Je, Uzinduzi Royal Tour ungekuwa na maana kama Rais Samia angetua kwa Dreamliner & ATC kuzindua Direct Flights from DAR-JFK-DAR/JRO-JFK-JRO?

Wanabodi,

Naendelea na zile makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya Leo ikiwa ni makala ya swali la hypothetical question (swali la kufikirika), Kwa njia ya "thinking aloud", yaani unawaza kwa sauti.

Hii ni makala mwendelezo wa makala hii Hongera Rais Samia, Kwenda US, Kuhutubia UN, Safari ya Kuzindua Filamu Yako ya Royal Tour, Tunaomba Tukusindikize, Dreamliner Yetu Itue New York

Ambayo pia niliandikia makala kwenye gazeti la Nipashe

View attachment 2188185

Swali ni hili "Jee uzinduzi wa filamu ya Royal Tour, unaofanyikia nchini Marekani, upi ungekuwa na maslahi zaidi kwa taifa kama Rais Samia angetua nchini Marekani kwa dege letu la Dreamliner, huku ATC ikizindua Direct Flights from DAR-JFK-DAR/JRO-JFK-JRO? au kuendelea kwenda kwa ndege za watu, kuzindua, kushangaa na kurejea, then what?.

Japo mimi sio mtaalam usafiri wa anga, lakini kusafiri nchi mbalimbali na katika misafa mbalimbali kumenipa exposure ya kutosha kuwaza kwa sauti.

Rais Samia na ujumbe wake, wako nchini Marekani, ambapo pamoja na mambo mengine, Rais Samia atafanya uzinduzi wa filamu yake ya Royal Tour.

Kwanza nitoe pongezi Kwa Sterling wa movie hiyo, mtu kuwa sterling wa movie yoyote kiukweli sii mchezo, ni kipaji!. Na kwa jinsi nilivyo ziona zile pati gazeti zake, "trailers", angekuwa ni Nyerere, asingeweza, Mwinyi, asingeweza, Mkapa ndio kabisa, na JPM asinge kubali hata huruhusu, mtu mwingine ambaye angalau angeweza kuwa starling wa movie kama hii ni JK, tena angepatia zaidi kwa sababu JK ni "hechibii" kumkaribia Steven Kanumba, Will Smith, Denzel Washington or Sidney Pointer.

Uzinduzi wa Royal Tour kufanyikia Marekani, ni mahali sahihi Kwa sababu huko ndio a catchment areas za watalii wenye fedha.

Kwa mawazo yangu, kwa vile lengo , pamoja na mambo mengine, ni ku promote utalii, hakuna kitu kinacho ongoza Kwa kupromote utalii kama usafiri wa ndege wa direct flights.

Na hakuna kitu kinaitangaza nchi kimataifa kama kupeperusha bendera ya nchi moja kwenye nchi nyingine, hakuna kitu kinaipeperusha vizuri bendera ya nchi kimataifa kama the national flag carriers, yaani ndege za mashirika yakitaifa kutua viwanja vya nchi nyingine.

Hii ni mara ya pili rais Samia kwenda Marekani, mara zote anakwenda Kwa ndege za mashirika ya ndege ya kibiashara ya nchi nyingine.

Rais Samia hasafiri safari za mbali Kwa ndege zetu ili kukwepa gharama. Kuliamsha Dreamliner letu kutua Marekani ni gharama kubwa. Lakini kama ni kweli tumedhamiria kwa dhati kuutangaza utalii wetu kimataifa, hatuwezi kukwepa gharama, lazima tuutangaze vivutio vyetu kimataifa. Namna bora ya kujitangaza kimataifa ni kupitia usafiri wa ndege wa kimataifa.

Tanzania na Marekani, tuna mkataba wa anga huria, hatuhitaji kuomba landing rights kwenye viwanja vyovyote vya Marekani, tunachohitaji ni kutoa tuu taarifa ili tutengewe a parking slot but we have a free access.

Dreamliner yetu ya Boeing 787 - 8 inabeba abiria 248 ambapo abiria ni 240 na 8 crew. Tuki reserves nafasi 40 kwa rais na ujumbe wake, halafu tukabeba abiria 200, kila abiria alipe nauli ya full package price ya US $ 5,000 kumsindikiza Mama Kuzindua Royal Tour, hao wasanii tuu wa Bongo Movies na Bongo Fleva wangeweza kuijaza. Ukijumlisha na wafanyabiashara, kampuni yangu ingepewa tender ya uhamasishaji hiyo trip, ningewapa abiria 500!.

Hii ni a Maiden trip, ya kitu kinachoitwa an "excursion" American tour kumsindikiza Mama kuzindua her movie The Royal Tour, na kazi itafanywa na a Tanzanian Tour Company ,aki partner na an American counterpart, the cost will be US $ 5,000 per person, Kwa Tanzania na US $.10,000 for Americans, the cost cover a round trip, includes a US Visa, 5 days 4 nights in New York, on a 2** hotel for Tanzanians and a 5***** tourist hotel in Arusha for the US Tourists. My role ni publicity only kuhamasisha. Nitawapata 💯 Bongo Movies na Bongo Music Stars wakiongozwa na Mondi, Kiba, Chinga, Mpoto ToT etc. 💯 journalist, 💯 ma pedejee wa Bongo ambao hawawezi kupata US visa wenyewe. 💯 wana CCM kumsindikiza Mwenyekiti, na 💯 wajasiriamali. There will be two trips, ndege itakwenda na 240 Watanzania, na kugeuza na 240 rich American tourist to Serengeti, Ngorongoro and Mt. Kilimanjaro.

The maiden trip ikifanikiwa tunaanza na a scheduled monthly monthly trips, then by-mothly ikibamba inakuwa weekly!. Na ili ndege isiende tupu US, naweza kuuza tuu a Disney Land School Trips Watanzania wenye uwezo wanaosomesha watoto wao Academy, wengi watawalipia. Na ikitokea tukakosa abiria wa Tanzania kujaza a scheduled direct flights, then tunafanya a monthly dege linaruka empty kuwabeba matajiri hao, kuwasubiria na kuwarudisha kama ile midege ya Kitaliano inayotua Zanzibar.

The only setback ni how to control the storeaways watakao taka kuzamia US!

Hivyo uzinduzi huo wa Royal Tour Nchini Marekani, would've made more sense kama Rais Samia angetua kwa Dreamliner na ATC kuzindua Direct Flights from JRO -JFK -JRO or from DAR-JFK-DAR.

Hakuna kitu kizuri kama Rais Samia angetua JFK Kwa Dreamliner na kupokelewa uwanjani hapo na Watanzania waishio Marekani kisha kuja nae hadi hotel aliyofikia.

Nikisema Watanzania ni wavivu kuchangamkia fursa, nitakuwa ninawaonea?. Kama ndege tunazo, abiria tunao, na soko lipo, hivi tuliinunua hii midege ya nini?!. Kweli ATC wanaona raha hii midege ya long distance haul, ikiruka domestic routes huku ikibeba vile vindoo vya samaki Sato kutokea Mwanza kuja Far na kwenda KIA pekee?. Tukisema pomoja na mambo mengine yote, lakini shirika letu la ndege kuendelea kupata hasara mwaka hadi mwaka kunachangiwa na menejinent kukosa wataalamu wa strategic thinking and planning kwenye airline business?.

Nawatakia uzinduzi mwema wa Royal Tour hiyo tarehe 18 na Pasaka Njema

Wasalaam.

Paskali
Rejea

Kweli Pasksli ww ni bonge la msukuma, kwa jinsi watu walivyokuwa wanashobokea ndege hapa nchini kipindi cha Magufuli,basi unadhani ni jambo litakalowastua hata wamerakani kuwa kuna ndege imetoka Tanzania. Ni sawa na watu watoke huko misungwi waje na Coaster hapa Dar utegemee eti watu wa Dar watanote kuna Coaster toka misungwi, hivyo waanze kuvutiwa na kwenda kutembelea misungwi. Kwa taarifa yako ni watu wachache sana huko US wanaojua kama kuna nchi inaitwa Tanzania,na hata wakiona hiyo ndege ya Magufuli watadhani ni ndege ya Ukraine imepotea kwenye uwanja wa vita. Huko kuna ndege za kutosha, kiasi hata ni ngumu kujua kuna ndege ya Tanzania imeingia huko. Ukitaka kujua ninachokuambia, fuatilia hata hiyo ziara ya rais, ni watu wachache sana huko wanajua kama Rais wa Tanzania yuko US. Yaani ni wa kawaida sana sembuse hiyo ndege?
 
biashara ya kurusha ndege kimataifa ni ngumu sana kwa serikali yetu. Nchi yetu haijulikani sana duniani hilo ni swala gumu sana ktk biashara ya anga. mwaka 1982 tulifungua route ya London. serikali ilikula hasara mbaya sana. Ilifikia mahala ndege inaondoka DSM bila abilia na kurudi kutoka London tupu! Tangaza nchi na fanya urafiki na bepari utavuna ngawila za biashara ya anga.
Kabisa, ili watu wajue kuna ndege imetoka Tanzania na kuingia US labda ipate ajali na kuangukia huko US, sio zaidi ya hapo.
 
All flights lazima zipite kwenye base yake na ku connect. Kwa Tanzania direct flights ni KQ only inaanzia DAR as a regional route to Nairobi, na ndipo inapiga shoot ndefu ya JFK. Ukipanda ndege nyingine yoyote, lazima upite base yake na ku connect, Ethiopia lazima upite Addis, BA lazima upite London, KLM lazima upite Amsterdam, Emirates unapita Dubai, SAA, unapita Joburg. Hakuna ndege yoyote ya US inayokuja direct hapa Bongo. Hiyo KQ ya direct New York, inategemea abiria kibao wa Tanzania, Royal Tour ni Fursa ya kuifungua Tanzania kwa soko kubwa tajiri la utalii wa Wamarekani.

Kuna watalii matajiri na watalii masikini, watalii matajiri hawataki shida, ndio wanaopanda direct flights na Arusha wanafikia 5 star hotels. Marekani ni Watalii matajiri. Watalii masikini wanasafiri hata magari ya watalii na kulala campsites.

To me itakuwa ni aibu kwa Tanzania, kama Mama anaifungua nchi kwa fursa kama hii fursa ya Royal Tour, halafu ATC ukashindwa kuchangamkia fursa, watalii wakaletwa na KQ!.
P
KQ inakuaje Direct flight to NY kwa abiria anayetokea TZ? Umezungumzia watalii matajiri nikawakumbuka ndugu zetu toka China na kidogo India (bahili kupitiliza) baadhi wanabebaga mpaka msosi
 
Mkuu Pascal Mayalla unaweza kuwa na mawazo mazuri lakini umesahau wale wadeni wetu waliopewa hati za kukamata mali zetu pindi wakipata fursa. Hili limefanya ndege zetu zingunguke humu humu ndani kama kuku mgeni
Tanzania hatudaiwi na mtu yoyote huko nje ambae anaweza kukamata ndege zetu. Hii kauli ameitoa juzi tu Waziri wa Fedha Bungeni.

Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
 
All flights lazima zipite kwenye base yake na ku connect. Kwa Tanzania direct flights ni KQ only inaanzia DAR as a regional route to Nairobi, na ndipo inapiga shoot ndefu ya JFK. Ukipanda ndege nyingine yoyote, lazima upite base yake na ku connect, Ethiopia lazima upite Addis, BA lazima upite London, KLM lazima upite Amsterdam, Emirates unapita Dubai, SAA, unapita Joburg. Hakuna ndege yoyote ya US inayokuja direct hapa Bongo. Hiyo KQ ya direct New York, inategemea abiria kibao wa Tanzania, Royal Tour ni Fursa ya kuifungua Tanzania kwa soko kubwa tajiri la utalii wa Wamarekani.

Kuna watalii matajiri na watalii masikini, watalii matajiri hawataki shida, ndio wanaopanda direct flights na Arusha wanafikia 5 star hotels. Marekani ni Watalii matajiri. Watalii masikini wanasafiri hata magari ya watalii na kulala campsites.

To me itakuwa ni aibu kwa Tanzania, kama Mama anaifungua nchi kwa fursa kama hii fursa ya Royal Tour, halafu ATC ukashindwa kuchangamkia fursa, watalii wakaletwa na KQ!.
P
Its obvious
KLM for Europeans.,
US ni kweli
Itakua wana sababu
 
Niliwahi kusikia route ya Mumbai,mara nikasikia ya DAR-Heathrow hivi hizi ziliishia wapi?? Ukitaka kuona hili shirika menejiment yake haipo serious waulize hizi Route kwanini zilikatishwa?
Route kati ya DAR na BOM bado ipo mara mbili kwa week - Jumatatu na Ijumaa.

Hiyo ya Heathrow uliisikia wapi?
 
Route kati ya DAR na BOM bado ipo mara mbili kwa week - Jumatatu na Ijumaa.

Hiyo ya Heathrow uliisikia wapi?
Tanzania tuna landing rights Heathrow, mpaka kesho, Kwa sasa Kwa vile hatuendi zinatumiwa na SAA. ATC ilipanga kutimba London, tena hadi mimi nilipanga kuwemo kwenye Maiden flight. Msikilize DG wa ATCL, Eng. Ladislaus Matinde akizungumzia route ya China

P
 
KQ inakuaje Direct flight to NY kwa abiria anayetokea TZ? Umezungumzia watalii matajiri nikawakumbuka ndugu zetu toka China na kidogo India (bahili kupitiliza) baadhi wanabebaga mpaka msosi
Wakenya wako so much business minded, Kwa mujibu wa sheria za anga, wanaweza kuruka direct flights only from Nairobi, to JFK, sasa wanachofanya ni ndege inaanzia DAR as a regional flight ikifika Nairobi ndio inakuwa International flight.
P
 
Wakenya wako so much business minded, Kwa mujibu wa sheria za anga, wanaweza kuruka direct flights only from Nairobi, to JFK, sasa wanachofanya ni ndege inaanzia DAR as a regional flight ikifika Nairobi ndio inakuwa International flight.
P
P! Kafuturu Kwanza naona swaumu inakuchanganya
 
Mkuu Paskal umeongea Jambo muhimu sana, ni Kama tumefungwa ufahamu.
Ndio tusaidiane kufunguana, juzi kati pale Dubai kwenye Expo Dubai, Watanzania walitimba usipime!. Wanachotaka Watanzania ni kuwa organised tuu, wahamasishwe, wanaojitokeza na Dreamliner linajazwa!, labda zitokee figisu za US visa, maana wazamiaji wasije kuutumia mwanya huo kuzamia!.
P
 
Niliwahi kusikia route ya Mumbai,mara nikasikia ya DAR-Heathrow hivi hizi ziliishia wapi?? Ukitaka kuona hili shirika menejiment yake haipo serious waulize hizi Route kwanini zilikatishwa?
Hakuna haja ya kuwauliza, ni changamoto za Covid 19, mashirika mengi ya ndege, yameyumba.
P.
 
Tanzania tuna landing rights Heathrow, mpaka kesho, Kwa sasa Kwa vile hatuendi zinatumiwa na SAA. ATC ilipanga kutimba London, tena hadi mimi nilipanga kuwemo kwenye Maiden flight. Msikilize DG wa ATCL, Eng. Ladislaus Matinde akizungumzia route ya China

P

Route ya China ipo na kwa mara ya kwanza tulienda April last year, baadaye wakasimamisha kwa sababu ya sheria za Covid-19. Kuna mashine ya kipimo walikihitaji, tumeshanunua na soon tutarudi Guangzhou.
 
Kuingiza ndege USA direct kutoka Tanzania sio rahisi kama unavyodhani. Kenya walikua na hiyo ruhusa sijajua kwa sasa wanaendeleaje.
Kuna michakato mingi sana ya kiusalama before kupewa hicho kibali.

Nitashangaa sana kama hata hili haulifahamu.
Kwanza unapata wapi abiria 200 plus wa kujaza ndege inayoenda Marekani direct toka Tanzania?!
Airlines zinatumia mtindo wa “Hub and Spoke”, yaani abiria wanakusanywa toka sehemu mbalimbali kwenye point(Hub) moja kama vile pale Dubai (Emirates) na kupelekwa sehemu husika.
Pia kukidhi masharti ya kuingia US kama airline sio mchezo. Kenya Airways waliona shughuli yake.
 
Back
Top Bottom