Jina lako lina-trend wapi leo?

Jina lako lina-trend wapi leo?

Mama Bikira Maria ndo kimbilio
Biblia haituambii tumkimbilie Bikira Maria. Kimbilio la kweli ni Yesu pekee. Maria mwenyewe alimhitaji Mwokozi (Luka 1:47), na aliwaambia watu wamtii Yesu, sio yeye (Yohana 2:5).
 
Leo, jina lako lina-trend katika jukwaa lipi? La Siasa, la Habari na Hoja Mchanganyiko au International Forum?

Ukitubu leo na kuamua kuokoka, jina lako lita-trend mbinguni. Na huko sio ku-trend tu, itakuwa Breaking News itakayowafanya malaika wote washangilie.
Luka 15:7
"Kadhalika nawaambieni, ndivyo kutakavyokuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya kutubu kwa mwenye dhambi mmoja, kuliko kwa ajili ya watu tisini na tisa wanaojiona kuwa wema, wasiohitaji kutubu.”

Mnaosema mada zangu ni ndefu, hamuwezi kusoma mpaka mwisho, semeni sasa: na hii mmeshindwa kuisoma mpaka mwisho au huwa ni geresha tu 🙂
Leo jukwaani kwa mwamposa
 
Mtumishi leo umeandika fupi hadi namie nimeisoma yote, ubarikiwe....uwe unaandika hivi ya kusomeka sio marefu kama ya Lucas Mwashambwa
Tatizo sio urefu wa mada. Tatizo ni kwamba huna njaa wala kiu ya haki. Kama unashindwa kusoma ukurasa mmoja tu, utawezaje kusoma Biblia yote, Mwanzo hadi Ufunuo x3?
Wanaosema mada zangu ni ndefu, sioni wakilalamikia mada ndefu za Udaku na masimulizi ya uzinzi na uasherati.
Mt 5:6
Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa
 
Hakuna dhambi inayotawala ndani yangu.


1 Yohana 1:8
“Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo ndani yetu.”

1 Yohana 1:10
“Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo, wala neno lake halimo mwetu.”

kila mtu ana dhambi, na kudai huna dhambi ni kujidanganya.
 
Tatizo sio urefu wa mada. Tatizo ni kwamba huna njaa wala kiu ya haki. Kama unashindwa kusoma ukurasa mmoja tu, utawezaje kusoma Biblia yote, Mwanzo hadi Ufunuo x3?
Wanaosema mada zangu ni ndefu, sioni wakilalamikia mada ndefu za Udaku na masimulizi ya uzinzi na uasherati.
Mt 5:6
Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa
Tupunguzie urefu ma mtumishi
 
Tatizo sio urefu wa mada. Tatizo ni kwamba huna njaa wala kiu ya haki. Kama unashindwa kusoma ukurasa mmoja tu, utawezaje kusoma Biblia yote, Mwanzo hadi Ufunuo x3?
Wanaosema mada zangu ni ndefu, sioni wakilalamikia mada ndefu za Udaku na masimulizi ya uzinzi na uasherati.
Mt 5:6
Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa
Hata mimi hujaona malalamiko yangu?
 
Leo, jina lako lina-trend katika jukwaa lipi? La Siasa, la Habari na Hoja Mchanganyiko au International Forum?

Ukitubu leo na kuamua kuokoka, jina lako lita-trend mbinguni. Na huko sio ku-trend tu, itakuwa Breaking News itakayowafanya malaika wote washangilie.
Luka 15:7
"Kadhalika nawaambieni, ndivyo kutakavyokuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya kutubu kwa mwenye dhambi mmoja, kuliko kwa ajili ya watu tisini na tisa wanaojiona kuwa wema, wasiohitaji kutubu.”

Mnaosema mada zangu ni ndefu, hamuwezi kusoma mpaka mwisho, semeni sasa: na hii mmeshindwa kuisoma mpaka mwisho au huwa ni geresha tu 🙂
Hii naisoma na naielewa.....neno la toba ni uzima
Sio wale wa kuhubiri ujumbe wa kutoa tuu wanasahau mahubiri ya to toba ya msamaha
 
Pole sana, kama huo uzi hujauelewa labda huu utakusaidia
Mama Bikira Maria kimbilio letu
 
Biblia haituambii tumkimbilie Bikira Maria. Kimbilio la kweli ni Yesu pekee. Maria mwenyewe alimhitaji Mwokozi (Luka 1:47), na aliwaambia watu wamtii Yesu, sio yeye (Yohana 2:5).
Nguvu ya makimbilio yetu mama Maria
 
Leo jukwaani kwa mwamposa
Dah, ume-trend jukwaani? Ulikuwa unafundisha somo hii?
 
Dah, ume-trend jukwaani? Ulikuwa unafundisha somo hii?
Kusikiliza upako kidigiti
 
1 Yohana 1:8
“Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo ndani yetu.”

1 Yohana 1:10
“Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo, wala neno lake halimo mwetu.”

kila mtu ana dhambi, na kudai huna dhambi ni kujidanganya.
Hayo Maandiko yanawahusu watu ambao bado hawajatubu dhambi kama Binti wa zamani na secretarybird
Mimi ungeninukulia Maandiko haya ningekuelewa:
1 Yohana 3:6, 9
"Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu."


Zab 16:3
"Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao."

1 Wakorintho 6:11
"...tumeoshwa, tukafanywa watakatifu, na kufanywa waadilifu na kupatanishwa na Mungu kwa Jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu."
 
Hayo Maandiko yanawahusu watu ambao bado hawajatubu dhambi kama Binti wa zamani na secretarybird
Mimi ungeninukulia Maandiko haya ningekuelewa:
1 Yohana 3:6, 9
"Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu."


Zab 16:3
"Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao."

1 Wakorintho 6:11
"...tumeoshwa, tukafanywa watakatifu, na kufanywa waadilifu na kupatanishwa na Mungu kwa Jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu."
Kwahiyo wewe dada mtakatifu hauna dhambi?

Anyway, mi nilishakuambia kwamba nina seat yangu kwa kaka Satan sitaki kufufuka wala kuishi milele huko mbinguni kwenu.

Ningesema mengi yasiyofaa kuhusu dhambi, ila kuna kaka mlokole humu tunaheshimiana, hiyo respect naiextend na kwako on his behalf.
 
Leo, jina lako lina-trend katika jukwaa lipi? La Siasa, la Habari na Hoja Mchanganyiko au International Forum?

Ukitubu leo na kuamua kuokoka, jina lako lita-trend mbinguni. Na huko sio ku-trend tu, itakuwa Breaking News itakayowafanya malaika wote washangilie.
Luka 15:7
"Kadhalika nawaambieni, ndivyo kutakavyokuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya kutubu kwa mwenye dhambi mmoja, kuliko kwa ajili ya watu tisini na tisa wanaojiona kuwa wema, wasiohitaji kutubu.”

Mnaosema mada zangu ni ndefu, hamuwezi kusoma mpaka mwisho, semeni sasa: na hii mmeshindwa kuisoma mpaka mwisho au huwa ni geresha tu 🙂
Mkuu salama?
SamalaizI tujue unaongelea trendi ipi, msije mkawa mna tredi foreksi kimyakimya
 
Kwahiyo wewe dada mtakatifu hauna dhambi?
Sina dhambi. Nilitubu dhambi zangu siku nyingi zilizopita.
Anyway, mi nilishakuambia kwamba nina seat yangu kwa kaka Satan sitaki kufufuka wala kuishi milele huko mbinguni kwenu.
Jamani, Binti wa zamani umenisikitisha sana kuongea hivyo. Maneno yako yanadhihirisha vita vya kiroho vinavyoendelea ndani yako. Yesu hakufa kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wenye dhambi kama wewe (Warumi 5:8). Zawadi anayokupa Mungu ni zawadi ya uzima wa milele, na inawezekana ukaipokea zawadi hiyo leo kabla hujachelewa.

Kusema kuwa una 'seat' kwa shetani ni kama kujisainia hukumu ya kifo mwenyewe. Mkatae shetani, hakufai — ni mwongo na muuaji. Badala yake, amua kukaa kwa Yesu. Yesu ndiye aliyetufia, akashinda kaburi, na anatupa tumaini la kweli.

Bado unayo nafasi ya kubadilisha uamuzi wako. Maadam hujafa, mlango wa rehema bado uko wazi.

Mada yako ya hivi majuzi umezungumzia "raha" uliyopata maishani. Raha uliyopata ni ya muda mfupi tu. Sasa kwanini unakataa raha ya milele aliyotuandalia Yesu? Kwanini uchague kukaa na shetani jehanamu kwenye mateso ya milele? Mkatae shetani, ni mwongo. Yeye mbingu anaijua. Alikuwa malaika huko mbinguni. Alipoingiwa na kiburi akafukuzwa huko; ndio sababu anatuonea wivu. Anatudanganya tumkatae Yesu ili tusiende mbinguni. Mkatae shetani kwa Jina la Yesu, sasa.

Leo, ikiwa mtaisikia sauti yake[Yesu], msifanye migumu mioyo yenu.” — Waebrania 3:15
Ningesema mengi yasiyofaa kuhusu dhambi, ila kuna kaka mlokole humu tunaheshimiana, hiyo respect naiextend na kwako on his behalf.
Asante Binti wa zamani kwa kujizuia kusema yasiyofaa. Mungu akubariki na akupe moyo wa toba.

Sasa kama umekubaliana na hayo niliyokuambia, omba sala ifuatayo, Mungu atakusamehe na kukuokoa; na Yesu akirudi utakuwa miongoni mwao watakaonyakuliwa kwenda mbinguni kwenye furaha na raha ya milele.

Fuatisha sala hii ya toba kwa moyo wako wa dhati, utaona mabadiliko ndani ya moyo wako sasa hivi, na kiu ya dhambi itakatika ghafla. Omba hivi:

"Ee Mungu Baba, nimetambua mimi ni mwenye dhambi. Leo nakuja mbele zako nikiomba msamaha wako. Natubu dhambi zangu zote. Nimeamua kuziacha kabisa. Nakiri kuwa Yesu Kristo ni Bwana, na Yeye ndiye Mwokozi wa ulimwengu. Yesu karibu moyoni mwangu utawale maisha yangu kuanzia leo. Naomba unipe nguvu ya kushinda dhambi na kuishi maisha matakatifu. Namkataa shetani na uongo wake wote. Asante Yesu kwa kuniokoa. Katika Jina la Yesu Kristo, ninaomba na kushukuru. Amen.”

Kama umeomba sala hiyo kwa moyo wako wa dhati, tayari umeokoka. Anza kusoma Biblia kila siku na kumuomba Mungu akusaidie kuishi maisha ya utakatifu. Tafuta pia Kanisa lolote linalohubiri wokovu na kufundisha utakatifu, ujiunge nalo, watakupa msaada zaidi wa jinsi ya kuendelea kiroho.

Mungu akutunze, akufunike kwa ulinzi wake, sasa na hata milele. Amen.
 
Back
Top Bottom