Jihadhari na mtu usiyemjua anayekushobokea

Jihadhari na mtu usiyemjua anayekushobokea

Tahadhari tumepewa,

Habari zenu mabibi na mabwana! Poleni na majukumu,

Napenda niwashirikishe jambo lililo nikuta ili kukuokoa wewe au mwingine. kuna wizi wa ajabu wa aina fulani ya madawa ya kupoteza ufahamu.

Jana nikiwa natoka kazini mida ya jioni nikapita Mlimani City. Baada ya kufika Mlimani City ghafla nilisikia mtu akiniita jina langu nilipogeuka nilimuona mtu akinichangamkia sana na kuniuliza habari za siku, uko wapi zikuhizi? Nikawa nimepigwa namshangao mana nikimuangalia simkumbuki kabisa anae nichangamkia. Mara yule bwana akanisogelea na kuniambia hunikumbuki tulisoma wote? Kabla sijamjibu Mara akatokea mtu mwingine kama wanafahamiana wakachangamkiana kisha yule bwana akaanza kunitabulisha kwa huyu bwana alietukuta pale.

Ghafla yule bwana akaniambia kuna mdudu kwenye jicho lako la kulia nilipotaka kutoa akaniambia samahani naomba nikutoe kama hutojali. Kabla sijamruhusu akachukua kitambaa chake akanipangusa nacho kwenye jicho na puani. Gafla nikaanza kujisikia vibaya na baada ya hapo sijajielewa tena mpaka nilipojikuta niko hospital Rabininsia Dar.

Nikaelezwa kuwa nimepelekwa hapo na wasamaria wakiwa wameniokota maeneo ya Vikawe nikiwa sijitambui pembezoni mwa barabara. Nilikuwa na pesa kama laki 320000 walichukua pamoja na card yangu ya crdb. Cha ajabu nilipotoka hospitali nikaenda moja kwa moja bank nikawaelezea wakaniambia nikaripoti police.

Kabla hawaja iblock ile card waliniangalizia balance wakakuta card imetoa pesa ATM mbili Jana na Leo sh. milioni 2. Tulipofatilia kwenye ATM mojawapo ya Jana yake ikakuwa aliezitoa hizo pesa ni mimi mwenyewe nikiwa na mtu alikuwa ameficha sura yake na kwenye ATM ya pili ikakutwa ni yule mtu aliye ficha sura yake.

So my Dear friend, usimruhusu mtu yeyote usiyemjua kukugusa au kukutoa kitu machoni. Maana si kukuibia tu bali wanaweza kukulewesha na wakakufanye vitendo vya wakakuingilia vibaya wakakuambukiza hata magonjwa hatari.
Pole mkuu
 
dolame, ndivyo inavyoitwa, hawa jamaa wapo wengi hasa magomeni..yupo dada mmoja walikaa nae wiki nzima, wanaenda nae, wanatoa pesa kisha wanarudi nae ghetto, mbaya zaidi walikuwa wakimwingilia pia, mpaka pesa zilipoisha walienda kumtupa Tegeta....
 
Hii mada imeshaletwa hapa jukwaani mkuu uwe una search kabla ya ku-post kiongozi.

Ahsante.
dah si ungempa hata pole kwa yaliyomkuta kwanza? kukimbilia kumshambulia unaona sawa? sasa hasinge post hata mimi nisingejua maana sikuwahi kuiona hiyo mada unayorejea.
 
Mkuu mimi namjua mtu kafanyiwa hivi hivi juzi kati, hawa jamaa sijui wanakupa nini yaani kaibiwa kila kitu na pesa alienda bank kutoa mwenyeww
 
dolame, ndivyo inavyoitwa, hawa jamaa wapo wengi hasa magomeni..yupo dada mmoja walikaa nae wiki nzima, wanaenda nae, wanatoa pesa kisha wanarudi nae ghetto, mbaya zaidi walikuwa wakimwingilia pia, mpaka pesa zilipoisha walienda kumtupa Tegeta....
very sad.
wanachuma dhambi Na laana pia
 
mimi ndio nimeuona huu uzi leo na pia sioni tatizo kama huu uzi ulishakuwepo kabla kwani kila cku kuna member wapya humu ndani
Uko kama mimi ....huu uzi mi sijawahi kukuona na namshukuru bujibuji kuuleta! Wengine tusingejua!
 
Hiki kitu kimenipata wiki mbili zilizopita, namshukuru Mungu waliniacha salama tu, hata mtu aniulize nilipewaje hizo dawa sikumbuki zaidi nilikuwa naongea na mtu niliyesoma naye Chuo mara ya mwisho.
Mmmh mkuu ilikuwaje...plz nimegee kidogo ili kujihadhari
 
Hii mada imeshaletwa hapa jukwaani mkuu uwe una search kabla ya ku-post kiongozi.

Ahsante.
Sio kila kibachopostiwa hapa kila mtu anakioni mkuu. Mi mwenyewe nashukuru kwa kuiona post ya huyu jamaa.
 
Back
Top Bottom