Je, wajua kuwa idadi ya wapiga kura nchini inakaribiana sana na idadi ya watu wenye kutumia mtandao (internet)?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,502
51,098
Kuna watu wanazibeza takwimu zinazotolewa mitandaoni. Takwimu ambazo nyingi kila mara zinaonyesha kuwa Tundu Lissu anamshinda Magufuli.

Binafsi ninaweza kusema kuwa hizi takwimu (polls) zinaweza kuwa credible (zenye kuaminika) zaidi nyakati hizi za sasa kuliko baadhi ya watu wanavyodhani na nitaelezea sababu za kitakwimu

Sababu zenyewe ni hizi zifuatazo

1. Aina ya Sampuli (Sampuli nasibu/random sampling)
2. Uwepo wa Taarifa unaoshabihiana na takwimu hizi (Triangulation of information)
3. Jumuia ambayo takwimu hizi zinatoka(credible population from which the sample is drawn

1. Aina ya Sampuli
Tumeona kuwa takwimu zinazochukuliwa ni kutoka kwa mtu yeyote anayeamua kwa utashi wake bila kulazimishwa na yeyote na hakuna wa kumzuia yeyote kupiga kura yake katika mtandao husika. Hii tayari inaonyesha kuwa kuna "nasibu" au randomness, kwa sababu hujui mtu atakayefuata atampigia nani, Kwa kigezo hiki tayari Takwimu za mitandaoni zinapata credibility

2. Uwepo wa Takwimu zinazoshabihiana na Taarifa hizi (Triangulation)
Mwaka 2017 Taasisi ya TWAWEZA ilionyesha kuwa umaarufu wa Magufuli umeshuka kutoka asilimia zaidi ya 90 mwaka 2016 hadi asilimia 55 mwaka huo.

Pili kwa mujibu wa Taarifa aliyoitoa Zitto Kabwe humu JF kuwa TISS imefanya utafiti mwaka 2018 na kuonyesha kuwa Uchaguzi ukifanyika mwaka huo basi Magufuli anashindwa.

Tatu kukosekana kwa takwimu yoyote ya mtandaoni iliyo wazi inayoonyesha Magufuli kumshinda Lissu, Isipokuwa ni Lissu tu ndo anaonekana kumshinda Magufuli hivi.
Kwa majumuisho ya sources hizi hii inaonyesha kuwa huenda ni kweli Lissu anakubalika kuliko Magufuli

3. Jumuia ya mtandaoni inaakisi Jumuia ya wapiga kura nchini (credible population)
Kwa mujibu wa NEC waliojiandikisha kupiga kura nchini ni milioni 29 na kwa mujibu wa TCRA zaidi ya Watanzania milioni 23 wana access ya mtandao (internet), Hii maana yake ni kuwa sampuli ya takwimu za mtandao inatoka kwenye population halisi ya wapiga kura nchini.

Kwa hiyo kutokana na vigezo hivyo vitatu huenda takwimu zinazotolewa mitandaoni, ambazo kila mara zinaonyesha Tundu Lissu anakubalika zaidi ya Magufuli zina ukweli ndani yake.

Lissu alikuwa sahihi kusema kuwa waachie CCM na ma TV yao na Magazeti yao ila washughulikiwe kwenye mitandao ikiwemo Whatsapp, huenda alijua ukweli huu kuwa Jamii ya Watanzania kwa sasa ni Jamii ya kidijitali zaidi (digital society)

Na huenda ndiyo maana serikali ya CCM imeanza kusumbuasumbua vijana wa mitandaoni wanaorusha maudhui ya Lissu. Hata hivyo wameshachelewa. Wananchi wanajua wapi pa kupata taarifa za Lissu wakizitaka, napo ni mtandaoni!

Hitimisho:
Huu uchaguzi siyo mwepesi kwa CCM hata kidogo, labda walete magumashi yao

Hapa chini ni Taarifa ya Shirika la habari la Reuters, ya mwaka 2018 wakiinukuu TCRA kuhusu kiwango cha watumia internet na wenye kutumia smartphones kuaccess mtandao

Img-1600638456520.jpg
 
Umesema kweli, shida watu kuukubali ukweli ndio shida!! Ukifatilia nyomi ya Mgombea uraisi kupitia Chama Cha CCM, inaonekana kubwa, lakini watu Hawa kila wakihudhuria mikutano hiyo, hawapati hata neno la faraja kutoka kwa mgombea wao.

Ndiyo maana, mgombea wa CCM imefikia mahala, ili kukonga nyoyo za wafuasi wake, akifika sehemu anaahidi kutoa pesa, kuweka kandalasi zisizofuata taratibu za kupeana kwa ujumla zaidi
 
Umesema kweli, shida watu kuukubali ukweli ndo shida!! Ukifatilia nyomi ya Mgombea uraisi kupitia Chama Cha CCM, inaonekana kubwa, lakini watu Hawa kila wakihudhuria mikutano hiyo, hawapati hata neno la faraja kutoka kwa mgombea wao. Ndiyo maana, mgombea wa CCM imefikia mahala, ili kukonga nyoyo za wafuasi wake, akifika sehemu anaahidi kutoa pesa, kuweka kandalasi zisizofuata taratibu za kupeana kwa ujumla zaidi
Teh teh teh, chukua mkutano wowote aliofanya Magufuli sehemu yoyote, then, angalia aina ya watu wanaohudhuria halafu utapata majibu kama wanna access na mitandao au hawana.

Hizo polls zinazofanywa na watu obviously matokeo yake yatategemea muelekeo wake. Unajua Nini kitatokea kwenye Poll iliyoanzishwa na Fatuma Karume au Maria Sarungi kwa sababu 90% ya wafuasi wake ni wale wanaopendezwa na misimamo yake. Matokeo yatakuwa hivo hivo kwenye page ya Gerson Msigwa, Antony Mavunde au Hamis Kigwangala.

So acheni kujipa matumaini bure, angalieni Population anayopata Magufuli tena barabarani na kwenye vimiji vidogo, angalia aina ya watu wanaokwenda kwenye mikutano ya Magufuli na wale wanaokwenda kwenye mikutano ya Loketo utaona tofauti.

Mmoja ana wapiga kura, mwingine ana wafuasi.
 
Umesema kweli, shida watu kuukubali ukweli ndo shida!! Ukifatilia nyomi ya Mgombea uraisi kupitia Chama Cha CCM, inaonekana kubwa, lakini watu Hawa kila wakihudhuria mikutano hiyo, hawapati hata neno la faraja kutoka kwa mgombea wao. Ndiyo maana, mgombea wa CCM imefikia mahala, ili kukonga nyoyo za wafuasi wake, akifika sehemu anaahidi kutoa pesa, kuweka kandalasi zisizofuata taratibu za kupeana kwa ujumla zaidi

Tena wanasombwa kutoka kila mahali kwa mabasi, watumishi wa umma wanalazimishwa kuhudhuria na tena wakishaingia kwenye hadhara ya mheshimiwa wanafungiwa kama mbuzi hawawezi kutoka tena kuendelea na shughuli zao, maana wakijaribu kutoka wanakutana na maaskari wanawazuia.

Halafu wananchi wanapewa chambo ya kwenda kuwaona wasanii wakubwa wakiperform.

Ukichunguza Interaction ya Magufuli na hadhira yake ni very poor, watu hawashangilii punchlines zake, yaani umma uko baridiiii, unachangamka tu ikiwekwa burudani ya msanii

Wakati kwenye mihadhara ya Lissu, watu wanakuja kwa utashi wao
Pili kuna atmosphere ya Umma kuinteract naye vyema na kuzifurahia points zake.
Hakuna wasanii wakubwa wa kuvuta hadhira.

It seems kuwa Licha ya kwenda kwenye mikutano ya Magufuli ambayo inaboa, miongoni mwa wananchi wengi tu waliolazimishwa au kupewa chambo ya kuhudhuria mikutano ya Magufuli, wengi watamkubali Lissu kwa kuwa anaongea masuala yao ya msingi.
 
Watakuboshia na kukwambia wazee vijiji wakati wanasahau kuwa wazee Wana wajukuu na watoto wamekosa mikopo na ajira ndani ya miaka 5.

Uko sahihi sana

Na pia demography ya wananchi imebadirika sana, kote nchini, vijijini na mijini kizazi cha Nyerere nchini kimepungua sana sasa hivi majority ya Watanzania ni kizazi cha Mwinyi na Mkapa
Ni kizazi cha vijana, kina sifa ya kuwa na exposure kujua huko duniani kuna nini.
Ni kizazi cha kidijitali kinachojua kujitafutia taarifa mitandaoni.

Vijana wana kiu ya mabadiriko
They are tired of the very same Old CCM story!

CCM na mgombea wake hawana mvuto kwa vijana ndiyo maana CCM inajaribu kutumia star power ya wasanii wakubwa angalau ikubalike, lakini vijana ni waelewa, burudani watakwenda kuiangalia lakini wapo na mtu mwenye kuwakilisha mahitaji yao yaani Tundu Lissu.
 
Kuna watu watashinda, lakini uchaguzi huu utawaacha wakiwa wamedhalilika sana.

Uchaguzi mwaka huu ni mgumu na muhimu kuliko awamu zote, ila kuna watu bado hawataki kusikia hilo.
 
Si kweli,

Hata nusu sina hakika kama wanafikia!

Unabisha bure, hebu tazama taarifa hii ya Reuters ya mwaka 2018 waliyoipata kutoka TCRA, watumiaji wako Milion 23, tena kati ya hao 82% wanaingia mitandaoni kwa kutumia Smartphone. Hapo ndo utajua power ya Whatsapp ambayo Lissu alisema tutawashughulikia CCM kupitia Whatsapp, hapo sijazungumzia mitandao mingine maarufu.

Img-1600638456520.jpg
 
Back
Top Bottom