Jenerali Mabeyo, unayasikia yasemwayo na makomandoo wetu mahakamani kwenye kesi ya Mbowe?

Kwani ni kila askari wa jwtz anaestaafu au kufukuzwa kazi anatendewa hayo waliyotendewa hao ex commandos?
Hao wamejiingiza kwenye vitendo viovu ndiyo maana yamewakuta hayo yaliyowakuta.
Sijui huu ujinga mtauacha lini aisee, je wameshakutwa na hayo makosa mpaka unahitimisha kwamba wamejiingiza kwenye vitendo viovu?? Na yule wa Tabora na wenziwe waliochiwa kwa kuonekana hawana hatia hayo mateso utayalipa wewe?? Mitizamo yenu finyu ya kisiasa unawapumbaza macho na kuonekana mapimbi.
 
Ipo siku utatamani kumeza haya maneno.
Mi naona tufike tu huko, hii dharau kwanza mwanamke halafu kutesa makomandoo ambao ndio icon ya jeshi lolote duniani na taarifa hizo za kudharirisha bora zingekuwa siri zinatolewa hadharani , sijui kijeshi hili limekaaje, mi nahisi JWTZ yote sasa imedharirishwa, na nahisi tuna watu ambao hawajui lolote kwenye mambo ya usalama halafu eti wanasema " , " MIPAKA YETU YOTE IPO SALAMA",
Kama ambavyo tumeona kuna watu wakifika vyeo fulani nchi hii hawaguswi ovyo, nadhani hao jamaa wangeshughulikiwa jeshini.
 
Niliwaahi andika humu, ila shida ni kutafutana.


Mimi Kaka yangu ( mtoto wa mama mkubwa)

Wakiwa pale kambi ya ukomandoo Morogoro...

Posho zao wakawa hawapewi, wakaamua kuja Dar makao makuu JWTZ kulalamikia.


maajabu, wakapewa Kesi za Uhaini, uhujum, uasi, uporaji wa Mali za Raia.


Walikua vijana 60 wa Mafunzo ya ukomando

30 wakasamehewa ...30 Wakafungwa jela mwaka 2015 akiwemo Kaka yangu huyo.


Waziri Mkuu anajua, Mwinyi anajua, Mwanasheria Mkuu wa wakat huo anajua,Mkuu wa Majeshi alopita anajua ..maana suala lao lilijitokeza 2013 .


WAKAFUKUZWA KAZI BILA KUPEWA BARUA YA KUACHISHWA KAZI, BILA KUPEWA MAFAO YAO, IKUMBUKE TOKA HUO MWAKA 2013 MPAKA 2015 ,MISHAHARA YAO ILISIMAMISHWA.


Walikua kuachiwa mwaka 2017 kwa msamaha

mpaka naongea hii Leo, Hawa vijana wamejitahidi kutafuta haki zao sanaaa ,wametumia wanasheria wapiiii..suala lao linaminywa chini chini.






KWA sasa wamebaki vijana 29. ..baada ya mmoja maisha kumchanganya, akaungana kwenye ujambazi,... Alipigwa risasi.
Hao walifeli mkuu, hilo lilikuwa ni test ila wao hawakujiongeza. Walikuwa wanapimwa uwezo wa kutumia maarifa yao kutatua matatizo unapokuwa huna msaada, walipaswa wafanye ukomandoo wapore mamilioni sehemu wajilipe, halafu jw na polisi wangewasiliana, hata daktari mwanafunzi anaweza kukuua akikosea,
 
Semeni nyie mnaoweza kusema. Tangazo la juzi la Msemaji wa Jeshi lilionesha mapungufu makubwa sana. Tulitaraji kama jeshi letu pendwa wangekuja na majina ya matapeli waliokuwa na nia ovu ya kulichonganisha jeshi letu na wananchi.

Jeshi hili lenye heshima kubwa nchini na nje ya nchi lina mbinu nyingi za kiintelijensia na kimedani zingewatia hatiani hao matapeli wanodanganya umma ahadi za ajira
Nilisema mwanzoni mwa msimu huu kuwa, hata mtoto anapokuwa hamuoni baba ana lelewa na single mother kuna saikoloji yake ya kiume inafeli , na wengi hupata madhara ukubwani,
Nilisema hii ni mbaya kwa majeshi yetu, ona sasa, mpaka makomandoo wamelegea hivyo, jeshi lipo tu kimya, halafu eti mipaka yetu ipo salama,
Salama kwa jeshi la hivyo, watu wanawachora tu mnavyoshuka chati, ngoja muishe ndio mtaelewa dunia!
 
kuwatupa mtu mtaani watu wenye mafunzo kama hayo ni hatari. Hata kama walionekana kuchanganyikiwa na hawastahili kukaa jeshini, kuwatupa tu mtaani si sawa, Magonjwa yao karibu wote wanasema yanahusiana na akili, inawezekana ni athari za kivita - tunawatupaje?
Askati wa vyeo vya juu wanapostaafu tunaona wanapewa ukuu wa wilaya, mkoa nk. hata hawa wa chini si vibaya wakawa wanapata kaposho fulani ili kujikimu kimaisha. Kumbukeni Jerry Rawlings hakuwa na cheo kikubwa!
Nchi haina kichwa kwa sasa....
 
Awamu hii pamoja na ya Magufuli ndio awamu JWTZ imedhalilishwa kupita kisi...

Kwanza ni inflitrattion iliyofanyika ya kugawa nafasi za Kisiasa kwa senior oficers wa JWTZ... Maana yake umewa- neutralize totally ukawafanya wanasiasa...

Shame shame shame...
 
Leo hii ukipita kwenye Makambi ya Jeshi kumejaa mafremu ya biashara na ma-bar yamejengwa... Jeshi la wafanya biashara... Inasikitisha sana
 
Mtani wangu na mkuu wangu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance Mabeyo, nakusalimu na kukutakia kazi njema. Nakuuliza tu kizalendo: unayasikia au kuyasoma maneno yasemwayo na makomandoo wetu walio washtakiwa na mashahidi kwenye kesi ya ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake? Hakika, makomandoo hawa (ingawa kwasasa wote hawako tena jeshini/kazini) wanazungumza vya kushangaza na kuogofya.

Kuanzia Kusekwa/Adamoo, Ling'wenya hadi Mhina wa jana wamezungumzia kukamatwa kiholela; kuteswa; kutwezwa; kudhulumiwa na madhila mengine. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watulinde. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watupiganie. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watutetee. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili waendeleze uzalendo na utii wao kwa nchi yetu. Kwanini wamepitishwa kwenye njia waisemayo?

Makomandoo wetu wamelalamika; wamelia; lakini hawana la kufanya hadi mwisho wa kesi. Wenzao wa 92 KJ na kwingineko wanajifunza nini? Wanapata ujumbe gani? Wanawaza nini? Wanawataja wenzao wengine kukamatwa na kuteswa pia. Wako wapi wale waliotajwa? Kazini? Hai? Ndugu yangu Mabeyo, utumishi wako umetukuka. Sina shaka nawe wala na jeshi unaloliongoza. Makomandoo hawa, kwa mujibu wao, waliathirika vitani. Wapewe haki zao. Wakumbukwe. Watendewe yaliyo mema.

Unaandika lakini mtani wangu Jenerali Mabeyo? Nitakuja pia nyumbani na ofisini kusisitiza hili

Wasiojulikana sasa wamejulikana?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Ni aibu sana kwa Mabeyo, anajifanya mtu wa dini kumbe 🚮 Yaani askari wake wanatekwa, wanateswa,wanatekwa,yeye kimya...hii aibu haijawahi kutokea kwa General mwingine yoyote kabla yake. Mbaya zaidi askari anafukuzwa kazi, mwaka mzima sasa hajalipwa stahiki zake, anazungushwa tu!!! Shame!!
 
Mtani wangu na mkuu wangu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance Mabeyo, nakusalimu na kukutakia kazi njema. Nakuuliza tu kizalendo: unayasikia au kuyasoma maneno yasemwayo na makomandoo wetu walio washtakiwa na mashahidi kwenye kesi ya ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake? Hakika, makomandoo hawa (ingawa kwasasa wote hawako tena jeshini/kazini) wanazungumza vya kushangaza na kuogofya.

Kuanzia Kusekwa/Adamoo, Ling'wenya hadi Mhina wa jana wamezungumzia kukamatwa kiholela; kuteswa; kutwezwa; kudhulumiwa na madhila mengine. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watulinde. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watupiganie. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watutetee. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili waendeleze uzalendo na utii wao kwa nchi yetu. Kwanini wamepitishwa kwenye njia waisemayo?

Makomandoo wetu wamelalamika; wamelia; lakini hawana la kufanya hadi mwisho wa kesi. Wenzao wa 92 KJ na kwingineko wanajifunza nini? Wanapata ujumbe gani? Wanawaza nini? Wanawataja wenzao wengine kukamatwa na kuteswa pia. Wako wapi wale waliotajwa? Kazini? Hai? Ndugu yangu Mabeyo, utumishi wako umetukuka. Sina shaka nawe wala na jeshi unaloliongoza. Makomandoo hawa, kwa mujibu wao, waliathirika vitani. Wapewe haki zao. Wakumbukwe. Watendewe yaliyo mema.

Unaandika lakini mtani wangu Jenerali Mabeyo? Nitakuja pia nyumbani na ofisini kusisitiza hili

Wasiojulikana sasa wamejulikana?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Hawakushindwa jujitetea Hawa makomando. Wameheshimu uzakendo zaidi ya uvumilivu. Kama pa private tu na migambo wakizinguliwa wanauwasha moto miyaani, kweli JWTZ wameshinda kulitetea jeshi na utu wake? Au JWTZ unaowapa ujumbe wajeshi kwamba wawe kondoo wadhaifu KWA kuonewa tu?

Hata kama wamestaafishwa vita ijiibuka hamtawahitaji kweli waendelee na jungle survival law? HAPANA. Jeshi liheshimiwe. Sijawahimwona Polisi akiwadhalilisha JWTZ mitaani, tuelewe kwamba utu wa mjeshi unabisha akistaafu au kusyaafishwa tena kwa kudhurika kazini? HAPANA.

Kutafuta ajira halali baada ya kustaafu ni haramu KWA askari wa JWTZ? Mnataka watumie Mafunzo na uzoefu wa jeshini ILI KUTUNZA familia zao? Nyie viongozi wa JWTZ ingekuwa no ninyi mngetulia hivyo? Shame on you.
 
Ndio kuna Sheria, hizo Sheria zao hazijali Haki ??? Yaan kumfukuza MTU bila kumpa barua??? Wala Mafao yake aloyatumikia muda wote huo!!!?.
Yaani mtu anafukuzwa kama mbwa! Komando anaishia kwenda kulima mahindi jembe la mkono!
 
Jeshini kunasheria zao
Kama taasisi zingine zilivyo za hovyo,hata jwtz ipo hivyo,hizo posho wanakula wakubwa!hiyo nafasi ya ukomandoo inakuwa kama umefanyiwa hisani,ukipiga kelele ndio hivyo haki zako zinaminywa.jinsi Rushwa ilivyokita mizizi,ajira siku hizi zinauzwa,mpaka kwenye taasisi nyeti ajira,zinauzwa tu,
 
kuwatupa mtu mtaani watu wenye mafunzo kama hayo ni hatari. Hata kama walionekana kuchanganyikiwa na hawastahili kukaa jeshini, kuwatupa tu mtaani si sawa, Magonjwa yao karibu wote wanasema yanahusiana na akili, inawezekana ni athari za kivita - tunawatupaje?
Askati wa vyeo vya juu wanapostaafu tunaona wanapewa ukuu wa wilaya, mkoa nk. hata hawa wa chini si vibaya wakawa wanapata kaposho fulani ili kujikimu kimaisha. Kumbukeni Jerry Rawlings hakuwa na cheo kikubwa!
Akina polepole na Bashiru waharifu hawatupwi mtaani angalau wanapewa hata ubunge wa kuteuliwa lakini askari aliyepata matatizo akiwa kazini wanamtupa mikono mitupu. Inafikirisha sana
 
Inaelekea JWTZ inathamini wanajeshi wakiwa na afya njema lakini pindi wakiumia au kupata maradhi wakiwa kazini inawatelekeza!

Amiri Jeshi Mkuu anapaswa kuangalia upya jambo hili kwani halina afya kwa ustawi wa jeshi letu.
bila elimu ya degree moja kwenye haya majeshi yetu ya tanzania ni shida tupu, utaishia kupigia watu saluti wakubwa, utatumiwa vibaya kama hawa kina Goodluck then ukizeeka unatupwa huko kwenu.

Training za ukomandoo ni ngumu mno zinahitaji uvumilivu wa hali ya juu, kijana anahitimu unamtumia miaka 5 then unamuacha tena kwa fedheha, hii si haki.
 
Mtani wangu na mkuu wangu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance Mabeyo, nakusalimu na kukutakia kazi njema. Nakuuliza tu kizalendo: unayasikia au kuyasoma maneno yasemwayo na makomandoo wetu walio washtakiwa na mashahidi kwenye kesi ya ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake? Hakika, makomandoo hawa (ingawa kwasasa wote hawako tena jeshini/kazini) wanazungumza vya kushangaza na kuogofya.

Kuanzia Kusekwa/Adamoo, Ling'wenya hadi Mhina wa jana wamezungumzia kukamatwa kiholela; kuteswa; kutwezwa; kudhulumiwa na madhila mengine. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watulinde. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watupiganie. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watutetee. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili waendeleze uzalendo na utii wao kwa nchi yetu. Kwanini wamepitishwa kwenye njia waisemayo?

Makomandoo wetu wamelalamika; wamelia; lakini hawana la kufanya hadi mwisho wa kesi. Wenzao wa 92 KJ na kwingineko wanajifunza nini? Wanapata ujumbe gani? Wanawaza nini? Wanawataja wenzao wengine kukamatwa na kuteswa pia. Wako wapi wale waliotajwa? Kazini? Hai? Ndugu yangu Mabeyo, utumishi wako umetukuka. Sina shaka nawe wala na jeshi unaloliongoza. Makomandoo hawa, kwa mujibu wao, waliathirika vitani. Wapewe haki zao. Wakumbukwe. Watendewe yaliyo mema.

Unaandika lakini mtani wangu Jenerali Mabeyo? Nitakuja pia nyumbani na ofisini kusisitiza hili

Wasiojulikana sasa wamejulikana?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Hili jambo la hawa Makomandoo wetu linaniumiza na kufikirisha sana.
 
Back
Top Bottom