lynxeffect22
JF-Expert Member
- Nov 12, 2010
- 626
- 250
ZA MWIZII...!!!:boxing:
arobaini au zimeongezeka?
ZA MWIZII...!!!:boxing:
..Labda tuwajibu wale wanaosema kuwa hawaoni kitu kwenye attachments za invisible.....
..kwa wanaofatilia kwa makini sakata hili watakua wamebaini kuwa hawa PAP waliolipwa pesa za escrow tayari si wamiliki halali wa IPTL bali ni matapeli...
..Ni matapeli kwa kuwa tayari wamegundulika kuwa wamefoji hati miliki ya 70% share za mechmar ili waweze kuchota hela za escrow...Wamefoji hatimiliki hiyo kwa kuonyesha TRA kuwa eti wamenunua 70% ya share za mechmar (aliyekua mmiliki halali) kwa sh. mil.6 tu toka kwa piperlink.....yaani sh.mil.6 kununua 70% ya share zote za IPTL(pamoja na mitambo yote!!)..
.Piperlink ni kampuni iliyodai kukabidhiwa jukumu la muflisi wa mechmar...Hawa piperlink nao hawana hti miliki ya share za mechmar kwani walinyang'anywa miliki hiyo kwenye kesi kule Virgin islands baada ya kugundulika kuwa walitaka kumiliki share za mechmar kitapeli.....na hivyo mahakama ikaamuru kuwa ati miliki hiyo wapewe SCBHK waliokuwa wanawakopesha hela IPTL wakati huo.....
..that said..kwa kwa kuwa imethibitika kuwa PAP si wamiliki halali wa IPTL....maana hata hizo 30% ya share walizowalipa VIP(kina James Rugemarila)zimetokana na pesa walizolipwa na BoT baada ya pesa za escrow kukwapuliwa nao...
..Sasa basi..hata nyaraka PAP walizosainishana na serikali(GoT)...yaani ile agreement ya release of funds na pia ile indemnity deed (kinga ya madai)..zoote hizi zinakua batili automatically na hazina nguvu ya kisheria tena....maana hawa PAP si wamiliki halali wa IPTL...na kwa mana hiyo hata makubaliano yao na serikali yanakosa uhalali wa kisheria automatically..
..that said...ile wanayodai ni kinga kwa serikali (indemnity)haitakua na nguvu ya kisheria panapo madai .....maana aliyesaini deed(yaani PAP)tayari kagundulika ni tapeli.....sasa umeona wapi tapeli/mwizi anatoa kinga ya kisheria kwa anaemtapeli????...kama imefika mahali watu wanasema hawa PAP wakamatwe na mitambo itaifishwe....watapataje hawa nguvu ya kisheria kwa madai kwa serikali??
...that said...kutokana na yote hapo juu..tayari SCBHK(kupitia wanasheria wao) wameshawaandikia tanesco wakiwapa siku 30 wawe wamerudisha pesa yote kwenye escrow account..maana wamegundua kuwa tanesco wamevunja makubaliano ya mkataba wa awali walipofungua escrow account...kwamba tanescow wamekubali pesa ya escrow kulipwa kwa third party (PAP)ambae hatambuliki kwenye mkataba wa awali wa ufunguzi wa acc. hiyo...
....Angalizo..... kuna watu kama Muhongo na Maswi...wamekua wanabeza ushiriki wa SCBHK kwenye sakata hili ....huku wakisahau kuwa hawa SCBHK ndio wamepelekana na tanesco hadi Mahakama ya kimataifa kuhusu tarrifs za umeme wa IPTL...leo eti kina Maswi wanasema hawawatambui???haya ni maajabu mengine ya watendaji hawa wa utawala huu....
.....Labda niwahoji wanaowatetea hawa PAP....kwamba PAP walikuja TZ na mtaji kiasi gani ili wainunue IPTL iliyokuwa na matatizo??mana tunaambiwa eti hawa PAP ni wawekezaji...mtuambie je walikuja TZ na mtaji kiasi gani ili kununua hisa zote za IPTL iliyokuwa na mgogoro???
.jibu hamtakua nalo aslani....maana PAP hawakuja na mtaji TZ..bali walipanga wapige hela za escrow ndipo wazitumie kununua hisa za IPTL...na wamefanikiwa kununua 30% ya hisa za kina Rugemarila(VIP) kwa kutumia hela ya escrow waliyolipwa na BoT. ...Huu ni utapeli wa kiwango cha juu..
....PAP wameshindwa kuzipata kihalali 70% share za mechmar....kwa kuwa walikosa hati miliki halisi....ikabidi wafanye forgery ili wachote hela BoT....napo wakafanikiwa....Lakini sasa wamebambwa...
,....Tutafakari...huu mchezo waliofanya PAP ni kama ilivyokua kwa Richmond..methodology za wizi wao hazitofautiani sana...
Unapiga porojo kama vile sisi hatujui kusoma? hati ya dhamana imetolewaa na IPTL, kasome tena juu.
Umeulizwa Mechmar hawakuwa hata na mlinzi kwenye mali na mitambo yote hiyo? umekwepa kujibu.
Ukifuatilia kwa makini haya madudu utashangaa nani ni mmiliki TANESCO. Hii taasisi imekuwa kama mbuzi wa jalalani. Yaani serikali inajiweka nayo mbali kabisa kama haiihusu!!!
Waliokula laazima waliwe. Hatuwaachii ng'oo. :glasses-nerdy:
Madudu makubwa kama haya yakitokea, whether rais kabariki au hakujua, both are impeachable offenses.
Inahitaji tuweke "utanzania" kando ili kuwa na ujasiri huu.
Kuna pipeline huko watu wamepiga dola bilioni moja wamegawana, habari ikija kubumbuluka wabongo watazimia.Hizi habari za escrow zitaonekana kama pesa ya kumpa mtoto anunue njugu.
Pia watu wanachimba mafuta off of Mtwara mwaka wa pili huu, sie tunaambiwa wanafanya "exploration".