Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Ndugu zangu wana Jf habari zenu.
Unajua kwenye haya maisha tunapitia mengi sana hasa katika utafutaji kwa upande wa Wanaume. Tunakutana na mambo mengi sana ya aibu, kukatishwa tamaa, kuachwa na tuwapendao na mauzauza mengi sana. Nakumbuka mzee mmoja alinambia mapambano ya kupata maisha mazuri sio rahisi inatakiwa ujasiri, kujitoa na kuwa na maamuzi magumu sana. Kila aliyefanikiwa ana siri nyingi ambazo sio rahisi kushare na mtu mwingine, sometimes tunakutana humu jf, tuna marafiki zetu wote hapa duniani tuna matatizo lakini matatizo yetu yametofautiana.

Mimi INSIDER nimepitia mambo mengi sana kiasi kwamba nilikata tamaa ya maisha unaweza ukasoma huu uzi wangu “Sitaomba kazi acha niwe jeuri tu”

Sitaomba kazi tena, wacha niwe jeuri tu!!

https://www.jamiiforums.com/index.php?threads/Sitaomba-kazi-tena%2C-wacha-niwe-jeuri-tu%21%21.1619876/ , na story yangu itaanzia hapa, ilikuaje mpaka nikaingia kwenye biashara ya uber??.
Hii ni story ya kweli na siyo ya kutunga, lengo langu nataka ndugu zangu mpate ujumbe kuhusu haya maisha. Kiufupi usikubali kukata tamaa hata kidogo, no matter what you fall, keep fighting, God has plans for all of us. Kwa wale ndugu zangu wa Uber/Bolt ambao mnataka kuingia kwenye hii biashara utaweza kupata mwanga mzuri kuhusu hii biashara maana nina experience ya kutosha. Tusichoshane acha nianze kumwaga asalii……..,,

…….wakati naandika ule uzi wa “ Sitaomba kazi tena wacha niwe jeuri” , nilikua nimerudi mkoani kwa wazazi kuwasalimia. Ofcourse maisha ya mkoani na niko home sikua na wasiwasi kabisa wazungu wanasema “HOME SWEAT HOME””. Chuo mimi nimemaliza moja ya chuo kikubwa hapa Dsm, baada ya kumaliza chuo sikutaka kurudi home kabisa. Maana niliwaza hata nikienda home kule nitafanya nini? Nikakae na mama tu? Niwe nakula na kulala? nikakukumbuka ule msemo unaosema mtoto kwa mama hakui bali analemaa akili.
Niliamua kwenda kwa Uncle wangu kukaa huku nikiendelea kutafuta kazi hapa mjini, alikua anaishi Mikocheni. Kipindi cha weekend nilikua natoka chuo nakwenda Mikocheni nashinda kule kwa Uncle then jumatatu narudi chuo, pale palikua kama home tu.

Nikaanza kusambaza CV kwenye mataasisi, makampuni, NGO’s kwenye mabank na sehem nyingi tu hapa Dsm lakini patupu sikufanikiwa kupata sehemu hata ya kujitolea. Kuna siku nilikuwa nimekaa na Uncle tunaongea akaniuliza umemaliza chuo sasa una mpango gani?. Nikamwambia abc zote kwamba nimepeleka maombi yangu sehemu mbalimbali nasubiri majibu kama nitafanikiwa ama laah. Akanambia kuanzia jumatatu tutaanza kwenda wote kazini, lakini utaweza mikiki ya Kariakoo?, nikamwambia ni bora nishinde huko kuliko kubaki hapa home, I hate that.

Kweli jumatatu ikafika tukaenda huko kwa Wachina, ile siku sikutaka kuuliza ni kazi gani lakini nilikua najua Uncle anafanya kazi kiwanda cha mabag. Tulivyofika pale kiwandani Uncle akanitambulisha kwa Mchina.
UNCLE: Hey Mr ping that is my Uncle, My sister’s son. Call him INSIDER.
MCHINA: Ooh you like alike I thought is your son, akacheka. huyu mchina alikua hajui kiswahili hata ngeli alikua anaibia kwa mbali. Mchina akanambia hey “Rafiki” karibu.

MIMI: Thank you.
Uncle akaniita niingie store akanambia kazi yangu itakua ni kusupply mabag kule Kariakoo. Hii kampuni yeye alikua ni Sales and Operation manager. Kampuni ilikua inatengeneza journey bags na backpack bags na pilot bags. Canter ilikua imefika pale tayari kwa upakizi, so tukaanza kupakia mabag mle kwa gari na kuyapanga kuyapeleka Kariakoo kwa wateja. “Ipo hivi pale kiwandani sio kwamba ndo wanaanza kutengeneza hapana wanafanya assembling tu, material zote zinatoka China, pale ni kuassemble na kuyapeleka sokoni”.
Ile siku nilipiga sana kazi nakumbuka tulipiga trip 2 ila kila tripu ilikua na bag 200, sio poa kupakua bag pale Kariakoo ni mtihani yaani foleni za watu zilikua zinakera sana. Uncle akawa ananilipa cash kwa siku 10,000/=, wakati naanza alikua ananinulia chakula ila baadae akaanza kunikataa so nikawa najilipia, kuhusu kwenda kazini tulikuwa tunaondoka wote kwa gari asubuhi.

Nikaimasta kazi kwa muda mfupi sana ikafika stage akawa ananiacha niende peke yangu na dereva mitaa ya Kariakoo na wateja nikawa nimewajua tayari haikuwa ngumu kwangu. Uncle akanambia upo vizuri ikafika stage hata madeni nikawa nakwenda kukusanya then napeleka bank, yaani unakuta nimekusanya madeni mpaka 80million, hiki ndo kipindi nilikua nashika pesa nyingi sana.

Nilikua nimejenga urafiki na baadhi ya wafanyakazi wa pale kiwandani, siku katika kupiga story jamaa akanambia naona sikuhizi umepanda cheo unapeleka mabag mwenyewe Kariakoo. Nikamwambia nimemasta kimtindo akanambia safi inabidi mzee wako majukumu yapungue maana umri unakwenda huko Kariakoo atuachie vijana. Jamaa akaniuliza posho si unapewa ukienda kupeleka mzigo?? nikamwambia sio haba kuliko kukaa bure, akauliza kwani unalipwa kiasi gani? nikamjibu 10,000. Jamaa akasema Uncle wako anakupiga atlist angekupa hata 50,000/= nikamwuuliza kwanini?, jamaa akanambia posho ya kwenda kupeleka mabag kwa siku ni 100,000/=

Jamaa akasema mzee wako anakuonea sio haki ile kazi ni risk, “hii kazi kama jamaa anavyosema kweli ni risk sababu unaweza kuibiwa kweupe, Kariakoo si mnaijua? “Kuna siku tulikua tunapakua mabag nilikua na moja ya wafanyakzi wa pale sasa jamaa alichanganya mafile akampa bag muhuni mwingine. Ilibidi akatwe kwenye mshahara, ni hivi tukikaribia Kariakoo tunawapanga wateja mapema. Kama mnavyojua maduka ya kariakoo yako barabarani plus yale mafoleni ni kichefuchef so huwa tunapakua mabag mlemle kwenye foleni. Mhusika anakuja na vijana wake wabebaji, inatakiwa uwakariri vzr maana ukizingua tu unaweza mpa mzigo mtu mwingine.”

Jamaa baada ya kufunguka hayo pia akanambia mzee wako kila bag anapata commision kwa bag la set 3 analipwa 1,000 na set 2 analipwa 700 (Zile bag za safari, set 3 ndani zinakuwa mbili yaani ukifungua zipu za bag kubwa ndani kuna kuwa na bag 2. Na hizi set 2 ukifungua zip ndani kunakuwa na bag 1). Nikawaza hata lunch najilipia, uncle anaplay fouls sio haki. Nikakumbuka matukio mengi tu mfano sometimes nikipeleka mzigo before sijaondoka atanambia ukifika Kariakoo piga simu kwamba TRA wamekukamata risiti sio sahihi, then utasema wanataka million 2, so mchina alikua anatuma hela. Nilikua nafanya hayo yote afu atanipa 50,000 tu au asinipe kabisa, nikikusanya madeni kama na million 30 atanambia ingiza kwa account ya kampuni maybe million 27 then million 3 nampelekea. Zile ndo zilikua commission zake, Uncle wangu alikua anapiga sana hela shida alikua na madem wengi sana.

Kufupisha hii story, Mchina akaanza kunikubali sababu nilikua nampa ushauri baadhi ya mambo, akawa close sana mimi. Hiki kitendo Uncle hakupenda aliona kama nataka kumpokonya ugali wake, nikaona anaanza kunikataa mara anipe kazi ya kwenda kuangalia madogo shuleni, sababu zikawa nyingi mara biashara imekua ngumu sijui mambo yakikaa sawa ataniita. Kama msomi nikajua hapa sina changu, maana jamaa kule kazini alikua ananipa mkanda mzima kinachoendelea. Ukweli hii kazi ilikua inanisaidia sikosi hata pesa za vocha na matumizi yangu binafsi.

Nikaanza kukaa home na Aunt yangu, yeye alikua ni mama wa home tu. Hakuna kitu kigumu kama kuishi na ndugu inahitaji moyo na uvumilivu sana. Aunt yangu ni mvivu sana hata kwenye masuala ya mausafi hayuko active, nafikir ni moja ya sababu Uncle akawa na michepuko mingi. Ubaya sasa Uncle alikua anamsikiliza sana Aunt kwa lolote alilokua anasema yaani ni shida. Sasa hapa home tulikua tunabaki mimi na Aunt, madogo 2 wako boarding mmoja wa kike ndo alikua mdogo ansoma anatoka asbh anarudi jioni.

Nikaanza kuwa house boy wa mle ndani naamka Asubuhi sa12 nimpikie mtoto chai, baada ya hapo nitafanya usafi na kuosha vyombo, mchana nitapika chakula, jioni ninakazi ya kupikia mbwa chakula na kumwagilia miti na maua. Hizo kazi zote nilikua nafanya mwenyewe kila siku na nilikua nafanya kwa moyo wote. Unaweza kushangaa mwanaume nawezaje kufanya hizo kazi lakini nilifunzwa nikiwa mdogo na mama yangu mzazi pamoja na dada yangu. Ikafika stage akaanza kunipa kufua nguo za Uncle na mdogo wangu ambaye ni mtoto wa mwisho (ambaye huwa naamka asubuhi kumpikia chai), nikaona haya mazoea yamezidi sasa.

Kuna siku nilikua natoka pale home Asubuhi kwenda mjini kwaajili ya interview na kusaka fursa, wahenga wanasema fursa haikufuati nyumbani unatakiwa ukaitafute. Sasa nikiondoka pale asubuhi mara nyingi anakua amelala na uncle wangu huwa anatoka sa11 au 12. Sometimes kuepusha makazi kama hayo nilikua nakwenda mjini au kwa washikaji kupoteza muda tu. Aunt wangu akawa anampa taarifa Uncle kwamba huwa naondoka bila kuaga afu narudi usiku. Kuna siku Uncle alinikaripia sana nikamwambia Uncle navyotoka huwa anakua kalala kumwamsha sio busara, napia nikitoka sio naenda kuzurura nakwenda kutafuta kazi. Uncle akasema kama umekua mkubwa humu ndani nenda kapange ili uwe huru. Kama mwanaume niakanza kufikiri namna ya kutoka pale ikiwezekana nikapange nianze maisha yangu ya kujitegemea.

Nikapata wazo tangu nimalize chuo sijawai kwenda home mkoa kusalimia acha niende home nikasalimie wazazi wanipe na baraka. Kuna siku Aunt alinitia hasira sana, ilikua usiku inakwenda saa 2 nikatoka kwenda dukani kununua vocha niliacha simu chumbani. Kumbe wakati nimetoka Uncle alirudi akaniulizia hakunikuta ikabidi apige simu ikawa haipokelewi. Wakati nimerudi nikaona gari ipo uwanjani nikajua mzee karudi naingia ndani namkuta seblen kavimba hatari. Nikamsalimia Uncle shikamoo pole na kazi hakujibu, akaniuliza ulikuwa wapi usiku huu? maana simu hupokei, kabla sijajibu Aunt akaropoka “huyu alikua kwa kidem chake kule bondeni taarifa zake zote ninazo kazi umalaya tu”. Nikaona hizi dharau sasa nakua kama mtoto nikamwambia Aunt mimi tayari ni mtu mzima hupaswi kunipangia mambo ya kufanya, mimi kama kijana pia nahitaji kuwa na mpenzi na haki yangu naomba uwe na mipaka, nikaenda zangu chumbani. Aunt akasema kama umekua mkubwa si uende ukapange ili uwe huru??, nikajua hapa nishachokwa sipaswi kuendelea kung’ang’ania, akufukuzaye hakwambii toka.

Huyu mwanamke ambaye Aunt alikua anasema kidem changu ndo mama junior wangu mpaka sasa. Ni mke wangu japo sijafunga ndoa ila taratibu zote nimekamilisha kama kulipa mahari, bado ndoa ya kanisani tu. Niseme tumetoka mbali sana from Nothing to something, ni mwanamke anayenipenda sana na kunijari anasifa zote za kuitwa mke. Namshukuru Mungu kwa kuniletea huyu mwanamke kwenye maisha ni moja ya mtu ambaye ameplay part kubwa kwenye mafanikio niliyonayo. Tumebarikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume ana miaka 2 sasa tumwite Junior.

Nilikua kwenye dimbwi kubwa la mawazo sana. Wakati niko room nikawaza jumamosi acha niondoke niende home mkoa kusalimia na pia niongee na wazazi juu ya mustakabali wa future yangu. Kesho yake nikamwaga mama Junior alishtuka sana mbona ghafla? something wrong? Nikamwambia NO! nataka nikawasalimie wazazi lakini nitarudi ASAP. Mama Junior akaomba tusex ilikua ni miez 5 toka tuanze mahusiano hatujawai kukutana. Ile jioni nikaona acha niwaage na hawa akina Uncle wanaweza kufikiri vibaya, nikategea Uncle amekaa seblen nikamsalimia, then nikamwambia Uncle Jumamosi mimi nitakwenda home kusalimia then nitarudi. Uncle akashtuka mbona haraka hivyo kulikoni? nikamwambia ni muda sijakwenda huko ni vizuri kwenda kuwajulia hali wazazi. Uncle akanambia bhasi kesho uende hata Kariakoo ununue vitenge vya mama, nikamwambia kesho ambayo ni “ijumaa” nitakwenda chuo kufuatilia cheti changu hivyo sitoweza kwenda Kariakoo. “Kumbe nilikua na timetable na mama Junior”, uncle akatoa hela akanipa kuhesabu ilikua 100,000 cash.

Jumamosi kweli nikaondoka kwenda home jioni nikiwa na bashasha nikafika mkoa nikashangaa jinsi mji ulivyojengeka maana ni miaka 3 ilipita bila kukanyaga. Nikachukua bajaji mpaka home kushuka mama akaja akanikumbatia….

MAMA: waaoohh mwanangu nilikumisi sana jamani, naona umepungua sana shida nini?
MIMI: Mama maisha haya na stress za ajira nitanenepaje?
MAMA: umerudi sasa ule kwa bidii, maziwa, mayai yapo yakutosha akatabasamu, twende ndani. “Maana wakati tunaongea haya tulikua nje getini”.

Kiukweli nilivyofika home nilifarijika sana moyo wangu ulijawa na furaha sana. Bhasi ile jioni tukala dinna as family, wakati tunakula mama akaongea huyu mdogo wako anasoma science lakini hesabu hawezi zero kabisa, itabidi uangalie namna ya kumsaidia. Nikamwambia mama haina shida kesho nitakaa naye chini tuongee vizuri. Baada ya dinna nikakaa na wazee tukaongea sana kuhusu maisha, wakanitia moyo sana, tukafanya maombi tukaenda kulala.

Kipindi naandika ule uzi “Sitaomba kazi acha niwe jeuri tu” nilikua nimeridhika na maisha tayar sina stress niko home. Ilikua ni kucheza PlayStations na masela wa huku home full raha niko home kwa mama stress za maisha natolea wapi!?. Naamka asubuhi chai ya maziwa, mayai 2 ya kuchemsha ya chienyeji, mkate umejaa blue band. Kama unawazazi jitahidi uwapende wazazi wako wakiwa hai, wazazi wanatuombea sana.

Itoshe kusema baada ya kurudi home milango ikafunguka sikukaa muda nikapata kazi.

ITAENDELEA...
Nasubiri
 
Tulipoishia, Kama unawazazi jitahidi uwapende wazazi wako wakiwa hai, wazazi wanatuombea sana. Itoshe kusema baada ya kurudi home milango ikafunguka sikukaa muda nikapata kazi.

INAENDELEA… EPISODE 02:

Ghafla simu yangu ikaanza kuita prirrr priirrrilikua namba ngeni, nikapokea, halooo

SIMU: Kwa majina naitwa “Rose Mutesi” napiga simu kutoka taasisi “X” nitakua naongea na INSIDER MAN?, nikamwambia yes ni mimi karibu. Dada akanambia hongera kwa kufaulu interview umechaguliwa kupata mafunzo kazi (Internship) kwenye taasisi yetu, jiandae mwanzoni October tutakupigia simu kwaajili ya kuanza kazi. Baada ya kuongea nae akakata simu .

Kiukweli sikuamini kama nikweli maana niliona kama ndoto hivi, nikasema hawa wanaweza kuwa matapeli, inshort sikuwa interested na ile simu. Sikumwambia mtu yoyote juu ya hili jambo hata mama sikumwambia maana niliogopa wasije wakawa matapeli. Hapo nilikua tayari nina miezi 2 niko home, wakati nimefika mzee wangu alikaa siku 3 akarudi Zambia.

Mzee wangu ni engineer kule kuna kampuni anafanyia kazi na pia mzee wangu kurudi home ni nadra sana anaweza kukaa hata miezi 3 na zaidi bila kurudi nyumbani. Nilikua naongea na mama mambo mengi sana hasa alikua anataka kujua pale kwa Uncle kama ninaishi vizuri. Ni kwamba mama yangu anamjua vizuri sana Aunt ni mtu wa namna gani, sikutaka kumwambia mama lolote kuhusu pale kwa Uncle niliamua kuyaweka moyoni. Japo mama alihisi kuna jambo halipo sawa,lakini alinisistiza sana kuwa na adabu na heshima. “Kila siku usiku tulikua tunapiga maombi na mama” mama yangu ni mtu wa dini sana.

Mwezi wa 9 mwishoni 2019, nikaamua kurudi Dar ili kuwa karibu endapo ningepigiwa simu na ile taasisi. Nikamwaga mama, akanifungia mchele wa kutosha, unga, mafuta ya kupikia gallon, maharage akanambia mpelekee Uncle. Niliamua kurudi palepale kwa Uncle lakini this time nilikua naplan zangu kichwani tayari. Baada ya kurudi Dar haikupita week nikapigiwa simu nikareport kazini nianze training.

Uncle nilimwambia kwamba kuna sehem nimepata part time, kazi ya muda nitakua natoka asubuhi, lengo langu nipate mkataba niwe na uhakika wa kumwambia. Lakini alisisitiza niwe nahakikisha mbwa wake wanakula ontime pamoja na kumwagilia maua yake. Kutoka na kurudi jion Aunt hakupenda siku nimerudi jion akanambia wewe sikuhizi umepata kazi na husemi?… nikamwambia hapana ningekua nimepata kazi mbona ningeliwaambia ila Uncle nilimwambia nimepata kazi ya muda. Dizaini hakupenda akanambia kwahiyo ukamwambia Uncle wako tu?, nikamwambia Aunt kwan kuna shida?. Akanambia sikuhizi hata kazi hufanyi… daah! . Nikamwambia huoni napikia mbwa chakula kila nikirudi jion? bado namwagilia miti namaua au unataka nifanye kazi gani??.

Aunt yangu alikua mtu wa gubu sana alikua na roho mbaya sana kama mtu wa hasira unaweza mtukana kabisa. Alikua ananichongea maneno sana kwa Uncle mpaka nikaona dizaini mzee baba kama anakua mbali na mimi.Kuna siku niliondoka na gari ya uncle kwenda kumchukua dogo shule, Uncle mara nyingi alikua anapenda kutumia gari ya ofisi ile yake inakaa home tu.
Sasa Uncle alivyorudi Aunt akamjaza maneno kuwa niliendesha gari yake eti siku nzima na nimeichibua gari. Uncle aliongea sana ile siku usiku “Sitaki uendeshe gari yangu kwanza hujui kuendesha gari, umenichubulia gari yangu. Gari ikiharibika unahela ya kulipa?? “. Ukweli ni kwamba ile michubuko ilikua vilevile, yale maeneo yalinichoma sana nikahapa kutokuja gusa ile gari hata aombe nimpelekee wapi.

Baada ya kumaliza training hatimaye nikapangiwa kituo cha kazi na nikaambiwa kesho niripoti pale ofisini. Sikuamini nilovyopewa ule mkataba kweli kesho yake nikaanza kazi nikapangiwa moja ya Idara kwenye ile ofisi. Hii ni moja ya taasisi kubwa sana hapa nchini na inategemewa sana sana.

Nilianza hii kazi bila malipo then nilikua niko vibaya sana kiuchumi ndugu zangu, mama Junior ndo alikua ananipiga tafu za nauli sometimes. Ilibidi nimwambie Aunt kwamba nimepata kazi kwenye taasisi X that day Uncle alikua safari nikaplan ntamwambia Uncle officially akirudi kwamba nimepata kazi face to face, Ukweli hizi taarifa Aunt hakuzifurahia ni kama nilimpiga na kitu kizito sana akaanza kuulizia mambo ya salary sikutaka kumwambia lolote.

Uncle akarudi toka safari nikaongea naye kuhusu kupata kazi na taasisi “X” japo hakuonesha ile furaha halisi niliona kuna unafiki hapa hajapenda. Akaniuliza nani kakutafutia nikamwambia nilifanya interview nikapigiwa simu, akauliza mambo ya mshahara nikamwambia hili suala bado ila ni kama nafanya kujitolea, kama kuna malipo nitakuambia. Huwezi amini Uncle hata hakusema neno “hongera”, nikaanza pata picha ninaishi na ndugu wa aina gani, hata mama alinambia niwe makini sana.

Pale ofisini baada ya mwezi nilikua nimeshazoeana na maofisa wa pale hasa idara yangu kama incharge/supervisor wetu alikua na roho nzuri sana. Alitokea kunikubali sana hizi ten ten nilikua nakula sana kila siku, yaani nilikua nafanya kazi kwa bidii sana na kujituma nikaweka urafiki na watu wa idara.

Pale kwenye kile kitengo chetu interns tulikua wawili mimi na dada mmoja hivi. Kadri siku zilivyokuwa zinakwenda nikawa nimezoeana na maofisa wa idara zingine wakawa wananipa kazi zao nafanya wananipa hela sikuwa nakataa kazi. Ikafika muda nikajikuta kwasiku sikosi 20,000 kuna kipindi napata mpaka 50,000/= au zaidi, hizi hela nikawa naziweka maana nilikua na mipango yangu kichwani ya kwenda kupanga.

Hii Taasisi niliyokuwa nafanyia kazi ina deal sana na wafanyabiashara hivyo nikaanza kupata connection na wafanyabiashara mbalimbali hasa pale Kariakoo.

Baada ya miezi 2 taasisi ikasema itaanza kutulipa 450,000 kwa mwezi zitusaidie bhasi kwangu ikawa sherehe. Nikaanza kununua vitu taratibu naacha madukani kwaajili ya kuanzia maisha. Nikawa nawaza njia ya kutokea pale kwa Uncle maana wangeanza maneno kapata kazi ameondoka sikutaka hizi kelele. Nikawaza hapa nitawaambia naenda safari ya kikazi Dodoma ndo itakua gia yangu ya kusepa pale.

Baada ya hapo sikuchelewa nilikua na iphone 7 plus nikaiuza 740,000 nikawa kidogo napesa ya kuanzia maisha. Nikamtafuta dalali tukapata chumba sebule na jiko kodi ilikua 180,000 kwa mwezi, nikalipa kodi ya miezi 4 kwanza. Eneo nililopata ilikua ni salasala (Mabanda mengi) pale Mbuyuni mataa ya kwenda tegeta na kunduchi, sasa kwa mbele kama unakwenda Tegeta kuna kibarabara kinakata kushoto kwenda salasala, kule ndo nilikoanzia maisha.

Nikaweka godoro langu chini, nikaweka jiko langu la gas, nikanunua gas mtungi mkubwa, sufuria na baadhi ya vyombo vya kuanzia maisha bila kusahau subwoofer “Sea piano” , raha ya geto mziki uwe unasikika.

Baada ya hapo nikaanza kuamisha vitu vyangu bila kushtukiwa mpango wangu. Baada ya hapo nikawaaga nitakwenda kikazi Dodoma sijui nitarudi lini wakaniambia safari njema, maisha ya geto niliyaanza March 2020.

Nimeingia pale sasa akili ya maisha ikaanza kuja kichwani, kwanza nimelala pale kuna baridi hatari sina hata shuka la kujifunika, madirisha hayana mapazia. Week ileile niliyohamia kwangu nikapambana nikanunua mapazia mazuri nikayaweka. Bad news haikupita hata week nikaibiwa yale mapazia na laptop .

Pale palikua na wapangaji watatu na wote tulikua tunatoka afu fense ilikua fupi mtu rahis kujua kama hakuna mtu, na pia geti lilikua tunarudishia si unajua tena maisha ya kupanga geti huwa halifungwi. Uzembe ulikua wangu maana sikufunga madirisha ilikua rahsi kuibiwa jama alichomoa mapazia yote mpaka seblen. Nilihisi aliyeniibia ni mzoa taka wala sio mtu mwingine maana ndo alikua na mazoea ya kuja pale home.

Mungu akaendelea kufungua milango, kutokana na kuwa na changamoto nikipika chakula kikibaki kinachacha nikaona kuna umuhimu wa kununua fridge. Nikafanya research yangu pale Kariakoo nikaona bora ninunue fridge la size ya kati bei ilikua ni 720,000 kwa kipindi kile.

Nikapambana sana pamoja na kukopa nikaweza kununua fridge, mama Junior naye hakua mbali akaniletea Micro wave ya kupashia chakula na mazaga mengine kama mashuka nknk. Ndani ya muda mfupi nikawa nimekamilika na kila kitu ndani kiasi kwamba ukiingiza pisi ndani lazima ipagawe. Baada ya hayo niakaanza kusave hela kila senti nayopata nikawa nasave kupitia vicoba na kucheza michezo.

November 2020, mama junior akaja kwangu akanambia ana mimba yangu hivyo kwao amekimbia hawezi kurudi anamwogopa baba yake. Hapo alikua anasoma chuo na mzee wake katoka kulipa ada afu sasa mzee wake ni mkorofi hatari ndomana akakimbilia kwangu hakutaka kutoa ile mimba.

Zile habari hazikunishtua niliona mtoto ni jambo la kheri then hata yeye nampenda nikamwambia kama mtoto ni wangu bhasi utakaa hapa huko kwenu tutaweka mambo sawa, si unajua wazee wa kichaga.

Nikampigia simu mama yake kumwambia bint yake yupo kwangu asihangaike kumtafuta mimi naandaa utaratibu nitakuja, mama yake alikua anajua natoka na bint yake hakua nashida na mimi. Akanambia kama yuko kwako mimi sina shida najua yuko sehem salama ila sasa baba yake ndo shida.

Tulikwenda hospital kuchek mimba ilikua na week 6, ikabd nichukue hatua zingine za haraka ili kukamilisha hili jambo, hatimaye tukalipa mahari.

Baada ya kuanza kukaa na mama Junior hapo ni mjamzito mambo yangu yakazidi kunyooka sana, nikawa mtu wa bahati sana. Kuna mwanamke ukiwa naye mambo yananyooka yenyewe. Nikaanza kutengeneza connections na wafanyabiashara wakubwa, stakeholders na watu mbalimbali maana sikuwa naona future ya kuajiriwa na hii taasisi.

Nikaanza kujiongeza mlemle Kariakoo na kufanya deals zingine nyingi, nikafungua biashara “workshop” ya kupaka rangi magari, services, lubricants, polishing nknk pale gerezani. Kwa kufupisha hii story baada ya kumaliza mkataba tukastopishwa kwenda kazini na mimi sikutaka kuhangaika na kuomba na kutafuta kazi. Hapo ilikua ni September 2021.

Sikushtuka sana, mimi binafsi nilikua nishajipanga tayari na nilishaona dalili mapema, savings binafsi nilizokuwa nazo za haraka cash in hand ni 24 million. Nikaagiza Toyota IST kutoka Japan iwe inanisaidia mishe zangu za hapa napale. Baada ya kununua gari, kukamilisha kila kitu nilitumia 14 million, nikalipa deni la kiwanja full 5,600,000/=nikamwekea wife 3 million kwa account maana mwakani 2022 alikua inabidi arudi chuo kuendelea na masomo alikua kashajifungua tayari. Nakumbuka sikubaki na kitu katika ile saving lakini nilikua na shares zangu kwa watu hivyo hata bila kazi ningesurvive.

Maendeleo ya Biashara yalikua mazuri sana nilikua na wateja wengi sana na pesa nilikua naiona kama faida. Ile September mwisho wa mwezi mwenye eneo/Landlord akanipigia simu.

LANDLORD: Kijana wangu hujambo? sasa nina habari mbaya nataka kukupa maana ipo chini ya uwezo wangu. Kutokana na ujenzi unaoendelea na upanuzi wa barabara nimepewa order ya kwamba nyumba zetu zitaweza bomolewa muda wowote. Na wewe kodi yako inaisha mwezi ujao, itabidi utafute eneo lingine mambo yatakapo kamilika nitakutaarifu kijana wangu.

Ukweli taarifa za Mzee zilinipa stress sana maana biashara ilikua imechanganya sana na kwa ile location ilikua nzuri sana. Niwaambie biashara ya workshops inalipa sana faida inaonekana sana. Mchawi ni location tu maana pale nilikua nakamata magari yanayotoka bandarini nknk.

Ofisi yangu ilikua Gerezani karibu na Round about ya kwenda Kurasini. Kama unatokea central before hujafika kwenye ile Round about kuna yard ya magari bhs mitaa ileile. Baada ya kuongea na mzee nikawa sijui niende wapi maana nilikua dilemma, pia watu wakanishauri ujenzi wa barabara unaondelea biashara itakua ngumu sana maeneo yale hivyo nisubiri niangalie upepo. Ikabidi nistop kwenye hii biashara kwanza,nikaplan nitarudi barabara ikikamilika. Ilikua kama mkosi naacha kazi na biashara nafunga niliona kama mtu ananichezea hivi.

Nikafunga biashara katikati ya October kodi ndo iliisha tarehe hizo, baada ya hapo nikawa sina hela maana hakuna nilichokua naingiza. Ile ile october kuna mhindi alikua jamaa yangu sana niliweka kiasi cha pesa kwenye biashara yake ni muda. Jamaa alinicheki akanambia anakwenda India na pale watasimamia ndugu zake itaweza sumbua kupata gawio zangu hivyo akanipa pesa magawiwo yote 6,000,000. Nikakusanya na madeni yangu na pesa zingine nikapata 3,400,000 jumla nikawa na 9,400,000/=.

Ikabidi nikae na wife chini tupange mipango maana alikua anajua kinachoendelea. Nikalipa kodi ya nyumba 1,800,000/= kwa miezi sita. Nikampa wife 2,500,000/= kwaajili ya matumizi ya mtoto, mshahara wa dada, bill za umeme na maji na mahitaji ya nyumbani yote (Miezi 6). Nikamlipia mtoto bima pamoja na mama yake kama 245,000/=.

Ilibaki kama 4,800,000 tukaplan hii amount tufungue biashara ya vinywaji. Lakini kuna dogo langu anayenifuatia yeye alikataa shule alisema anapoteza pesa za wazazi na muda. Toka muda alikua ameniomba nimkopeshe million 3, “alipataga hasara walimtapeli” dogo anaduka la vifaa vya simu na Huduma za kifedha. Dogo pia alinisave sana kipindi kile nakosa nauli za kwenda kazini, so nikampa dogo million 2 kama kaka yake. Nikamlipia dogo ada “yule ambaye mama alisema anataka sayansi ila math haipandi” nililipa million 1. Hapo unaona jinsi ambavyo pesa haikai kabsa.

Nilibakiwa na 1,500,000/= hivi nikasema hizo nilizotoa nitajazia. Ukitaka kuona mambo yanabadilika acha kazi ndo utaona kila rangi. Bhasi nikaanza kuwaza namna ya kutafuta pesa nikisema nisubiri pesa iishe nitakuja aibika huko mbeleni. Nikafikiri kuingia kwenye uber maana gari nilikuwa nayo tena yangu, kumpa mtu hapana bora nikomae mwenyewe tu. Kuna jamaa yangu wa uber alikua mshikaji sana nikamcheki…

DULLAH: oya tajiri vipi hatutafutani sikuhizi umenitenga hunipi kazi kama zamani hali ni mbaya.

MIMI: Tajiri sijakutenga sema pale nimetoka ndomana unaona kimya mwenyewe sina maisha ndomana nimekucheki unipe ramani.

DULLAH: Sasa tajiri mimi nakupa mchongo gani hapa nakomaa na uber tu hapa, siku za kati ya wiki tunafanya kuokoteza, cha muhimu mkono uende kinywani.

MIMI: Tajiri nahitaji tuonane nina jambo langu muhimu sana unipe code nianzie wapi ili kufanikisha.

DULLAH: Jambo gani tajiri unanitisha, kesho nitakua home siku nzima, leo nitakudanganya boss wangu. Wewe kesho njoo muda wowote tutayajenga.

MIMI: haina noma kesho asubuhi nitakucheki unipe code.

DULLAH: Imeisha hio tajiri

Asubuhi nikamcheki Dullah ilikua kama saa 2 asubuhi hivi akapokea akanielekeza anakaa Sinza madukani unakunja pale kwa vunja bei. Bila kupoteza muda nikaenda chap nikafanikiwa kufika kwa jamaa, tukaanza story…

DULLAH: Tajiri karibu sana naona upo na chombo mpya kabsa hii hata week haina. Hii chombo umechukua yard au umeagiza?

MIMI: , Tajir huoni kabisa hadi alama za bandarini hizo chuma imetoka Japani. Sikia ndugu yangu mchongo wenyewe naotaka tuongee ndo huo unaoushangaa.

DULLAH: Sijaelewa Tajiri unauza hii IST?? au

MIMI: Nataka kusajili Uber tajiri unanisaidiaje? Nataka maelekezo kutoka kwako wewe una experince ya muda mrefu.

DULLAH: Unataka kuendesha wewe au nikutafutie dereva?

MIMI: camon mimi bro!

DULLAH: Kama wewe sikushauri hii gari ubadilishe vibao tumia hivyohivyo vya njano, akaifungua ndani akaona gari nimetia seat cover, full unyunyu, Android Tv nch 10 imekaa pale, chini carpet. Mzee hii gari utapiga sana hela niamini mimi kama hawa mademu watakutafuta sana, utapata root privates nyingi, kama nilivyokwambia usiweke vibao vyeupe.

MIMI: kwanini nisiweke vibao vyeupe?

DULLAH: Vibao vyeupe miyeyusho ndugu yangu traffic mikono mingi, bado TRA yaani tunapata shida wahuni sikuhizi wanatumia vya njano.

MIMI: Basi poa nimekuelewa sasa najisajilije?

DULLAH: Kuna jamaa namjua ila sijawai kumwona kwa sura ni kama “Ghost” anakusaidia chap wewe andaa 100k. Kama unayo hata leo anaanza kazi baada ya siku 3 kila kitu kinakua sawa. Hapa anza na Bolt hii haichelewi huku unasubiri uber hii kidogo utasubiri.

MIMI: ongea na jamaa then nipe namba yake mwambie huyu ni ndugu yangu wa damu. Afu unaongeaje na mtu usiyemjua?? Kama tapeli?

DULLAH: , Tajiri nishafungua account nyingi sana na yeye hana noma usiwe na wasiwasi.

Dullah akaongea na jamaa walitumia muda kidogo baada ya hapo akanirudia akanambia nimeongea naye Freshy utampa 90,000 atafanya hiyo kazi. Nikamshukuru nikampa 10,000 ya Ahsante.

Nikampigia simu Ghost tukaongea maana alikua anajua tayari kuhusu mimi. Akanambia nimtumie baadhi ya documents kama kadi ya gari, ID, bima na picha ya gari na taktaka zingine. Akanambia ndani ya siku 3 itakua tayari.

Baada ya siku 3 akanicheki ghost akanambia account yako ipo tayari, akanipa password akanambia download bolt driver app kwa simu then anza kazi. Kweli nikafanya nikaona mambo yako supa nikaona sehem ya kwenda online kama unataka request, nika touch pale nikaona inasearch nikazima data nikalala, nikaplan kuingia mzigoni jioni.

Nimeshapata account ya bolt tayari nini kitaendelea? Mama Junior hajui kama nimeamua kufanya hii kazi atakubali?? Usikose mwendelezo story tamu ndo zinaanza sasa, usikose bando tu.

ENDELEA….

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
 
Tulipoishia, Kama unawazazi jitahidi uwapende wazazi wako wakiwa hai, wazazi wanatuombea sana. Itoshe kusema baada ya kurudi home milango ikafunguka sikukaa muda nikapata kazi.

INAENDELEA… EPISODE 02:

Ghafla simu yangu ikaanza kuita prirrr priirrrilikua namba ngeni, nikapokea, halooo

SIMU: Kwa majina naitwa “Rose Mutesi” napiga simu kutoka taasisi “X” nitakua naongea na INSIDER MAN?, nikamwambia yes ni mimi karibu. Dada akanambia hongera kwa kufaulu interview umechaguliwa kupata mafunzo kazi (Internship) kwenye taasisi yetu, jiandae mwanzoni October tutakupigia simu kwaajili ya kuanza kazi. Baada ya kuongea nae akakata simu .

Kiukweli sikuamini kama nikweli maana niliona kama ndoto hivi, nikasema hawa wanaweza kuwa matapeli, inshort sikuwa interested na ile simu. Sikumwambia mtu yoyote juu ya hili jambo hata mama sikumwambia maana niliogopa wasije wakawa matapeli. Hapo nilikua tayari nina miezi 2 niko home, wakati nimefika mzee wangu alikaa siku 3 akarudi Zambia.

Mzee wangu ni engineer kule kuna kampuni anafanyia kazi na pia mzee wangu kurudi home ni nadra sana anaweza kukaa hata miezi 3 na zaidi bila kurudi nyumbani. Nilikua naongea na mama mambo mengi sana hasa alikua anataka kujua pale kwa Uncle kama ninaishi vizuri. Ni kwamba mama yangu anamjua vizuri sana Aunt ni mtu wa namna gani, sikutaka kumwambia mama lolote kuhusu pale kwa Uncle niliamua kuyaweka moyoni. Japo mama alihisi kuna jambo halipo sawa,lakini alinisistiza sana kuwa na adabu na heshima. “Kila siku usiku tulikua tunapiga maombi na mama” mama yangu ni mtu wa dini sana.

Mwezi wa 9 mwishoni 2019, nikaamua kurudi Dar ili kuwa karibu endapo ningepigiwa simu na ile taasisi. Nikamwaga mama, akanifungia mchele wa kutosha, unga, mafuta ya kupikia gallon, maharage akanambia mpelekee Uncle. Niliamua kurudi palepale kwa Uncle lakini this time nilikua naplan zangu kichwani tayari. Baada ya kurudi Dar haikupita week nikapigiwa simu nikareport kazini nianze training.

Uncle nilimwambia kwamba kuna sehem nimepata part time, kazi ya muda nitakua natoka asubuhi, lengo langu nipate mkataba niwe na uhakika wa kumwambia. Lakini alisisitiza niwe nahakikisha mbwa wake wanakula ontime pamoja na kumwagilia maua yake. Kutoka na kurudi jion Aunt hakupenda siku nimerudi jion akanambia wewe sikuhizi umepata kazi na husemi?… nikamwambia hapana ningekua nimepata kazi mbona ningeliwaambia ila Uncle nilimwambia nimepata kazi ya muda. Dizaini hakupenda akanambia kwahiyo ukamwambia Uncle wako tu?, nikamwambia Aunt kwan kuna shida?. Akanambia sikuhizi hata kazi hufanyi… daah! . Nikamwambia huoni napikia mbwa chakula kila nikirudi jion? bado namwagilia miti namaua au unataka nifanye kazi gani??.

Aunt yangu alikua mtu wa gubu sana alikua na roho mbaya sana kama mtu wa hasira unaweza mtukana kabisa. Alikua ananichongea maneno sana kwa Uncle mpaka nikaona dizaini mzee baba kama anakua mbali na mimi.Kuna siku niliondoka na gari ya uncle kwenda kumchukua dogo shule, Uncle mara nyingi alikua anapenda kutumia gari ya ofisi ile yake inakaa home tu.
Sasa Uncle alivyorudi Aunt akamjaza maneno kuwa niliendesha gari yake eti siku nzima na nimeichibua gari. Uncle aliongea sana ile siku usiku “Sitaki uendeshe gari yangu kwanza hujui kuendesha gari, umenichubulia gari yangu. Gari ikiharibika unahela ya kulipa?? “. Ukweli ni kwamba ile michubuko ilikua vilevile, yale maeneo yalinichoma sana nikahapa kutokuja gusa ile gari hata aombe nimpelekee wapi.

Baada ya kumaliza training hatimaye nikapangiwa kituo cha kazi na nikaambiwa kesho niripoti pale ofisini. Sikuamini nilovyopewa ule mkataba kweli kesho yake nikaanza kazi nikapangiwa moja ya Idara kwenye ile ofisi. Hii ni moja ya taasisi kubwa sana hapa nchini na inategemewa sana sana.

Nilianza hii kazi bila malipo then nilikua niko vibaya sana kiuchumi ndugu zangu, mama Junior ndo alikua ananipiga tafu za nauli sometimes. Ilibidi nimwambie Aunt kwamba nimepata kazi kwenye taasisi X that day Uncle alikua safari nikaplan ntamwambia Uncle officially akirudi kwamba nimepata kazi face to face, Ukweli hizi taarifa Aunt hakuzifurahia ni kama nilimpiga na kitu kizito sana akaanza kuulizia mambo ya salary sikutaka kumwambia lolote.

Uncle akarudi toka safari nikaongea naye kuhusu kupata kazi na taasisi “X” japo hakuonesha ile furaha halisi niliona kuna unafiki hapa hajapenda. Akaniuliza nani kakutafutia nikamwambia nilifanya interview nikapigiwa simu, akauliza mambo ya mshahara nikamwambia hili suala bado ila ni kama nafanya kujitolea, kama kuna malipo nitakuambia. Huwezi amini Uncle hata hakusema neno “hongera”, nikaanza pata picha ninaishi na ndugu wa aina gani, hata mama alinambia niwe makini sana.

Pale ofisini baada ya mwezi nilikua nimeshazoeana na maofisa wa pale hasa idara yangu kama incharge/supervisor wetu alikua na roho nzuri sana. Alitokea kunikubali sana hizi ten ten nilikua nakula sana kila siku, yaani nilikua nafanya kazi kwa bidii sana na kujituma nikaweka urafiki na watu wa idara.

Pale kwenye kile kitengo chetu interns tulikua wawili mimi na dada mmoja hivi. Kadri siku zilivyokuwa zinakwenda nikawa nimezoeana na maofisa wa idara zingine wakawa wananipa kazi zao nafanya wananipa hela sikuwa nakataa kazi. Ikafika muda nikajikuta kwasiku sikosi 20,000 kuna kipindi napata mpaka 50,000/= au zaidi, hizi hela nikawa naziweka maana nilikua na mipango yangu kichwani ya kwenda kupanga.

Hii Taasisi niliyokuwa nafanyia kazi ina deal sana na wafanyabiashara hivyo nikaanza kupata connection na wafanyabiashara mbalimbali hasa pale Kariakoo.

Baada ya miezi 2 taasisi ikasema itaanza kutulipa 450,000 kwa mwezi zitusaidie bhasi kwangu ikawa sherehe. Nikaanza kununua vitu taratibu naacha madukani kwaajili ya kuanzia maisha. Nikawa nawaza njia ya kutokea pale kwa Uncle maana wangeanza maneno kapata kazi ameondoka sikutaka hizi kelele. Nikawaza hapa nitawaambia naenda safari ya kikazi Dodoma ndo itakua gia yangu ya kusepa pale.

Baada ya hapo sikuchelewa nilikua na iphone 7 plus nikaiuza 740,000 nikawa kidogo napesa ya kuanzia maisha. Nikamtafuta dalali tukapata chumba sebule na jiko kodi ilikua 180,000 kwa mwezi, nikalipa kodi ya miezi 4 kwanza. Eneo nililopata ilikua ni salasala (Mabanda mengi) pale Mbuyuni mataa ya kwenda tegeta na kunduchi, sasa kwa mbele kama unakwenda Tegeta kuna kibarabara kinakata kushoto kwenda salasala, kule ndo nilikoanzia maisha.

Nikaweka godoro langu chini, nikaweka jiko langu la gas, nikanunua gas mtungi mkubwa, sufuria na baadhi ya vyombo vya kuanzia maisha bila kusahau subwoofer “Sea piano” , raha ya geto mziki uwe unasikika.

Baada ya hapo nikaanza kuamisha vitu vyangu bila kushtukiwa mpango wangu. Baada ya hapo nikawaaga nitakwenda kikazi Dodoma sijui nitarudi lini wakaniambia safari njema, maisha ya geto niliyaanza March 2020.

Nimeingia pale sasa akili ya maisha ikaanza kuja kichwani, kwanza nimelala pale kuna baridi hatari sina hata shuka la kujifunika, madirisha hayana mapazia. Week ileile niliyohamia kwangu nikapambana nikanunua mapazia mazuri nikayaweka. Bad news haikupita hata week nikaibiwa yale mapazia na laptop .

Pale palikua na wapangaji watatu na wote tulikua tunatoka afu fense ilikua fupi mtu rahis kujua kama hakuna mtu, na pia geti lilikua tunarudishia si unajua tena maisha ya kupanga geti huwa halifungwi. Uzembe ulikua wangu maana sikufunga madirisha ilikua rahsi kuibiwa jama alichomoa mapazia yote mpaka seblen. Nilihisi aliyeniibia ni mzoa taka wala sio mtu mwingine maana ndo alikua na mazoea ya kuja pale home.

Mungu akaendelea kufungua milango, kutokana na kuwa na changamoto nikipika chakula kikibaki kinachacha nikaona kuna umuhimu wa kununua fridge. Nikafanya research yangu pale Kariakoo nikaona bora ninunue fridge la size ya kati bei ilikua ni 720,000 kwa kipindi kile.

Nikapambana sana pamoja na kukopa nikaweza kununua fridge, mama Junior naye hakua mbali akaniletea Micro wave ya kupashia chakula na mazaga mengine kama mashuka nknk. Ndani ya muda mfupi nikawa nimekamilika na kila kitu ndani kiasi kwamba ukiingiza pisi ndani lazima ipagawe. Baada ya hayo niakaanza kusave hela kila senti nayopata nikawa nasave kupitia vicoba na kucheza michezo.

November 2020, mama junior akaja kwangu akanambia ana mimba yangu hivyo kwao amekimbia hawezi kurudi anamwogopa baba yake. Hapo alikua anasoma chuo na mzee wake katoka kulipa ada afu sasa mzee wake ni mkorofi hatari ndomana akakimbilia kwangu hakutaka kutoa ile mimba.

Zile habari hazikunishtua niliona mtoto ni jambo la kheri then hata yeye nampenda nikamwambia kama mtoto ni wangu bhasi utakaa hapa huko kwenu tutaweka mambo sawa, si unajua wazee wa kichaga.

Nikampigia simu mama yake kumwambia bint yake yupo kwangu asihangaike kumtafuta mimi naandaa utaratibu nitakuja, mama yake alikua anajua natoka na bint yake hakua nashida na mimi. Akanambia kama yuko kwako mimi sina shida najua yuko sehem salama ila sasa baba yake ndo shida.

Tulikwenda hospital kuchek mimba ilikua na week 6, ikabd nichukue hatua zingine za haraka ili kukamilisha hili jambo, hatimaye tukalipa mahari.

Baada ya kuanza kukaa na mama Junior hapo ni mjamzito mambo yangu yakazidi kunyooka sana, nikawa mtu wa bahati sana. Kuna mwanamke ukiwa naye mambo yananyooka yenyewe. Nikaanza kutengeneza connections na wafanyabiashara wakubwa, stakeholders na watu mbalimbali maana sikuwa naona future ya kuajiriwa na hii taasisi.

Nikaanza kujiongeza mlemle Kariakoo na kufanya deals zingine nyingi, nikafungua biashara “workshop” ya kupaka rangi magari, services, lubricants, polishing nknk pale gerezani. Kwa kufupisha hii story baada ya kumaliza mkataba tukastopishwa kwenda kazini na mimi sikutaka kuhangaika na kuomba na kutafuta kazi. Hapo ilikua ni September 2021.

Sikushtuka sana, mimi binafsi nilikua nishajipanga tayari na nilishaona dalili mapema, savings binafsi nilizokuwa nazo za haraka cash in hand ni 24 million. Nikaagiza Toyota IST kutoka Japan iwe inanisaidia mishe zangu za hapa napale. Baada ya kununua gari, kukamilisha kila kitu nilitumia 14 million, nikalipa deni la kiwanja full 5,600,000/=nikamwekea wife 3 million kwa account maana mwakani 2022 alikua inabidi arudi chuo kuendelea na masomo alikua kashajifungua tayari. Nakumbuka sikubaki na kitu katika ile saving lakini nilikua na shares zangu kwa watu hivyo hata bila kazi ningesurvive.

Maendeleo ya Biashara yalikua mazuri sana nilikua na wateja wengi sana na pesa nilikua naiona kama faida. Ile September mwisho wa mwezi mwenye eneo/Landlord akanipigia simu.

LANDLORD: Kijana wangu hujambo? sasa nina habari mbaya nataka kukupa maana ipo chini ya uwezo wangu. Kutokana na ujenzi unaoendelea na upanuzi wa barabara nimepewa order ya kwamba nyumba zetu zitaweza bomolewa muda wowote. Na wewe kodi yako inaisha mwezi ujao, itabidi utafute eneo lingine mambo yatakapo kamilika nitakutaarifu kijana wangu.

Ukweli taarifa za Mzee zilinipa stress sana maana biashara ilikua imechanganya sana na kwa ile location ilikua nzuri sana. Niwaambie biashara ya workshops inalipa sana faida inaonekana sana. Mchawi ni location tu maana pale nilikua nakamata magari yanayotoka bandarini nknk.

Ofisi yangu ilikua Gerezani karibu na Round about ya kwenda Kurasini. Kama unatokea central before hujafika kwenye ile Round about kuna yard ya magari bhs mitaa ileile. Baada ya kuongea na mzee nikawa sijui niende wapi maana nilikua dilemma, pia watu wakanishauri ujenzi wa barabara unaondelea biashara itakua ngumu sana maeneo yale hivyo nisubiri niangalie upepo. Ikabidi nistop kwenye hii biashara kwanza,nikaplan nitarudi barabara ikikamilika. Ilikua kama mkosi naacha kazi na biashara nafunga niliona kama mtu ananichezea hivi.

Nikafunga biashara katikati ya October kodi ndo iliisha tarehe hizo, baada ya hapo nikawa sina hela maana hakuna nilichokua naingiza. Ile ile october kuna mhindi alikua jamaa yangu sana niliweka kiasi cha pesa kwenye biashara yake ni muda. Jamaa alinicheki akanambia anakwenda India na pale watasimamia ndugu zake itaweza sumbua kupata gawio zangu hivyo akanipa pesa magawiwo yote 6,000,000. Nikakusanya na madeni yangu na pesa zingine nikapata 3,400,000 jumla nikawa na 9,400,000/=.

Ikabidi nikae na wife chini tupange mipango maana alikua anajua kinachoendelea. Nikalipa kodi ya nyumba 1,800,000/= kwa miezi sita. Nikampa wife 2,500,000/= kwaajili ya matumizi ya mtoto, mshahara wa dada, bill za umeme na maji na mahitaji ya nyumbani yote (Miezi 6). Nikamlipia mtoto bima pamoja na mama yake kama 245,000/=.

Ilibaki kama 4,800,000 tukaplan hii amount tufungue biashara ya vinywaji. Lakini kuna dogo langu anayenifuatia yeye alikataa shule alisema anapoteza pesa za wazazi na muda. Toka muda alikua ameniomba nimkopeshe million 3, “alipataga hasara walimtapeli” dogo anaduka la vifaa vya simu na Huduma za kifedha. Dogo pia alinisave sana kipindi kile nakosa nauli za kwenda kazini, so nikampa dogo million 2 kama kaka yake. Nikamlipia dogo ada “yule ambaye mama alisema anataka sayansi ila math haipandi” nililipa million 1. Hapo unaona jinsi ambavyo pesa haikai kabsa.

Nilibakiwa na 1,500,000/= hivi nikasema hizo nilizotoa nitajazia. Ukitaka kuona mambo yanabadilika acha kazi ndo utaona kila rangi. Bhasi nikaanza kuwaza namna ya kutafuta pesa nikisema nisubiri pesa iishe nitakuja aibika huko mbeleni. Nikafikiri kuingia kwenye uber maana gari nilikuwa nayo tena yangu, kumpa mtu hapana bora nikomae mwenyewe tu. Kuna jamaa yangu wa uber alikua mshikaji sana nikamcheki…

DULLAH: oya tajiri vipi hatutafutani sikuhizi umenitenga hunipi kazi kama zamani hali ni mbaya.

MIMI: Tajiri sijakutenga sema pale nimetoka ndomana unaona kimya mwenyewe sina maisha ndomana nimekucheki unipe ramani.

DULLAH: Sasa tajiri mimi nakupa mchongo gani hapa nakomaa na uber tu hapa, siku za kati ya wiki tunafanya kuokoteza, cha muhimu mkono uende kinywani.

MIMI: Tajiri nahitaji tuonane nina jambo langu muhimu sana unipe code nianzie wapi ili kufanikisha.

DULLAH: Jambo gani tajiri unanitisha, kesho nitakua home siku nzima, leo nitakudanganya boss wangu. Wewe kesho njoo muda wowote tutayajenga.

MIMI: haina noma kesho asubuhi nitakucheki unipe code.

DULLAH: Imeisha hio tajiri

Asubuhi nikamcheki Dullah ilikua kama saa 2 asubuhi hivi akapokea akanielekeza anakaa Sinza madukani unakunja pale kwa vunja bei. Bila kupoteza muda nikaenda chap nikafanikiwa kufika kwa jamaa, tukaanza story…

DULLAH: Tajiri karibu sana naona upo na chombo mpya kabsa hii hata week haina. Hii chombo umechukua yard au umeagiza?

MIMI: , Tajir huoni kabisa hadi alama za bandarini hizo chuma imetoka Japani. Sikia ndugu yangu mchongo wenyewe naotaka tuongee ndo huo unaoushangaa.

DULLAH: Sijaelewa Tajiri unauza hii IST?? au

MIMI: Nataka kusajili Uber tajiri unanisaidiaje? Nataka maelekezo kutoka kwako wewe una experince ya muda mrefu.

DULLAH: Unataka kuendesha wewe au nikutafutie dereva?

MIMI: camon mimi bro!

DULLAH: Kama wewe sikushauri hii gari ubadilishe vibao tumia hivyohivyo vya njano, akaifungua ndani akaona gari nimetia seat cover, full unyunyu, Android Tv nch 10 imekaa pale, chini carpet. Mzee hii gari utapiga sana hela niamini mimi kama hawa mademu watakutafuta sana, utapata root privates nyingi, kama nilivyokwambia usiweke vibao vyeupe.

MIMI: kwanini nisiweke vibao vyeupe?

DULLAH: Vibao vyeupe miyeyusho ndugu yangu traffic mikono mingi, bado TRA yaani tunapata shida wahuni sikuhizi wanatumia vya njano.

MIMI: Basi poa nimekuelewa sasa najisajilije?

DULLAH: Kuna jamaa namjua ila sijawai kumwona kwa sura ni kama “Ghost” anakusaidia chap wewe andaa 100k. Kama unayo hata leo anaanza kazi baada ya siku 3 kila kitu kinakua sawa. Hapa anza na Bolt hii haichelewi huku unasubiri uber hii kidogo utasubiri.

MIMI: ongea na jamaa then nipe namba yake mwambie huyu ni ndugu yangu wa damu. Afu unaongeaje na mtu usiyemjua?? Kama tapeli?

DULLAH: , Tajiri nishafungua account nyingi sana na yeye hana noma usiwe na wasiwasi.

Dullah akaongea na jamaa walitumia muda kidogo baada ya hapo akanirudia akanambia nimeongea naye Freshy utampa 90,000 atafanya hiyo kazi. Nikamshukuru nikampa 10,000 ya Ahsante.

Nikampigia simu Ghost tukaongea maana alikua anajua tayari kuhusu mimi. Akanambia nimtumie baadhi ya documents kama kadi ya gari, ID, bima na picha ya gari na taktaka zingine. Akanambia ndani ya siku 3 itakua tayari.

Baada ya siku 3 akanicheki ghost akanambia account yako ipo tayari, akanipa password akanambia download bolt driver app kwa simu then anza kazi. Kweli nikafanya nikaona mambo yako supa nikaona sehem ya kwenda online kama unataka request, nika touch pale nikaona inasearch nikazima data nikalala, nikaplan kuingia mzigoni jioni.

ITAENDELEA…..
Nimeshapata account ya bolt tayari nini kitaendelea? Mama Junior hajui kama nimeamua kufanya hii kazi atakubali?? Usikose mwendelezo story tamu ndo zinaanza sasa, usikose bando tu.

Domhome
Watu8
Missy Gf
Chakula Kibaya
Copa Cabana
Cute Wife
Asanteeee usinisahau next
 
Back
Top Bottom