Jinsi siasa za 2015-2020 ziliniwezesha kumjua Mungu, Biblia, Qu'ran, Askofu Ngonyani na Othman Mazinge

Rasterman

JF-Expert Member
Feb 24, 2015
33,905
44,020
Hakuna ubishi kwamba sisi wapenzi wa siasa za Amani, umoja, haki na maendeleo ya watu siasa za Tanzania ktk kipindi kilichotajwa hapo juu zilitutia unyonge sana.

Zilitutia unyonge kwa sababu hatukua na mtetezi yeyote wa kututia moyo. Tumaini pekee lilibaki kwa Mungu.

Matajiri na maskini wote hali zao zilikuwa mbaya kila mtu kwa nafasi yake ilifika kipindi hata wazawa wa ndani ya chama pendwa chama tawala na wao walionja joto la jiwe.

Tuyaache hayo. Nini kilifata sasa baada ya hali ngumu?

Basi bwana ikawa tunajifariji tu kwa nyimbo za injili na maneno matukufu ya watumishi wa Mungu. Kama ni kipindi tumeomba na kusali sana basi ni kipindi hiki.

Nitataja watumishi wa Mungu wasio na Mawaaa ambao mimi binafsi kupitia wao nilifarijika na kuimarika kiroho na baadae kimwili.

1. Askofu Aurelian Ngonyani huyu ni askofu wa Kanisa la Truth Bible Fellowship.

Ni mtumishi ambaye kwa kiasi kikubwa anajikita kueleza na kufafanua siasa za Nchi ya Israel na tawala zake, changamoto na mafanikio. Huyu mtumishi alinifurahisha kwa vile anavyodadavua Nchi ya Israel kwa mikoa, majimbo hadi mitaa. Amefanya ziara na tour nyingi nchini humo na kuiva ktk historia yake.
Unaweza kumpata Ktk Youtube channel yake kwa jina hilo hilo.

2. Mwinjilist Godfrey Machota.
Huyu ni kijana mdogo Graduate wa Civil engineering 2016.

Kaka huyu amejikita katika masomo ya unabii na ufunuo.

Huzungumzia kwa kina kuhusu siasa, tawala na falme za dunia zilizopita za kuthibitisha Ufalme wa Mungu wa nyakati zijazo.

Ukimsikiliza kwa makini utafarijika sana hata kwa magumu ambayo Watanzania wanyonge wanapitia kutokana na uongozi mbovu.

Naye anapatikana Youtube channel kwa jina hilo hilo.


3. Maalim Othman Suleiman Mazinge.

Heshima kwako Ustadhi na Amir. Huyu mwamba ni mfano bora kabisa ktk utumishi wa kueneza Daawah kwa waja na ummat Muhammad.

Kupitia yeye nimefarijika sana kipindi ambacho uchumi ulikuwa mgumu lakini watz wakapigwa stop wasilalamike eti vyuma vimekaza.

Anatumia Mfano wa Mwanadamu aliye Mbora ktk wote Mtume Muhammad (s.a.w). Pia ana uzoefu na siasa za Tz na maisha yake ingawa yeye si mwanasiasa kabisa.

4. Dr Sule. Huyu anaonekana sana kwenye Daawah Tv Mtoro. Ni mwalimu mzuri ktk kutoa Elimu ya Dini, siasa na maisha ya watumishi wa Mungu wa kale.

5. Paul Semba

Jamaa huyu akiwa ktk Mkoa wa Arusha( kama sikosei) Njiro Hill huko anafundisha kwa kina masomo ya Utawala hasa ajirejea falme za Kale za Babeli, Uyunani, Umedi na Uajemi na Dola ya Rumi.
 
Walokole wengi hua wamegubikwa na mauza uza katika fikra zao (Hallucinating/tions)
Ndio maana jambo dogo tu wao hulifanya lionekane limekaa kimiujiza
Very stupid
 
Hakuba ubishi kwamba sisi wapenzi wa siasa za Amani, umoja, haki na maendeleo ya watu siasa za Tanzania ktk kipindi kilichotajwa hapo juu zilitutia unyonge sana.

Umasikini wa akili
Mungu hana siasa; kama unadhani ulivyokuwa unajisikia kuumia kwa kuzuiwa kufanya unachokitaka ndio kibali kwa Mungu umepotea. Ukiwa kwenye serikali unachokitekeleza hakiakisi Mungu anavyokuchulia; hawezi kukuadhibu kisa ulikuwa unatumia sheria kuwaadabisha watu waovu kisa ubinadamu badala ya kuponya wengi.

Je, kwa sasa unafanya siasa gani zinazokufanya ujihisi huru, furaha na mafanikio?

Kuna ushindani gani wa kisiasa kwa sasa au ni chuki zako kwa utawala wa kiboko cha waharifu ukiwemo wewe?
 
Walokole wengi hua wamegubikwa na mauza uza katika fikra zao (Hallucinating/tions)
Ndio maana jambo dogo tu wao hulifanya lionekane limekaa kimiujiza
Very stupid
Wapo walokole kama hao ofcourse. Lakini wapo watumishi wa Mungu wametumwa kuwafariji wenzao. Hiyo ni kanuni ya Mungu
 
Umasikini wa akili
Mungu hana siasa; kama unadhani ulivyokuwa unajisikia kuumia kwa kuzuiwa kufanya unachokitaka ndio kibali kwa Mungu umepotea. Ukiwa kwenye serikali unachokitekeleza hakiakisi Mungu anavyokuchulia; hawezi kukuadhibu kisa ulikuwa unatumia sheria kuwaadabisha watu waovu kisa ubinadamu badala ya kuponya wengi.

Je, kwa sasa unafanya siasa gani zinazokufanya ujihisi huru, furaha na mafanikio?

Kuna ushindani gani wa kisiasa kwa sasa au ni chuki zako kwa utawala wa kiboko cha waharifu ukiwemo wewe?
Siasa ni neno la kiswahili tu lakini linagonga mifumo yoote ya maisha ya binadamu. Na itabaki kuwa hivyo.
 
Hakuna siasa yoyote itakayokufanya uponye roho hata ukitenda wema wa kiwango gani Mungu hapendelei.
Siasa ni za wanadamu na wanadamu ni wa Mungu.

We Inteligence Justice mbona unakuwa mbishi.
Mi najua unaelewa mantiki ya thread hii lakini unazunguka zunguka tu.

Heshima yako kwenye jukwaa hili ilinde basi mkuu
 
Siasa ni za wanadamu na wanadamu ni wa Mungu.

We Inteligence Justice mbona unakuwa mbishi.
Mi najua unaelewa mantiki ya thread hii lakini unazunguka zunguka tu.

Heshima yako kwenye jukwaa hili ilinde basi mkuu
'Criminal mind'
Methods to control the slave's mindset
1. Whip him/her
2. Cause him or her to tout a bird song all the time in order to make the master take pride in your loyalty

Slave Codes
1. The slave owes his master and all his family total respect and absolute obedience. He must instantly obey all orders he receives from them. You are to be obedient to your master in all things. You are not to be eye—servants. You are to serve your masters with cheerfulness, reverence, and humility irrespective of the challenges you may face
2. No slave can own anything of his own without the consent of his master. No slave can sell anything he has made without his master’s consent.
3. No slave can be a witness in any case against a master.
4. Slaves shall always be considered real estate and may be a mortgage for the master's affluence.
 
Back
Top Bottom