Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Mkitafuta uwajibikaji wa viongozi bila uwajibikaji wa wananchi ni kazi bure!
Ama kwa hakika manispaa ya Ilala tumepata hasara, huyu ndiye meya na huu ndio uwezo wake wa kufikiria! amesahau kwamba wananchi wanawajibika kila siku, na ndio hao waliosababisha ongezeko la mapato ya manispaa toka sh.16bilioni hadi sh.26bilioni.
Sasa Jerry, unataka uwajibikaji gani zaidi ya huu wa wananchi kuendelea kuchangia miradi ya maendeleo lakini viongozi mnaishia kufanya ufisadi? Jaribu kutueleza hizi fedha zinazotajwa hapa chini ziko wapi!!?? kama sio wizi wa nguvu za wananchi??
Suala la huduma za serikali za mitaa Ukonga:
Hii ni changamoto kubwa ya kwanza ambayo inakela sana wananchi wa Ukonga na maeneo mengine ya Manispaa ya Ilala. Katika maeneo yote Wenyeviti wa serikali za mitaa ya Ukonga ambao wote ni maswaiba wako wazuri unaowatumia kukupigia kampeni za kuusaka ubunge 2015, wamejifanya miungu watu na wanataka waabudiwe na wamekuwa wafujaji wazuri wa fedha za uma. Mathalani rafiki yako mkubwa ndugu Alfred Kipondya, mwenyekiti wa mtaa wa Madafu ambaye ni kinara wa kuwachangisha wanachi michango isiyokuwa na kichwa wala miguu. Mmekuwa mkishirikiana nae kula pesa za miradi mbalimbali ya uma kama huu wa maji Mzambarauni kama ambavyo nimeelekeza hapo chini. Hali kadhalika unatueleza mmeongeza magari ya kuzoa taka ya municipal council ilihali wewe na Kipondya mnaendelea kuwachangisha wananchi kila kaya 3,000Tshs fedha ambazo zinaingia katika kampuni yenu binafsi, na hili ninakuombeni acheni mara moja mkija kwetu na wafungulia mbwa. Mbaya zaidi umekuwa ukiwashinikiza wenyeviti pamoja na watendaji wa serikaliza mitaa wakusanye 2,00Tshs kwa kila mtu anayekwenda kwa ajili ya kusainiwa document yoyote ile, ili muulize vizuri swaiba wako Kipondya hatokaa anisahau pale aliponiomba hela kwa ajili ya kunisainia document hukuakitaka kunipa risiti ya cash book yenye muhuli wa serikali ya mitaa. Wananchi huwa tunajiuliza Ilala Municipal Council kwenye hayo makusanyo mnayokusanya si kuna fedha mnazorudisha zitumike katika ofisi zetu za kata pamoja na serikali za mitaa, zinafanya kazi gani?? Jamani mbona hamtuonei huruma? Gharama za maisha zimepanda acheni kutunyonya sana.
Suala la Mgogoro wa Ardhi Kinyerezi:
Halmashauri ya Ilala imepitisha mpango wa upimaji wa viwanja kwenye maeneo ambayo watu wanaishi kule kinyerezi, ambapo mmewaambia wananchi wachangie gharama za upimaji ambapo katika kila square metre moja wanatakiwa kuchangia shilingi 1500. Ukishindwa kulipia gharama kwa ajili ya upimaji unanyanganywa eneo na unalipwa fidia. Na unajua fika kesi iko mahakamani ambapo wananchi wanapinga gharama ya uchangiaji na hali kadhalika mnajua fika kabisa hata kama mtu akishindwa kulipa gharama za upimaji, gharama za ufidiaji haziendani kabisa na gharama ahalisi za ardhi. Mwanasheria wako wa manispaa ya Ilala aliieleza mahakama kuu mbele ya Judge Shangwa kwamba fedha hizo mnazotaka kuwalipa wananchi mmezikopa bank. So mnataka hizo interest ndio wananchi wawasaidie kulipa?? Huu ni mradi ambao una harufu ya ufisadi na wewe unahusika moja kwa moja kwenye hili pamoja na maswaiba zako.
Mradi wa maji Ukonga Mzambarauni:
Mh mstaiki meya Jerry Slaa hili linaniuma sana kwani lina nigusa sana na watu wa Ukonga hawatokaa walisahau milele katika kipindi chao chote cha maisha yao hapa Duniani. Wananchi wote walichangishwa shilingi 5,000 Tshs kwa kila kaya kwa ajili ya mradi huu tena uchangiaji huo ulikuwa ni wa lazima kwa ajili ya kuondoa shida ya maji, na mkawaambia wananchi mtawasambazia mabomba kuanzia pale mzambarauini kwenda sehemu zingine mbalimbali kama Madafu,Mombasa, Gongo la Mboto, Mwisho wa Lami, mpaka Mazizini. Hivi huwa ukipita pale Mzambarauni roho huwa haikuumi kuona mmekula pesa za wananchi na huduma hakunailiyopatikana?? Muogopeni mwenyezi mungu tendeni haki panapostahili.
Halafu bila aibu kabisa mtu kama huyu anataka awe mbunge!! Kwa utumishi gani, kwa sifa gani unazoweza kuwaeleza watu wakuchague? kama umeshindwa kuonyesha uwezo wako na kipaji chako ukiwa kama diwani, utaweza kukopa wapi akili ya kuwa mbunge bora??