JF bora Kuliko FaceBook...

Tushakosa vya kujadili sasa, tunalinganisha Social Network na Forum?
 
Wewe ndo huna cha kuchngia.Wote wliochangia ni wajinga siyo? Haya mwenye akili leta vya kuchangia.

Hakuna aliyeita watu wajinga bali wewe ndio unataka kuanza, na pili nimetoa mawazo yangu/nimeuliza (tunalinganisha social network site na Forum site?), naomba unijibu ilo swali.

kwenye blue hapo pameniacha hoi hahahaaa.
 
Kwa muda mfupi nilioshiriki hapa JF, nimeona kama hapa ni pazuri kuliko kwenye FACEBOOK.

Hapa JF, mada huchambuliwa kwa umakini mkubwa.

Taarifa muhimu hupatikana kwa haraka sana.

Members wana takwimu za kila aina.

Hapa JF hapajakaa kihuni huni.

Members wa JF, wanatunza heshima zao.

Sasa nitaanza kuwajibika kuiendeleza forum hii.

BIG UP waanzilishi wa JF.
Umejaribu TWITTER?
 
Mkuu jina lako limenivutia sana KYACHAKICHE! ungekuwa mchezaji 'one day' mtangazaji angekata ulimi,.... kama ndiyo unakata chenga na mtangazaji anakutaja mfululizo!! Kyachakiche, Kyachakiche,Kyachakiche,Kyachakiche.....x10!

Lakini safi sana mkuu! hongera, napenda sana majina ya kiafrika.

Mkuu Mzizi wa Mbuyu:
Nashukuru kwa pongezi za jina langu. Naamini kama ungekuwa mtangazaji wala usingepata shida kulitamka kwani kwa mujibu wa sentesi yako hapo juu unapenda majina ya kiafrika, tatizo ni kwamba, hata uwanjani siendi sembuse kucheza!
 
Back
Top Bottom