JF member tupeane pole na kufarijiana kwa kuambiana siku yako ilikuwaje

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Mar 10, 2022
17,796
32,148
Hello habari,

Nimeona niadhishe hii thread kwasababu watu wengine siku zao zinakuwa mbaya wanakwazika lakini hawana watu wakuwapa pole hawana watu wakuwafariji au ata kuwapa ongera kwa hatua waliyo fikia kwa siku hiyo.

Nianze na mimi;

Mimi siku yangu ilikuwa mzuri sana lakini ilikuja kuvurugwa na wageni ambao walinitembelea leo, lakini nimekaa poa sana.

Kwanini ilikuwa na furaha, kwasababu nilipata taarifa juu ya wageni hao na nilikuwa na shauku kitu kilicho nilalazimu kuingia mfuko kuwaanda wageni ili wafurahi sana.

Ujio wao ulikuwa ni kuja kumuona mjukuu wao, kwahio familia ikachagua sehemu nzuri ni kwangu kwasababu ya nafasi lakini pia ukaribu wa eneo ambalo wageni wanatokea.

Walifika, baada ya kufika nikaanda mashambulizi lakini chaa ajabu nawauliza ujio wenu hapa ni nini? Kama mjomba, kama kaka, hawajui kujieleza hata kidogo, kitu kilichonichefua sana. Baadae nikashusha hasira nikawapa utaratibu wafuate ,nikawapa mtoto wamuone kwa huruma zangu.

Tukafurahi nikawasindikiza, but nashukuru sana kwa siku ya leo. Je, wewe ilikuwaje siku yako leo?
 
Back
Top Bottom