Jicho la tatu: Wapinzani waliokosa Ubunge kuingia katika mtihani wa kupewa Teuzi Serikalini ili wasaliti vyama vyao lengo likiwa kuua upinzani

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Napenda kuwaleza mapema juu ya utabiri wangu huu ili yakianza kutokea msishangae na pengine kufadhaika bali mjipange kuyapokea yatayotokea.

Katika kutekeleza makakati/mpango huo,wanaoweza kuwa wanasiasa wa mwanzo kushawishiwa kukubali teuzi hizo ni watu/wanasiasa kama Prof.Jay, Sugu, Msigwa na wengineo ambao wanaweza kupewa vyeo kama U-RC, U-DC,U-RAS n.k.

Watu kama Lema na Mdee itakuwa vigumu kuwashawishi ingawa nao wanaweza kufuatwa kwa lengo hilo hilo la kuwataka wakubali teuzi.

Huu kwao utakuwa ni mtihani kwani kwa sasa hawana ubunge na pia hiki kitakuwa kipimo cha wao kusimama na vyama vyao na zaidi kusimamia msimamo wao kuwa Uchaguzi hakuwa halali(haukuwa huru na wa haki) kwani kukubali uteuzi maana yake umekubali kuwa aliekuteua alishinda kihalali na hivyo unakubali kuwa uchaguzi ilikuwa huru na wa haki.

Mbowe, Lissu na Zitto wanaweza kuwa treated tofauti ili kurudisha Umoja wa Kitaifa kwa lengo la kutuliza kama sio kumaliza kabisa kelele za nchi wahisani juu ya uchaguzi huu ambapo hata kesi zinazowakabili zitafutwa.

Mbowe na Lissu kupewa teuzi hizo sio rahisi kwani ni vigumu kwa wao kukubali hizo nafasi(hata wakipewa ubalozi bado watakataa) labda zitto ingawa hata nae sio rahisi kukubali.

Kuhusu Zitto,kama chama kitamruhusu Maalim Seif na yeye mwenyewe akakubali kuwa makamu wa Rais huko Zanzibar, basi tunaweza pia kufikiria uwezekano wa Zitto kupewa ubalozi ila ajue tu kama ikitokea hivyo na yeye akakubali, huo ndio utakuwa mwanzo wa yeye na chama chake kujimaliza kisiasa.

Malengo yatakuwa ni matatu: kupoza wahisani, kujaribu kurudisha Umoja wa Kitaifa na kupoza hasira au machungu ya dhuluma za Uchaguzi na tatu ni kuendeleza mkakati wa kudhoofisha upinzani kwa wataokubali uteuzi.

Tunaingia katika awamu nyingine ngumu zaidi kwa upinzani na silaha pekee ya kushinda vita hii ni kuzishinda kwanza njaa zetu maana njaa kila mtu anayo ingawa kila mtu na kiwango chake.

Hard times for opposition is not yet over.

Time will tell.
 
Sio rahisi kihivo ni Hadi wawe na akili badala ya nguvu.
Wapewe teuzi Hali wajiandae kutembelea ndala maaana hizo Kodi wazitegemee kwenye bness zao. Kuanzia kesho ni siku ya uchungu, vilio, mateso na dhiki kwa watz
 
Na kwa kuwa wapinzani wapo kwa ajili ya matumbo yao,hawatokataaa kabisaaaa kwenda kutumbua maisha
Napenda kuwaleza mapema juu ya utabiri wangu huu ili yakianza kutokea msishangae na pengine kufadhaika bali mjipange kuyapokea yatayotokea.

Katika kutekeleza makakati/mpango huo,wanaoweza kuwa wanasiasa wa mwanzo kushawishiwa kukubali teuzi hizo ni watu/wanasiasa kama Prof.Jay, Sugu, Msigwa na wengineo ambao wanaweza kupewa vyeo kama U-RC, U-DC,U-RAS n.k..
Kumbuka wapinzani wao Ni CCM-B
 
Napenda kuwaleza mapema juu ya utabiri wangu huu ili yakianza kutokea msishangae na pengine kufadhaika bali mjipange kuyapokea yatayotokea...
Huu ni unabii na utatimia.
Roho wa Bwana aliyekuwa anasema nami ndani yangu alitokaje akaja kusema na wewe!
HAYA NI MAONO TOKA KWA MUNGU

Huyu hana nia njema na upinzani
Ee! Mwenyezi Mungu tusikie kilio chetu,na utuondolee dudu hili baya kabisa kuwahi kutokea ulinwenguni!
 
Siamini kama mchungaji msigwa anaweza kukubali teuzi ya Jiwe la pembeni.
 
Akifanya hivyo ndiyo atazidi kukizamisha chama cha ccm maana wengi watakosa teuzi, kwahiyo migogoro itakuwa mikubwa zaidi vile maccm yamepambana yakijua yatapata teuzi! lakini wanaletwa wengine nakupewa nafasi zao tena ni wale waliokuwa wakiwadhihaki.
 
Sidhani kama ataweza kugusa wanasiasa toka Chadema, hicho chama anakichukia, hapendi hata kukisikia, sababu watu wake wanajielewa, hawataki kuburuzwa na kusifia hovyo.

Kama akifanya hivyo, basi atawatafuta wale "soft" kama Prof J na Mnyika; lakini sio kina Lema, Sugu, Heche, na Mbowe, huko hagusi, na akigusa ataumbuka.

Wapinzani halisi hawatakiwi kamwe kukubali cheo chochote toka CCM, wakikubali watajitia doa ambalo litakuwa gumu kufutika, wananchi watapoteza imani nao, kama Mbatia anavyoonekana sasa, hivyo itakuwa ngumu kwao kugombea kupitia upinzani na washinde next time. Kwasasa watafute vitu wafanye, come 2025 warudi kugombea tena, bado wataaminiwa na wapiga kura.

Nikutoe wasiwasi, upinzani wa kweli nchi hii hauwezi kufa, walifanya mikutano wenyewe nchi nzima kwa miaka mitano, wakanunua wapinzani wepesi, lakini bado kwenye uchaguzi wakatengeneza rundo la kura feki lililowarudisha madarakani, mikoa yote ambayo ni ngome ya upinzani itarudi upinzani come 2025, kwa hilo sina shaka labda watengeneze kura feki nyingine.
 
Mkuu Salary Slip , kwanza asante kwa objectivity kwenye uchambuzi wako, maana kwenye hii jf ya sasa, wachambuzi mahiri ni adimu sana.

Kwa kuanzia nauponda uchambuzi wako kwa Halima Mdee, kufuatia aggregate ya kura za ubunge na urais, chama kilichopata zaidi ya asilimia 5% ya kura zote, kinapata nafasi za wabunge wa viti maalum, hivyo Chadema itavuna nafasi kama 5 au zaidi, hivyo Mdee atarejea Bungeni.

Hili la wapinzani kuteuliwa, lengo sio kuudhoofisha upinzani bali wapinzani watakao teuliwa ni uteuzi wa aina tano
1. Wapinzani moderates waliogombea urais ili tuu kuonekana, hawa walimuunga mkono JPM na kuonyesha wako tayari kuunga mkono juhudi hivyo Queen Sendiga na yule mgombea urais mdogo kuliko wote, watateuliwa.

2. Wapinzani puppets - Hawa ni wapinzani 00
query oilambao wako upinzani kwa vile upinzani upo, lakini ni wapinzani puppets wa CCM na Magufuli, hawa ni kama Mbatia, Lipumba, Mrema, Cheyo etc.

3. Wapo wapinzani ambao ni good ones and assets, wako upinzani in a wrong way, huko upinzani they are just wasting their precious time, watateuliwa ili tu put uwezo wao to a good use. Huo ni uteuzi wa watu kama Dr. Kitila Mkumbo, hivyo ndani ya upinzani bado kuna some good assets, ambazo bila kuingia Bungeni it's a waste kama JJ.Mnyika, hawa wanaweza kuteuliwa kumsaidia Magufuli.

4. Kuna Wapinzani wanateuliwa just to save their faces, wasiumbuke. Hawa ni wapinzani ambao ni spent force, they have no value to add, lakini wanateuliwa kuwanusuru na kufulia, hivyo mtu kama Mrema au Cheyo akiteuliwa ni just saving faces. Hata Dr. Slaa ameteuliwa kundi hili baada ya kutangaza anashindia mihogo hadi kuitwa Dr.Mihogo!, kule Toronto akaajiriwa kibarua kubeba box super market, huku ni kumdhalilisha na hivyo ameteuliwa saving his face.

5. Uteuzi wa wapinzani kuimarisha upinzani. Baada ya CCM kushinda ushindi wa kishindo katika uchaguzi Mkuu huu uliokuwa huru na wa haki, Watanzania wamewakataa wapinzani na kuichagua CCM kutokana na kazi nzuri ya JPM, Bunge la sasa ni CCM dominated, Bunge hilo litabore na kukosa msisimko kwenye mijadala, hivyo tumependekeza, wapinzani wachache ambao ni wapinzani wa kweli, wateule ili kuimarisha upinzani Bungeni na kuleta msisimko, hawa ni wapinzani kama Zitto, Lissu, Heche, Bulaya, JJ.Mnyika etc

hivyo uteuzi wao sio kudhoofisha upinzani bali kuimarisha upinzani!.
P
 
Magu anajua kutandika watu vibao, akifanikiwa tu jua 2025 CCM watapita kirahisi sana tena. Na kiukweli mtu kama Msigwa, Prof J, Sugu and the likes wakipewa RC au DC hawachomoi, wapinzani wote wana price tag hadi Mbowe na Lissu , wote wana price tag.
Kijana alieleta uzi atakuwa mmoja wa waliotandikwa ktk uchaguzi huu na kumpelekea msongo wa mawazo. Na ndio maana kila asubuh, mchana, jioni au usiku analeta uzi zisizokuwa na maana hapa jukwaani ili kuuchafua mfumo wetu mzuri wa demokrasia uliotumika kumchagua raisi, wabunge na madiwani. Ila pa1 na yote hii haimsaidii yeye wala wenzie na ndiomaana wachangiaji wa nyuzi zake siku hizi wamekuwa wachache, hii inamaana wengi wanampuuza
 
Ni kweli kabisa mkuu...mm mtu ambaye sina Imani nae Sana....Ni katibu mkuu wa sasa wa Chadema....naona kama amekaa kwa kuegesha tu... Naona kama ataunga juhudi wakati wowote....tatizo kubwa Africa....siasa pia ni kazi ya kudumu.
 
Mkuu Salary Slip , kwanza asante kwa objectivity kwenye uchambuzi wako, maana kwenye hii jf ya sasa, wachambuzi mahiri ni adimu sana.

Kwa kuanzia nauponda uchambuzi wako kwa Halima Mdee, kufuatia aggregate ya kura za ubunge na urais, chama kilichopata zaidi ya asilimia 5% ya kura zote, kinapata nafasi za wabunge wa viti maalum, hivyo Chadema itavuna nafasi kama 5 au zaidi, hivyo Mdee atarejea Bungeni...
Sioni sababu ya CCM kushinda kwa hila halafu waje kuwateua wapinzani wanaojielewa ili "wakasisimue" bunge, mlitengeneza kura feki ili mkajaze lile bunge kwa ulafi wenu, sasa "kasisimuaneni" wenyewe.

Kuhusu Dr. Slaa, natumai lumumba wengine nao watasoma na kuelewa ulivyom-describe, halafu waache zile kelele zao.
 
Halafu ndio mlikua mnahamasisha vijana wa watu waingie road kuandamana kwa maslahi ya matumbo yenu,

Vijana wa Kitanzania msikubali kutumiwa na hawa wanasiasa hawajali kuhusu leo yenu wala kesho yenu, wanaajiangalia wao na familia zao,

Tanzania ni ya wachache, kama umetoka kwenye familia isiyojulikana ni vema kujipinda utoboe kivyako.
 
Sisi tunawasikitikia nyinyi ambao mnadhani upinzani ni itikadi wakati wenzenu ni fursa za kuishi hapa duniani.

Bado utagundua mengi zaidi, pole mkuu.
 
Back
Top Bottom