Omulangi
JF-Expert Member
- Feb 12, 2008
- 1,036
- 265
Wiki iliiyopita tarehe 10 kitongojini Kashebeya, Kijiji Kaibanja, Kata Kaibanja wilaya Bukoba vjijini katika familia moja ya mzee Bagandanshwa kulikuwa na arusi. Vijana wake 3 walifunga ndoa. Wanakijiji wakaamua kusherehekea arusi hadi usiku na disco la Bwana Fokas toka Bukoba mjini. Km kama 6 tokea hapo kijijini kuna seminari ya kiislamu inayoitwa Katoro Islamic Seminari iliyopo eneo la Mujuga. Vijana wakatumwa kwenda kuudhibiti ukafiri. Wakaingia kijijini Kashebeya waka round up watu na kuwapa kichapo cha sawa sawa kwa fimbo na mawe. Kisha wakavunja vunja vyombo vya muziki na kutokomea. Ila katika kukimbia mmoja akakamatwa na akafikishwa kituo cha polisi Katoro. Kijana ni mzanzibari akakiri kuhusika katika tukio kwa agizo la Mkuu wa shule. Kijana akaongeza kuna hela nyingi zimetolewa kwa shughuli hiyo. Mara kwa mara vijana hawa wa seminari wamewapa walevi kichapo katika vibaa vya kijiji kama walivyofanya Kayoro mwaka jana, wamewahi kuvunja vyombo vya disko tena kwani wanadai ni ukafiri. Waliwahi kutaka kuchoma moto nguruwe aliyechinjwa Kakoronto. Kuna habari za kusadikika kuwa wanajifunza pia kutumia silaha!!!