Jerry Silaa kashindwa kazi?

Slaaa kashajaa kwenye mtego wa J4

Na JF manjua kuwaleta hawa waheshimiwa hapa....

Kwanza kaja Omari Nundu , then kaja Lazaro na sasa kaja Jerry Slaa

Nakuomba sana Jerry andaaa data kamili maana najua wenzako watakuja hapa na maswali kede kede na uweze kujayibu ipasavyo
 
J4Mayoka na Wana JF,
Nafikiri wana JF ni ma Great Thinker, sasa ukisoma habari hii tunajifunza nini au kuna hoja gani hapa?
tuwekee madudu yake hapa watu wachangie, tusiwe na Siasa za Chuki,
angalizo sipo pande yoyote
Utaifa mbele, Tanzania itajengwa na Watanzania wenyewe
Nawakilisha
Hivi huyu tangu achaguliwe kuwa meya wa Ilala kashafanya yepi ya kubadilisha hili jiji?

Maana mie humwona Runway, Mafian Lounge na kule kwenye baa ya Rose Garden anauza sura tuu lakini la kusema anaweza kujivunia kama Meya wa Ilala hakuna zaidi ya kuhusishwa kwenye kashfa ya wizi wa mabilioni ya UDA na meya mwenzie bwana Masaburi.

Halafu hamuishi kuja kulalama kuwa mnataka vijana waje kuchua nchi.

Sasa kama vijana wenyewe ni sampuli za Jerry Silaa naona bora tubaki na hawa hawa wazee.

Sasa wana JF huyu naye tumwachie au?

Maana hii ni 2012
 
Sawa Jerry umetoa statistic nzuri za 16B to 26B kama kawaida yenu magamba.

Lakini people ni 'TOMASO' wanataka waone physical issues.

Kwa mfano (hii ni kwa kukusaidia) ile barabara ya Mombasa-Mazizini-Moshi bar, inakuwa okay, hospital/dispensary ya Mongorandege inakua na equipment na reagents pamoja na personnel.

Jerry, acha bla bla, 1 day utakuja kuzomewa kama L. Masha! Kumbuka, siasa inahitaji watu makini! Afu nimekumbuka, unakumbuka tulipomaliza form IV Pugu afu ukataka usome V na VI in 1 year? Ikabidi uende Jitegemee, wakakuchomolea. Piga kazi, kama unataka kula bata, mwisho wa siku itakula kwako bro!
Haunisaidii,

Soma katiba ujue wajibu wako.

Wakati unangoja tujenge barabara ya mombasa, kama hauna jambo binafsi, waseme na waliojenga road reserve na wanakimbilia mahakamani na kutaka billions za compansation as if hiyo barabara haitawanufaisha wao.

Kama unakaa Mongolandege sema tukuteue ujumbe wa kamati ya usimamizi ya zahanati ambayo hata hivyo vifaa vikienda na wewe na wananchi wenzako badala ya kusimamia physically mkasimamia humu JF na mkaningoja mimi, mtaandika volume.
 
Haunisaidii,

Soma katiba ujue wajibu wako.

Wakati unangoja tujenge barabara ya mombasa, kama hauna jambo binafsi, waseme na waliojenga road reserve na wanakimbilia mahakamani na kutaka billions za compansation as if hiyo barabara haitawanufaisha wao.

Kama unakaa Mongolandege sema tukuteue ujumbe wa kamati ya usimamizi ya zahanati ambayo hata hivyo vifaa vikienda na wewe na wananchi wenzako badala ya kusimamia physically mkasimamia humu JF na mkaningoja mimi, mtaandika volume.
Bro! Shusha templer unaharibu sasa Muheshiwa diwani wa Gongola mboto. Naona kama unapiga ngumi mkuki hapo bwashehe....
Ikibidi weka wakili wakusaidie kujibu hoja
 
Mkuu Jerry Slaa,andika kwa aya ili hoja zako zisomeke vizuri na kwa urahisi.Hii siyo 'chuki',ni kuwekana sawa tu

Ndugu yangu anayehoji kwa hoja nitamjibu kwa hoja, lugha itayotumika nayo ina majibu yake. Na wengine naawacha maana sielewi hata wanachozungumza. Kama mtu haoni impact ya 62.5% increment ya revenue toka 16 B mpaka 26B sasa huyu majibu ambayo ningempa Judge Kaganda angeniita kwenye baraza.
 
Bro! shusha templer unaharibu sasa Muheshiwa diwani wa Gongola mboto. Naona kama unapiga ngumi mkuki hapo bwashehe....
Ikibidi weka wakili wakusaidie kujibu hoja
Mkumbuke mnazungumza na mtu wa Gongolamboto, mtume na Yesu tu ndio walitolewa nyongo.

Kwa wasionifahamu mimi sirembi maneno na kuwaambia watu wajibu wao.

Ndio maana nasema na narudia kusema Kuendesha council sio rahisi kama mnavyodhani, naamini natekeleza wajibu wangu 300% na wakati wote nakumbusha kila mtu atimize wajibu wake kwa mujibu wa katiba na sheria.
 
I can imagine leo mheshimiwa kaamua kupambana na screen ya computer yake. Dah!!. pole sana kama unaweza kuivulia koti hoja ya mtu usiemjua kisa kakuhoji ufanisi wako, vipi leo utaenda kwa kimbau kula mishikaki?
 
Sikujua kama kuna msemaji wangu.

Kwa taarifa jimbo la Ukonga nilishiriki kwa asilimia kubwa kuhakikisha linagawanywa na ningekuwa na nia ya ubunge ningegombea 2010.

Keep the revord clear, sigombei Ubunge 2015.
Jerry unachangamoto kubwa, manispaa ya ilala pamoja na kuwa manispaa tajiri kuliko zote bado unalalamikia source za fund! Mwaka sasa umeisha bado unazungumzia mipango!

Wewe ni kijana mdogo sana unapaswa kujituma na tukuone ukipiga kazi acha kulalamikia muingiliano wa madaraka, toa maamuzi yakwame tuone, kama tatizo ni madaraka unaweza kudhibitisha maamuzi yalikwama kwasababu hiyo? Tunajua muingiliano upo lakini hata uchafu! Fanya yaliyo ndani ya uwezo wako tuyaone kwanza.
 
afu huko kula bata na mamiss mheshimiwa inauhusiano gani na PR? Yaani Mheshimiwa unasingizia PR!!! Kwi kwi kwi! Ngoja nicheke kijuha juha kama Zitto!
 
Afu kuna jamaa kanitonya eti kuna ma supplier uliokataa kuwabeba ndio wanaotaka kukuchafua humu nikamshushua kwani macho yangu hayaoni? Zaidi ni mapicha akila bata!
 
Kaka, nashukuru mungu tumeelewana na angalau umesema yalofanyika kwa kirefu sana.

Humu ndani huyu Mwita Manyara sijui Manyanga anaboa sana, huyu ilibidi mie jana nipakaziane nae kavukavu japo hajui hata asemalo maskini, kaishia kuniponda eti hoja zangu ni za hovyo huku akisahau asili yake na tabia ya makabila kama yake, niwie radhi kuwaweka wote wa kabila lake humo, huyu ni mtu tu anayehitaji kumhurumia na nahisi anatumiwa bila kujijua ama kwa kujua.

Nilimwambia kama anataka aje ofisini kwako akuhoji moja baada ya jingine kuliko kujifanya ujuaji humu JF. Kimsingi ni aibu kwa Mwita kusimamia hoja mfu bila kufanya utafiti. Mimi mkuu sikujui ila nililazimika kumuelimisha huyu jamaa bila mafanikio, mwisho wake mke wangu akaniambia nitafakari jinsi watu wanavyoweza kuwa wanafikiri kwa mujibu wa Dr Masaburi.

Pangu Pakavu.

Najibu humu kwa mambo mawili, moja kuweka kumbukumbu sahihi, mbili kuwapa taarifa sahihi watu wanaovisit JF.

Kwanza ifahamike kuendesha halmashauri its beyond hata Mayoka anavyoweza kuimagine. Ni taasisi kubwa iliyoundwa na kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, na si ukiwa meya unaweza ukaamka asubuhi na kuamua jambo au ukafukuza mtumishi au ukaajiri au ukaweka mkandarasi au kumfukuza anayeharibu.

Halmashauri ina zaidi ya watumishi 7000 watanzania, wakiwemo ndugu na rafiki wa Mayoka, ambao kila mtu asipojituma na ukizingatia kazi za serikali ni mtambuka anakwamisha maendeleo na kazi nyingine.

Kazi zimefanyika nyingi, Ingawa Hosam amejaribu kueleza tuliyoyafanya sekta ya afya bado naona wenye nia zao hawataki kuelewa.

Kiufupi tuna matatizo ya rasilimali fedha, mfumo wa sheria na muingiliano madaraka wa taasisi za umma na uyendaji mbovu wa watendaji wa halmashauri. Tumetumia muda mwingi kwenye kuongeza mapato na kupunguza matumizi maana mambo mengi yanajitaji fedha.

Mfano: Soko la Ilala lililokuwa linakusanua 3-4m kwa mwezi sasa tunakusanya 9-10m. Eventually mapato yameongezeka toka 16B 2010/2011 mpaka 26B 2011/2012. Tumepunguza matumizi toka dev 40% vs recurrent 60% mpaka Dev 60% vs recurrent 40% kwa maelekezo ya kila shilingi moja senti 60 zihamishiwe dev account bila kuchelewa tofauti na taasisi nyingine zinazotumia kwanza recurrent zikibaki ndio zinaenda dev.

Tumekuwa halmashauri ua kwanza kuanzisha mfumo wa kukusanya mapato kupitia Bank ka kuitumia benki ya wananchi wa Dar es salaam kupunguza mianya ya kuvuja mapato.

Tuta-install a computerized revenue collection system kuongeza tija. Tunafanya mabadiliko mengi ya sheria ili kuendana na wakati na sasa sheria mpya ya usafi iko functional na pamoja na kubadilisha utaratibu wa kupata na kusimamia makandarasi wa usafi tulitarget 1st January tunze lakini tumechelewa mpaka 1st March kutakuwa na mabadiliko makubwa.

Tumenunua malori 9 ya taka kuongeza nguvu. Tunanunua greda 2 na moja tulilonalo yutakuwa 1st council sio tu kumiliki greda zaidi ya moja bali matatu kwa ajili ya kuchonga njia za mitaani ambazo ni unpaved.

Tumekuwa council ya kwanza kukopa TIB kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisutu ambalo litamilikiwa 100% na wana ilala na si mikataba ya JV ya kifisadi ambayo kila siku watu wanakuja ofisini kwangu kuomba. Yote haya yapo kwa internet ambapo picha mlioiona ni hii tu.

Kwa taarifa hii ilikuwa shear charity ball ya mwaka juzi ambayo ni jitihada za mjasiliamali mzawa kusaidia wenye shida. Pesa iliyopatikana hapa ilienda CCBRT kusaidia kina mama wenye fistula.

Mayoka jiulize ni lini umejitoa kwenye jamii. Humo humo ulikopata hizo picha zipo nikiwa na mke wangu na ndio maana nasema mazungumzo haya myapeleke FB maana profile zetu zipo wazi.

Halmashauri ni taasisi inayofanya marketing and PR na katika hilo meya huwezi kumwacha kila aliyetumia neno "kuuza sura" ameonyesha uwezo wake finyu wa kufahamu mambo, kama wanavyosema wanazuoni "intellectuals discuss issues not personality" najua ni ngumu mtu akijiangalia umri wake na achievement alizorecord kukubali failure, ila it doesn't make u a better person kwa kushambulia wengine.

Mfano UDA inamilikiwa na Halmashauri ya jiji na mimi ni meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, unaniingizaje huko.

Mwisho mimi ni kijana na kama binadamu mwengine nina haki ya kusocialize na sioni mahusiano na kazi za umma. Naamini wapenda maendeleo wamenielewa, as usual na karibisha comments and critics.
 
I can imagine leo mheshimiwa kaamua kupambana na screen ya computer yake. Dah!!. pole sana kama unaweza kuivulia koti hoja ya mtu usiemjua kisa kakuhoji ufanisi wako, vipi leo utaenda kwa kimbau kula mishikaki?

Nitapita pale baadae.
Sina tabu na hao nisiowajua maana hawana confidence ua kukosoa hadharani. Sie tumeamua kufanya kazi za public mtu ana haki ya kudai sio kuomba maelezo. Kosa kumtukana mtu. Najibu kwa kuwa kuna watu in thousands wanasoma haya na silence ina maana nyingi sana. Nikijaliwa muda ni vyema kuweka kumbukumbu kwenye saver za JF clear!
 
Nashukuru ndugu yangu,

Mambo ni meeengi, Ilala is not a joke. Ni council very challenging. Yapo mengi lakini kila mtu ana interest zake. Tunafanya siasa, tuna maadui wa asili , tuna wenye chuki binafsi huwezi kuwazuia, huruma ni kwa watu wanaovisit humu wanaweza amini ndio maana sometimes tunatumia muda kuweka kumbukumbu sahihi.

Wenye kuona wataona na mengine mwenyezi Mungu atatulipia.

Kila ninapoongelea FB sio kwamba nami siudhiwi na watu wanopost upuuz na picha za kipuuz, lakini angalau tunaona profile ya mtu ukajua unadeal na mtu wa aina gani.

Obrigado.

Kaka, nashukuru mungu tumeelewana na angalau umesema yalofanyika kwa kirefu sana.

Humu ndani huyu Mwita Manyara sijui Manyanga anaboa sana, huyu ilibidi mie jana nipakaziane nae kavukavu japo hajui hata asemalo maskini, kaishia kuniponda eti hoja zangu ni za hovyo huku akisahau asili yake na tabia ya makabila kama yake, niwie radhi kuwaweka wote wa kabila lake humo, huyu ni mtu tu anayehitaji kumhurumia na nahisi anatumiwa bila kujijua ama kwa kujua.

Nilimwambia kama anataka aje ofisini kwako akuhoji moja baada ya jingine kuliko kujifanya ujuaji humu JF. Kimsingi ni aibu kwa Mwita kusimamia hoja mfu bila kufanya utafiti. Mimi mkuu sikujui ila nililazimika kumuelimisha huyu jamaa bila mafanikio, mwisho wake mke wangu akaniambia nitafakari jinsi watu wanavyoweza kuwa wanafikiri kwa mujibu wa Dr Masaburi.

Pangu Pakavu.
 
Mkuu kama kweli wewe ni Jerry Slaa siasa za nini? umeulizwa swali hujibu isipokuwa unakuja kujenga fikra za watu kwamba kuna uadui na siasa.

Binafsi tumekutana ukiwa bado naibu Meya na sijui kama unanikumbuka lakini nakushangaa sana unapochukulia mjadala huu hapa ni ktk mbinu za kukupakaza wakati ndivyo wananchi wanavyokuona.. Kwanini usichukue muda na kuwasikiliza wao maana wasemayo hayana uongo na wala huyapingi isipokuwa huna majibu ktk utendaji kazi..
 
MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI UNACHEKI SURA NA MAMBO YAKE?
hawa ndio vijana wa kileo kawaoneni oneni pale Mnazi mmoja kwa Mkama wanavyojipitisha kwa MKAMA wakitafuta mapande ya Ukuu wa WILAYA.
 
Awali ya yote nikushukuru kwa kujitokeza na kujibu hoja.Pengine ni mwanzo mzuri.Ukiwa kama kijana watu wengi walitegemea kuona ukiwa karibu nao. Pili, elewa kuwa jumuiya ni mchanganyiko wa watu wenye fikra tofauti na lazima uwe katika nafasi ya ustahamilivu. Lakini pia imechangiwa na wewe mwenyewe kuwa na kauli zenye jazba.
Kwanza ifahamike kuendesha halmashauri ni taasisi kubwa iliyoundwa na kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, na si ukiwa meya unaweza ukaamka asubuhi na kuamua jambo au ukafukuza mtumishi au ukaajiri au ukaweka mkandarasi au kumfukuza anayeharibu
Nadhani hili ulilitambua wakati unagombea, na ni kwa mkakati wako ulijiaminisha kuwa una uwezo wa kukabiliana na changamoto zitokanzo. Unapolalamika inatupa picha kuwa upo 'on job training' hili jaribu kuliepuka

Kiufupi tuna matatizo ya rasilimali fedha, mfumo wa sheria na muingiliano madaraka wa taasisi za umma na uyendaji mbovu wa watendaji wa halmashauri. Tumetumia muda mwingi kwenye kuongeza mapato na kupunguza matumizi maana mambo mengi yanajitaji fedha
Jerry, unaongoza manispaa tajiri na yenye vyanzo vingi vya pesa kuliko mji,manispaa au jiji lingine kwa kuzingatia eneo. Hakuna tatizo la chanzo cha mapato labda utuambie kuna tatizo la ubunifu. Unaposema hayo, mtu atakuuliza meya wa halmashauri ya kule kwetu Handeni atasema nini.

Mfano: Soko la Ilala lililokuwa linakusanua 3-4m kwa mwezi sasa tunakusanya 9-10m. Eventually mapato yameongezeka toka 16B 2010/2011 mpaka 26B 2011/2012. Tumepunguza matumizi toka dev 40% vs recurrent 60% mpaka Dev 60% vs recurrent 40% kwa maelekezo ya kila shilingi moja senti 60 zihamishiwe dev account bila kuchelewa tofauti na taasisi nyingine zinazotumia kwanza recurrent zikibaki ndio zinaenda dev
Jerry, kukusanya mapato ni sehemu ya kazi za kila siku na ni wajibu. Kwahiyo kuongeza ukusanyaji wa mapato ni kuiwezesha manispaa kutimiza wajibu wake na sio mafanikio hata kidogo. Kama huko nyuma walikuwa hawakusanyi huo ni uzembe na usiweke wajibu wako katika mizani na uzembe. Hoja hii ni dhaifu sana na haina mashiko. Hata kama utakusanya bilioni 100 kwa mwezi hiyo ni kazi yenu wananchi wanataka kuona matokeo(results) na si wewe unasaini nini au unafanya vikao gani n.k. Wanataka kuona matokeo ya wewe kuwepo ofisini.

Tumekuwa halmashauri ua kwanza kuanzisha mfumo wa kukusanya mapato kupitia Bank ka kuitumia benki ya wananchi wa Dar es salaam kupunguza mianya ya kuvuja mapato
Hili pili ni wajibu kwasababu kulinda rasimali za jijij ni sehemu ya kazi zenu. Tunataka kuona, je kupitia mfumo huo kitu gani kimeweza kutokea. Tunardui pale pale (result).
Je ni kwanini bank ya wananchi na isiwe bank nyingine kama CRDB zenye matawi ili kuwapunguzia walipa kodi kazi za kutafuta bank yenye matawi mawili au matatu. Huoni kuleta huduma karibu na wananchi ni sehemu ya ufanisi.

Tunafanya mabadiliko mengi ya sheria ili kuendana na wakati na sasa sheria mpya ya usafi iko functional na pamoja na kubadilisha utaratibu wa kupata na kusimamia makandarasi wa usafi tulitarget 1st January tunze lakini tumechelewa mpaka 1st March kutakuwa na mabadiliko makubwa
Uwepo wa sheria haumaniishi ufanisi mzuri. Tunasheria za kila aina mfano ni sheria za rushwa lakini unaona nchi inavyotapeliwa kila uchao. Kuna sheria ya makazi lakini muziki kila nyumba kumi n.k. Wananchi wanataka kuona sheria hizo zinasimamiwa vipi ili kuleta matokeo. Hiyo ndiyo changamoto.
Hivi Jerry si kuna sheria ya afya inayozuia watu kujisaidia hovyo! mbona wapiga debe shule ya uhuru wana choo cha wazi, unataka kutuambia ukibadilisha maandishi basi wapiga debe wataacha kukojoa hovyo!!!
Tumenunua malori 9 ya taka kuongeza nguvu. Tunanunua greda 2 na moja tulilonalo yutakuwa 1st council sio tu kumiliki greda zaidi ya moja bali matatu kwa ajili ya kuchonga njia za mitaani ambazo ni unpaved
Je malori hayo yatabeba taka kama ilivyokusudiwa au yachukua vifusi vya mchanga kwa 'wazee'. Je, malori hayo yana usimamizi wa kutosha kuhakikisha kila lita ya mafuta na matengenezo yanafanyika kulingana na taratibu?
Umekiri kuwa manispaa ni taasisi kubwa, hivi huoni kuwa badala ya kununua malori, manispaa ilitakiwa iwe na utaratibu wa kueleweka na wa kisheria unaozingatia taratibu wa kuweka 'private sector' kufanya kazi hiyo? Kwa uzooefu wa nchi yetu serikali haiwezi kusimamia baadhi ya huduma na kwa mfumo wa soko tulilo nalo, kampuni binafsi zinaweza kufanya vema kama kuna utaratibu usioingiliwa na rushwa. Kazi ya manispaa iwe kusimamia wakandarasi wachache na si kila mtaa ili kutoa nafasi ya kufanya shughuli zingine.
Changamoto hapa ni rushwa na miradi ya wazee, na ndipo kiongozi makini angeweza kujitofautisha na sisi tukasem kweli anaweza.
Halmashauri ni taasisi inayofanya marketing and PR na katika hilo meya huwezi kumwacha kila aliyetumia neno "kuuza sura" ameonyesha uwezo wake finyu wa kufahamu mambo, kama wanavyosema wanazuoni "intellectuals discuss issues not personality" najua ni ngumu mtu akijiangalia umri wake na achievement alizorecord kukubali failure, ila it doesn't make u a better person kwa kushambulia wengine
Kauli kama hizi hazifai mheshimiwa Meya. Watu wote hawawezi kuwa mameya lakini haiwafanyi wajisikie hawana mafanikio. Unaposema hivyo una maanisha wananchi wako wasioweza kununua aspirini baadhi yao nao ni failure.
Nadhani hasira zimetawala na busara imeondoka, punguza jazba. Hapa unawakashifu wengi na sio uliyemkusudia
Mfano UDA inamilikiwa na Halmashauri ya jiji na mimi ni meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, unaniingizaje huko
Wakazi wa Ilala wanataka usafiri wa uhakika wa umma. Jukumu la usafiri wa umma katika manispaa ya Ilala lipo mikononi mwako. Kama UDA wanafanya hivyo kama Jiji, Ilala ni sehemu ya jiji na maamuzi mengi unahusika kwa njia moja au nyingine.
Unapojitoa ni kukwepa wajibu wako hueleweki. Sasa tuambie mbadala wa UDA uliopo Ilala ni upi.
Kwasababu kuna ufisadi UDA hiyo haifanyi utelekeze jukumu la usafiri ndani ya Ilala. Ndivyo Mameya wote wanavyofanya huko duniani kuliko na uwajibikaj
Mwisho mimi ni kijana na kama binadamu mwengine nina haki ya kusocialize na sioni mahusiano na kazi za umma. Naamini wapenda maendeleo wamenielewa, as usual na karibisha comments and critics
Unapokuwa kiongozi wa umma unakuwa umepeoteza sehemu kubwa sana ya uhuru wako. Wewe unakuwa ni mtu wa umma na kila jambo unalofanya linaangaliwa kama kiongozi na si Jerry. Mfano, ukimwaga chai hotelini hiyo ni habari kubwa hata kama kuna mtu amemwaga birika zima jirani na wewe.
Unahaki ya ku-socialize lakini ukumbuke kuwa unapokuwa katika social activities kuwepo na mstari wa kutenga social na social activies za kikazi. Unaweza kufanya hivyo kwa njia ya kuepeuka picha katika magazeti hata unapokuwa na shughuli binafsi. Hii ni gharama nyingine ya kujenga public image na popularity haiepukiki.

Jerry, unapkouwa na social activities za kikazi ukiwa 'umezungukwa nao' halafu wale wenye vichanga wamelala sakafuni pale Amana hospitali inawatatiza wadau. Think about that and try to make a sharp contrast between Silaa at home and Silaa at work.

Mwisho, kiongozi mzuri ni yule anayesikiliza watu wake wana hoja gani. Ni yule aliye tayari kuwasiliana nao ikibidi na asiye na jazba
 
Mwisho, kiongozi mzuri ni yule anayesikiliza watu wake wana hoja gani. Ni yule aliye tayari kuwasiliana nao ikibidi na asiye na jazba
Nimekuongeza kwenye list yangu ya Ma great thinker wa JF!! Sina cha kuongeza mkuu!
 
Kaka, nashukuru mungu tumeelewana na angalau umesema yalofanyika kwa kirefu sana.

Humu ndani huyu Mwita Manyara sijui Manyanga anaboa sana, huyu ilibidi mie jana nipakaziane nae kavukavu japo hajui hata asemalo maskini, kaishia kuniponda eti hoja zangu ni za hovyo huku akisahau asili yake na tabia ya makabila kama yake, niwie radhi kuwaweka wote wa kabila lake humo, huyu ni mtu tu anayehitaji kumhurumia na nahisi anatumiwa bila kujijua ama kwa kujua.

Nilimwambia kama anataka aje ofisini kwako akuhoji moja baada ya jingine kuliko kujifanya ujuaji humu JF. Kimsingi ni aibu kwa Mwita kusimamia hoja mfu bila kufanya utafiti. Mimi mkuu sikujui ila nililazimika kumuelimisha huyu jamaa bila mafanikio, mwisho wake mke wangu akaniambia nitafakari jinsi watu wanavyoweza kuwa wanafikiri kwa mujibu wa Dr Masaburi.

Pangu Pakavu.

Acha kujipendekeza wewe mtoto wa kiume. Tafuta mkate wa watoto kihalali kama mimi.
Mimi ninaishi ukonga, huyu Jerry alikuwa diwani wangu 2005-2010 na sasa ni diwani wa gongolamboto, pacha na jirani yetu.

Kama kuna mafanikio ama failures ktk uongozi wake ninazifahamu vizuri sana, sisimuliwi kama wewe. Hata hoja nilizomuuliza hapa hajazijibu, ameonyesha kiburi na dharau lakini anafahamu ukweli wake.
Ndio maana utaona mimi nazungumzia issues za kijamii na wajibu wake, sizungumzii personal affairs.
 
Back
Top Bottom