Jenerali Ulimwengu na makala zake

Gamaba la nyoka,
Zingatia ni nini zaweza kuwa athari za kauli ya Jenerali kwamba vyama havina misingi ya kifalsafa. hapa si suala la kutanguliza maslahi ya vyama. Kauli kama hiyo aliyoiandika inatosha kabisa kudhohofisha jitihada zote za wanamageuzi nchini. Jiulize kauli ya Mwalimu aliposema wapinzani hawana sera iliudhohofisha kiasi gani mfumo wa mageuzi nchini. Aliitoa kauli hiyo wakati akimnadi 'Mr. Clean'
Au fikiria kauli kama za akina Jaji Warioba aliyepata kusema, tuna chama kimoja na wapiga kelele 17
Vijineno kama hivi vinavuruga sana harakati za kuwang'oa mafisadi, mara utasikia wengine wanasema, wapinzani hawana jipya, na kisha watu wanawaamini kwa sababu ya umaarufu wao.
Maslahi ya taifa hayawezi kulindwa au kutetewa kwa kutoa kebehi za kudhalilisha vyama vinavyotetea maslahi hayo hayo.
Aondoe kauli yake hiyo, hayo mengine aliyoyaandika ni ugonjwa ulioko kwenye chama ambacho yeye ni mwanachama. kama ana nia ya dhati ya kuutibu aje kambi ya mageuzi tushirikiane badala ya kuvunja watu moyo.

..upinzani kama ni dhoofu ni dhoofu tu.

..ukweli unaposemwa watu wajifunze na kukubali kuonyeshwa mapungufu.
 
..ndo maana nikasema hawatafautiani sana na ccm!


Huu nao ni upotoshaji na ni kujaribu kutoa majibu rahisi kwa maswali magumu! Huwezi kusema vyama vya upinzani havitofautiani na CCM wakati CCM imeshakuwa madaraka miaka yote wakati vyama vingine havijawahi kushika serikali. Huwezi kuvipima vyama vya siasa kwa mujibu wa maandishi ya katiba zao tu. Vyama hupimwa kwa kutazama mafanikio na athari ziliyoleta vikiwa katika serikali. Ndio maana leo hii huko America Democrats wanajivunia utendaji wao walipokuwa serikali wakati wakiponda ule wa Republicans chini ya Bush. Vivyo hivyo leo hii Labour wanapowaponda Conservatives wanalinganisha mafanikio yao baada ya kuwa madarakani kwa miaka kumi ukilinganisha na ile miaka Conservatives walipokuwa madarakani. Hawajivunii eti kwamba itikadi yao kwenye katiba ni nzuri sana! Sasa kulinganisha vyama on the basis ya kilichoandikwa kwenye katiba zao tu ndio huo nauita upofu wa kisiasa. Hivyo kusema vyama vya upinzani vya Tanzania ni sawa na CCM ni kuvionea kwa sababu unalinganisha vitu ambavyo havifanani in the first place.

Na inabidi uelewe kwamba hakuna anayekataa mapungufu ya vyama vya siasa hapa wala anayesema kwamba vyama vya upinzani vimekamilika. Tunachokataa ni kujaribu kubambikia watu mapungufu ambayo hayapo ambayo yanatokana na hisia za mtu badala ya hali halisi ya mambo. Ukosoaji wa aiana ya Ulimwengu, kama alivyosema Kahangwa, haujajengwa kwa minajiri ya kurekebisha mambo bali katika kujaribu kukatisha tamaa watu wanaopigania kukuza demokrasia ya vyama vingi nchini na kujenga chama mbadala kwa CCM ambayo imeshindwa kutawala. Tuna haki ya kukataa na kuukemea ukosoaji wa namna hii.
 
..kitila,

..ulimwengu hamkatishi tamaa mtu yeyote,labda ungesema yeye amekata tamaa na hizi siasa!

..halafu hata nikiandika sana haitasaidia."ukubwa wa pua si wingi wa makamasi"

..ukweli ni kuwa watanzania bado hatuna mwamko wa kutosha kudai stahiki zetu toka kwa wanasiasa na viongozi. kwa mfano,jijini dar hivi sasa ni kichekesho kitupu[na bado viongozi watajiita viongozi]maji machafu kila kona,barabara mbovu na uchafu unazidi. haya makosa ya nani? viongozi wa upinzani hawayaoni haya? au ishu za ufisadi zimewajaa akilini hadi macho hayaoni pande nyingine?

..ni mambo kama haya yanaposimamiwa na kutatuliwa ndio wananchi wanakuwa na imani na viongozi wao!

..kuna mabadiliko mengine hayawezekani[ccm hawatayakubali/yapitisha]mpaka pale upinzani utakapoongezeka bungeni. sasa,fanyeni kazi huku chini,mpate wawakilishi wa kutosha bungeni ili mlete hayo mabadiliko.

..punguzeni mahubiri!
 
Ulimwengu yuko mbioni kuanzisha Chama cha siasa cha wajamaa wanaojitegemea

PM

"Wajamaa wanaojitegemea" is an oxymoron.

"Ubepari na kujietgemea" sawa.

"Ujamaa na kutegemeana" sawa

Ujamaa maana yake ni kuishi kwa kutegemeana, kujitegemea maana yake ni kila mtu kivyake hamna ujamaa jamaa.

Ndiyo maana hata siasa za CCM za "Ujamaa na Kujitegemea" zilishindwa, msingi wake ulikuwa mambo mawili yaliyo mutually exclusive kama pande mbili za shilingi.Ama wewe ni mjamaa au unajitegemea, Viwili hivi haviendani.
 
Tunachokataa ni kujaribu kubambikia watu mapungufu ambayo hayapo ambayo yanatokana na hisia za mtu badala ya hali halisi ya mambo. Ukosoaji wa aiana ya Ulimwengu, kama alivyosema Kahangwa, haujajengwa kwa minajiri ya kurekebisha mambo bali katika kujaribu kukatisha tamaa watu wanaopigania kukuza demokrasia ya vyama vingi nchini na kujenga chama mbadala kwa CCM ambayo imeshindwa kutawala. Tuna haki ya kukataa na kuukemea ukosoaji wa namna hii.

Wananchi wengi hatujakata tamaa na wala hatusumbuliwi na waliokwisha kata tamaa, Ulimwengu hawezi kuweka mkono kwenye nyama na mkono kwenye kunde, kwa expense yetu wananchi,

He had his time, sasa ni wakati wa wengine, ni simple fact ambayo haina ubishi ila ni yeye kukubali tu yaishe!
 
Kama vyama havina sera, au havifuati sera zake zilizoandikwa, Ulimwengu siyo tu ana haki, bali pia wajibu wa kukosoa.

Kama ataamua kutoa maoni yake ya kipi kifanyike au la, hiyo ni juu yake.Lakini ana haki na wajibu wa kukosoa, na kukosoa wala siyo kuvunja moyo.Ni kujenga misingi imara vya "scrutiny" katika wimbi la mageuzi.

Kama Ulimwengu amekosea tuandike alipokosea, lakini tusiseme anavunja watu moyo.Ukivunjwa moyo na strong criticism you are most probably a weakling ambaye utavunjwa moyo hata na kivuli chako mwenyewe anyway.
 
Kama vyama havina sera, au havifuati sera zake zilizoandikwa, Ulimwengu siyo tu ana haki, bali pia wajibu wa kukosoa.

Mkuu Pundit,

Heshima mbele, ni wajibu wa Ulimwengu kukosoa sera kama zipo, lakini sio sera ambazo hazipo, CCM haijawahi kuwa na sera, ni Mwalimu aliyekuwa na sera zake binafsi, lakini CCM kama chama haijawahi kuwa na sera, zaidi ya ubabaishaji tu

Infact, Kitila amekwenda too deeep kwenye kujaribu ku-explain sera ambazo hazikuwepo, lakini labda za Chadema ambazo hazijawahi kujaribiwa, otherwise Ulimwengu kama kiongozi wa zamani wa taifa ni fair game kumtwanga personal na hoja zake finyu!
 
bwanae hata Chadema yaleyale..hakuna jipya,,,,maaana tunasikia ni cha wachaga mara sijui nini?? dawa ni kuanzisha JF-Party naona ndio tuna msimamo na mwelekeo uliotukuka
 
Hiyo lebo ya conservative kuwa siasa kali mimi naikataa. Ni kali kivipi na kwa kipimo gani? Kwa sababu hata mimi conservative nawaona maliberali wa mlengo wa kushoto kabisa kuwa na siasa kali. Sasa kwa nini ukiwa Conservative unabatizwa kuwa na siasa kali? Hizo siasa kali ni zipi?

Nyani,

Naomba nijisahihishe kidogo kuhusiana na hivi viraka na vipachikwa vya Conservative, centrist na liberal.

Hizi ni kanuni kuu za ama itikadi au falsafa na zinaweza kuwepo katika chama kimoja chenye Itikadi moja.

Mfano, enzi za enzi, Kingunge na Paulo Sozigwa (pamoja na wengine) walijulikana kama conservatives wa CCM. Katika CCM kuna pande zote hizi tatu, wenye siasa kali (wakifuatia kila kitu kiimla na kwa nguvu za msukumo wa kijamaa), wenye siasa za kati (kina Mr. Win-Win situation), na kuna liberals (wanaokubaliana hata na vyama au siasa ambazo si za kimsingi za CCM kwa kutumia Itikadi na Falsafa).

Sasa basi, kwa kuwa sisi bado tunajijenga katika mchepuo wa vyama vingi, mfano wa Kitila wa Chadema ya Mtei, haukifanyi Chadema kuwa mlengo wa Kulia (Conservative) kwa kuwa msimo wa Chadema nyakati za Mtei, zilikuwa ni kupingana na CCM kwa kusema kuwa kama CCM ni wajamaa, basi wao Chadema ni Mabepari au Makabaila.

Sasa utakuta labda Mtei alikuwa ndio mwenyewe conservative, akisema watu binafsi washikilie uchumi, kodi za matajiri zipunguzwe, Makani akawa ni wa Kati akisema, no tuendelee kuwa na mashirika ya Serikali na kodi ziwe sawa kwa wananchi wote, then anakuja Kitila ambaye labda alikuwa akiegemea sana kufanana na CCM au kuwa the other extreme ya Mtei kwa kudai kodi ziongezwe, Serikali na watu binafsi wafanye ubia kuendesha uchumi.

Hivyo hakuna dhambi au kosa kwa mtu kuegemea upande ambao anauamini.

Swali langu la Mirengo enzi zile ilikuwa ni kujua, je kama tumekulia katika Ujamaa na KUjitegemea, je hivi vyama vipya vina siasa gani ambazo ni tofauti na CCM? je ni vya Kikomunisti, Kijamaa, Kibepari, Kikabaila au Mambosasa kama Kitila alivyosema kuwa Chadema ya Mbowe ndivyo ilivyo?

Sasa tukishabaini hivyo, ndipo unakuja kwenye sera, kama mfano wa kodi, je Chadema sera zao kwa mambo ya Ushuru na Kodi yatakuwa tofauti kabisa na CCM? je wataongeza viwango vya kodi, kufuta misamaha ya ushuru na kodi na kuhakikisha watu binafsi wanachangia kwa dhati ujenzi wa Taifa, au watafuata blue print ya CCM kwenye Uwekezaji?

Je Chadema, CUF au mwingine atakayechukua nchi ambaye si CCM (Hata kama itakuwa kutoka CCM) atakuwa na sera gani kuhusu masuala ya uwekezaji, mazingira, kilimo, biashara na madini?

Je watakuwa ni wenye mwamko wa kusema soko huria au soko dhibitiwa?

Sasa kutoka hapo, ndio tuanze tena kunyumbulisha ni nani katika chama au vyama ambavyo vinafanana kifalsafa na kiitikadi, ndiye conservative, centrist na liberal?

Its all about win win situation ;)
 
Nyongeza tu....maelezo yako kuhusu hizi kanuni yameelemea zaidi ktk mambo ya kiuchumi. Masuala ya kijamii, kidini, na kimaadili huwa ni mambo yanayosababisha midahalo mikali (kwenye nchi za wenzetu, of course)...
 
Nadhani tunashindwa kumwelewa Ulimwengu na ujumbe wake. Hizi falsafa na Itikadi za kimagharibi ambazo kimsingi sio utamaduni wetu hazitatufikisha kokote.

Hebu tutawatendee haki wale wenye mtazamo tofauti na vile tunavyofikiria, sio lazima kwamba maoni ya wengi ni sahihi,mara nyingine wachache huwa wapo sahihi.

Ndio maana enzi zile Mwl alijaribu kujenga ujamaa kwa kufuata nadharia ya Kifabian ya evolution,kwa kuamini kwamba ujamaa ni imani hivyo akijitahidi kuhubiri imani hiyo taratibu tutapata jamii ya kijamaa bila kufuata misingi ya Kimarx! Sasa ujumbe wa Ulimwengu ni kwamba baada ya vita baridi kuisha Maliberali wanafurahia ushindi kwa kuamini kwamba sasa dunia yote ni ya Kiliberali

Hebu tuangalie ukweli wa nadharia hiyo hapa Tanzania,ni chama gani kinaweza kikajidai kwamba hakijakopi itikadi na falsafa ya kiliberali na je jamii yetu imeendelea kufikia hatua ambayo tunaweza kila mmoja akaenda kivyake yaani individualism kama inavyohubiriwa na Maliberali? tunayaona matokeo yake leo hii pale tulipofungulia milango!

Tuna wachache wanaojifanya juu chini kuhakikisha wanakuwa matajiri bila kujali maslahi ya Taifa! Nachelea kusema kwamba inawezekana kabisa kwa hali tuliyokuwa nayo sasa Chama chochote kitachoingia madarakani ama kitakuwa sawa na CCM ama kitafanya vibaya zaidi kuliko CCM,

Ni vyema tusaidiane kujenga misingi bora kama nchi na baada ya hapo huo upuuzi wenu unaoitwa demokrasia ya kimagharibi uendelee kwani tutakuwa na wananchi na Taasisi zitakazokuwa makini katika kufuatilia hali ya mambo.

Ni mtizamo tu,na sisi tunaweza tafuta model zetu wenyewe bila kukopi na kupaste Afrika ina utajari wa tamaduni na mifumo ambayo ikitengenezwa na kuboreshwa inafaa kabisa kuendeshea nchi.
 
Nadhani tunashindwa kumwelewa Ulimwengu na ujumbe wake. Hizi falsafa na Itikadi za kimagharibi ambazo kimsingi sio utamaduni wetu hazitatufikisha kokote.

Hebu tutawatendee haki wale wenye mtazamo tofauti na vile tunavyofikiria, sio lazima kwamba maoni ya wengi ni sahihi,mara nyingine wachache huwa wapo sahihi.

Ndio maana enzi zile Mwl alijaribu kujenga ujamaa kwa kufuata nadharia ya Kifabian ya evolution,kwa kuamini kwamba ujamaa ni imani hivyo akijitahidi kuhubiri imani hiyo taratibu tutapata jamii ya kijamaa bila kufuata misingi ya Kimarx! Sasa ujumbe wa Ulimwengu ni kwamba baada ya vita baridi kuisha Maliberali wanafurahia ushindi kwa kuamini kwamba sasa dunia yote ni ya Kiliberali

Hebu tuangalie ukweli wa nadharia hiyo hapa Tanzania,ni chama gani kinaweza kikajidai kwamba hakijakopi itikadi na falsafa ya kiliberali na je jamii yetu imeendelea kufikia hatua ambayo tunaweza kila mmoja akaenda kivyake yaani individualism kama inavyohubiriwa na Maliberali? tunayaona matokeo yake leo hii pale tulipofungulia milango!

Tuna wachache wanaojifanya juu chini kuhakikisha wanakuwa matajiri bila kujali maslahi ya Taifa! Nachelea kusema kwamba inawezekana kabisa kwa hali tuliyokuwa nayo sasa Chama chochote kitachoingia madarakani ama kitakuwa sawa na CCM ama kitafanya vibaya zaidi kuliko CCM,

Ni vyema tusaidiane kujenga misingi bora kama nchi na baada ya hapo huo upuuzi wenu unaoitwa demokrasia ya kimagharibi uendelee kwani tutakuwa na wananchi na Taasisi zitakazokuwa makini katika kufuatilia hali ya mambo.

Ni mtizamo tu,na sisi tunaweza tafuta model zetu wenyewe bila kukopi na kupaste Afrika ina utajari wa tamaduni na mifumo ambayo ikitengenezwa na kuboreshwa inafaa kabisa kuendeshea nchi.

NA HII IMEKOPIWA WAPI?

SEHEMU YA SITA:
MFUMO HAKI WA UCHUMI (JUSTIFIABLE ECONOMY)


Mfumo wa uchumi unaoheshimu haki unatambua uwepo wa haki ya raslimali asili, haki ya mwenye mtaji na haki ya mwenye nguvukazi. Mfumo huu unasisitiza kwamba sharti kuwepo maridhiasawa (amicability) kati ya pande tatu; raslimali asili, mtaji na nguvukazi au kati ya pande mbili; mtaji na nguvukazi/ raslimali asili na nguvukazi; kuhusu gawio (dividend) la uzalishaji. Maridhiasawa yanaweza kufahamika kimahesabu kwa kutambua thamani ya mtaji = (kizio chake ni HISA) na thamani ya nguvu kazi = ustadi wa nguvukazi x masaa ya kazi x 1% ya mtaji (kizio chake ni HISA-SHIRIKI)

Itikadi ya haki inasisitiza kuwa, daima rasilimali za nchi fulani ni mali ya wananchi husika na kamwe haimilikishwi kwa watu wasiokuwa raia wa nchi hiyo. Chini ya itikadi hii sharti mwenye mtaji aumiliki kihalali na si vinginevyo. Vile vile mfumo haki hauruhusu mtu awaye yeyote kupata gawio lisitahililo nguvukazi kama mtu huyo hakuitumia nguvukazi yake katika uzalishaji husika. Aidha mwenye nguvukazi sharti aitumie kujipatia ridhiki na kuiendeleza jamii yake.


Source: Jamii Intelligence Forum
 
Wana JF ni vizuri tukikumbuka kuwa Ulimwengu ni mtu ambaye yuko kwenye kundi la watu wanaopinga upinzani na wanaopinga walioko madarakani. NI mtu ambaye yuko kwenye kundi la kipekee. Kuna watu wengine ni wa kupinga tu na Ulimwengu is of that type.

Naweza kuungana naye kwenye kusema kuwa sasa hivi chama cha mapinduzi kimepoteza mwelekeo, Nasema hivi kwa sababu sasa hivi hakuna mtu kutoka kwenye chama tawala anayeweza kusema CCM inatekeleza itikadi gani, au CCM inafuata falsafa ipi kwenye uongozi wa nchi. Kinachoonekana ni kama vitu vya kudonoadonoa tu, hakuna mwelekeo ambao sasa hivi JK anaweza kusema anaedesha nchi kuelekea mahali fulani.

Kuhusu watu wa opposition sifahamu, inawezekana wameandika itikadi zao kwenye katiba zao na manifesto zao, lakini kama kweli lengo lao ni hilo na watafanya hivyo wakichukua dola, it is something thatwe need to wait and see.
 
CCM Chama cha Mafisadi..
CCM Chukua chako mapema...
Sis!! sote bado...Kualumiana Ndio Tuanajua..Lakini Kuwajibika hatujuai...

Na kipimo cha Kukomaa ni kuacha kulaumu..
 
Ninachoona hapa ni kuwa:

1. Kuna watu hawakubaliani na Ulimwengu kama Ulimwengu katika kuchambua hoja.Kimsingi hawakubaliani naye katika mengi.

2. Kuna watu wanazibwa sana na ushabiki wa vyma kiasi kiasi kwamba chama chao kuambiwa hakina dira it sounds too offensive.

3. Hapa kiachoonekana ni wengi kulalia upande wao,wapo waliochoka na CCM kiasi kwamba juhudi zao ambazo angalau kwa sasa zinaonekana kuleta changes fulani naturally wasingependa kuoneshwa udhaifu wao (ambao kimsingi upo kwani ni WANASIASA tena wa kiafrika).

4. Wapo wanaofikiri kwa kuwa Ulimwengu ni drop-out wa CCM/system na mtu anayeonekana kutofautiana na waliopo madarakani na kwa kuwa ni (undisputedly) influential figure kwa jamii yetu,basi baadhi yetu tungependa kumwona akielema upande wa wapinzani,yaani awasifu kwa mabo yanayoendelea kwa sasa nchini (in short awe strategist wao,so to say) ndio hao wanaolalamika kuwa anawavunja moyo.

5. Hii inathibisha kwamba kumbe vyama vyote viko sawa kabisa tofauti ni kwamba kimoja kiko madarakani vingine viko nje,na mifano tunayo (Kibaki, Bakili Muluzi, Chiluba, etc)...

Hitimisho:

Mimi namuunga mkono Ulimwengu kwa maana kuwa ameandika makala hii kwa kufuata mtazamo mpana zaidi wa kijamii kuliko matashi ya kisiasa.Ndo sababu kila mara hatuachi kusikia "hii hoja ni wapinzani","hii hoja sio ya CCM"...damn!Tunaangalia utaifa au uchama?
 
Mimi nafikiri ukiona mtu anajenga hoja ambazo unafikiri zinakatisha tamaa harakati za mageuzi dawa ni kujenga hoja zenye nguvu zaidi yake na kujinadi kwa kujipambanua kwa uzuri wa hoja na sera zako.

Kama hoja ya Mwalimu kwamba "Upinzani bora utatoka ccm" imekuwa ni kikwazo kikubwa cha upinzani mbele ya macho ya watanzania, na kwa miaka yote hiyo tangu kauli hiyo itolewe wapinzani wameshindwa kuikata makali kauli hiyo basi kuna tatizo la kujinadi ndani ya upinzani ambalo inabidi walitatue kama wanataka wakubalike mbele ya macho ya wananchi.

Wapinzani wasitegemee mteremko, kupigiwa vigelegele,na kutupiwa maua kwa hatua zozote watakazofanya ili kuwaconvice wananchi kwamba wapewe dola.

Kama kweli mnashindwa kuvunja hoja ya ulimwengu mtaweza kweli kuvunja hoja za World bank na Imf kuhusu sera complicated za uchumi-jamii?, au mtaendeleza stutus quo ya kuwalalamikia wakubwa juu ya sera zisizotunufaisha?

Wapinzani ni lazima mtambue kwamba chuma cha pua hakiwi chuma cha pua mpaka kipitie kwanza kwenye tanuri la moto. hii ya ulimwengu ni rasha rasha tu ya hoja ngumu zilizo mbele yenu mnazotakiwa kuzijibu mbele ya wananchi ili mpate kukubalika
 
4. Wapo wanaofikiri kwa kuwa Ulimwengu ni drop-out wa CCM/system na mtu anayeonekana kutofautiana na waliopo madarakani na kwa kuwa ni (undisputedly) influential figure kwa jamii yetu,basi baadhi yetu tungependa kumwona akielema upande wa wapinzani,yaani awasifu kwa mabo yanayoendelea kwa sasa nchini (in short awe strategist wao,so to say) ndio hao wanaolalamika kuwa anawavunja moyo.

5. Hii inathibisha kwamba kumbe vyama vyote viko sawa kabisa tofauti ni kwamba kimoja kiko madarakani vingine viko nje,na mifano tunayo (Kibaki, Bakili Muluzi, Chiluba, etc)...

Hitimisho:

Mimi namuunga mkono Ulimwengu kwa maana kuwa ameandika makala hii kwa kufuata mtazamo mpana zaidi wa kijamii kuliko matashi ya kisiasa.Ndo sababu kila mara hatuachi kusikia "hii hoja ni wapinzani","hii hoja sio ya CCM"...damn!Tunaangalia utaifa au uchama?


Ibambasi kula tano....fagilia waa waaa!!
 
Kama Ulimwengu amekosea tuandike alipokosea, lakini tusiseme anavunja watu moyo.Ukivunjwa moyo na strong criticism you are most probably a weakling ambaye utavunjwa moyo hata na kivuli chako mwenyewe anyway.

Pundit,
Huoni kosa analoandamwa kwalo? ni kusema vyama vyote havina FALSAFA.
Kama hajakosea hapo, basi aje na ushahidi kwa kupitia chama kimoja hadi kingine na kuthibitisha madai yake. Si vyema kufanya majumuisho kama ya samaki mmoja kaoza basi wote wameoza. ILIYOOZA NI CCM YAKE, tena critique zisizo na uthibitisho hazina ustrong wowote. NO empirical evidence no right to disseminate generalization (sijui ndio ujenerali wenyewe)

ULIMWENGU KAMA UNASOMA HAPA, UNADAIWA USHAHIDI WA MADAI YAKO, kama hamna ku-withdraw statement sio kugumu.
 
Ninachoona hapa ni kuwa:

1. Kuna watu hawakubaliani na Ulimwengu kama Ulimwengu katika kuchambua hoja.Kimsingi hawakubaliani naye katika mengi.

2. Kuna watu wanazibwa sana na ushabiki wa vyma kiasi kiasi kwamba chama chao kuambiwa hakina dira it sounds too offensive.

3. Hapa kiachoonekana ni wengi kulalia upande wao,wapo waliochoka na CCM kiasi kwamba juhudi zao ambazo angalau kwa sasa zinaonekana kuleta changes fulani naturally wasingependa kuoneshwa udhaifu wao (ambao kimsingi upo kwani ni WANASIASA tena wa kiafrika).

4. Wapo wanaofikiri kwa kuwa Ulimwengu ni drop-out wa CCM/system na mtu anayeonekana kutofautiana na waliopo madarakani na kwa kuwa ni (undisputedly) influential figure kwa jamii yetu,basi baadhi yetu tungependa kumwona akielema upande wa wapinzani,yaani awasifu kwa mabo yanayoendelea kwa sasa nchini (in short awe strategist wao,so to say) ndio hao wanaolalamika kuwa anawavunja moyo.

5. Hii inathibisha kwamba kumbe vyama vyote viko sawa kabisa tofauti ni kwamba kimoja kiko madarakani vingine viko nje,na mifano tunayo (Kibaki, Bakili Muluzi, Chiluba, etc)...

Hitimisho:

Mimi namuunga mkono Ulimwengu kwa maana kuwa ameandika makala hii kwa kufuata mtazamo mpana zaidi wa kijamii kuliko matashi ya kisiasa.Ndo sababu kila mara hatuachi kusikia "hii hoja ni wapinzani","hii hoja sio ya CCM"...damn!Tunaangalia utaifa au uchama?

Lengo la kuchaguliwa kwa hao unaowataja,ni kwamba it was a necessary evil.Sio kwamba lilikuwa chaguo bora,ilikuwa ni kipindi cha mpito kutoka siasa za kikiritimba kwenda siasa zenye kutafuta mabadiliko endelevu.Hiyo imejionyesha Kenya,Kibaki amesalimishwa aibu kiutu-uzima naamini kabisa kosa kama hilo la tume ya uchaguzi halitarudiwa.Natoa rai kwa wanamageuzi msikatishwe tamaa na cynism hivyo ni vikwazo vya kuvivuka kufikia mafanikio na ni dalili ya kudhoofika kwa mawazo ya hofu.
 
Nahisi watu wengi wamemiss point , Ulimwengu either ajui alikuwa anaongelea nini au amechanganya mambo . Kichwa cha habari na habari yenyewe haviendani kabisa .Kwanza kabisa ni lazima Ulimwengu atambue ya kuwa tatizo linalokabili nchi yetu sio itikadi wala sheria zetu bali ubinafsi wa viongozi wetu.Huu ni utamaduni mbaya sana ulioshamiri kwenye nchi yetu mpaka hapo tutakapoutokomeza ..... Tatizo kubwa watanzania tunakariri sana hatuko creative at all, nataka Ulimwengu aniambie ni itikadi Kagame anazotumia kujenga uchumi kwa kasi ya ajabu . Nadhani tunahitaji kiongozi mwadilifu na visionary hivi vitu vingine vitakuja tuu...

Halafu pia statement zake nyingi ziko too vague hakuna substance waungwana kusema vyama vingi Afrika havina itikadi bila ya kucite source information ni kudanganya. Mimi nadhani itakuwa vizuri kwa ulimwengu kuchambua vitu kwa undani kabla ya kuanza kutoa lawama ambazo anashindwa kuzi-backup .
 
Back
Top Bottom