Da! Nilikutana na hii kitu mwaka 2013.hawa jamaa wananusa Sana hela.
Jamaa alikua Anatokea stendi kashika Bahasha akanisimamisha,baada ya salamu, "samahani unaifahamu hoteli(akaitaja) nikamjibu ndio, akaniambia yeye ni Mgeni anaenda kukutana na mtu hapo ampe mzigo(akafungua kidogo ile bahasha) mamaaaaaaaaaaaa vitu vinang'aa hatari. Akasema hizi ni dhahabu natakiwa kwenda kumkabidhi anipe hela,naomba unipeleke.KICHWANI ZIKAWA ZISHACHAJI MDA MREFU NIKAWA NA MCHORA TU! Nikamwambia,me nna kazi zangu saizi ntakuelekeza hutapotea.
Akatokea jamaa mwingine akawa kama anatupita hivi(mwenzake) akamsimamisha,akamuuliza kama ana ijua hiyo hotel, akasema haifahamu, jamaa akasema huyu anapafahamu ila anasema hana muda,akamwambia kama alivoniambia Mimi na akamwonesha madini hewa. Jamaa akatuahidi hela nzuri tukimpeleka. Basi jamaa akaanza kunishawishi balaa.. Kimoyo moyo nikawa nawacheka tu.nikawambia sasa hizo hela utatoa kweli, jamaa akasema ndio, nikawambia sasa nisubirini kidogo(dakika sifuri) niweke huu mzigo (nilikua nimeshika spea ya gari naelekea garage.
Wakanambia poa, SIJUI KAMA BADO WANANISUBIRI MPAKA LEO, mfukoni nilikua na hela moja hivi! Wale jamaa sio watu wazuri,ukiingia Tamaa tu umelia
POLE MKUU KWA USUMBUFU WALIOKUSABABISHIA NA HONGERA KWA KUWATAMBUA