Je, Watanzania hatuaminiani?

Je, Watanzania hatuaminiani?

Mtanzania

Platinum Member
Joined
May 4, 2006
Posts
4,822
Reaction score
710
Wanasiasa Tanzania hawaaminiki (From Majira)

*Wamo polisi, wafanyabiashara, mabosi NGOs
*Imani zaidi ni kwa ndugu, kabila, wanadini
*D'Salaam yaongoza kwa watu wasioaminiana

Na Joseph Lugendo

WAKATI wananchi wakisubiri uchaguzi wa Tarime, unaotarajiwa kufanyika kesho, utafiti wa kundi la watu linaloaminiwa zaidi nchini umebainisha kuwa wanasiasa, wafanyabiashara, viongozi wa asasi zisizo za Serikali na polisi ni watu 'wasioaminika' kwa jamii.

Utafiti huo uliotolewa hivi karibuni Dar es Salaam, umefanywa na mfumo wa usimamizi wa Mkakati wa Kupunguza Umasikini na Kukuza Uchumi Tanzania (MKUKUTA), ulio chini ya iliyokuwa Wizara ya Mipango Uchumi na Uwezeshaji.

Takwimu hizo zinaonesha kuwa wanasiasa wameshika nafasi ya 11, viongozi wa NGO ya 12 na polisi ya 13 kati ya makundi 18 yanayoaminika katika jamii.

Kwa mujibu wa takwimu zake, asilimia 78 ya wananchi wanaamini kuwa jamii haina uaminifu huku Jiji la Dar es Salaam likiongoza kuwa na kiwango cha juu cha kutoaminiana cha asilimia 85 ikilinganishwa na vijijini, ambako kiwango cha kutoaminiana ni asilimia 75.

"Watu wazima waliosailiwa waliulizwa, je, kwa ujumla unaweza kusema kwamba siku hizi watu wengi wanaaminika au kwamba watu wengi hawaaminiki? Idadi ndogo tu ya watu wazima waliosailiwa (22%), wanaamini kuwa watu wengi ni waaminifu," inaeleza sehemu ya utafiti huo.

Katika takwimu hizo, kundi linalohudumia jamii lililopewa nafasi ya juu za kuaminika katika jamii ni la viongozi wa dini walioshika nafasi ya pili kwa kuaminika katika jamii na kufuatiwa na kundi la walimu lililoshika nafasi ya nne.

Hata hivyo, takwimu hizo zinaonesha kuwa viongozi hao wa dini wanaaminika sana vijijini kuliko mijini na hasa Dar es Salaam.

Zinaonesha kuwa wakati vijijini viongozi wa dini wanaaminika kwa wastani wa asilimia 48, katika miji mingine wanaaminika kwa wastani wa asilimia 37 na Dar es Salaam kwa asilimia 36.

Kundi lingine linaloaminika kuliko wanasiasa ni kundi la wenyeviti wa vijiji na kata, lililoshika nafasi ya nane likifuatiwa na madaktari na wauguzi, ambao wameshika nafasi ya tisa na viongozi wa Serikali za mitaa walioshika nafasi ya 10.

Udugu na ukabila wakolea

Utafiti huo pia umebainisha kuwa Watanzania wengi wanawaamini ndugu zao wa familia moja au wanaotoka kabila moja kuliko mtu baki.

Hali hiyo imetokana na wasailiwa wengi kutaja kuwaamini wanafamilia, watu wa ukoo na watu wa kabila moja, ambao wameingia katika 'tano bora' ya makundi yanayoaminika katika jamii.

Nafasi ya kwanza ya watu ambao wanaaminika zaidi imeshikwa na ndugu wa familia, nafasi ya tatu ndugu wa ukoo na ya tano watu wa kabila moja.

Uzee ni busara

Mbali na viongozi wa dini, walimu na ndugu wa karibu, watu wenye umri mkubwa pia wamekuwa miongoni mwa makundi bora kumi yanayoaminika katika jamii.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, wanawake wazee wameshika nafasi ya sita na kufuatiwa kwa karibu na wanaume wazee. Hata hivyo, Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa kutoamini wazee ikilinganishwa na miji mingine na vijijini.

Vijana ni balaa

Takwimu hizo zimeonesha kuwa vijana wa kike wameshika nafasi ya 16 ya kundi linaloaminiwa katika jamii wakifuatiwa kwa karibu na vijana wa kiume, walioshika nafasi ya 17 huku kundi la wageni wasio Watanzania likishika nafasi ya mwisho ambayo ni ya 18 kwa kuaminika katika jamii. Nafasi ya 15 ilishikwa na wageni Watanzania.
 
Nini hasa tatizo la kukoseana uaminifu hapo?Ndio swali la kwanza la kujiuliza!Fedha imefanywa kuwa kila kitu na umaskini wa kupindukia.
Vilevile Ukabila,Ubinafsi na Uchoyo.
 
Njaa ndio mama wa matatizo yote hayo ya kutoaminiana, ukabila, udini, udugu nk.
 
Ni habari muhimu lakini jinsi ilivyoandikwa inanifanya nisielewe baadhi ya mambo. Wanasiasa wanashika nafasi ya 11 kwa kutoaminika na viongozi wa NGO nafasi ya 12. nani anashika nafasi ya kwanza, ya pili, ya tatu n.k?
basisi ya utafiti huu wote ni nini? Mkukuta si inahusika na masuala ya umasikini, nini kiliwaplekea kufanya utafiti wa aina hii? Si kwamba nakosoa utafiti wenyewe, naangalia tu relevance ya Mkukuta kufanya research hiyo
 
Ni habari muhimu lakini jinsi ilivyoandikwa inanifanya nisielewe baadhi ya mambo. Wanasiasa wanashika nafasi ya 11 kwa kutoaminika na viongozi wa NGO nafasi ya 12. nani anashika nafasi ya kwanza, ya pili, ya tatu n.k?
basisi ya utafiti huu wote ni nini? Mkukuta si inahusika na masuala ya umasikini, nini kiliwaplekea kufanya utafiti wa aina hii? Si kwamba nakosoa utafiti wenyewe, naangalia tu relevance ya Mkukuta kufanya research hiyo

MN,

Kama utasoma vizuri inaonyesha kuaminika kunaanzia chini, namba moja ni familia.

MKUKUTA wanaweza kuhusika maana miradi ya TZ kwa asilimia kubwa chanzo cha mtaji sio banks, ni familia, marafiki nk. Kuaminiana na umaskini vina uhusiano.

Yaani NGO inaaminiwa kidogo kuliko wanasiasa? Hii ni hatari kabisa.

Binafsi naona utafiti huu ni muhimu sana na unaonyesha jinsi jamii zetu zilivyoporomoka. Hata viongozi wa dini hawaaminiki sana.
 
Na mpango wenyewe wa mkukuta unaaminika kiasi gani miongoni mwa wananchi?
 
Mtanzania,

Nashukuru kwa kuileta hii habari hapa. Pamoja na kuwa natamani sana niulize hivi MKUKUTA wanweza kutuambia wako umbali gani kukamilisha safari ya madhumuni ya kuanzishwa, inabidi niongelee kuhusu kura hizi za maoni.

Naliangalia kwa macho ya kisiasa na kuhoji ikiwa Wanasiasa hawaaminiki, inakuwaje tunaendelea kuwa na viongozi na wanasiasa wale wale kila baada ya miaka mitano?

Pili inaelekea wenyeviti wa kata na vijiji wanaaminika sana, je wenzetu wa Upinzani wameliona hili na kulichukulia kwa umakini kwa nini CCM inawapiga ngwala kila uchaguzi?
 
Ni habari muhimu lakini jinsi ilivyoandikwa inanifanya nisielewe baadhi ya mambo. Wanasiasa wanashika nafasi ya 11 kwa kutoaminika na viongozi wa NGO nafasi ya 12. nani anashika nafasi ya kwanza, ya pili, ya tatu n.k?
basisi ya utafiti huu wote ni nini? Mkukuta si inahusika na masuala ya umasikini, nini kiliwaplekea kufanya utafiti wa aina hii? Si kwamba nakosoa utafiti wenyewe, naangalia tu relevance ya Mkukuta kufanya research hiyo

Mimi nafikiri wanasiasa wanastahili kushika nafasi ya kwanza kwa kutoaminika akina fisadi Mkapa, Kikwete, Rostam, Chenge, Karamagi, Mkono, Mzindakaya, Mramba, Lowassa, Makamba na wenzao kutokana na scandals za IPTL, Mkapa kufanya biashara akiwa Ikulu, Kukupua Kiwira kutoka kwa Watanzania, kuhusika na ufisadi wa Rada, ufisadi wa uuzaji nyumba za serikali, kusaini mikataba mibovu ya uchimbaji wa madini ambayo haina maslahi kwa Tanzania, ununuaji wa magari na helicopters za jeshi, kukabidhi ripoti ya madini kwa Sinclair kabla ya Watanzania hawajaiona, kushindwa kuwachukulia hatua za kisheria mafisadi wa EPA, Richmond, Meremeta, ujenzi wa Twin Towers, kujipatia mabilioni ya shilingi toka BoT kwa kazi ambazo wameshindwa kuzithibitisha n.k. nadhani wanaofuata wanastahili kuwa polisi halafu mahakama.
 
Mtanzania,

Nashukuru kwa kuileta hii habari hapa. Pamoja na kuwa natamani sana niulize hivi MKUKUTA wanweza kutuambia wako umbali gani kukamilisha safari ya madhumuni ya kuanzishwa, inabidi niongelee kuhusu kura hizi za maoni.

Naliangalia kwa macho ya kisiasa na kuhoji ikiwa Wanasiasa hawaaminiki, inakuwaje tunaendelea kuwa na viongozi na wanasiasa wale wale kila baada ya miaka mitano?

Pili inaelekea wenyeviti wa kata na vijiji wanaaminika sana, je wenzetu wa Upinzani wameliona hili na kulichukulia kwa umakini kwa nini CCM inawapiga ngwala kila uchaguzi?

Ingelikuwa huku West, NGO ingechukua nafasi ya juu. Kwa TZ ziko hata chini ya wanasiasa. Hawa ndio walitakiwa kusaidia jamii hasa za wanyonge.

Hii ni dalili ya mafisadi kuingia kwenye sectors zote muhimu za kushughulikia jamii.
 
Hali hiyo imetokana na wasailiwa wengi kutaja kuwaamini wanafamilia, watu wa ukoo na watu wa kabila moja, ambao wameingia katika 'tano bora' ya makundi yanayoaminika katika jamii.
Nafasi ya kwanza ya watu ambao wanaaminika zaidi imeshikwa na ndugu wa familia, nafasi ya tatu ndugu wa ukoo na ya tano watu wa kabila moja.
When a country loose leadership... this is what U get!

Ukitazama kwa makini hoja nzima ya MKUKUTA inalenga kutazama leadership kwani kuamini mtu kunatanguliwa nafasi ya mtu huyo ktk jamii nzima..na tatizo kubwa linalojenga uongozi mbaya hutanguliwa na Mawasiliano kati ya mtu huyo na walengwa.
Hivyo utaona kwamba watu waliochukua nafasi za juu ni wale wenye mawasiliano ya karibu kila siku na wananchi kuliko wale walioko mbali..
Tujiulize ni Wabunge wangapi wanaishi ktk wilaya walizogombea?...
 
When a country loose leadership... this is what U get!

Sawa sawa Mkandara

Natamani kusema kuwa JK anatakiwa achukulie huu uchunguzi serious, but then......oh well!

My point ni kwamba, kwenye uongozi ambao huko makini kwenye kudeliver, report kama hii ndio hasa unapotakiwa kuitumia kujenga msingi imara wa jamii yake.

Kama kiongozi imara, unaweza kutumia report hii kushughulikia matatizo ya kijamii. Unajua kuwa jamii haina imani na polisi, then you got business to take care in the police department......and so on.

But then Watanzania tumeula wachuya. Tutazidi tu kuvuna magugu, kwani ndiyo hayo hasa tuliyoyapanda 2005. So until msimu wa kulima utakapoanza tena (hopefully tutapanda mazao msimu mpya), hatuna budi kuendelea kuumia matumbo kwa kula magugu.

Hiyo report inazidi kuongeza maumivu kwenye kidonda
 
Na Maggid Mjengwa,
NAANDIKA haya nikiwa nchini Hispania. Nilipata bahati pia ya kutembelea nchi ya Poland yapata wiki moja iliyopita. Hizi ni nchi mbili ambazo zinafanana katika mambo mawili makubwa; zote mbili zina historia ya kuongozwa kidikteta kabla ya kufikia hatua hii ya kuwa nchi za kisasa na kidemokrasia.

Hispania ilikuwa na utawala wa kidikteta (Dikteta Franco) hadi alipofariki mwaka 1975, ndipo mabadiliko ya kijamii, kiuchumi na kisiasa yakapamba moto. Poland ilikuwa na udikteta wa chama kimoja ( Ukomunisti) hadi ukuta wa Berlin ulipoangushwa na mageuzi ya kisiasa , kiuchumi na kijamii yalipopamba moto. Na nchi zote hizi mbili ni za Kikatoliki na zina idadi ya watu inayolingana. Zote zina wakazi milioni 40.


Mifumo kandamizi ambayo nchi hizi ilipitia ndiyo iliyosababisha zikawa kwenye matatizo makubwa. Na kubwa zaidi, imani ilikosekana.


Na hakika, tatizo letu kubwa Watanzania kwa sasa ni kukosekana kwa imani miongoni mwetu. Hatuaminiani. Na mfumo uliotufikisha hapa bado hatujaubadili kwa kiwango cha kuridhisha.

Hili ni tatizo la nchi nyingi barani Afrika. Ndiyo, mathalan, Serikali nyingi Afrika hazipendi kuwepo kwa Tume Huru za Uchaguzi kwa vile hutoa nafasi kwa walio kwenye upinzani kuingia madarakani.

Na kwa vile hawana imani nao, kwa maana ya wapinzani, mara na wao watakapoingia madarakani, Serikali hizo huona ni vyema kutokuwepo kwa Tume Huru za Uchaguzi. Hilo la mwisho linawabakishia matumaini ya kuendelea kubaki madarakani. Maana, anayeamua hatima ya uchaguzi si mpiga kura, bali mhesabu kura na mtangaza matokeo ya mwisho ya uchaguzi.


Mfano, katika katiba yetu ijayo, kama itapendekezwa kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi , basi, huo utakuwa ni mwanzo wa mapinduzi makubwa ya kuifanya nchi yetu kuwa ya kisasa zaidi.

Nahofia Tume Huru ya Uchaguzi itasubiri mpaka tuchinjane kwanza kwa kutuhumiana kuibiana kura kwenye chaguzi. Tatizo ambalo lingeweza kumalizwa kwa kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi itakayoaminika na pande zote zinazoshiriki chaguzi. Itakayoaminika na wananchi.

Kuna wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki- Moon alitamka; kuwa tatizo kubwa la Serikali nyingi si nakisi ya bajeti bali nakisi ya imani ya Wananchi kwa Serikali hizo. Ndiyo, kupungua kwa imani. Ndiyo, inahusu imani na ni wajibu wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi kuirudisha imani ya wananchi kwa Serikali na chama hicho.


Niliwahi kuandika kuwa nchi yetu iko njiapanda. Mbele yetu kuna njia mbili; moja inaelekea tunakopita sasa. Kwenye hali ya ‘kujifunga’ na kubaki tulipo bila kupiga hatua za haraka za maendeleo huku baadhi (wakiwamo viongozi), wakiwa na udhibiti mkubwa wa hali ya mambo.


Njia nyingine inaelekea kwenye uhuru zaidi wa wananchi na uwezo wa kuwadhibiti na kuwawajibisha viongozi wao. Ni njia inayoelekea kwenye ustawi wa nchi.

Watanzania wengi kwa sasa wana kiu kali ya kuianza safari ya kuipita njia ya pili. Njia yenye uhuru zaidi na matumaini ya ustawi wa taifa. Njia itakayotufanya tuondokane kabisa na njia ya kwanza, njia inayotufunga na kutubakisha hapa tulipo.

Na siku zote, nchi haiwezi kupiga hatua za maendeleo ya kiuchumi bila kuwa na utulivu wa kisiasa. Kuna dalili, huko twendako, hakutakuwa na utulivu wa kisiasa kama tutaicha hali hii ya sasa iendelee kama ilivyo. Hali ya kutoaminiana na kukosekana kwa mwafaka wa kitaifa wa kisiasa.

Na Profesa wa Uchumi, Jeffrey Sachs ana mfano hai wa Poland. Katika kuwashauri kuinuka kiuchumi Wapolandi,

Profesa Sachs aliwaambia; “Political power must be shared”. Kwa tafsiri yangu ni kwamba; kuna umuhimu wa vyama kuwa na utayari wa kugawana madaraka ya uongozi wa kisiasa.


Ndiyo, Fundi Umeme yule Lech Walensa wa chama cha wafanyakazi na aliyeanzisha vuguvugu la mapinduzi ya kujikomboa kutoka Ukomunisti aliambiwa hivi na Profesa Jeffrey Sachs; “ Chama chako cha Solidarity kiwe radhi kuunda Serikali ya Mseto na Chama Cha Kikomunisti”.


Baada ya uchaguzi ikawa hivyo, kimoja kikatoa Waziri Mkuu na kingine Rais. Kukawepo utulivu wa kisiasa. Poland ikaanza kupiga hatua za maendeleo ya kiuchumi. Ndiyo, hakuna uchumi unaokua bila uwepo wa utulivu wa kisiasa. Katiba Mpya itakayohakikisha, mbali ya mambo ya mengine inatupa Tume Huru Ya Uchaguzi. Nahitimisha.


Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo
+46 736 966032
 
Uko sahihi kabisa.Tukiacha ubinafsi na tukaamua kwa dhati kuaminiana katika ujenzi wa Taifa hili tutashuhudia maendeleo makubwa na ya haraka. kuna mambo yanatukwamisha kama jamii kusonga mbele. mambo yanayo tukwamisha ni; UBINAFSI, MATUMIZI MABAYA YA RASILIMALI ZETU,USIMAMIZI MBOVU WA FEDHA ZA UMMA,POOR INVESTMENT KATIKA ELIMU NA KUTOKUJUA PRIORITY.Utajiri tulionao watanzania ungekuwa ni wa kenya wangekuwa kama ulaya.
 
Maandiishi mengi,,,lakini ilo la kutoaminiana hapa kwetu lipo na linafanywa na chama cha mabwepande CCM, imani yetu ipo juu ya CHADEMA aka nguvu ya umma na ndipo maana kikaasisi kuundwa kwa katiba mpya magamba wanachofanya nikuujumu mchakato tu,

Wasalimu huko ughaibuni usirudi bongo kuna kitu kinaitwa MABWEPANDE chini ya ACP Msangi na Zoka wananyofoa kucha na meno balaa, usirudi mkuu.
 
Tanzania na Morroko zimetajwa ndiyo nchi zisizokuwa aminifu zaidi duniani kati ya nchi 159 zilizofanyiwa utafiti. Utafiti huo umefanywa na jarida la week la Nature ambao umegusa maeneo ya Rushwa, Udanganyifu wa Kodi, Siasa, Kivuli cha Uchumi, Kipato cha mwananchi, Haki za kisiasa, Ufanisi wa serikali, Kuwalazimisha Watendaji nk.. Kenya pia imo katika orodha hiyo nchi zisizo aminifu. Nchi zilizotajwa kuwa aminifu zaidi kuliko zote duniani ni Uingereza, Uholanzi na Austria.

Tafsiri:

A study conducted by Nature, an international weekly journal of science, has named Tanzania and Morocco as the most dishonest countries in the world. The most honest countries, according to the study, were the United Kingdom, Austria and the Netherlands, while other dishonest countries included Kenya, Indonesia and Guatemala. The report, which examined 159 countries for their varying levels of corruption, political and tax fraud, also studied shadow economies, the prevalence of rule violations, government effectiveness, GDP per capita, political rights, constraint on executives and individualism.

wabongo.png


Source: Intrinsic Honesty and the Prevalence of Rule Violations across Societies
 
ndio maana tunaogopa kuungana na majirani kwenye mambo mengi maana hatuaminiki na hatuaminiani.

Hizi tafiti ni aibu tena kipindi ambapo hata bunge liko gizani, matumizi ya pesa hayaeleweki, siasa ziko kapuni. Unaweza kuja kugundua ulipigwa mwaka 2017 mwaka 2023.

Kuna haja kama taifa tukae tujitafakari tulianguka wapi ili tuirudie njia kuu
 
Back
Top Bottom