Je, wajua? Marekani waliwahi kupiga marufuku pombe

TheChoji

JF-Expert Member
Apr 14, 2009
4,975
15,316
Kuanzia mwaka 1920 -1933 pombe zilipigwa marufuku nchini Marekani. Ilikua ni kinyume cha sheria kuzalisha, kusafirisha au kuuza pombe nchini humo. Lengo lilikua ni kupunguza matatizo yaliyokua yanatokana na ulevi kama uhalifu, rushwa, matatizo ya kijamii, mporomoko wa maadili, afya duni nk pia kupunguza gharama za kuhudumia wafungwa waliotokana na matatizo ya ulevi.

Matokeo:

Hakuna manufaa yoyote ya maana yaliyopatikana. Uhalifu uliongezeka, rushwa ziliongezeka, magereza yalizidi kujaa wafungwa na serikali ilipoteza kiasi kikubwa zaidi cha kodi. Wanywaji wengi walihamia kwenye matumizi ya dawa za kulevya, bangi, na pombe za kienyeji zilizotengenezwa vichochoroni ambazo zilikua hatari kiafya.
 
Katika kipindi hiko ndo Babake John F Kennedy alipotajirika

Alikuwa anafanya biashara hiyo ya pombe akishirikiana na Italian mafia.

Baadae hawa mafia wakaja kumsaidia mwanae kuiba Kura akaja kuwa Rais wa Kwanza mkatoliki USA.

John F Kennedy akamteua mdogo wake
Robert F Kennedy kuwa mwanasheria mkuu
Ambae akaja kuendesha opereshen kubwa ya kukamata na kuwafunga mafia members.

Mafia wakamtuma Baba yao, waambie wanao wawe na shukrani. Robert hakutaka hata kumsikiliza Baba yake.

Wote John F Kennedy na mdogo wake walipigwa risasi na kufariki.

Mafia business is still alive
 
Katika kipindi hiko ndo Babake John F Kennedy alipotajirika

Alikuwa anafanya biashara hiyo ya pombe akishirikiana na Italian mafia.
Baadae hawa mafia wakaja kumsaidia mwanae kuiba Kura akaja kuwa Rais wa Kwanza mkatoliki USA.

John F Kennedy akamteua mdogo wake
Robert F Kennedy kuwa mwanasheria mkuu
Ambae akaja kuendesha opereshen kubwa ya kukamata na kuwafunga mafia members.

Mafia wakamtuma Baba yao ..waambie wanao wawe na shukran. Robert hakutaka hata kumsikiliza Baba yake..

Wote John F Kennedy na mdogo wake walipigwa risasi na kufariki.

Mafia business is still alive
Bonge moja la summary. Kwahiyo yule former marine lee oswald aliemshoot ilikua ni hoax tu au?
 
Ndiyo wakaibuka wakina Al capone. Wauza pombe za magendo. Pharmacy zikatajirika maana zilikuwa zinaruhusiwa kuuza pombe kama dawa. So uhalifu na mauaji vikaongezeka.

Hili liwe funzo kwetu, kukataza kataza vitu visivyo na msingi ni kukaribisha matatizo. Kataza kutoa takwimu, kataza twita, kataza mikutano ya siasa, kataza, kataza, piga marufuku, zuia, kataza, kataza,kataza kufungua akaunti youtube, kataza sherehe, zuia, kataza, kataza, kataza kukosoa, kataza kuongelea meli.......
 
Kuanzia mwaka 1920 -1933 pombe zilipigwa marufuku nchini Marekani. Ilikua ni kinyume cha sheria kuzalisha, kusafirisha au kuuza pombe nchini humo. Lengo lilikua ni kupunguza matatizo yaliyokua yanatokana na ulevi kama uhalifu, rushwa, matatizo ya kijamii, mporomoko wa maadili, afya duni nk pia kupunguza gharama za kuhudumia wafungwa waliotokana na matatizo ya ulevi.

Matokeo:

Hakuna manufaa yoyote ya maana yaliyopatikana. Uhalifu uliongezeka, rushwa ziliongezeka, magereza yalizidi kujaa wafungwa na serikali ilipoteza kiasi kikubwa zaidi cha kodi. Wanywaji wengi walihamia kwenye matumizi ya dawa za kulevya, bangi, na pombe za kienyeji zilizotengenezwa vichochoroni ambazo zilikua hatari kiafya.
BOOTLEG! Pombe ikawa bidhaa adimu! Bidhaa bora na ndio chanzo cha Wahalifu Wakubwa waliounda Familia 5 hatari za Uhalifu wa Kimafia (Mafia Crime Syndicates) kama Kina Charles Lucky Luciano,Al Capone,Babyface,Vincent Gigante na nk.
 
Katika kipindi hiko ndo Babake John F Kennedy alipotajirika

Alikuwa anafanya biashara hiyo ya pombe akishirikiana na Italian mafia...
Baadae hawa mafia wakaja kumsaidia mwanae kuiba Kura akaja kuwa Rais wa Kwanza mkatoliki USA...

John F Kennedy akamteua mdogo wake
Robert F Kennedy kuwa mwanasheria mkuu
Ambae akaja kuendesha opereshen kubwa ya kukamata na kuwafunga mafia members..

Mafia wakamtuma Baba yao ..waambie wanao wawe na shukran... Robert hakutaka hata kumsikiliza Baba yake..

Wote John F Kennedy na mdogo wake walipigwa risasi na kufariki...

Mafia business is still alive

David Nasaw Biographer wa Joseph Kennedy anadai alijaribu kutafuta vyanzo nyeti kuhusu hili lakini aligundua ni stori tu na umbea wa Wamarekani na kwamba Mzee Joseph Kennedy hakutajirika kwa sababu ya biashara ya pombe, ingawaje hili lilivuma sana marekani kuwa chanzo cha Utajiri wake ni Biashara ya Magendo ya Pombe (Bootlegging).

JFK na RFK waliuwawa kwa Nyakati Tofauti na Vyanzo vya Vifo vyao mpaka leo bado ni Utata sana!

JFK inasemekana (Chanzo) kuwa aligombania mwanamke (Marilyn Monroe) na Mafia Family na wale Wajuba walikuwa hawachangii Mwanamke na yeyote.

Wengine wanadai ni pale Rais Kennedy alipozorotesha Uhusiano na ISRAEL na kutowaunga mkono kwenye masuala yao mengi - MOSSAD wakaaamua kumastermind kifo chake.

RFK aliwahi kuteuliwa kuwa Kiongozi wakati wa Kamati ya Mc Clellan 1957 - Ambapo aliwanyoosha watu waliojihusisha na biashara zote za kihalifu na haramu - inasemekana hii ilimtengenezea maadui ambao walibakia na maumivu na uchungu na ndio yawezekana walichochea kifo chake baadae.(Probably - La Cosa Nostra).
All in All inawezekana kabisa Waliofanya haya yote ni MAFIA TU na kwa sababu nyingi tu.


The BOSS you're RIGHT. - MAFIA lawama zote zinawaangukia wao! na shida ni kwamba (HAWAWEZI KUKIRI HILI HATA KAMA WALIFANYA) ndio Kiapo Chao.
 
Movie ya "the intouchables " inaeleza vizuri kipindi cha prohibition
 
Katika kipindi hiko ndo Babake John F Kennedy alipotajirika

Alikuwa anafanya biashara hiyo ya pombe akishirikiana na Italian mafia...
Baadae hawa mafia wakaja kumsaidia mwanae kuiba Kura akaja kuwa Rais wa Kwanza mkatoliki USA...

John F Kennedy akamteua mdogo wake
Robert F Kennedy kuwa mwanasheria mkuu
Ambae akaja kuendesha opereshen kubwa ya kukamata na kuwafunga mafia members..

Mafia wakamtuma Baba yao ..waambie wanao wawe na shukran... Robert hakutaka hata kumsikiliza Baba yake..

Wote John F Kennedy na mdogo wake walipigwa risasi na kufariki...

Mafia business is still alive
Very interesting
 
Back
Top Bottom