saa moja kabla ya kulala.

3. Usinywe maji chini ya saa moja kabla ya kulala.

4. Tumikisha mwili au akili vizuri mchana ili ulale vizuri usiku.

5. Hakikisha chumba, matandiko na nguo za kulala ni safi, hakuna chawa, kunguni, etc.

6. Nguo za kulala ziwe nyepesi na laini.

7. Kitanda kiwe kikubwa na godoro liwe nene.

8. Egemeza shingo vizuri kwenye mto laini usio mkubwa wala mdogo sana.

9. Hakikisha chumba kina mzunguko mzuri wa hewa.

10. Hakikisha chumba kina giza totoro. Zima taa zote chumbani.

11. Zima simu au alarm zote kwenye simu.

12. Hakikisha hakuna kelele zozote ndani na nje ya chumba, zima redio, tv, etc

13. Lala kati ya saa 2 na saa 4 usiku.

14. Usilale kifudifudi.

15. Tumia chandarua kama kuna mbu

16. Usitumie caffeine kabla ya kulala hii ipo kwenye kahawa, chai, cocoa na vinywaji vyenye cola eg Coca Cola, pepsi cola, etc

17. Acha kujamiiana katikati ya usiku

18. Usilale na mtu anayekoroma. Malkia Elizabeth alilala chumba tofauti na mumewe Prince Andrew ili apate usingizi mzuri.

19. Usilale mchana

20. Usiendekeze mawazo hasi unapokwenda kulala

21. Sali kabla ya kulala. Omba Mungu ulinzi na usingizi mwema wakati wa usiku

NB: Jijengee mazoea ya kulala mapema utafurahia maisha zaidi na utakuwa na nguvu nyingi kimwili, kiakili na kiroho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom