Je ushawahi kulala lock up? Ilikuwaje mpaka ukalala?

Je ushawahi kulala lock up? Ilikuwaje mpaka ukalala?

Ni ushauri wa bure kabisa.

Kabla hujapelekwa lockup hasa kwa makosa ya kawaida jaribu kumalizana nao mapema, lugha wanayoelewa ni pesa $$$, mara nyingi mnaweza malizana kwa kiasi kichozidi laki 1, jipinde unavyoweza wape hio pesa, ukifika kituoni kuna mnyororo mrefu na kiasi kinaongezeka

Hakikisha unapigia simu watu wako wa karibu hasa familia na ndugu, ukiingia kituoni ni ngumu kupata simu

Watu wengi huwa wanapuuzia haya kwa kudhani watatotoka asubuhi, kosa kubwa sana ! unaweza kukaa zaidi ya wiki hadi mwezi na wakikuchoka wanakutupia mahabusu waweza kaa miaka
 
Harakati za mtu mweusi

Nililala kituo cha msimbazi then siku ya tatu nikapelekwa kituo cha mbweni nikalala siku moja(2024)

✅Msimbazi kuna mbu balaa harufu kali,jasho,muda wote kelele za pikipiki na magari hadi manane ya usiku

Kelele za magari ukiongeza na kuchnganyikiwa na kesi full depreesion
✅Siku ya tatu nilihamishiwa kituo cha mbweni
Tuache mashihara kile kituo ni kizuri mno kuanzia mazingira ya lockup had vyoo vinafanyiwa usafi wa hali ya juu had unahisi ni kama vya nyumbani.
Kulikua na hewa mzuri ,
😁Kubwa kuliko ni kwamba kulikua na dawa ya mbu yani usku kabla ya kulala inaletwa dawa ya mbu ya kupaka,kisha munalala usingizi safi hadi unasahau kama upo locke up

Pongezi kwa kituo cha mbweni wakuu😁
 
Nipo na Chapati hapa nasubiri ndugu zangu waje na CHAI kabambe..!

Nimekaa siti ya mbele kabisa... unakuta mtu hata kituo cha polisi hakijui ila skilizia sasa anavyoondoka na kijiji..
Chapati za kusukuma au kumimina?
 
Nilipelekwa nikalipa 5000 pale Simu 2000 nikaachiwa kabla hata ya masaa mawili ashkuriwe Mungu kwa kuwapa polisi mshahara mdogo lasivyo tungeteseka sana.
Hahaha eti mshahara mdogo?
 
Haikuwa lock up - gerezani/ mahabusu moja kwa moja .

Ilikuwa hivi;

February 4 2025 nipo mahakama ya wilaya ( sita itaja) nasubili zamu yangu kuitwa case - castod of child, mshitaki mimi mwenyewe na kesi nikiwa nimeshinda tayari ni kukabidhiwa tu mtoto.

Mda ukiwa bado kuitwa , kaja afande full kama yuko vitani. Magojiano yakaanza.

Afande ; wewe jamaa unafanya nini hapa? Huku anininyenyua.

Mimi ; nasubili kuitwa mahakamani .

Afande ; unakesi gani? (huku akisukuma kunilazimisha kutembea kuelekea mahakama ya mwanzo)

Mimi ; afande kwani shida nini , kama vipi subiri nikiitwa karibu usikae kesi yangu.

Afande ; kwa ukali - we Jeuri sio eeh! ( huku akinipiga tanganyika jeki.

Mimi ; nikatia mgomo na kumwambia kesi yenyewe Isha isha Kwan wewe unashida gani na mimi?

Afande; kwa upole haya mambo yanazungumzika we twende , (afande mwingine akaongezeka kutia nguvu) wakanibeba na kuniingiza chumba maalumu kusubiri kesi.

ndani ya chumba nilikuta watu 7 na mimi nikiwa wa nane

Afande ,(mwingine wa kike) ; unaitwa nani

Mimi ; kimya (kauliza mara tatu ) sikujibu chochote

Afande ; (kaita mwenzie) afande.......... Huyu m*mng hataki jibu. Akaongezeka (mwingine wa kiume)

Afande ( wa kiume); huku unanishika begani jamaa ukifanya haya mambo kuwa makubwa zaidi tunaomba taarifa zako. Wa kike akadakie

Afande wa kike ; kwa kukusaidia waite ndg zako wakuwekee mdhamana.

Mimi ; kosa lipi ?

afande wa kiumbe ; we m*g usitusumbue kama hutaki msaada unaenda jera . kwanza unatishia kupiga tena mwanamke ..... -matusi yakafuata hapa .

Kesi kizimbani - namwona yule mwanamke nileye umeshinda custody nikiwa nimeisha ijua picha yote.

Hakimu (Mwanamke ) ; Bagwele bin Venom umri miaka kadha (kaitaja) je, ni majina yako? - Swali je taarifa zangu alizitoa wapi maana sikufanyiwa mahojianao?

Mimi ; ndio mheshimiwa

Hakimu ; ananisomea kesi na vifungu vinyoaminika kuvunjwa case MTUHUMIWA UNATUHUMIWA KUMTISHIA BI ( katajwa mwanamke yule ) TUKIO ULILO LIFANYA DECEMBER 23 2024. AKAULIZA JE NI KWELI?

Mimi ; sio kweli mh

Mh; mlalamikaji , mtuhumiwa amekana mashitaka je , unamashahidi wangapi?

Mlalamikaji ; kimya

Mh; akauliza kwa mara ya tatu

Mlalamika ( kwa kudeka) ; shahidi ni mimi mwenyewe.

Hakimu; anaandika na kuahilisha kesi, na kusema - mtuhumiwa mdhamana wako uko wazi kama uko tayari uwasilishe kama haiko tayari asikari mpeleke gerezani.

Mimi; inawezekana VIP mheshimiwa nina kesi mahakama ya wilaya dhidi ya huyu aliye nishitaki Leo. Hi sio haki mheshimiwa. Huku nakokotwa na asikari wawili.

nilichukuliwa moja kwa moja hadi gerezani .

stori ni ndefu sana nashukuru nilimaza kila kitu na February 14 nilimchukua mwanangu.
 
Kuna kipindi fulani nimemaliza chuo,nikawa sina mishe ya maana.



Sasa katika kujitafuta nikahamia sehemu fulani kupambana,changamoto hilo eneo umeme wa TANESCO ulikuwa haujafika.



Nikawa na kawaida nisipotoka kwenda mjini,simu huwa nachaji kwa jirani,(anatumia solar) tukazoena.



Bwana wee kunasiku watu wakaingia wakaiba. Tv,simu,na baiskeli ya mtoto,kibaya zaidi hiyo siku sikutoka kabisa,nilikuwa naumwa malaria na usiku wake nlianza mseto.

Bwana wale watu wakajadili wee,wakafikia hitimisho mimi ndo niliiba au nilichora ramani.

Sina hili wala lile,polisi hawa hapa. Nikashikwa nikapakiwa kwenye gari,walikuja na private,nikatiwa na pingu.

Watu hao kituo kikubwa na pensi yangu.

Bila maelezo,nikawekwa lockup.

Mungu sio mzee mkumbo,wakati niko ndani,mwizi akakamatwa na vidhibiti vyote.

Nashangaa kumekucha,yule yule aliyeniweka lockup ndo anakuja kunitoa.

Nimeifupisha ila nilichojifunza kijana kama unajitafuta na huna mchongo wa maana,tumia mda wako kutafuta mishe,ukikosa,kaa kwako.
 
niliuziwa simu ya wizi,
ikafuatiliwa nikaja kukamatwa nilikaa siku 5.
pananukaa,jashooo,hamna hewa,mmejazana maji wanaoga wababe tu.hauwezi amini siku zote hizo sijaenda haja kubwa
Hatari,Mazingira machafu..Nakumbuka kuna Father aliletwa Full kuhara..Misosi mingi ili letwa kama sio Ninja hugusi
 
niliuziwa simu ya wizi,
ikafuatiliwa nikaja kukamatwa nilikaa siku 5.
pananukaa,jashooo,hamna hewa,mmejazana maji wanaoga wababe tu.hauwezi amini siku zote hizo sijaenda haja kubwa
Tatizo hujazoea kunya huku unatizamwa...ukawa unajibana🤣🤣🤣
 
Habari,
Je ulishawahi kulala lock up au selo? Ulikuaje mpaka ukalala?

Karibuni wajumbe ili tuelimike
Wewe itoshe tu kujua kwamba pale Lock up ndo mahali Polisi wanapowakomoaga raia. Kigezo ni ww tu uwe ni mtuhumiwa - utaingia.
 
Ni ushauri wa bure kabisa.

Kabla hujapelekwa lockup hasa kwa makosa ya kawaida jaribu kumalizana nao mapema, lugha wanayoelewa ni pesa $$$, mara nyingi mnaweza malizana kwa kiasi kichozidi laki 1, jipinde unavyoweza wape hio pesa, ukifika kituoni kuna mnyororo mrefu na kiasi kinaongezeka

Hakikisha unapigia simu watu wako wa karibu hasa familia na ndugu, ukiingia kituoni ni ngumu kupata simu

Watu wengi huwa wanapuuzia haya kwa kudhani watatotoka asubuhi, kosa kubwa sana ! unaweza kukaa zaidi ya wiki hadi mwezi na wakikuchoka wanakutupia mahabusu waweza kaa miaka
Ila cha ajabu wanakuwepo baadhi yao hao hao Polisi kituoni wana huruma na wanakupa connection namna ya kutoka - wenyewe wanaita kuchomoa.
 
Back
Top Bottom