Bin Maryam
JF-Expert Member
- Oct 22, 2007
- 685
- 13
Jenerali Ulimwengu ameweka vyama vyote kwenye kapu ikiwemo vya upinzani kuwa havina falsafa wala itakadi:
http://www.raiamwema.co.tz/08/04/23/4.php
Hebu mlio karibu na Raia Mwema mumwambia asome hapa:
http://www.chadema.net/maoni/kijue.php
ili wiki ijayo aendelee kujadili kama CHADEMA nao hawana falsafa wala itikadi?
Asha
Rufiji,
sidhani kama ni sahihi kudai kuwa statements za Ulimwengu ziko vague kwani wakati mwingine upuuzi wa siasa za Afrika unashindwa hata kizelezea ka ufasaha zaidi,kwani kama mtu anashindwa kuelewa tu kitu rahisi kama Mugabe /ZANU-PF kukatalia madarakani ilhali wananchi hawamtaki na uchumi umeanguka kwa 160,000%,itakuwa rahisi kweli kuelewa/kuelezea nini hasa falsafa/itikadi ya ZANU-PF/Mugabe?
Hapo hujaongelea madudu ya CCM hapa Tz na siasa njaa zetu.Tumeshuhudia kila mara kina Tambwe Hiza,Lamwai,Mrema,etc ambao kila kukicha wao ni kutafuta vyama tu,kama watu hawa wana falsafa na/au iktikadi thabiti itakuwaje mtu abadilike tu overnight na kusema wapinzani ni njaa tu au CCM majambazi kisha huyo kwenye chama kingine?Mbona Nyerere hakuwahi kuwa hivyo (ningependa kukubaliana na FMES aliposema kuwa itikadi/falsafa ya CCM alikuwa nayo Nyerere tu)?
Hivi mtaelezeaje tamko la Kolimba (RIP) aliposema CCM imekosa mwelekeo/dira (isomeke falsafa/itikadi)?
Najua wengi mnampinga Ulimwengu kuwa si kweli kuwa vyama vyote havina itikiadi/falsafa,nahisi ni kwa vile mnakifiria CHADEMA na viongozi wake wa sasa kina Mbowe,Zitto,Dr. Slaa,lakini kumbuke hawa wana misimamo yao binafsi (kama vile alivyokuwa Nyerere au Sokoine kwa CCM),swali ni kuwa mmeshawahi kuifikiria CHADEMA bila Zitto,Mbowe,Dr. Slaa/Tundu lissu?
Au CUF bila Maalim Seif au Lipumba?Vinaweza kusimama?
Pundit,
Huoni kosa analoandamwa kwalo? ni kusema vyama vyote havina FALSAFA.
Kama hajakosea hapo, basi aje na ushahidi kwa kupitia chama kimoja hadi kingine na kuthibitisha madai yake. Si vyema kufanya majumuisho kama ya samaki mmoja kaoza basi wote wameoza. ILIYOOZA NI CCM YAKE, tena critique zisizo na uthibitisho hazina ustrong wowote. NO empirical evidence no right to disseminate generalization (sijui ndio ujenerali wenyewe)
ULIMWENGU KAMA UNASOMA HAPA, UNADAIWA USHAHIDI WA MADAI YAKO, kama hamna ku-withdraw statement sio kugumu.
Kama Ulimwengu amekosea tuandike alipokosea, lakini tusiseme anavunja watu moyo.Ukivunjwa moyo na strong criticism you are most probably a weakling ambaye utavunjwa moyo hata na kivuli chako mwenyewe anyway.
Nadhani tunashindwa kumwelewa Ulimwengu na ujumbe wake. Hizi falsafa na Itikadi za kimagharibi ambazo kimsingi sio utamaduni wetu hazitatufikisha kokote.
Hebu tutawatendee haki wale wenye mtazamo tofauti na vile tunavyofikiria, sio lazima kwamba maoni ya wengi ni sahihi,mara nyingine wachache huwa wapo sahihi.
Ndio maana enzi zile Mwl alijaribu kujenga ujamaa kwa kufuata nadharia ya Kifabian ya evolution,kwa kuamini kwamba ujamaa ni imani hivyo akijitahidi kuhubiri imani hiyo taratibu tutapata jamii ya kijamaa bila kufuata misingi ya Kimarx! Sasa ujumbe wa Ulimwengu ni kwamba baada ya vita baridi kuisha Maliberali wanafurahia ushindi kwa kuamini kwamba sasa dunia yote ni ya Kiliberali
Hebu tuangalie ukweli wa nadharia hiyo hapa Tanzania,ni chama gani kinaweza kikajidai kwamba hakijakopi itikadi na falsafa ya kiliberali na je jamii yetu imeendelea kufikia hatua ambayo tunaweza kila mmoja akaenda kivyake yaani individualism kama inavyohubiriwa na Maliberali? tunayaona matokeo yake leo hii pale tulipofungulia milango!
Tuna wachache wanaojifanya juu chini kuhakikisha wanakuwa matajiri bila kujali maslahi ya Taifa! Nachelea kusema kwamba inawezekana kabisa kwa hali tuliyokuwa nayo sasa Chama chochote kitachoingia madarakani ama kitakuwa sawa na CCM ama kitafanya vibaya zaidi kuliko CCM,
Ni vyema tusaidiane kujenga misingi bora kama nchi na baada ya hapo huo upuuzi wenu unaoitwa demokrasia ya kimagharibi uendelee kwani tutakuwa na wananchi na Taasisi zitakazokuwa makini katika kufuatilia hali ya mambo.
Ni mtizamo tu,na sisi tunaweza tafuta model zetu wenyewe bila kukopi na kupaste Afrika ina utajari wa tamaduni na mifumo ambayo ikitengenezwa na kuboreshwa inafaa kabisa kuendeshea nchi.
Kukosekana kwa mwelekeo ndani ya chama si ugonjwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) peke yake. Ni kweli kwamba kwa muda mrefu hicho ndicho kilichokuwa chama pekee nchini, lakini hili halikukifanya kiwe pekee kupoteza dira miongoni mwa vyama vya nchi za Bara la Afrika.
Kwa hakika katika makala zangu za mwanzo kabisa za mfululizo huu nilikwisha kutoa rai kwamba vyama karibu vyote vya nchi za Kiafrika, hata vile vilivyoanza vikiwa na mwelekeo ulioeleweka, havina tena maaana yo yote ya kifalsafa na kiitikadi.
Ujuha huu ndio unaotufanya tuachie mali zetu zichukuliwe na wageni kwenda kuwaneemesha watu wao ughaibuni wakati watu wetu wanaendelea kuishi maisha ya mbwa nchini mwao. Ndivyo hivyo tulipofikia hali ya nchi za Kiafrika zenye rasilimali kubwa sana ndizo pia zinazoongoza kwa kuwa na raia hohe hahe.. Nigeria, Angola, Kongo, na nyingine
Ndivyo hivyo tulipofikia mahali nchini Tanzania kwamba watawala wetu wala hawajui ni kiasi gani cha dhahabu kinachimbwa nchini na kupelekwa nje. Kisa? Wafadhili wanajua, na wakijua inatosha
Klepto, Klepto, Klepto.
I appreciate the depth, hapa Ulimwengu anatupeleka kwa John Mbiti mazee, lakini tuko tayari?
This sorta goes back to the argument I was making on the importance of changing institutions and mindsets/eductaion before or during regime change.The Afrocentrism dimension is a whole different plane to be explored.
Katiba zetu in some aspects ni nzuri kuliko za hao wa west tuliowa copy, kwa sababu tumecopy paste na hatujapata ugumu wa kuziandika from experience, matokeo yake pale ambapo Mmarekani ana ainisha freedoms na entitlements za raia sisi tunaenda a step further mpaka kuainisha sio tu freedoms na entitlements but also duties.
Lakini swali linakuja, how real are these documents? Wenzetu wanazipigania kweli kweli, your political belief is a part of you complete with some somewhat embarrassing bumper stickers and badges and what not.Sisi tunaweza kusema hivyo? Kwa nini?
Hivi nchi gani ya Kimagharibi inafuata falsafa kama ya CHADEMA ya "Nguvu ya Umma"? Mbona mi naona hii nayo ni home grown? Halafu itikadi ya CHADEMA ni ya 'mrengo wa kati'? Mbona tunaona left left and right? Mi naona CHADEMA wamekuwa unique kuja na mrengo wa kati.
Asha
Wananchi wengi hatujakata tamaa na wala hatusumbuliwi na waliokwisha kata tamaa, Ulimwengu hawezi kuweka mkono kwenye nyama na mkono kwenye kunde, kwa expense yetu wananchi,
He had his time, sasa ni wakati wa wengine, ni simple fact ambayo haina ubishi ila ni yeye kukubali tu yaishe!
Asha,Hivi nchi gani ya Kimagharibi inafuata falsafa kama ya CHADEMA ya "Nguvu ya Umma"? Mbona mi naona hii nayo ni home grown? Halafu itikadi ya CHADEMA ni ya 'mrengo wa kati'? Mbona tunaona left left and right? Mi naona CHADEMA wamekuwa unique kuja na mrengo wa kati.
Asha
CCM haijawahi kuwa na sera, ni Mwalimu aliyekuwa na sera zake binafsi, lakini CCM kama chama haijawahi kuwa na sera, zaidi ya ubabaishaji tu.
duh! ..kwa taarifa yako ccm ilikuwa na ina sera hata leo. tatizo ni utekelezaji. ni kawaida ya waswahili kuwa na mipango lakini bila utekelezaji!
..si kweli ccm ni ubabaishaji,bali wababaishaji wako wengi.
..kauli kama hizi ndizo zinawafanya wananchi wa-shy away from upinzani. chumvi nyingi kwenye kila kitu,mpaka haviliki!
..ccm isingekuwa na sera na ingekuwa chama cha ubabaishaji[tofautisha wababaishaji]hii nchi isingekuwa hapa!
]..tuwe rational at times!it helps a lot![/B
Asha:
Kwa maoni yangu binafsi naona Jenerali Ulimwegu anachemsha BIG TIME.
Vyama vya siasa katika nchi zilizoendelea vina Itikadi lakini Itikadi hizo sio zao la mawazo ya mtu mmoja bali ni matokeo ya kisiasa na mabadiliko ya kijamii yalizozikumba nchi hizo.
Issa, ..sorry..Bin Maryam,
Additionaly new theories are almost always built on existing theories, and sometimes nothing is really new, thats the way we end up having paradigms
Nyongeza tu....maelezo yako kuhusu hizi kanuni yameelemea zaidi ktk mambo ya kiuchumi. Masuala ya kijamii, kidini, na kimaadili huwa ni mambo yanayosababisha midahalo mikali (kwenye nchi za wenzetu, of course)...
Nahisi watu wengi wamemiss point , Ulimwengu either ajui alikuwa anaongelea nini au amechanganya mambo . Kichwa cha habari na habari yenyewe haviendani kabisa .Kwanza kabisa ni lazima Ulimwengu atambue ya kuwa tatizo linalokabili nchi yetu sio itikadi wala sheria zetu bali ubinafsi wa viongozi wetu.Huu ni utamaduni mbaya sana ulioshamiri kwenye nchi yetu mpaka hapo tutakapoutokomeza ..... Tatizo kubwa watanzania tunakariri sana hatuko creative at all, nataka Ulimwengu aniambie ni itikadi Kagame anazotumia kujenga uchumi kwa kasi ya ajabu . Nadhani tunahitaji kiongozi mwadilifu na visionary hivi vitu vingine vitakuja tuu...
Halafu pia statement zake nyingi ziko too vague hakuna substance waungwana kusema vyama vingi Afrika havina itikadi bila ya kucite source information ni kudanganya. Mimi nadhani itakuwa vizuri kwa ulimwengu kuchambua vitu kwa undani kabla ya kuanza kutoa lawama ambazo anashindwa kuzi-backup .
The central political debate of the 20th century was over the role of government. The right stood for individual freedom while the left stood for extending the role of the state. But the central debate of the 21st century is over quality of life. In this new debate, it is necessary but insufficient to talk about individual freedom.