Je, Zitto Kabwe alijisahau na kuanza kuung'ata mkono unaomlisha?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Kwa mtu anayezijua vizuri siasa za nchi hii lazima atakuwa anajua kuwa bila ''mkono'' wa CCM, Zitto Kabwe asingekuwa hapa alipo kisiasa!

Ukweli huu ndio ambao ulimfanya Zitto Kabwe kutoaminika ndani ya chama chake cha mwanzo (CHADEMA) mpaka chama kikaamua kumfukuza uanachama!

Malezi yake ya kisiasa kuanzia chuo kikuu yamefanywa na mashine/mitambo ya CCM mpaka kufikia hapa alipo.

Hata pale viongozi wa juu wa CHADEMA walipoamua kumfukuza uanachama, ni mitambo/mashine za CCM zilizohakikisha anabakia katika uwanja wa siasa ambapo alisaidiwa kwa haraka kuanzisha chama cha ACT-Wazalendo!

Kwa wale wazoefu hapa Jamiiforums nadhani watakumbuka hii mada ambayo ilileta michango mirefu na mizito kuhusu ACT-Wazalendo;

Ni CCM ambayo imekuwa ikimuachia Jimbo huko Kigoma kuanzia mwaka 2005 kiasi kwamba hata kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu, wagombea wa Urais wa CCM walikuwa hawafiki katika Jimbo analogombea Zitto kumpigia kampeni mgombea wa CCM. Hii ilikuwa inafanyika ili kumpa Zitto fursa ya ushindi!

Zitto kwa kujua au kutojua, baada ya kukaa bungeni kwa miaka 15, nadhani akadhani amekuwa ''indispensable'' na kuanza kuung'ata mkono unaomlisha! Hii haina tofauti na mtoto kuanza kujipima ''ubavu'' na baba yake!

Uungwaji mkono kutoka kwa ''wapambe'' kwenye mitandao ya kijamii ulimfanya akadhani anaweza hata kuung'ata ''mkono'' unaomlisha na maisha yakaendelea kama kawaida!

Link>>>Zitto Kabwe: Niko mbioni kuanza mazungumzo na Jumuiya za Kimataifa ili kupambana na utawala wa Rais Magufuli

Wenye ''mkono'' wakaanza kumuonya kuhusu tabia yake ambayo ilianza kuvuka mipaka ya kisiasa!

Ieleweke kuwa Zitto hana tofauti na Nape Nnauye na January Makamba ambao pia wamefika hapo walipo kisiasa kutokana na mashine/mitambo ya CCM. Nape na Makamba Jr pia walianza kuung'ata mkono unaowalisha baada ya kudhani wamekuwa ''indispensable'' lakini kabla mambo hayajawaharibikia zaidi waliomba msamaha haraka sana! Kilichowatokea kila mwenye uelewa wa siasa anajua!

Zitto Kabwe alishindwa kuelewa kuwa CCM huwa haitishwi na ''kinyago ilichokichoga''! CCM is ruthlessness in the game of power politics! CCM ikiona unaanza kuhatarisha nguvu zake za kisiasa inakupa onyo au inakushughulikia!

Mwezi wa Januari 2020, Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally alifanya ziara katika Mkoa wa Kigoma na kusema wamedhamilia kulichukua Jimbo la Kigoma Mjini katika uchaguzi Mkuu 2020.

Yaliyotokea katika Jimbo la Kigoma Mjini baada ya uchaguzi huu kila anayefuatilia siasa nchini anajua!

Kilichobaki kwa sasa ni Zitto kujisalimisha na kuomba msamaha kama walivyofanya Nape na Makamba Jr ili arudi kwenye ''system'' ama kama atazidi kupiga kelele na kuleta siasa kali kuna uwezekano wenye chama chao wakakihitaji na anaweza kujikuta anarudi CHADEMA baada ya ACT-Wazalendo kuondoka mikononi mwake!

Zitto Kabwe anatakiwa atambue kuwa sikio haliwezi kuzidi kichwa!
 
Kama kweli CCM wanajiona wana ubavu, ilikuaje wanaiba kura kijinga tena mchana kweupe? Nadhani CCM hawana nguvu yeyote, zito amewachapa asubuhi tu na wala hawajashinda.
Tatizo lako nadhani umesoma bandiko langu lakini hujaelewa!
 
Nguvu za CCM zipo kwenye kuiba Kura na kutumia apparatus za usalama kubadili matokeo.wapinzani hawakufanya siasa 5yo Bado CCM wamelazimika kuiba Kura kwa kiwango Cha aibu.
No. Tatizo lenu Mr Mzungu aliwapatieni matarajio makubwa ambayo hata yeye asingeweza kutimiza. "Tutashinda uchaguzi huu kwa Tume hiihii!" ~ Mr Mzungu
 
Kwa kifupi wapinzani wengi walikuwa wanashinda audha kwa kuachiwa nafasi na ccm au mpasuko wa ccm kuelekea uchaguzi mkuu..hata lowasa 2015 alipata kura nyingi sababu ya mpasuko ndani ya ccm.

Nani asiyejua kuwa msigwa, lema, sugu na kuna bulaya walipita sababu ya mipasuko na wagombea wa ccm kupita kwa rushwa pasipokukubalika..

Hata jimbo la mtama 2015 nape alitaka kupoteza sababu ya mpasuko..safari hii wakiwa na umoja kapita bila kupingwa.
 
Kwa kifupi wapinzani wengi walikuwa wanashinda audha kwa kuachiwa nafasi na ccm au mpasuko wa ccm kuelekea uchaguzi mkuu..hata lowasa 2015 alipata kura nyingi sababu ya mpasuko ndani ya ccm.

Nani asiyejua kuwa msigwa, lema, sugu na kuna bulaya walipita sababu ya mipasuko na wagombea wa ccm kupita kwa rushwa pasipokukubalika..

Hata jimbo la mtama 2015 nape alitaka kupoteza sababu ya mpasuko..safari hii wakiwa na umoja kapita bila kupingwa.
Mkuu;
Umedadavua vizuri sana!
Nakushukuru kwa maoni yaliyoenda shule!
 
Kama kweli CCM wanajiona wana ubavu, ilikuaje wanaiba kura kijinga tena mchana kweupe? Nadhani CCM hawana nguvu yeyote, zito amewachapa asubuhi tu na wala hawajashinda.
Zitto Kabwe anajua ukweli woote, Zile kura feki za Zitto Kabwe zilikuwa ni za movie. Tukiisambua movie ilivyoandaliwa naona Zitto Kabwe ndo itakuwa Mwisho wake kwenye siasa. Nina Video zote za Mikakati ya Zitto namna akihitaji Majimbo ya Kigoma
 
Kwa hiyo wakati Zitto anakuwa Mbunge kwa miaka 15, nguvu za CCM za kuiba kura hazikuwepo au miaka hiyo CCM haikuiba kura?
Uchaguzi huu wizi bila akil ndio maana walikataa kuwapa nakala ya matokeo mawakala.chaguzi za nyuma ukiwa na mawakala makini, waadilifu,wazalendo na wapenda demokrasia unapata matokeo yenye unafuu na nakala yako unapata
 
Kama kweli CCM wanajiona wana ubavu, ilikuaje wanaiba kura kijinga tena mchana kweupe? Nadhani CCM hawana nguvu yeyote, zito amewachapa asubuhi tu na wala hawajashinda.
Uliiba wewe na sio CCM,
Huwezi shindana na mtu hana miguu kisha umwibie,
Chadema ni nyumbu ambao ukiwaonyesha mto wa maji wanatumbukia woye bila kujua urefu wa mto na mamba kiasi gani wamo.

Kama mmeibiwa basi hata nyie mngefikisha hata milioni 8 hapo ungeweza kulalama, uzidiwe milioni 10 kisha useme umeibiwa?
Nyumbu mna shida sana.
 
Hakuna sifa yoyote ya maana kwa ccm..

Yoyote yule aliye timamu, anaiona ccm kama kusanyiko la wapumbavu..

Umaarufu wenu ccm kwa sasa dunia nzima inawafahamu kama majambazi ya kura kwenye chaguzi.
Kinachosikitisha ni kwamba Watanzania wengi hawatopiga kura tena maishani, ipo kazi kuwaaminisha tena kwamba uchaguzi ndio njia ya kupata viongozi.
 
Back
Top Bottom