Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,916
Unaweza kushangaa na hata kujiuliza kwamba mtu mchawi anawezaje kupigwa kujeruhiwa na hata kuuliwa na watu wa kawaida kabisa wasio wachawi
Kuna baadhi ya mambo ni lazima uvae vazi maalum yani kama watu wa maabara kwenye kemikali Kali, wazima moto, waendao anga za mbali nknk... Yaani hawa ni baadhi wafanyao shughuli ambazo vazi rasmi ni lazima kwenye uchawi na ushirikina nako ni hivyo hivyo
Kwa wale waliowahi kufika kwa waganga wa kienyeji wanalifahamu hili vema, unapoenda kwake, kama hayuko kikazi atakuchukua mpaka chumba maalum, kule atavaa mavazi maalum ndio aingie kazini
Mavazi yale avaayo ndio NGUVU na utii na ukuu wa NGUVU za giza, ndio kibali na kitambulisho cha kuweza kufanya atakayokufanya
Kwahiyo hata wale wanga na wachawi wanaosafiri usiku wana mavazi na vitendea kazi maalum kwa kazi hiyo.... Nje ya hapo ni wachumba tu.. Na ndio maana huweza kudhuriwa ama kudhurika kwa urahisi kabisa,! Ndio maana nao huugua magonjwa mengine ya kawaida kabisa ya kutibiwa hospitali za kisasa, ndio maana nao hufa vifo vya kawaida kabisa
Mchawi mshirikina ama mganga hawezi kuzivaa hizo NGUVU muda wote, ni nzito na zenye mambo ya kutisha sana, wachawi na waganga wa kweli anapokuwa amevaa NGUVU husika huona mengi yasiyoonekana kwa macho ya kawaida na mengi yanatisha mno...... Mwili huu wa nyama hauwezi kuhimili kubeba nguvu za giza kwa muda mrefu.... Ikitokea hivyo mtu hachukui round anakufa
Wanaokufa wengi kishirikina, wakati mwingine sio kwamba kafanyiwa chochote kibaya, bali ni kubebeshwa tu zigo zito la hizo NGUVU kwa muda mrefu na hatimaye mwili kuchoka na kushindwa kuhimili uzito na kufa kifo cha kawaida kabisa
Kuna baadhi ya mambo ni lazima uvae vazi maalum yani kama watu wa maabara kwenye kemikali Kali, wazima moto, waendao anga za mbali nknk... Yaani hawa ni baadhi wafanyao shughuli ambazo vazi rasmi ni lazima kwenye uchawi na ushirikina nako ni hivyo hivyo
Kwa wale waliowahi kufika kwa waganga wa kienyeji wanalifahamu hili vema, unapoenda kwake, kama hayuko kikazi atakuchukua mpaka chumba maalum, kule atavaa mavazi maalum ndio aingie kazini
Mavazi yale avaayo ndio NGUVU na utii na ukuu wa NGUVU za giza, ndio kibali na kitambulisho cha kuweza kufanya atakayokufanya
Kwahiyo hata wale wanga na wachawi wanaosafiri usiku wana mavazi na vitendea kazi maalum kwa kazi hiyo.... Nje ya hapo ni wachumba tu.. Na ndio maana huweza kudhuriwa ama kudhurika kwa urahisi kabisa,! Ndio maana nao huugua magonjwa mengine ya kawaida kabisa ya kutibiwa hospitali za kisasa, ndio maana nao hufa vifo vya kawaida kabisa
Mchawi mshirikina ama mganga hawezi kuzivaa hizo NGUVU muda wote, ni nzito na zenye mambo ya kutisha sana, wachawi na waganga wa kweli anapokuwa amevaa NGUVU husika huona mengi yasiyoonekana kwa macho ya kawaida na mengi yanatisha mno...... Mwili huu wa nyama hauwezi kuhimili kubeba nguvu za giza kwa muda mrefu.... Ikitokea hivyo mtu hachukui round anakufa
Wanaokufa wengi kishirikina, wakati mwingine sio kwamba kafanyiwa chochote kibaya, bali ni kubebeshwa tu zigo zito la hizo NGUVU kwa muda mrefu na hatimaye mwili kuchoka na kushindwa kuhimili uzito na kufa kifo cha kawaida kabisa