JF Exclusive: Ka-Nzi kwenye kikao cha kampeni ya CCM, Busanda!

hakuna mtu anaweza akatuwekea minutes za aina kama hii wakati wa uchaguzi wa tarime,ili tujue hopes za wakati ule kama zinaendana endana na hizi?
 
mwanakijiji sijajua nia ya kuweka hizi minutes za ccm, hazina hoja kwa mtazamo wangu...na inawezekana wamelikisha maskudi kama shalom alivyohisi, kusambaza hii ni sawa na kuwasaidia kupiga kampeni tu, siumeona wanavyojifanya kujua matatizo ya kila eneo?

inaonekana mshindani mkuu ni chadema....
 
Kwa kuwa Zitto yupo humu sasa hivi, naamini ataangalia mapungufu yao(Sisiem) yalipo ili CHADEMA wayatumie kama silaha ya kuombea kura, hasa kwenye vipengele walivyoviita "KERO NA MATATIZO". Waangalie kila kata Sisiem iliona kero gani ili na wao wawaeleze wananchi ahadi hewa za Sisiem tangu 2005.
 
Rev. Kishoka,
Ikiwa hapa JF kuna asilimia 60 (hesabu ya kufikirika) hawaamini kuwa Rostam ni fisadi kwa sababu ati hakuna ushahidi.. Vipi wananchi wa Busanda wanaweza kufikiria kinyume!
Tukubali tu mkubwa yaishe.. NDIVYO TULIVYO!

Hili hadi hivi sasa linabakia kuwa ni jibu la mwezi!
 
Nimesoma majibu yote yaliyotolewa na watu mbalimbali kufuatia ripoti hii ya "kanzi".. Kuna kitu kimoja hata hivyo ambacho watu wanasahau au hawajazingatia umuhimu wake. CCM ni chama cha siasa.

CCM siyo shirika au kampuni fulani, ni chama chenye malengo ya kisiasa. Malengo hayo yanahitimisho moja tu nalo ni kutawala. Mambo mengine yote yanazunguka kwenye hilo moja.

Maana yake nini?
Maana yake ni kuwa CCM wana utaalamu wa kufanya siasa. Ndani ya CCM tangu enzi na enzi wamejifunza suala zima la propaganda na sanaa ya siasa. Tangu enzi za vita baridi CCM imepeleka makada wake Chezch, Yugoslavia, Romania, Urusi na hata Uchina na katika kilele cha kuwaandaa viongozi wake kilianzisha Chuo cha Chama pale Kivukoni (siku hizi kina shughuli nyingine nasikia).

Maana yake ni kuwa CCM kinaelewa maana ya siasa na mikakati ya siasa.

CCM hadi hivi sasa ukisoma vizuri utaona kuwa wame concede Katoro na na mji mwingine, kwenye makao makuu kama walivyofanya Kiteto mjini. Kura za CCM hazitatoka mjini bali vijijini.

Nilizungumza na Mbunge mmoja jana ambaye aliniambia kitu kimoja cha uhakika sana kuwa ushindi wao utakuwa ni wa asilimia 70! Akanieleza reasoning yao kuwa Chadema na CUF (ambao alisema nao wanapata wafuasi wengi tu) watagawana kura za mjini na CCM watakomba kura za vijijini ambako a. CCM inajulikana hata usingizini na b. wapinzani ndio wanaibukia wakati wa kampeni.

Kwa maneno mengine ni kuwa CCM wanajua wapiga kura wao; na hicho ndicho ripoti inasema. Kwamba, pamoja na matatizo yao yote hao wananchi kama yalivyoanishwa wao CCM bado wanaleta tumaini zaidi kuliko wapinzani. ni ya yale yale ambayo yametokea mijini ambapo watu wanaipigia kura CCM na siyo mgombea.

Zitto katika hotuba yake ile iliyowasisimua wengi alikuwa anajaribu kuwapa wana Busanda sababu nyingine ya kupiga kura. Lakini cha kusikitisha ni kuwa mara nyingi ushindi wa namna hii hautokei wakati wa kampeni ni kabla ya kampeni!

CCM wanalitambua hili vizuri na wana utalaamu wa kulifanyia kazi.

Hata hivyo, wapinzani wanahitaji kitu kidogo sana kuweza kubadilisha mwelekeo wa ushindi kwani wao wanahitaji kushinda angalau asilimia 50 za kura za vijijini na kushinda asilimia angalau 60 ya kura mijini basi ushindi utakuwa wao. Nje ya hapo, CCM wakishinda, nitakuwa mtu wa mwisho kushangaa.

Tusione umati kwenye mikutano tukatafsiri kura; vitu hivyo viwili havihusiani!
 
Nawashauri viongozi wa juu wa upinzani wagombee ubunge 2010 ili kuimarisha nguvu ya upinzani bungeni. Tatizo kila mmoja anataka awe rais ndio maana tunakuwa na imani haba kwao. aungwe mkono mmoja, wengine wapandishe nguzo ya ubunge. Or else tutaona nao tamaa tupu!
 
Hali halisi ccm base yake ni vijijini nitaendelea kuwa hivyo kwa muda. Nilichowahi kusema awali ni kwamba vyama vya upinzani vinahitaji kutafuta base ya wapiga kura wapya ambayo mimi nawaita watu wa kati.

Wengi wa hawa watu wapo mjini na kwenye vijiji mara nyingi huwa wananafasi fulani. Hii ni kada ambayo upinzani haitatumia pesa nyingi kuijenga kwani wao wanachotafuta ni matumaini ya mabadiliko. Kada hii pia inamuunganiko wake na watu wa vijijini kwahiyo itaunganisha chama. Pili vyama vya upinzani vihakikisha vinavuta wapiga kura wapya ambao hawajawahi kupiga kura - vijana na wafanyakazi.

Mwisho ndio ifuate hizo kura za vijijini. Kuchukua kura za vijijini sio lelemama, ccm wamejenga hiyo himaya kwa muda na kunasababu nyingi za kihistoria zilizofanya wafanikiwe. Lengo la upinzani liwe hata kupata asilimi 30 za kura za vijinini na kura asilimia 80 za mjini.

Kwa uchaguzi wa busanda swala lisiwe ushindi tu, liwe ni kujenga base ya upinzani. Kutumi resources za uchaguzi zilizopo kuweka mtandao wa vyama vya upinzani.
 
Nimesoma majibu yote yaliyotolewa na watu mbalimbali kufuatia ripoti hii ya "kanzi".. Kuna kitu kimoja hata hivyo ambacho watu wanasahau au hawajazingatia umuhimu wake. CCM ni chama cha siasa.

CCM siyo shirika au kampuni fulani, ni chama chenye malengo ya kisiasa. Malengo hayo yanahitimisho moja tu nalo ni kutawala. Mambo mengine yote yanazunguka kwenye hilo moja.

Maana yake nini?
Maana yake ni kuwa CCM wana utaalamu wa kufanya siasa. Ndani ya CCM tangu enzi na enzi wamejifunza suala zima la propaganda na sanaa ya siasa. Tangu enzi za vita baridi CCM imepeleka makada wake Chezch, Yugoslavia, Romania, Urusi na hata Uchina na katika kilele cha kuwaandaa viongozi wake kilianzisha Chuo cha Chama pale Kivukoni (siku hizi kina shughuli nyingine nasikia).

Maana yake ni kuwa CCM kinaelewa maana ya siasa na mikakati ya siasa.

CCM hadi hivi sasa ukisoma vizuri utaona kuwa wame concede Katoro na na mji mwingine, kwenye makao makuu kama walivyofanya Kiteto mjini. Kura za CCM hazitatoka mjini bali vijijini.

Nilizungumza na Mbunge mmoja jana ambaye aliniambia kitu kimoja cha uhakika sana kuwa ushindi wao utakuwa ni wa asilimia 70! Akanieleza reasoning yao kuwa Chadema na CUF (ambao alisema nao wanapata wafuasi wengi tu) watagawana kura za mjini na CCM watakomba kura za vijijini ambako a. CCM inajulikana hata usingizini na b. wapinzani ndio wanaibukia wakati wa kampeni.

Kwa maneno mengine ni kuwa CCM wanajua wapiga kura wao; na hicho ndicho ripoti inasema. Kwamba, pamoja na matatizo yao yote hao wananchi kama yalivyoanishwa wao CCM bado wanaleta tumaini zaidi kuliko wapinzani. ni ya yale yale ambayo yametokea mijini ambapo watu wanaipigia kura CCM na siyo mgombea.

Zitto katika hotuba yake ile iliyowasisimua wengi alikuwa anajaribu kuwapa wana Busanda sababu nyingine ya kupiga kura. Lakini cha kusikitisha ni kuwa mara nyingi ushindi wa namna hii hautokei wakati wa kampeni ni kabla ya kampeni!

CCM wanalitambua hili vizuri na wana utalaamu wa kulifanyia kazi.

Hata hivyo, wapinzani wanahitaji kitu kidogo sana kuweza kubadilisha mwelekeo wa ushindi kwani wao wanahitaji kushinda angalau asilimia 50 za kura za vijijini na kushinda asilimia angalau 60 ya kura mijini basi ushindi utakuwa wao. Nje ya hapo, CCM wakishinda, nitakuwa mtu wa mwisho kushangaa.

Tusione umati kwenye mikutano tukatafsiri kura; vitu hivyo viwili havihusiani!
Asante MMKJJ kwa tathmini yakinifu.
Tathmini kama hizi ndizo zinatakiwa kutumiwa na wanasiasa makini kuchukua ushindi. Pia zinatoa darasa safi kwa wanaJF wenye nia ya dhati kufuatilia mustakabala wa siasa za Tanzania na wakati huo huo, kuwafungua macho na masikio, wale mashabiki vipofu, na viziwi lakini sio mabubu, hivyo huishia kupiga kelele sana za debe tupu kushabikia siasa.
Nilisema Busanda ni CCM kwa wapinzani kushindwa kuungana. Na 2010 ni Jk tena kwa sababu hizo hizo.

Kama rafiki yangu Zitto bado yupo, namuhakikishia bado hawajachelewa kuunganisha nguvu na CUF na kuiteka Busanda.
Hakuna ubishi CCM ni weaker in Busanda na the dorminant ni Chadema na CUF ndio mafahali, hivyo mgombea wa CCM anaishia kuzoa kura zote za compasion na compromise ya wapinzani kutompa yoyote bora wampe mtu baki.
Prediction ya ushindi wa CCM ni asilimia 40%
Wakati Chadema na Cuf watanyanganyana asilimia 60%.
When will the opposition in Tanzania learn!?.
 
Nionavyo mimi data za ushindi zilizotolewa na makada wa CCM katika kikao chao zinatokana na shinikizo na vitisho kutoka kwa wakuu wao. Kutokana na hofu ya makada kupoteza nafasi zao katika kata wameona kheri kutengeneza data ili tu kuwaridhisha viongozi wao wa juu. Pamoja na kwamba baadhi ya wana JF hapa wanaona hizi data ni za kweli, binafsi siamini hivyo. Hizi data ni za kupigwa ili tu kuwaridhisha kina Mkuchika. Swali la kujiuliza, kama CCM inaona mambo ni shwari Busanda kwa nini wanakaa vikao usiku hadi karibu na asubuhi? Ni imani yangu kuwa huko Busanda CCM inaona ni maji marefu.
 
Hata hivyo, wapinzani wanahitaji kitu kidogo sana kuweza kubadilisha mwelekeo wa ushindi kwani wao wanahitaji kushinda angalau asilimia 50 za kura za vijijini na kushinda asilimia angalau 60 ya kura mijini basi ushindi utakuwa wao. Nje ya hapo, CCM wakishinda, nitakuwa mtu wa mwisho kushangaa.

Tusione umati kwenye mikutano tukatafsiri kura; vitu hivyo viwili havihusiani!

Mkuu yote uliyosema ni sahihi kabisa. Japokuwa wengi wa waliopitia pale Kivukoni hawako katika harakati zinazoendelea Busanda. Ila mbinu zinajulikana kwa wengi wao.

Upinzani siku zote ndio chachu ya CCM kushinda uchaguzi. Huwa hawaamini kuwa CCM ina mbinu safi tu za kshinda hasa baada ya kujidanganya na wingi wa wahudhuriaji kwenye vikao vyao. Watu wengi huudhuria kushuhudia jinsi wanasiasa wanavyoisema serikali na mwisho hubadilika wanapofikia karatasi ya kura.
 
Ajenda ya wiki hii ya mwisho kwa Chadema iwe "kura kwa CUF ni kura kwa ccm!"
 
Usipoona ya Musa ama kweli utaona ya Farao! yaani sisi majizi wanajua kuorodhesha shida za wananchi wakati wa kampeni ili wakawaibie?
Ama kweli! kua uone! Mbona sioni wakitoa ni suluhisho gani la shida walizoorodhesha wanalo wezi vibaka wakubwa hawa? Yaani tuwape kura tu!? Hii ni sababu nyingine ya kunifanya niwachukie majambazi hawa milele mpaka Yesu atakaporudi.
 
Hata hivyo, wapinzani wanahitaji kitu kidogo sana kuweza kubadilisha mwelekeo wa ushindi kwani wao wanahitaji kushinda angalau asilimia 50 za kura za vijijini na kushinda asilimia angalau 60 ya kura mijini basi ushindi utakuwa wao. Nje ya hapo, CCM wakishinda, nitakuwa mtu wa mwisho kushangaa.

Tusione umati kwenye mikutano tukatafsiri kura; vitu hivyo viwili havihusiani!

MKjj,
sijawahi kufika kwenye hili jimbo but i think kote ni vijijini. Pia Chadema walishafanya Usangara huku. Do you want to tell me there is no +ve effect on this? if yes, then chadema will win. My worry ni kuwa upinzani utashinda ila kiti kitachukuliwa na ccm. Kama Lipumba angekuwa mzalendo angesema Oscar ajitoe, but i failed to understand what is he doing there.....
 
Back
Top Bottom