Jinsi nilivyonusurika kutapeliwa!

Jinsi nilivyonusurika kutapeliwa!

hv kweli mtu na akili zako timamu unamuamini vp mtu anaekwambia atakupa milion kwa kumsindikiza tuu??

wajinga ndo wanaoliwa siku zote
Well done mkuu, ukiyafikiria hayo pia fikiria kuna nguvu ya tamaa..
 
Sasa maelezo mbona yanakinzana na uhalisia.Yaani aogope kwenda Posta wakati kuja hapo mlipokutana hajaogopa?
Kwa akili za kawaida huoni kwamba hii ni stori ya kutunga tu?
Usilolijua ni kiza kinene mkuu.
 
MIMI MPK SASA NAJIULZA, MATAPELI WATAKUJA NA MBNU GAN HAD WAFANIKIWE KUNIIBIA? NAONA HAIPO TU.. LABDA WATUMIE BASTOLA NA HUO CYO UTAPELI NI UJAMBAZ.

WENG WANAOTAPELIWA NI WAPENDA DEZO NA TAMAA... MIMI NIKIWA BENK KWANZA NAKUWA BUSY, HALAFU MTU AKINIULZA MASWALI NAMJBU 'NENDA KWA WAHUSIKA'
Sawa mkuu, Share experiences unajikinga vip?
 
Mie 2015 nilikutana nao posta nimetoka zangu kuchukua dollar zangu kidogo nipo mwendo nawahi kidogo eti dada nina madini kuna mtu kanielekeza huku nimechanganya halafu ni mwanamke tena jimama bila hata aibu nikamgomea akaja mbaba hapo nikaachana nao ile napiga hatua ile kugeuka hata mmoja sikumuona kilichoniokoa nilikuwa nawahi ibada hawa watu jamani
Pole sana mamy
 
hv kweli mtu na akili zako timamu unamuamini vp mtu anaekwambia atakupa milion kwa kumsindikiza tuu??

wajinga ndo wanaoliwa siku zote
Wanakuhadaa kwanza kabla ya yote bila shaka huwa na nguvu ya ziada jamani
 
Wakuu habari

Jana wakati nikiwa benki(jina kapuni) nilifanya taratibu zote, kuandikia form ya kuwekea pesa nikapanga mstari tayari kwa huduma... gafla akaja kaka mmoja hivi na kuniita falagha

" samahani naomba unisaidie kuandika hapa" yule kaka aliongea huku akiwa ameshika payinslip(fomu ya kuweka pesa) huku akitoa bahasha yenye USdollar alidai kuwa kapewa na wachina kwenye sheli flan( jina kapuni) thamani ya USD15000

Sijaanza kumwelekeza mara dada mmoja alikuwa karibu yetu akaingilia" hizo dollar hazi badilishwi hapa, labda benki ya postal"

Basi sababu mi niliitwa nitoe msaada niliamini kuwa jamaa kashapata msaada aende zake benki tajwa..

Ile nataka kuondoka nirudi kwenye line yule kaka mwenye dollars akasema " Naogopa kwenda peke yangu kama vip nisindikizen kisha pesa zitazotoka nitawapa milioni moja moja" mmh! Kusikia hivyo nikahairisha kwenda kwenye line.... nazidi kuingia kwenye mtego

"Nna haraka sana kama inawezekana iwe saivi" aliongea huku akitoka nje ya benki haraka haraka, tukabaki mi na yule dada " twende au tuache pesa ziende tu mm! Nikamwambia twende ila tuwahi maana nna pesa za watu hapa.....

NJIANI
...yule dada akawa anapiga simu " hallow eeeh hivi rate ya kubadili dollar ni shingapi?..... kama dollar 15000 hivi?...... duh haya haya tunakuja saivi(call ended)

Akanivuta pembeni kidogo na kwa sauti ya chini kusudi yule kaka asisikie ( dogo amesema rate siku ya leo ni kubwa hivyo ni milioni 32,000,000)

Kufika sehem jamaa akagoma kwenda eti anaogopa, twende sisi tukamchekie kwa yule mtu aliokuwa akiwasiliana na yule dada akatoa note moja ya dollar50, nakusema chukieni hii mkanichekie....

Tukakubaliana sawa tukaenda tukiwa mimi na yule dada ambaye hata simfaham wala sijawahi muona mayala!

Tulivyorudi
"Dollar iko sawa" yule dada aliongea, na sijui kwanini kila jambo yule dada alianza kuongea yeye( nahisi yule dada na yule kaka lao moja)

"Sasa mimi ngoja niwape mkanibadilishie mimi naogopa kutembea tembea" yule kaka aliongea na nilishindwa kuelewa anamaanisha nini

"Mimi siwaamini naombeni hela zenu mlizonazo na mimi niwape hizi dollar mkisha badili basi nitawapa hela zenu" yule kaka aliongeza .... hapo nilipata wasi wasi sana kwanini tumwachie pesa zetu.

Binasfi nilikuwa nna milion 1 ambayo ilitakiwa nii-deposit ambayo kwa mda huo niliiweka mfukoni, yule dada alikuwa amebeba begi na alisema ana milioni 5.

Kilicho nichanganya ni kumwachia pesa yule kaka kisha sisi twende kubadili pesa..

to be honest
Pesa sikutoa niligoma kata kata, yule dada alikuwa mstari wa mbele kunibembeleza nitoe pesa nilikataa na kuondoka kasiii....

PENDEKEZO
tufanye kazi, tuachee tamaa matapeli wangenizidi akili wangenitapeli...

Nawasilisha...
Wako hivyo.

Mlimani City siku moja nakunywa Kahawa mule ndani opposite bank ya Exim zamani. Akatokea mama mweupe akanisalimia. Akaketi akidai aelekezwe ofisi ya Buzwagi kule Masaki akauze dhahabu. Nikamwelekeza kwani nilipafahamu.

Ghafla kijana mmoja meza ya pili akadakia. "Mbona huko mbali! Hapo TRA, karibu na Kanisa la ....... , Mwenge yupo mchungaji ananunua dhahabu."

Nikamwambia, "basi mpeleke mama!" Akasema, " nipo kazini, mimi ni dereva wa benki ya ........" Akaniomba, "We mpeleke sio mbali."

Akapiga simu kwa yule Mchungaji mnunuzi kwamba tunakwenda atupokee. Tukaondoka na yule mama ndani ya gari yangu hao mpaka karibu ya lile Kanisa. Tukafika tukapaki mita 20 hivi toka getini.

Baada ya muda akatokea mtu amevaa suti ya Kaunda na msalaba. Akafika na kunisalimia kikristo. Nikamjibu. Akapanda ndani ya gari. Mama akatoa kimkebe kimejaa mawe yaliyofanana na dhahabu.

Yule "mchungaji" akatoa kifaa mfukoni kama bisibisi akaipima ile "dhahabu." Akasema hasa hii ni "dhahabu" nitanunua. Mimi nami niliamini kuwa ni dhahabu kweli.

Akamgeukia mama akamwuliza, "Unayo akaunti benki?" Mama akajibu, "sina!" Yule "Mchungaji" akanigeukia, "wewe ndugu msaidie mama huyu. Unayo akaunti benki?" Nikasema, "ndiyo ninayo." Akaniagiza, "tupatie namba basi!" Ndipo nikapata mashaka.

Nikamwambia yule mama,

"Mama unafanya biashara hii huna akaunti benki? Siku zote unategemea akaunti za watu wengine? Iweje mniombe nikulete hapa kisha nigeuke kuwa wakala wa malipo. Benki wakiona kuna sh milioni 50,000,000 zimeingia ghafla Je, hawatashangaa zimetoka wapi. Unafanya mauzo ya aina hii hata gari huna kweli?"

Nikawashusha kutoka kwenye gari nikaondoka nimenusurika kuibiwa kwa njia waliokuwa wakiijua wao.

Mama alidai alikuwa anawakilisha umoja wa kina mama wachimbaji toka wilaya mpya moja kule Tanga. Utapeli mtupu.

Nimeandika kukazia hii mbinu ameitaja mleta mada - kuwepo kwa mtu wa pili- ambaye hujitokeza wakati muafaka kuchochea njama za kitapeli. Yule dereva katika tukio langu ndiye aliyekuwa mtu wa pili. Ukiona mtu wa pili anajitokeza ujue basi huo ni wizi.
 
Wako hivyo.

Mlimani City siku moja nakunywa Kahawa mule ndani opposite bank ya Exim zamani. Akatokea mama mweupe akanisalimia. Akaketi akidai aelekezwe ofisi ya Buzwagi kule Masaki akauze dhahabu. Nikamwelekeza kwani nilipafahamu.

Ghafla kijana mmoja meza ya pili akadakia. "Mbona huko mbali! Hapo TRA, karibu na Kanisa la ....... , Mwenge yupo mchungaji ananunua dhahabu."

Nikamwambia, "basi mpeleke mama!" Akasema, " nipo kazini, mimi ni dereva wa benki ya ........" Akaniomba, "We mpeleke sio mbali."

Akapiga simu kwa yule Mchungaji mnunuzi kwamba tunakwenda atupokee. Tukaondoka na yule mama ndani ya gari yangu hao mpaka karibu ya lile Kanisa. Tukafika tukapaki mita 20 hivi toka getini.

Baada ya muda akatokea mtu amevaa suti ya Kaunda na msalaba. Akafika na kunisalimia kikristo. Nikamjibu. Akapanda ndani ya gari. Mama akatoa kimkebe kimejaa mawe yaliyofanana na dhahabu.

Yule "mchungaji" akatoa kifaa mfukoni kama bisibisi akaipima ile "dhahabu." Akasema hasa hii ni "dhahabu" nitanunua. Mimi nami niliamini kuwa ni dhahabu kweli.

Akamgeukia mama akamwuliza, "Unayo akaunti benki?" Mama akajibu, "sina!" Yule "Mchungaji" akanigeukia, "wewe ndugu msaidie mama huyu. Unayo akaunti benki?" Nikasema, "ndiyo ninayo." Akaniagiza, "tupatie namba basi!" Ndipo nikapata mashaka.

Nikamwambia yule mama,

"Mama unafanya biashara hii huna akaunti benki? Siku zote unategemea akaunti za watu wengine? Iweje mniombe nikulete hapa kisha nigeuke kuwa wakala wa malipo. Benki wakiona kuna sh milioni 50,000,000 zimeingia ghafla Je, hawatashangaa zimetoka wapi. Unafanya mauzo ya aina hii hata gari huna kweli?"

Nikawashusha kutoka kwenye gari nikaondoka nimenusurika kuibiwa kwa njia waliokuwa wakiijua wao.

Mama alidai alikuwa anawakilisha umoja wa kina mama wachimbaji toka wilaya mpya moja kule Tanga. Utapeli mtupu.

Nimeandika kukazia hii mbinu ameitaja mleta mada - kuwepo kwa mtu wa pili- ambaye hujitokeza wakati muafaka kuchochea njama za kitapeli. Yule dereva katika tukio langu ndiye aliyekuwa mtu wa pili. Ukiona mtu wa pili anajitokeza ujue basi huo ni wizi.
Mbinu zao ni kama zina mfanano hivi

Unakuta wamejipanga zaidi ya mmoja kufanikisha utapeli

Duuh pole sana kaka
 
Hakika mkuu nimejifunza,

Kaka next time husisaidie mtu yoyotee yule ...awe mmama au mbabu...we fanya mambo yako....matapeli wa namna iyo ni wengiii sanaa sikuiziii...nashangaa yaani imekuaje kuaje mpaka wamekutoa nje ya bank bila ww kuwagutukiaaa....yna wamejazana sana mjinii kua makini....me sikuiz nishasema bora nionekane nna roho mbaya tu....nikiitwa na mtu yoyote sirespond naendelea na safar yangu....una bahat sana maana kuna wengine ukiongea nao tu wanakua washakuekea madawa
 
Shukrani mkuu,

Unajua hizi mambo unaweza ziona simpo, lkn ni mambo magumu sana, ukizingatia wengine wanatumia mpaka nguvu za giza kufanikisha utapeli!
kweli kabisa mkuu hata mimi nilishawahi tapeliwa kwenye ofisi yangu kwa njia ya hizi za nguvu za giza yaani unajikuta mwenyewe unatoa pesa yaani akili inapotea kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom