DR SANTOS
JF-Expert Member
- Mar 11, 2019
- 10,519
- 21,441
Shalom wapendwa,
Leo nimekumbuka kisa hiki, kilichonitokea mwenyewe nikiwa katika harakati Mkoa wa Njombe. Narudia tena hii sio stori ya kufikirika imenitokea mwenyewe.
Uchawi hauna faida yoyote ni ujinga uliokomaa, ni utumwa. Walio wachawi wanamani kutoka ila there is no way out there. Ninamiliki maduka ya dawa za binadamu yaliyopo maeneo ya vijijini huko, kazi yangu hua ni kuzunguka na kutafuta watu wa kuuza tu na kufunga mahesabu mwisho wa mwezi.
Siku Moja kuna dada wa ADDO aliyekuwa akiuza moja kati ya maduka alipata dharura na kwakua nilikuwa na nafasi nilimruhusu aende nami nikaenda kumpokea kuuza dawa Ili clients wasikose huduma mpaka atakaporejea. Sasa hapo ndipo tatizo lilipoanzia.
Hiyo siku nimeamka vizuri kabisa nikashinda vema jioni imefika nikafunga hesabu na kulikua na pesa kwenye draw nilizibeba na kwenda nazo nyumbani kwa sababu za kiusalama, nikaacha kiasi kadhaa pia kwenye draw. Baada ya kufikia nyumbani nikaweka pesa vizuri nikawasha data niperuzi kidogo Kisha nikalala.
Naamka asubuhi nimelala nje😂😂😂 kwenye shimo Moja lilikua jirani na nyumba. Kitu kilichonishangaza nililala na boksa nikaamka nje nikiwa na nguo zangu nilizovaa jana😨
Kitendo cha kutaka kurudi ndani nakuta mlango umefungwa kwa ndani, nikawa najiuliza nilitokea wapi? Nikajaribu kupush mlango ukafunguka kuingia ndani nakuta panya sita kitandani wametulia wananiangalia tu😂😂😂 nikarusha kiatu wakapanda darini na kupotea ghafla kukawa kimya.
Impact za tukio lile, pesa nilizorudi nazo jana hakukua na hata kumi iliyokuepo😬 (zilipotea)
Sikuweza kukaa tena kule, nikafunga duka mpaka yule dada aliporudi kusongesa gurudumu. Kwa Sasa nikienda huwa silali kabisa hata iwe late kiasi gani nitarudi mjini.
Kama hujapita Njombe hujaona uchawi bado.
Leo nimekumbuka kisa hiki, kilichonitokea mwenyewe nikiwa katika harakati Mkoa wa Njombe. Narudia tena hii sio stori ya kufikirika imenitokea mwenyewe.
Uchawi hauna faida yoyote ni ujinga uliokomaa, ni utumwa. Walio wachawi wanamani kutoka ila there is no way out there. Ninamiliki maduka ya dawa za binadamu yaliyopo maeneo ya vijijini huko, kazi yangu hua ni kuzunguka na kutafuta watu wa kuuza tu na kufunga mahesabu mwisho wa mwezi.
Siku Moja kuna dada wa ADDO aliyekuwa akiuza moja kati ya maduka alipata dharura na kwakua nilikuwa na nafasi nilimruhusu aende nami nikaenda kumpokea kuuza dawa Ili clients wasikose huduma mpaka atakaporejea. Sasa hapo ndipo tatizo lilipoanzia.
Hiyo siku nimeamka vizuri kabisa nikashinda vema jioni imefika nikafunga hesabu na kulikua na pesa kwenye draw nilizibeba na kwenda nazo nyumbani kwa sababu za kiusalama, nikaacha kiasi kadhaa pia kwenye draw. Baada ya kufikia nyumbani nikaweka pesa vizuri nikawasha data niperuzi kidogo Kisha nikalala.
Naamka asubuhi nimelala nje😂😂😂 kwenye shimo Moja lilikua jirani na nyumba. Kitu kilichonishangaza nililala na boksa nikaamka nje nikiwa na nguo zangu nilizovaa jana😨
Kitendo cha kutaka kurudi ndani nakuta mlango umefungwa kwa ndani, nikawa najiuliza nilitokea wapi? Nikajaribu kupush mlango ukafunguka kuingia ndani nakuta panya sita kitandani wametulia wananiangalia tu😂😂😂 nikarusha kiatu wakapanda darini na kupotea ghafla kukawa kimya.
Impact za tukio lile, pesa nilizorudi nazo jana hakukua na hata kumi iliyokuepo😬 (zilipotea)
Sikuweza kukaa tena kule, nikafunga duka mpaka yule dada aliporudi kusongesa gurudumu. Kwa Sasa nikienda huwa silali kabisa hata iwe late kiasi gani nitarudi mjini.
Kama hujapita Njombe hujaona uchawi bado.