Jenerali Ulimwengu na makala zake


Asha:

Kwa maoni yangu binafsi naona Jenerali Ulimwegu anachemsha BIG TIME.

Vyama vya siasa katika nchi zilizoendelea vina Itikadi lakini Itikadi hizo sio zao la mawazo ya mtu mmoja bali ni matokeo ya kisiasa na mabadiliko ya kijamii yalizozikumba nchi hizo.

Pamoja na nchi zilizoendelea kuwa na vyama vya kisiasa vyenye itikadi, malengo makubwa yanabakia ni kutoa viongozi mbalimbali watakaoongoza nchi. Na viongozi hawa wanapokuwa madarakani, wanaongoza nchi kwa kufuata ukweli wa mambo na sio itikadi ya vyama vyao. Hivyo itikadi mara nyingi inatumika katika kupatia kura za uchaguzi.

Kama lengo la vyama vya kisiasa ni kutoa viongozi wa kutawala nchi sioni sababu ya ulazima wa vyama vya kisiasa vya Tanzania kuwa na itikadi za kusimamia na kupigania. Inatosha kwa chama cha kisiasa kuonyesha ni mambo gani watayafanyia kazi wakiwa madarakani na vilevile inatosha kwa vyama vya siasa kutoa upinzani pale chama kilichopo madarakani kinakosea (CHECK AND BALANCE).

Siasa sio rocket science na tusijaribu kuifanya hivyo.
 
Rufiji,

sidhani kama ni sahihi kudai kuwa statements za Ulimwengu ziko vague kwani wakati mwingine upuuzi wa siasa za Afrika unashindwa hata kizelezea ka ufasaha zaidi,kwani kama mtu anashindwa kuelewa tu kitu rahisi kama Mugabe /ZANU-PF kukatalia madarakani ilhali wananchi hawamtaki na uchumi umeanguka kwa 160,000%,itakuwa rahisi kweli kuelewa/kuelezea nini hasa falsafa/itikadi ya ZANU-PF/Mugabe?

Hapo hujaongelea madudu ya CCM hapa Tz na siasa njaa zetu.Tumeshuhudia kila mara kina Tambwe Hiza,Lamwai,Mrema,etc ambao kila kukicha wao ni kutafuta vyama tu,kama watu hawa wana falsafa na/au iktikadi thabiti itakuwaje mtu abadilike tu overnight na kusema wapinzani ni njaa tu au CCM majambazi kisha huyo kwenye chama kingine?Mbona Nyerere hakuwahi kuwa hivyo (ningependa kukubaliana na FMES aliposema kuwa itikadi/falsafa ya CCM alikuwa nayo Nyerere tu)?

Hivi mtaelezeaje tamko la Kolimba (RIP) aliposema CCM imekosa mwelekeo/dira (isomeke falsafa/itikadi)?

Najua wengi mnampinga Ulimwengu kuwa si kweli kuwa vyama vyote havina itikiadi/falsafa,nahisi ni kwa vile mnakifiria CHADEMA na viongozi wake wa sasa kina Mbowe,Zitto,Dr. Slaa,lakini kumbuke hawa wana misimamo yao binafsi (kama vile alivyokuwa Nyerere au Sokoine kwa CCM),swali ni kuwa mmeshawahi kuifikiria CHADEMA bila Zitto,Mbowe,Dr. Slaa/Tundu lissu?

Au CUF bila Maalim Seif au Lipumba?Vinaweza kusimama?
 

Mwanzoni wa miaka ya 90 hakuna aliyeweza kufikiria CHADEMA bila Mtei. Mwanzoni mwa miaka ya 2000 hakuna aliyeifikiria CHADEMA bila Bob Makani. Kwa hiyo Mbowe, Dr Slaa, Tundu Lissu na Zitto watapita lakini CHADEMA itasimama milele. Kama CHADEMA ingekuwa haina misingi, falsafa na itikadi ambayo viongozi wake wanaendana nayo ingekuwa ni mkusanyiko wa mafisadi wa aina mbalimbali. CCM imekuwa kokoro!

Asha
 


Kama Ulimwengu amekosea tuandike alipokosea, lakini tusiseme anavunja watu moyo.Ukivunjwa moyo na strong criticism you are most probably a weakling ambaye utavunjwa moyo hata na kivuli chako mwenyewe anyway.

1.Sijasema lolote kwamba Ulimwengu kakosea au hajakosea, nilichosema ni kuwa asishambuliwe kwa sababu "anavunja watu moyo".Nimesisitiza tuandike alipokosea, ikiwa ni pamoja na hapo unaposema wewe kwamba hajatoa ushahidi (ingawa makala yake inaendelea bado)

2.Mtu hajamaliza makala, inaendelea kwa hiyo shambulizi la kakosa ushahidi siyo or any meaningful and comprehensive criticism of this piece at this point will reveal more about the idealism ya mshambulizi kuliko anayeshambuliwa na mawazo yake.
 

Klepto, Klepto, Klepto.

I appreciate the depth, hapa Ulimwengu anatupeleka kwa John Mbiti mazee, lakini tuko tayari?

This sorta goes back to the argument I was making on the importance of changing institutions and mindsets/eductaion before or during regime change.The Afrocentrism dimension is a whole different plane to be explored.

Katiba zetu in some aspects ni nzuri kuliko za hao wa west tuliowa copy, kwa sababu tumecopy paste na hatujapata ugumu wa kuziandika from experience, matokeo yake pale ambapo Mmarekani ana ainisha freedoms na entitlements za raia sisi tunaenda a step further mpaka kuainisha sio tu freedoms na entitlements but also duties.

Lakini swali linakuja, how real are these documents? Wenzetu wanazipigania kweli kweli, your political belief is a part of you complete with some somewhat embarrassing bumper stickers and badges and what not.Sisi tunaweza kusema hivyo?

Kwa nini?

Misingi ya vyama vya Africa imekaa top down.Mengistu anaenda kwenye Ukomunisti, anapewa misaada anafanya nchi iwe ya kikomunisti.Nchi haina soviets wala mfumo wa kikomunisti.Kila kitu top down, Zidumu Fikra za mwenyekiti, zidumu.Watu hata hawaelewi fikra hizi ni zipi!

Tatizo la Afrika kwa sasa hivi ni kwamba huwezi kuwa na vyama vya kifalsafa kama huna middle class, huna watu wengi walioelimika.Utakuwaje na uchambuzi wa falsafa zako wakati less than 2% ya watu wana access ya kusoma magazeti?Utawaelezeaje watu wa vijijini mambo abstract ya kifalsafa wakati hawajala na wanakufa kwa magonjwa?
 
Ibambasi,

Bado nitazidi kuitetea kauli yangu kwamba statement za Ulimwengu ziko vague ! Nimesoma article yake kama mara mbili na kiasi fulani nimehuzunishwa na standard ya uandishi wa huko nyumbani . Nitajaribu kuonyesha vitu ambavyo mpaka sasa sijaelewa nini haswa huyu muungwana alikuwa anazungumzia.


Baada ya kusoma hiyo kauli nikafikiria ya kuwa Ulimwengu amefanya Research ya vyama vyote vya siasa afrika na kuangalia kwa undani itikadi na falsafa za hivyo vyama . Lakini sio hivyo , huyu bwana ajatuonyesha source kwa hiyo alichofanya ni kuassume ya kuwa kwa kuwa Tanzania hali hiko hivi basi afrika itakuwa hivyo pia . Argument yake imejaa fallacy anageneralize tuu.


Kwa mara nyingine tena Ulimwengu anaonyesha dhahiri ya kuwa hajui chanzo cha matatizo yetu . Tatizo sio itikadi za chama au falsafa kama yeye anavyosema , tatizo ni utamaduni wa wizi na ubinafsi wa viongozi wetu.Itikadi kama itikadi bila kuwa na viongozi madhubuti wa kuzisimami hizo ni itikadi ni kupoteza muda.

Ndivyo hivyo tulipofikia mahali nchini Tanzania kwamba watawala wetu wala hawajui ni kiasi gani cha dhahabu kinachimbwa nchini na kupelekwa nje. Kisa? Wafadhili wanajua, na wakijua inatosha

Hii ni statement ya kijinga isiyo na facts zozote . Watawala wetu wanajua ni kiasi gani cha dhahabu kinaenda nje ila awajali kwa sababu wameweka maslahi binafsi mbele. Ulimwengu, tafadhali ukipata muda tembelea migodini kabla ya kutoa statement ukiwa hapo Dar.
 

Hivi nchi gani ya Kimagharibi inafuata falsafa kama ya CHADEMA ya "Nguvu ya Umma"? Mbona mi naona hii nayo ni home grown? Halafu itikadi ya CHADEMA ni ya 'mrengo wa kati'? Mbona tunaona left left and right? Mi naona CHADEMA wamekuwa unique kuja na mrengo wa kati.

Asha
 

Dada,

Nguvu ya Umma na Social Democrat haina tofauti, hata jina la chama lenyewe linaonyesha "Chama Cha Democrasia na Maendeleo" Progressive Democrats.

Unanichekesha kukataa ku operate kwenye misingi ya wenzetu wakati hiyo template unayoitumia kujidistinguish righ, centre and left ni yao.
 
Sorry if this messes up the flow of the topic but for those of you who want institutional reforms before regime change: how much time are you talking about before we can have regime change? To me you sound as if you are okay with letting them (CCM) continue to jack things up for as long as it will take.....just curious
 
Tatizo la Ulimwengu anaongelea vyama na vyama havitakuwa solution kwa nchi yetu. Nchi yetu isingekuwa na vyama ingekuwa pazuri zaidi
 


..na ndio maana anatoa mawaidha! kama kuna mtu anamwona kuwa anataka kurudi ulingoni[ambako hajawahi kuwa,by the way],huyo atakuwa anatazama makengengeza!

..anachokisema huwa kina maana. sasa,mwenye ufahamu atachukua yanayochukulika,yasiyochukulika atamwachia!
 
Asha,
Demos(watu/umma), cratos(nguvu), demoscratos= demokrasia= nguvu ya umma. that is the logic. Msisitizo; chadema maana yake ni chama cha nguvu ya umma na maendeleo, nachelea kusema wazi kuwa chadema sio original authors wa demos cratos, wanaweza tu kuwa wana version yao.
 
CCM haijawahi kuwa na sera, ni Mwalimu aliyekuwa na sera zake binafsi, lakini CCM kama chama haijawahi kuwa na sera, zaidi ya ubabaishaji tu.

..duh!

..kwa taarifa yako ccm ilikuwa na ina sera hata leo. tatizo ni utekelezaji. ni kawaida ya waswahili kuwa na mipango lakini bila utekelezaji!

..si kweli ccm ni ubabaishaji,bali wababaishaji wako wengi.

..kauli kama hizi ndizo zinawafanya wananchi wa-shy away from upinzani. chumvi nyingi kwenye kila kitu,mpaka haviliki!

..ccm isingekuwa na sera na ingekuwa chama cha ubabaishaji[tofautisha wababaishaji]hii nchi isingekuwa hapa!

..tuwe rational at times!it helps a lot!
 
1.
duh! ..kwa taarifa yako ccm ilikuwa na ina sera hata leo. tatizo ni utekelezaji. ni kawaida ya waswahili kuwa na mipango lakini bila utekelezaji!

CCM ilikuwa na sera, under Mwalimu, naomba uniambie Mwinyi alikuwa na sera ipi? Zaidi tu ya kuwaachia watu kutolipa kodi au hiyo ilikuwa ni sera?

2.
CCM ingekuwa na sera tusingekuwa tulipo after 45 years za uhuru, hivi kweli nchi yetu kwako inaonekana kuwa imekuwa huru na inayojitawala kwa miaka yote hiyo?

3.
..tuwe rational at times!it helps a lot![/B
]

Kuwa rational ni pamoja na kukubali ukweli, ndio maana ninasema kama ni sera za kisiasa nimeziona chini ya utawala wa Mwalimu, alipoondoka tu sijawahi kuona sera tena, nilichoona tu ni kwamba under Mwinyi wananchi walikuwa hawalipi kodi, chini ya mkapa mashirika yetu nimeyaona yakiuzwa kwa bei poa, kama hizo ni sera then yes lakini kwangu siamini kuwa zilikuwa ni sera, ninaamini kuwa ulikuwa ni ujanja tu wa viongozi wachache wa CCM waliotaka kujitajirisha kwa haraka haraka and they did!

Kama ninamuelewa vizuri Ulimwengu, ni kwamba anataka wa-Tanzania turudi kwenye ujamaa, ninasema hiyo haitakuja kutokea tena na ninamuomba abaki na hayo maawazo yake!

Ahsante Mkuu!
 

Issa, ..sorry..Bin Maryam,
Additionaly new theories are almost always built on existing theories, and sometimes nothing is really new, thats the way we end up having paradigms
 
Issa, ..sorry..Bin Maryam,
Additionaly new theories are almost always built on existing theories, and sometimes nothing is really new, thats the way we end up having paradigms

Kuna maandishi nayapitia hapa na ninachoona majadiliano ya kuwa na itikadi katika vyama vya kisiasa sio suala jipya barani Afrika. Nchi karibu zote za Kiafrika zilipopata uhuru ziliingia katika majadiliano makubwa ya kufuata itikadi gani. Na kipindi hicho kulikuwa na extremy mbili za political spectrum: Ujamaa na Ubepari.

Na nchi kama Tanzania, Ghana na Guinea zilitumia mamilioni ya pesa kuanzisha vyuo vya itikadi. Tanzania ilikuwa na chuo kikuu cha chama Kivukoni na vyuo hivyo vilienea katika ngazi za wilaya. Pamoja na juhudi zote hizo, hakuna kilichomfanya mtanzania aingiwe damuni na mawazo ya Itikadi.

Bottom Line: Cha muhimu katika maisha ya binadamu ni kuboresha maisha yake. Na itikadi ya kisiasa ni moja ya njia za kutumia kuboresha maisha.

Matatizo yanayokuja kwa nchi za Kiafrika ni kuwa Itikadi zao zilijaa details kiasi cha kwamba wafuasi wa Itikadi hizo walishindwa kutumia akili, vipaji vyao au maarifa waliyo nayo kuboresha maisha. Na matokeo yake watu wakawa wanatumia muda wao kuiboresha Itikadi badala kuitumia Itikadi kuboresha maisha yao.

Nchi zote za kiAfrika zina serikali zinazoendesha kama Enterprises. Serikali zinajenga mabarabara, mahospitali na miradi mingi ya maendeleo. Katika nchi kama hizi ni muhimu kuwa na TECHNOCRATS watakaoweza kusaidia nchi kuliko kuwa na wanasiasa wenye fine details za Itikadi.

Toka vita vya pili vya dunia vimalizike Italy imebadilisha serikali zaidi ya mara 55. Kwa wastani chama tawala kinakaa madarakani chini ya mwaka mmoja. Kama Itikadi ya chama ni muhimu basi Italy ingekuwa ni moja ya nchi masikini duniani. Kinachosaidia wa-Italy ni technocrats wanaoendesha shughuli za serikali kila siku bila kujali nani yupo madarakani.
 
Nyongeza tu....maelezo yako kuhusu hizi kanuni yameelemea zaidi ktk mambo ya kiuchumi. Masuala ya kijamii, kidini, na kimaadili huwa ni mambo yanayosababisha midahalo mikali (kwenye nchi za wenzetu, of course)...

Nyani,

Sisi bado hatujaanza kuhangaishana kisiasa kuhusu utoaji mimba, ushoga n.k.
 

Rufiji,

Hii makala haijaanza kwenye hili toleo ambalo Mzee ES kaliweka hapa ukumbini. MImi nimekuwa nafuatilia hizi makala za Jenerali kwa wiki zaidi ya 12. Ni mlolongo wa makala ambazo zinabadilika sura kila siku na inawezekana kabisa ukapotea maboya kama unaisoma kwa mara ya kwanza na kutobaini kuwa ilibidi usome makala ya wiki iliyopita kupata mwelekeo wa anakokwenda.

Inaelekea kana kwamba Jenerali anaandika kitabu au kijarida fulani na anatumia wiki moja moja kuwakilisha sehemu fulani ya jarida lake!
 
Naungana mkono na wote wenye kuona kuwa Falsafa na Itikadi ni kile kiongozi anacho PRACTISE na sio kilichoko kwenye maadishi ya katiba zao au any of the paper works.

What was writen down during Nyerere, Mkapa, Mwinyi na Kikwete kinaweza kikawa almost ni kilekile! But wote wamepractise vitu tofauti kulingana na mioyo yao inavyo watuma! Na matokeo ya kila mmoja yako wazi!

Vigumu sana kuwa na haya mambo kwenye ukweli wake!

Nafikiri hiyo ndio maana ya politics!! AU?
 
Kitila na wengine,

David Brooks wa New York Times katoa maana moja poa sana na inabidi tuangalie kama inawiana na Siasa za Afrika na hasa sisi kwetu Tanzania.

Namnukuu


http://www.nytimes.com/2008/05/09/opinion/09brooks.html
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…