JF Exclusive: The Buzwagi Contract

JF Exclusive: The Buzwagi Contract

4.3 Local Government rates and taxes shall not be:

4.3.1 in excess of those generally applicable on Tanzania, or

4.3.2 based on profit, turnover, sales or output from mining operations, or

4.3.3 based on the value of land used for the mine, mining infrastructure or installations,

provided that the aggregate of such local Government rates and taxes charged shall not exceed United States Dollars Two Hundred Thousand (US$ 200,000) in any one calendar year.


Katika mkataba mzima so far hakuna mahalai nimezimia kama kwenye hiki kifungu, hebu check this out, hebu naomba wakuu mksome tena hiki kipande halafu mtoe maana zake maana ziko nyingi sana za kutufanya wananchi na serikali yetu kuwa ni majuha!

Mkulu FMES..

hii ni moja ya sababu inayofanywa mikataba kama hii iwe siri na watu wasiruhusiwe kuiona.

Hapo hakuna kodi wala mapato ya serikali bali hiyo dola laki 2 ambayo haijulikani inaenda wapi so far.... jamaa wame-dictate hadi local govt.... hii ni kali!
 
Dah!
Kwa Mujibu wa maelezo ya kichuguu kwamba Mkataba huo tunaouona Hauna seal ya serikali. hivi serikali wakija na hoja kwamba huo mkataba tuliouona ni feki, ni uzushi wa wapinzani,na kwamba yeyote anayetaka kuona mkataba halali afuate taratibu zilizowekwa ataupata.
Hivi hii si inaweza kubadirisha upepo wa siasa kwa sasa?

Wanajua kuwa wakifanya hivyo watafungua front nyingine ya kuweka wazi mikataba yoooooote wanayoingia kila siku......

Sasa hivi draft zote za huu mkataba ziko mbioni ku-leak kwa hiyo kila siku utajua mengi sana kuhusu Buzwagi... hata wakibadilisha vipi bado wote utakuja tu hapa JF

Viva JF......... I love this forum
 
Nadhani ni uvivu wa kusoma na kufuatilia mambo ya nchi kwa undani na kwa uzalendo, kulisema taifa lako kwa mabaya sio jambo la kusheherekea, mbona Busha anaboronga vita ya Iraq lakini wananchi wake wako naye karibu;
Kwa mawazo yangu mimi nisiyesoma sheria kujadili taarifa ambayo taifa letu limesaini kwamba itakuwa ya siri sio jambo la kujivunia sana, ingawa sisemi kilichomo ndani ni kizuri ama la kwa kuwa sio mtaalamu wa madini wala wa sheria.

Kwa majibu ya swali lako yako hapa http://www.parliament.go.tz/Polis/PAMS/Docs/16-2004.pdf

Nenda moja kwa moja PART IV: Section 16; Title "Establishment of the National Economic Epowerment Fund

Tujaribu kuwa wazalendo kwa kutendea taifa letu haki kwa kusema mambo kwa research zaidi, kumbuka munayoandika hapa yatakaa kwenye computer za watu wengi wa maitaifa mengi, miaka na miaka... let no think you are chating with kilitime and it will end there!

Hili jambo nalifananisha na kukata tawi ulilokalia!!! Sisi ni Watanzania na Tutaendea kuwa watanzania aidha chini ya waziri X, au Waziri Y, au Waziri Z, au etc... so let be fair to our nation,

Kilitime,

Kama jina lako, inaonyesha ni kweli wewe una "kill time" tu hapa.
Bush gani unayemzungumzia?? kama ni Dubya basi mwenzio ni "lame duck president" na hiyo is NOT a good thing.
Kila nchi iliyoendelea wananchi wanaichachafya serikali yao hadharani!! mie sioni ubaya wa hatari kwa taifa,kwa hawa mafedhuli kukomwa nyani giladi...........muheshimiwa sana kama huna la maana la kuchangia,kama si mtaalamu wa sheria na masuala ya madini na kama pia mvivu wa kusoma maelezo marefu basi usije hapa na agenda zako za uzalendo fake....uzalendo wa kizamani, uzalendo wa zidumu fikra sahihi wakati unajua si sahihi. Kuwa cheerleader kwenye sidelines pia ina ruhusiwa, ngoja nikutafutie pongpong na kibwaya ili uweze kuwa hamasisha wakina mwanamke mwafrika na wengine wakituchambulia majambozi hapa!!!!!!!!.
 
Kilitime,

Kama jina lako, inaonyesha ni kweli wewe una "kill time" tu hapa.
Bush gani unayemzungumzia?? kama ni Dubya basi mwenzio ni "lame duck president" na hiyo is NOT a good thing.
Kila nchi iliyoendelea wananchi wanaichachafya serikali yao hadharani!! mie sioni ubaya wa hatari kwa taifa,kwa hawa mafedhuli kukomwa nyani giladi...........muheshimiwa sana kama huna la maana la kuchangia,kama si mtaalamu wa sheria na masuala ya madini na kama pia mvivu wa kusoma maelezo marefu basi usije hapa na agenda zako za uzalendo fake....uzalendo wa kizamani, uzalendo wa zidumu fikra sahihi wakati unajua si sahihi. Kuwa cheerleader kwenye sidelines pia ina ruhusiwa, ngoja nikutafutie pongpong na kibwaya ili uweze kuwa hamasisha wakina mwanamke mwafrika na wengine wakituchambulia majambozi hapa!!!!!!!!.

Matusi nimepokea kwa mikono yote, lakini soma content ya url niliyoweka! Wakati huo ukumbuke kwamba kuna part ambayo haitendewi haki, serikali yenu chachafyeni kadri mnavyotaka lakini part ya pili ya huo mkataba hamuwapi haki yao!
 
Matusi nimepokea kwa mikono yote, lakini soma content ya url niliyoweka! Wakati huo ukumbuke kwamba kuna part ambayo haitendewi haki, serikali yenu chachafyeni kadri mnavyotaka lakini part ya pili ya huo mkataba hamuwapi haki yao!

Jamani kilitime....

JF ni jamvi ambalo kila upande unaweza kuweka mambo yake hapa. Ulichoanza ni kizuri sana, hiyo link imetoa upande mwingine na imejibu maswali hapa.....

Itakuwa vizuri sana kama utaleta upande wa pili hapa na kuupatia haki hiyo unayosema badala ya kuanza tu kulaumu kuwa huo upande haujapewa haki....

Wewe ni memba wa JF na unaweza kabisa kutetea upande wako......
 
Nimeweka parts zote za article 4 maana ndiyo article inayohusu pesa na ndiyo inaonyesha Tanzania itapata nini toka kwa huu mkataba...

Articles zingine zitaendelea tena baadaye au kesho...

Thanks
 
Dada Mwafrika wa Kike na Alles,

Sina matatizo na kukosoa serikali, na sina matatizo na wanaosema mimi kweli na kili time nadhani wana maana mimi naponda muda tu,,, pia hiyo kwangu sawa.

Wasiwasi wangu ni kwamba Serikali yetu kuu, kwa niaba ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeingia mkataba mzuri/mbaya sijui, kwa sababu terms za negotiation sizijui, lakini imeingia mkataba na Mwekezaji tena sio mwekezaji wa mfukoni hapani ni kampuni linalotambulika ulimwenguni...

Sasa sijui lakini generally mikataba hii wakisaini ni ya siri, sio kwamba serikali tu ndiyo inapenda mikataba iwe siri lakini mwekezaji yeyote ikiwa pamoja na wale waliokuwa wanasupply mchicha kwenye mashule ya sekondari na magereza enzi zile... sasa leo hii mkataba unawekwa hadharani ati kwamba tunaikosoa serikali... wakati huo tujue hatumtendei haki mwekezaji ambaye hana hatia yoyote...

Hayo ndio maoni yangu tu... mimi ninaye kili time!

Wakati huo huo tukumbuke kwamba ni kosa kutoa report au makabrasha ya mtu/taasisi bila ridhaa yake,,, nadhani kama umefakiwa kuipata kwa njia ambayo unaijua mwenyewe si vyema kuisambaza kama hivi,,, maoni yangu tu kama mzalendo halisi wa taifa hili changa, ambalo linahitaji upendo zaidi ili kutoka kwenye dimbi la umaskini...

Ningekuwa mwekezaji ambaye nataraji kuja hapa,,, ningefikiria mara mbili kama mikataba itakuwa inafanyikwa kama tunavyofanya, naombeni sana tuangalia mambo kwa mbali zaidi, tusiangalie kwa nia ya kuongoza nchi, kesho itakuwa UDP, CHADEMA etc... lakini taifa ni hili hili
 
Matusi nimepokea kwa mikono yote, lakini soma content ya url niliyoweka! Wakati huo ukumbuke kwamba kuna part ambayo haitendewi haki, serikali yenu chachafyeni kadri mnavyotaka lakini part ya pili ya huo mkataba hamuwapi haki yao!

Kila siku mie naamini mijadala ya hapa JF ipo "fair and balanced" kama Fox News Channel kwikwikwikwi. So huo upande wa pili hoja zao ziwapi? Wao wamewatendea waTZ haki gani?...in away its like pay back time,Karamagi ana haki sawa ya kuface vyombo vya habari na kujibu mapigo kama hilo anaona gumu basi aibuke JF ajibu mapigo!!!. ndugu yangu hata siku moja uwezi kumtendea haki asiye kutendea haki.............na amini kwamba watu wengi wanao usasambua mkataba huu ambao so far nadhani ni one of many blunders and nightmares kwa taifa letu ni wazalendo tena pengine kushinda wewe.
Nakuomba usome ulichoandika hapo juu kwa sauti na ujisikilize mwenyewe, utaona kwamba upo over the boiling point!!!!!!!! I'm sorry to say...
Muwekezaji gani? kama ni Barrick, basi think again.
 
Ukiona mtu mzima anaria ujue kuna jambo.Hapa mimi naona dawa ni civil dis-obedience tu iri kiereweke,mengine haya ya kusema ooh subiri 2010 huku watu wanazidi kukandamiza mikataba ya aina hii tutacherewa!!
Poleni mura
 
kweli kara ametuuza hadi wajukuu wake hawana chao. angekuwa mungwana angejiuzulu hivi amesoma akaelewa anayo saini? ninavyo muonaga Ngonja wa wizara ya fedha anavyo anguka ma sahihi sidhani naye kama anasoma au anafanya kwa mazoea ya kuwahi kama kara. kweli hao watu ni mafisadi tena wahujumu uchumi wetu.
 
Dada Mwafrika wa Kike na Alles,

Sina matatizo na kukosoa serikali, na sina matatizo na wanaosema mimi kweli na kili time nadhani wana maana mimi naponda muda tu,,, pia hiyo kwangu sawa.

Wasiwasi wangu ni kwamba Serikali yetu kuu, kwa niaba ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeingia mkataba mzuri/mbaya sijui, kwa sababu terms za negotiation sizijui, lakini imeingia mkataba na Mwekezaji tena sio mwekezaji wa mfukoni hapani ni kampuni linalotambulika ulimwenguni...

Sasa sijui lakini generally mikataba hii wakisaini ni ya siri, sio kwamba serikali tu ndiyo yakupenda mikataba iwe siri lakini mwekezaji yeyote ikiwa pamoja na wale waliokuwa wanasupply mchicha kwenye mashule ya sekondari na magereza enzi zile... sasa leo hii mkataba unawekwa hadharani ati kwamba tunaikosoa serikali... wakati huo tujue hatumtendei haki mwekezaji ambaye hana hati yoyote...

Hayo ndio maoni yangu tu... mimi ninaye kili time

Kilitime, kuna mikataba inayohusu taifa ambayo usiri wake si wa lazima. Usiri wa mikataba unakuwepo wakati wa majadiliano na mazungumzo ya awali (ndivyo inavyofanyika sehemu nyingi duniani). Lakini mnapokaa chini kusaini mkataba basi mkataba ule unakuwa ni mali ya umma kwani unahusu maslahi ya watu na ni wananchi wenye uamuzi wa mwisho. HAIWEZEKANI hata kidogo serikali iingie mkataba na mtu, taasisi, au chombo chochote halafu ikatae kuuweka mkataba huo hadharani ili wananchi walioiweka madarakani wauone. Hilo linawezekana katika nchi ya kikomunisti au yenye utawala wa kiimla.

Baada ya kusema hivyo, nitoe shukrani za dhati kwa kutuwekea sheria iliyounda economic empowerment fund kwani imezidi kuthibitisha matatizo ya mkataba huo na mapungufu ya sheria zote mbili ya madini na hiyo ya Baraza la uwezeshaji.

Hapa ndipo palipo na mgongano:

4.1.3 for each year of production the amount of US$ 125,000
by 31st December of each calendar year a contribution
to the Empowerement Fund

Ni kwanini mchango wa kampuni hiyo katika uwezeshaji uwe ni Dola 125,000? Kama mkataba huu ndio umeboreshwa zaidi basi sina shaka kuwa michango ya makampuni mengine kwenye mfuko huo yatakuwa chini ya hapo.

Pili, Endapo kampuni ya madini inatengeneza faida (net profit) ya Dola milioni 20 kwa mwaka, dola 125,000 kutoka kwenye faida hiyo ni sawa na asilimia 0.0625 ya faida. Je hilo ni sawa? Kama kweli tutaweka kipengele kama hicho kwa miaka yote ijayo ya maisha mgodi huo hivi ni kweli mfuko wetu utafaidika?

Tatu, mwaka wa uzalishaji unaanza lini? Bila ya shaka ni baada ya faida kuonekana au kufikia kiwango fulani cha uzalishaji. Ina maana kwamba kama watazalisha bila kufikia kiwango cha uzalishaji kinachodefine "production year" ina maana wanaweza kujikuta wanachangia mara moja tu au mara mbili tu kabla maisha ya mgodi kuisha.

Kwanini serikali isianzishe mfuko wa tofauti kabisa ambao utachangiwa na sekta za madini na utalii na wenye lengo la kuendeleza makazi, miundo mbinu, na nguvu kazi.? na ukiongozwa na sheria tofauti kabisa?
 
waoooo hii statement imenimaliza kabisaaaaa...

Kama anavyosisitiza mwenyewe kwamba ana kill time.........labda investor mwingine he is talkin' about na sio hao barrick.
Barrick hawa-deserve kutendewa haki ya aina yoyote, kwani kutokana na maelezo mengi ya uchambuzi wa mkataba huo..hawa jamaa nia yao haikuwa nzuri na hawakututendea haki. Mazee basi mnunulia Ng'ombe wako chandarua asing'atwe na mbu!!!!!!!! They are animals,and deserve this kind of treatments(harsh and nasty). Beast amekuwa unleashed, thats what happen when humane fails!! Bro get real.
 
Nimeweka parts zote za article 4 maana ndiyo article inayohusu pesa na ndiyo inaonyesha Tanzania itapata nini toka kwa huu mkataba...

Articles zingine zitaendelea tena baadaye au kesho...

Thanks

Sasa sijui kesho ipi. Kwangu ndio kunakaribia kucha na ndio nimeamka. Well, nafurahi umetekeleza wajibu wako vema. Kila mtu yu huru kutoa maoni ili mradi asitukane. Mawazo ya Kilitime ni ya wengi walio upande wake hivyo ana haki kabisa ya kuitetea serikali kadiri ya uwezo wake. Ndio raha ya uhuru wa maoni!

Mkuu kilitime; uko right na huenda ukipewa maelezo ya ziada ukagundua uko right kabisa au ukagundua wapi ulikuwa hujaona ubaya wa serikali.

Serikali kama serikali haina makosa... Karamagi? Anamwakilisha nani? Mihuri aliipataje ya kwenda nayo London? Alipewa na nani ruksa ya kusaini mkataba huu nje ya ubalozi wetu?

BTW: Sahihi ya Karamagi ndiyo hiyo uionayo kwenye document. Binafsi nakuunga mkono mkuu kilitime... But we need to look into it DEEPLY!
 
Wakuu baadaye mkipata nafasi angalieni news kwenye channel 10, login www.jumptv.com, halafu utaona nchi nyingi tafuta bongo halafu bonyeza kisha upande wa kulia utaona channel mbili channel 10 na tv star ukuweka channel ten ni free watch, utapata news za leo,

wananchi wa Ifakara/Mahenge wakiwapiga maswali kama haya yetu hapa forum mawaziri wadogo Chikawe na Siame, kwenye mkutano wa hadhara, yaani utafikiri hao wananchi wa kawaida wanaingia hapa forum na maswali yao ya kuhusu madini,

I mean inatia moyo kuwa finally, wananchi bongo wameamuka kiasi hiki, kwa hiyo we are on the right track!
 
Ni kwanini mchango wa kampuni hiyo katika uwezeshaji uwe ni Dola 125,000? Kama mkataba huu ndio umeboreshwa zaidi basi sina shaka kuwa michango ya makampuni mengine kwenye mfuko huo yatakuwa chini ya hapo.

Hili hapa kwa uzoefu wangu mdogo na kwa sheria nyingi zilizotungwa, na kanuni mbalimbali zote utakuta zinaweka viwangu rigid/static na sio dynamic, kwa hiyo sishangai sana...

Mfano, faini ya kosa la barabarani liliwekwa miaka fulani kwamba ni sh. 20,000/- itaendelea kuwa hivyo labda kwa miaka kumi zaidi, mto akimtelekeza mtoto aliyemzaa kwenye nyumba ndogo/kubwa nikiwango cha kumtunza labda ni elfu 5000/- kwa mwezi kwa mfano; na mifano iko mingi,,, hii ndivyo wataalamu wetu walivyozoea hawataki kuweka dynamic number, mfano % of x, where x is probably net profit, x is revenue etc... kwa hiyo hata sheria nyingi zinamatundu haya haya mimi sishangai kwa hili kabisa,,, ingawa siungu mkono kuweka static figures,,, how much i can't know lazima niseme ukweli kwa kuwa sijui how much you invest in equipment, ukiwa ume-borrow from bank at what intrest rate na ukitegemea kuzalisha baada ya muda gaini


Pili, Endapo kampuni ya madini inatengeneza faida (net profit) ya Dola milioni 20 kwa mwaka, dola 125,000 kutoka kwenye faida hiyo ni sawa na asilimia 0.0625 ya faida. Je hilo ni sawa? Kama kweli tutaweka kipengele kama hicho kwa miaka yote ijayo ya maisha mgodi huo hivi ni kweli mfuko wetu utafaidika?

Kama nilivyosema ukipitia sheria nyingi utaona hili tatizo, na ukiniuliza nitasema ni tatizo la uvivu wa kufikiria la watanzania wengi, ikiwemo waandaaji wa mikataba, na ni kwa sababu mwanasheria ana-claim ajua accounts/mathematics etc.


Tatu, mwaka wa uzalishaji unaanza lini? Bila ya shaka ni baada ya faida kuonekana au kufikia kiwango fulani cha uzalishaji. Ina maana kwamba kama watazalisha bila kufikia kiwango cha uzalishaji kinachodefine "production year" ina maana wanaweza kujikuta wanachangia mara moja tu au mara mbili tu kabla maisha ya mgodi kuisha.

Nadhani wenzetu ni makini, na nawasifu kwa hili, kwa maana huwezi kulipa mikodi kabla ya kuzalisha, sasa watakapokuwa wanazalisha ndio watawalipa, sasa kama mtakuwa mumeajiri watu wanaopenda kula ambao hata uzalishaji ukianza watasema bado hilo ni tatizo la watanzania,,, kutoweka tarehe ni sawa kabisa maana in implementation kuna matatizo mengi yanaweza delay production


Kwanini serikali isianzishe mfuko wa tofauti kabisa ambao utachangiwa na sekta za madini na utalii na wenye lengo la kuendeleza makazi, miundo mbinu, na nguvu kazi.? na ukiongozwa na sheria tofauti kabisa?

Well hizi ni subject mbili tofauti, mfuko wa uwezeshaji unachangiwa na wengi sio migodi tu, sasa kuuweka ndani ya sheria ya madini is wrong...

Ni haki uwe-independent na uchangiwe na sekta mbalimbali na utakuwa rahisi kumanage na kwenye mambo ya kuuboresha itakapotakiwa
 
Kuna mwizi alim-sue mwenye Nyumba aliyotaka kuiba kwamba ka-trip kwenye ngazi na kuvunja mguu wake wa kuume....hiyo ilitokea wakati kakurupushwa na owner,mwizi anataka kulipwa gharama za matibabu,lost wages na maumivu.!!!
Barrick ni wezi na hivi sasa ndio wanakurupushwa, suala la kuwatendea haki ni kama vile mwizi niliyemzungumzia hapo juu, Je unadhani mwezi yule alifaa kulipwa?!!. Issue ipo wazi kwamba investors lazima walindwe na mikataba inatakiwa iwe siri..........lakini kama investor ni tapeli basi ataogopa haya yanayotokea kwa barrick na kinyume chake ni faida kwetu sisi waTZ.
 
Ningekuwa mwekezaji ambaye nataraji kuja hapa,,, ningefikiria mara mbili kama mikataba itakuwa inafanyikwa kama tunavyofanya, naombeni sana tuangalia mambo kwa mbali zaidi, tusiangalie kwa nia ya kuongoza nchi, kesho itakuwa UDP, CHADEMA etc... lakini taifa ni hili hili

Ungekuwa mwekezaji fair, usingeogopa hata kidogo. lakini kwa sababu mikaba ina kila aina ya ulaghai lazima mwekezaji ywyote aogope.

Pia kama faida yenyewe ndiyo hiyo, basi ni afadhali tuyaache madini yetu huko chini ili wajukuu zetu watakaokuwa na akili nzuri kuliko sisi wataingia mikataba fair. Maana sisi bado akili zetu ziko 1880, kipindi cha akina Karl peters.

Mikataba kuvuja ni sehemu ya watendaji walioko serikalini kuchoshwa na propaganda za viongozi huku wenyewe wakibaki choka mbaya. ukumbuke kwamba inawezekana wengine ndio hao wanaoshiriki ktk kuandaa hiyo mikataba, lakini at the end wao maisha yao hubaki pale pale huku akina Karamagi et al wakizidi kuwa mabilionea wakutupwa.

Kuna msemo usemao, ukitaka kufaidi vizuri, kula na wenzako vinginevyo hutafaidi kwa amani.
 
nilikuwa naangalia CNBC last night kipindi cha Jim Crammer...basi anakuambia green(dollar) is getting dumped so the best thing you can do wit ur portfolio ni gold na company to put your money ni XBF yaani Barric Gold maana ni one of the most profitable katika Dow Jones for the last five yrs na reason behind the profit akasema they have a new & huge gold mining somewhere in Africa(mwananangu hapo nikasikia click click click klak klak bongo hiyooooo karamagi katuuza)..kweli tungekuwa makini tungekuwa sawa na South Africa tuu lakini naona tumegeuzwa hapo kama waarabu na record profit in history ya Exxon Mobile kutoka kwa waarabu huku wenyewe wakifa kama kuku,haya mambo wazee sio joke angalieni Sierra Leone mambo ya Diamond,Congo gold,mafuta Nigeria ni kutokana na injustice ya mikataba kama hii ndio maana watu wanaingia msituni,i dont suggest tupigane lakini kutufunga na contract ya 50 yrs huku tukibaki na umaskini uliokithiri na mali ni yetu watu watachoka na kitakachotokea kila mtu anajua
 
Back
Top Bottom