Jenerali Ulimwengu na makala zake

Mimi nafikiri Ulimwengu angesema kuwa hajazisoma au hakubaliani na itikadi za vyama vya siasa vilivyopo sasa TZ. Kusema kwamba vyama havina itikadi ni dharau na wakati mwingine ni kujaribu prove a self fullfilling prophecy. Kuna watu hapa duniani hawawezi kuona jambo la maana linafanyika hadi wawe wameshiriki wao. Ninaogopa kusema kwamba Ulimwengu ni moja wao. Moja ya uthibitisho wa hili ni ukweli kwamba Ulimwengu ni mwandishi mzuri lakini baada ya Rai kutekwa nyara hakuandikia gazeti lolote hadi alipoanzisha gazeti lake tena. Hapa maanake ni kwamba hakuona gazeti lolote la maana baada ya Rai.
 
Mimi nafikiri Ulimwengu angesema kuwa hajazisoma au hakubaliani na itikadi za vyama vya siasa vilivyopo sasa TZ. Kusema kwamba vyama havina itikadi ni dharau na wakati mwingine ni kujaribu prove a self fullfilling prophecy. Kuna watu hapa duniani hawawezi kuona jambo la maana linafanyika hadi wawe wameshiriki wao. Ninaogopa kusema kwamba Ulimwengu ni moja wao. Moja ya uthibitisho wa hili ni ukweli kwamba Ulimwengu ni mwandishi mzuri lakini baada ya Rai kutekwa nyara hakuandikia gazeti lolote hadi alipoanzisha gazeti lake tena. Hapa maanake ni kwamba hakuona gazeti lolote la maana baada ya Rai.

Kitila

Umesema maneno ya mazito sana. Kwanini usiandike makala ya kumjibu ulimwengu kabla hajaendeleza msimamo wake huu katika makala zinazofuata? Nani ana anwani ya Ulimwengu tumtumie link haya hii thread aone mawazo ya wananchi ya watu wengine kuhusu makala yake?

Naona Mnyika aliwahi kuandika mwaka jana kuhusu suala hili la itikadi na falsafa katika gazeti la Rai

http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_23.html

Hivi kwanini aliishia katika kuandika kabla ya kufikia utawala wa Kikwete? au amemwogopa Kikwete?

Asha
 
Hata CCM wana itikadi lakini je wanatekeleza? Unaweza kuandika itikadi yako lakini kama unaitumia tu kama njia ya kudanganyia wananchi na huitekelezi kwa matendo, ni kupoteza muda bure.

Vyama vijitahidi kuja na itikidi ambazo kweli wanaziamini na wanaweza kutekeleza na sio mambo kibao wakati wanatekeleza vitu tofauti kabisa.



CHADEMA mbona wanatekeleza wanachokisema? Nenda halmashauri ya Karatu iliyo chini ya CHADEMA au fuatilia michango ya wabunge wa CHADEMA bungeni uone kama haiendani na falsafa na itikadi ya CHADEMA.

Soma Makala ya Mbowe kwenye Tanzania Daima

http://www.chadema.net/makala/mbowe/mbowe_27.html

Makala nyingine ya Mbowe:
http://www.chadema.net/makala/mbowe/mbowe_28.html

Soma hapa pia ameendelea kujadili kuhusu falsafa na itikadi:

http://www.chadema.net/makala/mbowe/mbowe_29.html

Sasa haya yaliandikwa magazetini: Je, ulimwengu hakuyasoma? Na haya yanazungumzwa pia katika ziara za vijijini, Je, ulimwengu hajawahi kusikia?

Lakini je, watanzania wanapenda kusikia kuhusu ITIKADI au kuhusu UFISADI?

Asha
 
Mimi nafikiri Ulimwengu angesema kuwa hajazisoma au hakubaliani na itikadi za vyama vya siasa vilivyopo sasa TZ. Kusema kwamba vyama havina itikadi ni dharau na wakati mwingine ni kujaribu prove a self fullfilling prophecy. Kuna watu hapa duniani hawawezi kuona jambo la maana linafanyika hadi wawe wameshiriki wao. Ninaogopa kusema kwamba Ulimwengu ni moja wao. Moja ya uthibitisho wa hili ni ukweli kwamba Ulimwengu ni mwandishi mzuri lakini baada ya Rai kutekwa nyara hakuandikia gazeti lolote hadi alipoanzisha gazeti lake tena. Hapa maanake ni kwamba hakuona gazeti lolote la maana baada ya Rai.

Nafikiri Ulimwengu yuko sahihi.Hizo sio itikadi maana hawanfanyi kama zinavyodai itikadi zao.Chama gani chenye itikadi ya ufisadi?
Magazeti yapo sawa lakini si unayajua Kitila.Ulimwengu anataka gazeti makini.
Kusema ukweli sijui kama mtu au watu wanajua itikadi au njia ya kwenda huko kwenye maendeleo ya kweli.Kama wapo wajitokeze na itikadi zao kwa matendo.Kama ulimwengu na wenzake wa aina hiyo wakaanzisha chama basi vizuri.
 
Historia haijafikia tamati

Jenerali Ulimwengu
Aprili 23, 2008


KUKOSEKANA kwa mwelekeo ndani ya chama si ugonjwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) peke yake. Ni kweli kwamba kwa muda mrefu hicho ndicho kilichokuwa chama pekee nchini, lakini hili halikukifanya kiwe pekee kupoteza dira miongoni mwa vyama vya nchi za Bara la Afrika.

Kwa hakika katika makala zangu za mwanzo kabisa za mfululizo huu nilikwisha kutoa rai kwamba vyama karibu vyote vya nchi za Kiafrika, hata vile vilivyoanza vikiwa na mwelekeo ulioeleweka, havina tena maaana yo yote ya kifalsafa na kiitikadi.

Katika mazingira yetu mapya (ya “vyama vingi”) ugonjwa uliokuwa wa chama-tawala umeambukizwa kwa vyama vilivyozaliwa kuanzia mwaka 1992 na kuendelea.

Navyo vimeanzishwa, na vimeendelea kufanya kazi zake, bila kuwa na misingi yo yote ya kifalsafa.

Hali hii si ya kushangaza, si hapa kwetu wala duniani. Kwa muda mrefu kidogo,(labda miongo miwili hivi) dunia imekuwa ikiambiwa kwamba sasa tumefikia tamati ya historia, na kwamba masuala makuu yote yaliyosababisha malumbano, mifarakano na mapigano na vita kuu, sasa yametatuliwa kimsingi, na kilichobaki ni vijineno vyepesi vyepesi ambavyo havina uzito mkubwa katika mahusiano miongoni mwa binadamu, kati ya matabaka na wala baina ya mataifa.

Hii ndiyo injili iliyohubiriwa na baadhi ya wasomi wazito katika utetezi wa hali ilivyokuwa baada ya “Vita Baridi” kwisha na Marekani na nchi za Magharibi kupata ushindi dhidi ya himaya ya Sovieti. Kazi imekwisha, tumeshindwa, twendeni nyumbani, kwani hatuna cha kujadili tena.

Maana ya mtazamo huu ni kwamba hatuna budi kukubali hali kama ilivyo na wala tusijisumbue kujaribu kuibadilisha kwa sababu hata tungetaka tunsingeweza kuibadilisha.

Kila kitu kimekwisha kuamuliwa, matatizo yote yametatuliwa, na sasa tunachohitaji ni kujipanga upya katika himaya mpya iliyotamalaki duniani chini ya diktat (imla) mpya ya Marekani, hali ambayo imebatizwa jina la pax americana, au amani kama ilivyopangwa na Marekani.

Kwa maneno mengine, tunachoambiwa ni, “Kubalini yaishe. Tumeshindwa nanyi mmeshindwa. Hamna chenu tena, na wale watakaojidai kufurukuta tutawashughulikiwa kwa nguvu zetu zote, nao watajuta. Baadhi yenu mtakaodiriki kupinga ukweli huu usiopingika tutawanyima misaada, na baadhi yenu mnatakaozidisha ukorofi tutawachapa.

Tunao uwezo wa kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia, kijeshi na kiutamaduni na ninyi hamna uwezo wo wote. Mnaweza kufanya nini bila sisi?”

Watawala wetu walio wengi katika nchi nyingi za Afrika wameikubali injili hii bila kuisaili. Hakuna wanachofanya bila kuzungumiza “wafadhili” na miradi mingi ambayo ingekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi imekuwa ikiwekwa pembeni kwa muda mrefu kwa sababu eti “hajapatikana mfadhili”. Wafadhili wanatafutwa hata pale ambapo rasilimali zetu wenyewe zingetosha kabisa bila kumsubiri ye yote.

Ujuha huu ndio unaotufanya tuachie mali zetu zichukuliwe na wageni kwenda kuwaneemesha watu wao ughaibuni wakati watu wetu wanaendelea kuishi maisha ya mbwa nchini mwao. Ndivyo hivyo tulipofikia hali ya nchi za Kiafrika zenye rasilimali kubwa sana ndizo pia zinazoongoza kwa kuwa na raia hohe hahe.. Nigeria, Angola, Kongo, na nyingine.

Ndivyo hivyo tulipofikia mahali nchini Tanzania kwamba watawala wetu wala hawajui ni kiasi gani cha dhahabu kinachimbwa nchini na kupelekwa nje. Kisa? Wafadhili wanajua, na wakijua inatosha. Ujuha mkubwa kuliko huo unatoka wapi.

Na hao “wafadhili” wanawapongeza na kuwasifu watawala wetu kwa kuwa “wamefungua milango”, “wanaheshimu wawekezaji” na “wanainua uchumi wa nchi”.

Kiwango cha ujuha wa watawala wetu kinatisha. Tangu serikali ya “awamu ya tatu” (Sijui kwa nini wanaziita awamu, kwani binafsi naona awamu moja ndeeefu ya umasikini usio na maelezo) tumekuwa na serikali zilizojaa mawaziri na makatibu wakuu na watawala wengine wenye digrii za uzamili na udaktari wa kila aina. Hawa wamesoma hapa nchini na katika vyuo vikuu vya pembe zote za dunia, na wanapozungumza katika semina utadhani wana akili.

Lakini mara nyingi wanachofanya wakiwa wamekabidhiwa madaraka ya uongozi ni ujuha mtupu. Au ni ujuha kweli? Inawezekana si ujuha kwa upande wao, bali ni ujuha kwa upande wetu, sisi tunaoendelea kuwapa madaraka, tena kwa kuwapigia kura wakati tumekwisha kuona mara kadhaa, na kwa muda mrefu, kwamba maslahi yao hayapatikani katika utumishi kwa wananchi bali katika kushibisha matumbo yao.

Sasa, inapotokea, kama inavyotokea leo, kwamba wakubwa wa dunia walioshinda “Vita Baridi” ambao wanatuambia kwamba “tukubali yaishe,” wakakutana na watawala wetu wanaosaka nafasi za uongozi kwa udi na uvumba, na haya makundi mawili yakakubaliana jinsi watakvyozitafuna nchi zetu, ujue tumeliwa.

Ubia baina ya wakuu wa dunia na wakuu wetu, ubia huu haramu ndicho kiama chetu wananchi wa kawaida na hatimaye mataifa yetu yote.

Nimewaona watawala wetu wanavyovaa tabasamu paaana wanaposifiwa na wakuu wa nchi za Magharibi, kama mtoto wa shule ya msingi anavyotabasamu anaposifiwa na kutolewa mfano na “hedi masta” wake. Na kweli, uhusiano kati yetu na hao wakubwa ni huo huo, wa mtoto wa shule na “hedi masta”. Kila anachosema sisi hatuna budi kusema “Yessah.”

Huku tukitabasamu tabasamu zetu za kijuha, mali zetu zinayoyoma. Madini yetu yanasafirishwa nje ya nchi kwa bei ya bure, si kwa kutoroshwa na wageni, bali kwa kusindikizwa na watawala wetu wenyewe. Wakuu wetu, hao hao wenye digrii na digrii, wanaingia mikataba ya kitoto, si kwa sababu hawajui wanalolifanya, bali kwa sababu hao wameingia ubia na mabeberu ambao kimsingi wamewanunua na kuwageuza wapagazi wao.

Fikiria hili; Kampuni la kibeberu linahitaji kuwekeza katika sekta fulani nchini. Ili kampuni hilo likubaliwe kuwekeza linahitajika lifuate taratibu kadhaa, ikiwa ni pamoja na kujali mazingira, kujali maslahi ya wananchi watakaoathirika na uwekezaji huo, kuzingatia viwango vya kodi na vile vya mapato mengine yaliyowekwa na Bunge, n.k.

Hasara zinazoweza kutokana na kutokujali mazingira labda hazipimiki katika mizania ya fedha, lakini zinaweza kuwa kubwa, zisizotabirika na za muda mrefu. Lakini katika eneo la mapato ya serikali hasara zinazotokana na kutokujali kwa watawala wetu zinapimika kwa sababu vipo viwango vinavyotambulika kimataifa.

Kwa kila mkataba wa “uwekezaji” uliotiwa saini katika kipindi cha miaka 20 iliyopita tunaweza kukadiria ni kiasi gani cha fedha nchi imepoteza kutokana na huo ujuha usiokuwa ujuha wa watawala wetu na maofisa wao, ambao kwa kupewa “shangingi” moja ambalo bei yake haizidi shilingi milioni 80 watagawa bure kwa wageni mali za Taifa zenye thamani ya shilinggi bilioni 500.

Huu si ujuha bali ni ugonjwa wa akili.

Katika hali ya nchi zetu zilizoelemewa na umasikini, ujinga na maradhi, hali kama hii haiwezi kuachiwa iendelee kwa sababu tu tumeambiwa kwamba huu ndio mwisho wa historia na masuala yote makuu yamekwisha kushughulikiwa. Hatuwezi kukubali ujuha kama huu uendele kwa kuegemea mantiki-kilema.

Lakini inaelekea watawala wetu wanakubali ujuha huu uendelee, alimradi wakuu wanawasifu na kuwamwagia “misaada”!.

Ndiyo maana Rais Benjamin Mkapa alikuwa haelewi ni kwa nini watu wa ndani wanamsakama wakati wakuu wa nchi za nje wanamsifu. Kana kwamba hao ndio waliomchagua!


Itaendelea wiki ijayo....

Ujumbe wa Ulimwengu ni huu hapa, labda tuuchambue kwa kina, huku tukizingatia ukweli kwamba Ulimwengu amekuwa kwenye political system yetu kwa muda mrefu sana na rafiki wa karibu sana wa mkapa!
 
Ndugu Ulimwengu,
Kama walivyo watanzania wote, nawe unao uhuru wa kutoa maoni.Aidha jambo moja ni hakika 'some opinions are not based on facts'
Baki na maoni yako lakini usiupotoshe umma, nakuhakikishia vyama vinazo falsafa, kama huzitaki sema hilo.
Kwa uungwana katika mwendelezo wa makala yako, ni vyema ututake radhi.
 
Nini maana ya Itikadi?

Nini maana ya falsafa?

Je ufuataji wa siasa za mirengo ya kushoto au kulia kunaweza kubainisha falsafa na itikadi za chama?

Je viongozi na vyama vinafanya kazi gani na kutumia nguvu gani kujiuza na kuhakikisha kuwa "Itikadi" na "Falsafa" za vyama hivi vinawiana na maisha na mienendo ya jamii?

Mfano, na fikiri Itikadi ya CCM ni Ujamaa na Kujitegemea. Falsafa ya CCM ni kuwa Kila binadamu ni sawa.

Kwa kuangalia hizo Falsafa na Itikadi za CCM ambazo tumekuwa nazo kwa miaka nenda rudi, je ni kweli CCM bado inatimiliza siasa zake za Mrengo wa kijamaa ambazo zinawiana na Itikadi na Falsafa yake?

Je viongozi na wanachama wake wanafuatilia Itikadi na Falsafa hizi?

Wenzetu, siasa zimegawanyika katika makundi matatu, Conservative (siasa kali), Centrist (not too conservative and not too liberal) na Liberals (Hakuna mikingamo sana).

Niliwahi kuuliza swali hili mara kadhaa kuwa Siasa zetu Tanzania na Afrika kwa ujumla, je zinachukua mkondo gani nyakati hizi za mageuzi ya kiuchumi na kisiasa duniani?

Labda tukichukulia kuliangalia hili suala la makala ya Ulimwengu kwa kutumia vigezo hivyo tunaweza kumuelewa na kujenga hoja kumjibu.
 
Mimi nafikiri Ulimwengu angesema kuwa hajazisoma au hakubaliani na itikadi za vyama vya siasa vilivyopo sasa TZ. Kusema kwamba vyama havina itikadi ni dharau na wakati mwingine ni kujaribu prove a self fullfilling prophecy. Kuna watu hapa duniani hawawezi kuona jambo la maana linafanyika hadi wawe wameshiriki wao. Ninaogopa kusema kwamba Ulimwengu ni moja wao. Moja ya uthibitisho wa hili ni ukweli kwamba Ulimwengu ni mwandishi mzuri lakini baada ya Rai kutekwa nyara hakuandikia gazeti lolote hadi alipoanzisha gazeti lake tena. Hapa maanake ni kwamba hakuona gazeti lolote la maana baada ya Rai.

..kwanini aandikie gazeti lingine wakati alikuwa na nia na uwezo wa kuanzisha la kwake?

..au na ile tv anayoendesha kipindi ni ya kwake?

..kimsingi nakubaliana na alichokisema ulimwengu!
 
Kitila

Umesema maneno ya mazito sana. Kwanini usiandike makala ya kumjibu ulimwengu kabla hajaendeleza msimamo wake huu katika makala zinazofuata? Nani ana anwani ya Ulimwengu tumtumie link haya hii thread aone mawazo ya wananchi ya watu wengine kuhusu makala yake?

Naona Mnyika aliwahi kuandika mwaka jana kuhusu suala hili la itikadi na falsafa katika gazeti la Rai

http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_23.html

Hivi kwanini aliishia katika kuandika kabla ya kufikia utawala wa Kikwete? au amemwogopa Kikwete?

Asha

..mkitaka kumjibu vizuri ulimwengu,mjibuni kwa matendo zaidi!

..ninyi hamna tafauti sana na ccm,tofauti iliyopo[ukiondoa mambo mengine] ni kuwa mko upinzani!
 
Ujumbe wa Ulimwengu ni huu hapa, labda tuuchambue kwa kina, huku tukizingatia ukweli kwamba Ulimwengu amekuwa kwenye political system yetu kwa muda mrefu sana na rafiki wa karibu sana wa mkapa!

..ndio maana alimsakama kwenye suala la uraia?wakati akijua na wake una utata?
 
Ujumbe wa Ulimwengu ni huu hapa, labda tuuchambue kwa kina, huku tukizingatia ukweli kwamba Ulimwengu amekuwa kwenye political system yetu kwa muda mrefu sana na rafiki wa karibu sana wa mkapa!

FMES,

Kuwa rafiki haina kuwa ni mshiriki mzuri. Urafiki wao ni batili baada ya yule ambaye alikuwa rafiki wa kweli, kuongea ukweli kwa rafikiye.

Ikiwa katika urafiki wetu utaniambia kitu cha wazi na ukweli, nami nikachukia kwa kuwa sitakikuambiwa ukweli wa mambo na kuanza kukuzushia mambo hata kukuhujumu, basi mimi si rafiki mwema tena.

Makala bado inaanza, ni nzuri, lakini sijaona mnyumbulisho wa Itikadi na Falsafa jinsi mada hii ilivyoliweka. Hivyo tusubiri toleo lijalo au tupitie toleo lilopita.
 
Ndiyo maana kuna watu wanasema, baadhi ya watu wanaweka mbele maslahi ya chama kuliko ya Taifa, asilimia kubwa ya makala ya Ulimwengu imezungumzia rasilimali za taifa, tabia za viongozi wetu mintaarafu kutokuweka maslahi ya taifa mbele, lakini kwa sababu Ulimwengu kagusia kwamba vyama vya siasa havina itikadi, basi looh salaaale, watu wanataka aombe radhi!. badala ya kujibu kwa hoja watu wanaanza eti kwa nini Ulimwengu alipoondoka rai hakwenda kuomba kibarua kwenye gazeti lingine utadhani kwamba wao ndo wanampangia ulimwengu aishi vipi.

My take mkosoeni Ulimwengu kwa hoja siyo kwa kumshambulia yeye binafsi.
 

My take mkosoeni Ulimwengu kwa hoja siyo kwa kumshambulia yeye binafsi.


Hamna mtu anayemshambulia Ulimwengu binafsi. Ambacho tunasema hapa ni kwamba kusema kwamba vyama vyote TZ vinafanana na havina itikadi ni oversimplication of a complex phenomenon. Kuna lundo la vitabu vimeandikwa kuhusu itikadi ya vyama vya siasa na waandishi karibu wote hitimisho lao ni hili: "Parties are as easy to regonise but as difficult to define their ideological stance as elephant"! Ndio maana hata nchi kama Uingereza ambavyo vyao vyao vikuu vya Conservatives na Labour vina miaka nenda rudi hadi leo hii hakuna mtu anayeweza kukupa clear ideological stance zao lakini haina maana kwamba watu hawawezi kuvitofautisha hivi vyama. Ulimwengu ana haki ya kukataa misimamo ya vyama vya siasa Tanzania lakini hana haki ya kuwachanganya wananchi kwa kuwaambia kwamba vyama vyote vinafanana! Anachojaribu kusema Ulimwengu ni sawa na kusema kwamba vyama vyote havifai, sasa hiyo ni kuleta confusion na kujaribu kuwanyima wananchi uhuru wa kuchagua miongoni mwa vyama tulivyo navyo. Hatuwezi kwenda nchi zingine kuazima vyama vyao vya siasa vije kutuongoza, so practically and pragmatically we have to work with the people, and by extension, with the parties we have.
 
Ndiyo maana kuna watu wanasema, baadhi ya watu wanaweka mbele maslahi ya chama kuliko ya Taifa, asilimia kubwa ya makala ya Ulimwengu imezungumzia rasilimali za taifa, tabia za viongozi wetu mintaarafu kutokuweka maslahi ya taifa mbele, lakini kwa sababu Ulimwengu kagusia kwamba vyama vya siasa havina itikadi, basi looh salaaale, watu wanataka aombe radhi!. badala ya kujibu kwa hoja watu wanaanza eti kwa nini Ulimwengu alipoondoka rai hakwenda kuomba kibarua kwenye gazeti lingine utadhani kwamba wao ndo wanampangia ulimwengu aishi vipi.

My take mkosoeni Ulimwengu kwa hoja siyo kwa kumshambulia yeye binafsi.
Gamaba la nyoka,
Zingatia ni nini zaweza kuwa athari za kauli ya Jenerali kwamba vyama havina misingi ya kifalsafa. hapa si suala la kutanguliza maslahi ya vyama. Kauli kama hiyo aliyoiandika inatosha kabisa kudhohofisha jitihada zote za wanamageuzi nchini. Jiulize kauli ya Mwalimu aliposema wapinzani hawana sera iliudhohofisha kiasi gani mfumo wa mageuzi nchini. Aliitoa kauli hiyo wakati akimnadi 'Mr. Clean'
Au fikiria kauli kama za akina Jaji Warioba aliyepata kusema, tuna chama kimoja na wapiga kelele 17
Vijineno kama hivi vinavuruga sana harakati za kuwang'oa mafisadi, mara utasikia wengine wanasema, wapinzani hawana jipya, na kisha watu wanawaamini kwa sababu ya umaarufu wao.
Maslahi ya taifa hayawezi kulindwa au kutetewa kwa kutoa kebehi za kudhalilisha vyama vinavyotetea maslahi hayo hayo.
Aondoe kauli yake hiyo, hayo mengine aliyoyaandika ni ugonjwa ulioko kwenye chama ambacho yeye ni mwanachama. kama ana nia ya dhati ya kuutibu aje kambi ya mageuzi tushirikiane badala ya kuvunja watu moyo.
 
KUKOSEKANA kwa mwelekeo ndani ya chama si ugonjwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) peke yake. Ni kweli kwamba kwa muda mrefu hicho ndicho kilichokuwa chama pekee nchini, lakini hili halikukifanya kiwe pekee kupoteza dira miongoni mwa vyama vya nchi za Bara la Afrika.

CCM haikuwahi kuwa na dira hata simu moja, isipokuwa ilikuwa na maneno yaliyopangiliwa kielimu kwenye vitabu na kuonekana kana kwamba ni muelekeo wa CCM, lakini ukweli ni kwamba kama uliwahi kuwepo, basi ulikuwa ni muelekeo wa Mwalimu peke yake, au binafsi, regardless kama ulikuwa mzuri au mbaya kwa taifa, lakini karibu wananchi wote wa Tanzania tunakubaliana kuwa Mwalimu, siku zote alikuwa na nia njema kwa taifa.

Sasa kwa sababu muelekeo haukuwepo anyways, si kweli kwamba umepotea au eti dira imepotezwa, katika miaka yetu 45 ya uhuru Tanzania tumekuwa tukitegemea misaaada ya wafadhili, hatujawahi hata mara moja kujitegemea wenyewe kwa bajeti yetu, au kwa kila kitu chetu, tofauti tu ni kwamba under Mwalimu, tulikuwa tunawategemea wa-Russia na China, sasa tumebadilika tunawategemea hata mabepari ambao ndio hasa waliotushinikiza kuanzisha muundo wa vyama vingi vya siasa, meaning kwamba hata akili hiyo sisi binafsi as a nation including Ulimwengu, ambaye enzi hizo alikuwa ni kiongozi wa juu wa CCM, hatukuwa nayo ni akili au idea tuliyopewa na hao hao wazungu ambao CCM iliwakataa kata kata kushirikiana nao kabla ya kwisha kwa vita vya baridi,

Sasa tatizo kubwa la hii article ya Ulimwengu, ni yeye either kwa kutokujua au kwa makusudi, kutokubali kuwa hata kuwa na vyama vingi haikuwa idea yetu, sasa iweje leo tuwe na muelekeo? Hatukupoteza dira yoyote kwa sababu hatukuwahi kuwa nayo, isipokuwa ni Mwalimu tu aliyekuwa na dira yake binafsi, ambayo iliiisha pale tu aliponga'tuka, ndio maana hata alipotoka hakutuambia sababu, alijua kuwa katika miaka yake yote ya uongozi, hakuweza kuwaelewesha wananchi dira yake wakaielewa na kuikubali,

Kwa hiyo kwako Ulimwengu, unless wewe unaifahamu hiyo dira utuwekee kwenye makala yako nyingine, ukweli ni kwamba hatukuwa nayo anyaways, sasa ni waste of time kujadili something we never had!

Kwa hiyo mkuu Gamba, ndio maana hapa wananchi wanamshambulia Ulimwengu, binafsi ni sawa kabisa kwa sababu hana hoja!
 
Nini maana ya Itikadi?


Wenzetu, siasa zimegawanyika katika makundi matatu, Conservative (siasa kali), Centrist (not too conservative and not too liberal) na Liberals (Hakuna mikingamo sana).

Niliwahi kuuliza swali hili mara kadhaa kuwa Siasa zetu Tanzania na Afrika kwa ujumla, je zinachukua mkondo gani nyakati hizi za mageuzi ya kiuchumi na kisiasa duniani?

Labda tukichukulia kuliangalia hili suala la makala ya Ulimwengu kwa kutumia vigezo hivyo tunaweza kumuelewa na kujenga hoja kumjibu.

Rev Kishoka: Huku nyuma tulijadili sana hili hapahapa kwenye forum. Vilevile, kulikuwa na makala mfulilizo zilizokuwa zina debate ideological positions ya CHADEMA na CCM kati ya Prince Bagenda, Kafulila na mimi mwenyewe. Kwa siyo kweli kwamba mjadala wa itikadi ndio anaanzisha ulimwengu leo, umekuwepo na utaendelea kuwepo kwa sababu ni subject complex na haiwezi kuwa na a clear cut consensus.

Kimsingi misimamo ya vyama vya siasa kiitikadi huwa inayumba na kubadilika kutokana na kiongozi wa chama kwa kipindi husika. Na ndivyo ambavyo imekuwa ikitokea Tanzania. Kifalsafa, CCM ilikuwa tofauti wakati wa Nyerere, ikawa tofauti wakati wa Mwinyi na Mkapa. Tatizo likaja kwa JK. Yeye alisema hatabadilisha chochote bali atapokea kijiti tu. Kwa hiyo kimsingi na kwa mujibu wa JK CCM ya leo ni ileile ya wakati wa Mkapa lakini ni tofauti kabisa na wakati wa Mwinyi na Nyerere!

Labda nijibu swali lako kidogo kwa kuhusu vilipo vyama vya siasa Tanzania in the left-centre-right political continuum. Nitajaribu kuibu hili kwa kutumia mfano wa CHADEMA. Mzee Mtei wakati anaanzisha CHADEMA alikuwa anajaribu ku-counter failure za sera za CCM chini ya Mwalimu Nyerere hasa katika uchumi, tofauti ambayo ndiyo iliyomtoa katika serikali ya mwalimu. Sera kubwa ambazo mzee Mtei alikuwa anazipinga ni zile za serikali kuhodhi kila kitu katika uendeshaji wa uchumi ikiwemo kuminya sector binafsi pamoja na kuzuia mfumo wa vyama vingi katika mambo ya siasa. Alikuwa anataka pia kukuza uhuru wa watu binafsi katika mchakato wa kujitafutia maisha kiuchumi na ushiriki wao katika mambo ya siasa na kijamii. Kwa hiyo katika continum ya left-centre-right politics alikusudia chadema iende kulia kabisa wakati CCM ilitarajiwa kuendelea kubaki kushoto. Hii maana yake ni kwamba kama CHADEMA ingepata nafasi ya kuendesha serikali kipindi hicho tungeshuhudia: sekta binafsi ikikua, serikali kujivua jukumu la kuendesha mambo ya biashara, kuwajengea watu binafsi uwezo wa kiuchumi na na ushiriki wao katika mambo ya siasa kupanuka zaidi ikiwemo kuruhusiwa watu kugombea nafasi za uongozi bila kuwa mwanachama wa chama chochote. Kwa hiyo kiuchumi, kimsingi, kama CHADEMA ingeshinda serikali ingekuwa na mwelekeo wa sera ambazo Mkapa alijaribu kuzitekeleza bila mafanikio.

Hata hivyo baada ya Mtei kuondoka kwenye nafasi ya uenyekiti kumetokea na kumeendelea kutokea mabadaliko katika mwelekeo wa kifalsfa na kiitikadi. kwa mfano, mzee Bob Makani yeye alijaribu kuipeleka CHADEMA katikati (centre) ambayo iliifanya CHADEMA ionekana ni liberal zaidi. Tatizo moja la siasa za uliberali ni kwamba mnaonekane kama mnakubaliana na chochote madamu mtu ampependa kufanya na hakimuathiri mtu mwingine. Ndio maana vyama vinavyofuata siasa za uliberali huwa havina mvuto sana na unaweza kuelewa kwa nini CHADEMA wakati wa Mtei ilikuwa imepooza na kupoa sana.

CHADEMA chini ya Mbowe ningeweza kusema inafuata a realistic and practical attitude approach which is increasingly becoming a dominant ideology in the contemporary political world in general, and in developing countries in particular. Hapa ni kwamba CHADEMA itatekeleza what will give the best value to the tax payers’ money and which will take the country forward as fast as is practicable and possible.

Kwa hiyo kusema kwamba vyama vyote vyta siasa Tanzani vinafanana kifalsafa na kiitikadi kama anavyodai Ulimwengu ni ukipofu wa kisiasa. Tunamshauri Ulimwengu avisome tena hivi vyama akiwa open minded atatambua tofauti zao.
 
Nini maana ya Itikadi?

Nini maana ya falsafa?

Je ufuataji wa siasa za mirengo ya kushoto au kulia kunaweza kubainisha falsafa na itikadi za chama?

Je viongozi na vyama vinafanya kazi gani na kutumia nguvu gani kujiuza na kuhakikisha kuwa "Itikadi" na "Falsafa" za vyama hivi vinawiana na maisha na mienendo ya jamii?

Mfano, na fikiri Itikadi ya CCM ni Ujamaa na Kujitegemea. Falsafa ya CCM ni kuwa Kila binadamu ni sawa.

Kwa kuangalia hizo Falsafa na Itikadi za CCM ambazo tumekuwa nazo kwa miaka nenda rudi, je ni kweli CCM bado inatimiliza siasa zake za Mrengo wa kijamaa ambazo zinawiana na Itikadi na Falsafa yake?

Je viongozi na wanachama wake wanafuatilia Itikadi na Falsafa hizi?

Wenzetu, siasa zimegawanyika katika makundi matatu, Conservative (siasa kali), Centrist (not too conservative and not too liberal) na Liberals (Hakuna mikingamo sana).

Niliwahi kuuliza swali hili mara kadhaa kuwa Siasa zetu Tanzania na Afrika kwa ujumla, je zinachukua mkondo gani nyakati hizi za mageuzi ya kiuchumi na kisiasa duniani?

Labda tukichukulia kuliangalia hili suala la makala ya Ulimwengu kwa kutumia vigezo hivyo tunaweza kumuelewa na kujenga hoja kumjibu.

Hiyo lebo ya conservative kuwa siasa kali mimi naikataa. Ni kali kivipi na kwa kipimo gani? Kwa sababu hata mimi conservative nawaona maliberali wa mlengo wa kushoto kabisa kuwa na siasa kali. Sasa kwa nini ukiwa Conservative unabatizwa kuwa na siasa kali? Hizo siasa kali ni zipi?
 
Rev Kishoka: Huku nyuma tulijadili sana hili hapahapa kwenye forum. Vilevile, kulikuwa na makala mfulilizo zilizokuwa zina debate ideological positions ya CHADEMA na CCM kati ya Prince Bagenda, Kafulila na mimi mwenyewe. Kwa siyo kweli kwamba mjadala wa itikadi ndio anaanzisha ulimwengu leo, umekuwepo na utaendelea kuwepo kwa sababu ni subject complex na haiwezi kuwa na a clear cut consensus.

Kimsingi misimamo ya vyama vya siasa kiitikadi huwa inayumba na kubadilika kutokana na kiongozi wa chama kwa kipindi husika. Na ndivyo ambavyo imekuwa ikitokea Tanzania. Kifalsafa, CCM ilikuwa tofauti wakati wa Nyerere, ikawa tofauti wakati wa Mwinyi na Mkapa. Tatizo likaja kwa JK. Yeye alisema hatabadilisha chochote bali atapokea kijiti tu. Kwa hiyo kimsingi na kwa mujibu wa JK CCM ya leo ni ileile ya wakati wa Mkapa lakini ni tofauti kabisa na wakati wa Mwinyi na Nyerere!

Labda nijibu swali lako kidogo kwa kuhusu vilipo vyama vya siasa Tanzania in the left-centre-right political continuum. Nitajaribu kuibu hili kwa kutumia mfano wa CHADEMA. Mzee Mtei wakati anaanzisha CHADEMA alikuwa anajaribu ku-counter failure za sera za CCM chini ya Mwalimu Nyerere hasa katika uchumi, tofauti ambayo ndiyo iliyomtoa katika serikali ya mwalimu. Sera kubwa ambazo mzee Mtei alikuwa anazipinga ni zile za serikali kuhodhi kila kitu katika uendeshaji wa uchumi ikiwemo kuminya sector binafsi pamoja na kuzuia mfumo wa vyama vingi katika mambo ya siasa. Alikuwa anataka pia kukuza uhuru wa watu binafsi katika mchakato wa kujitafutia maisha kiuchumi na ushiriki wao katika mambo ya siasa na kijamii. Kwa hiyo katika continum ya left-centre-right politics alikusudia chadema iende kulia kabisa wakati CCM ilitarajiwa kuendelea kubaki kushoto. Hii maana yake ni kwamba kama CHADEMA ingepata nafasi ya kuendesha serikali kipindi hicho tungeshuhudia: sekta binafsi ikikua, serikali kujivua jukumu la kuendesha mambo ya biashara, kuwajengea watu binafsi uwezo wa kiuchumi na na ushiriki wao katika mambo ya siasa kupanuka zaidi ikiwemo kuruhusiwa watu kugombea nafasi za uongozi bila kuwa mwanachama wa chama chochote. Kwa hiyo kiuchumi, kimsingi, kama CHADEMA ingeshinda serikali ingekuwa na mwelekeo wa sera ambazo Mkapa alijaribu kuzitekeleza bila mafanikio.

Hata hivyo baada ya Mtei kuondoka kwenye nafasi ya uenyekiti kumetokea na kumeendelea kutokea mabadaliko katika mwelekeo wa kifalsfa na kiitikadi. kwa mfano, mzee Bob Makani yeye alijaribu kuipeleka CHADEMA katikati (centre) ambayo iliifanya CHADEMA ionekana ni liberal zaidi. Tatizo moja la siasa za uliberali ni kwamba mnaonekane kama mnakubaliana na chochote madamu mtu ampependa kufanya na hakimuathiri mtu mwingine. Ndio maana vyama vinavyofuata siasa za uliberali huwa havina mvuto sana na unaweza kuelewa kwa nini CHADEMA wakati wa Mtei ilikuwa imepooza na kupoa sana.

CHADEMA chini ya Mbowe ningeweza kusema inafuata a realistic and practical attitude approach which is increasingly becoming a dominant ideology in the contemporary political world in general, and in developing countries in particular. Hapa ni kwamba CHADEMA itatekeleza what will give the best value to the tax payers’ money and which will take the country forward as fast as is practicable and possible.

Kwa hiyo kusema kwamba vyama vyote vyta siasa Tanzani vinafanana kifalsafa na kiitikadi kama anavyodai Ulimwengu ni ukipofu wa kisiasa. Tunamshauri Ulimwengu avisome tena hivi vyama akiwa open minded atatambua tofauti zao.

Kitila

Hapa umenikosha kabisa, kwanini haya majibu yako humu usiyaweke kama makala ukamjibu Ulimwengu kupitia Raia Mwema au hata Tanzania Daima?

Nimengalia makala zako nimeona hii kuhusu Itikadi nayo imenigusa sana: http://www.chadema.net/makala/mkumbo/kitila_9.html

Ulimwengu anatakiwa ajibiwe kwa kweli. Kuna mtu ana email address yake anipatie kwenye ashabdala@yahoo.com nimtumie hii link asome huu mjadala unaondelea? Hakika akisoma hapa atabadili mwelekeo wa makala yake ya wiki ijayo

Asha
 
Hamna mtu anayemshambulia Ulimwengu binafsi. Ambacho tunasema hapa ni kwamba kusema kwamba vyama vyote TZ vinafanana na havina itikadi ni oversimplication of a complex phenomenon. Kuna lundo la vitabu vimeandikwa kuhusu itikadi ya vyama vya siasa na waandishi karibu wote hitimisho lao ni hili: "Parties are as easy to regonise but as difficult to define their ideological stance as elephant"! Ndio maana hata nchi kama Uingereza ambavyo vyao vyao vikuu vya Conservatives na Labour vina miaka nenda rudi hadi leo hii hakuna mtu anayeweza kukupa clear ideological stance zao lakini haina maana kwamba watu hawawezi kuvitofautisha hivi vyama. Ulimwengu ana haki ya kukataa misimamo ya vyama vya siasa Tanzania lakini hana haki ya kuwachanganya wananchi kwa kuwaambia kwamba vyama vyote vinafanana! Anachojaribu kusema Ulimwengu ni sawa na kusema kwamba vyama vyote havifai, sasa hiyo ni kuleta confusion na kujaribu kuwanyima wananchi uhuru wa kuchagua miongoni mwa vyama tulivyo navyo. Hatuwezi kwenda nchi zingine kuazima vyama vyao vya siasa vije kutuongoza, so practically and pragmatically we have to work with the people, and by extension, with the parties we have.

Kitila

Ni kweli CHADEMA ni pragramatic! Hivi Ulimwengu hajawahi kusoma makala haya yaliandikwa na David Kafulila kumjibu Profesa Bavu wakati wa uchaguzi 2005?

http://www.chadema.net/makala/kafulila/david_5.html

Yeye si ndie alikuwa mwenyekiti wa habari corporation wakati huo na hii habari ilitoka kwao? Hasomi au amepitiwa?

Asha
 
Ndiyo maana kuna watu wanasema, baadhi ya watu wanaweka mbele maslahi ya chama kuliko ya Taifa, asilimia kubwa ya makala ya Ulimwengu imezungumzia rasilimali za taifa, tabia za viongozi wetu mintaarafu kutokuweka maslahi ya taifa mbele, lakini kwa sababu Ulimwengu kagusia kwamba vyama vya siasa havina itikadi, basi looh salaaale, watu wanataka aombe radhi!. badala ya kujibu kwa hoja watu wanaanza eti kwa nini Ulimwengu alipoondoka rai hakwenda kuomba kibarua kwenye gazeti lingine utadhani kwamba wao ndo wanampangia ulimwengu aishi vipi.

..ndo maana nikasema hawatafautiani sana na ccm!
 
Back
Top Bottom