Je, unaweza kumbadili mtu mzima tabia?

Buhaya Empire

Senior Member
Aug 3, 2016
116
299
Moja kati ya mambo ambayo yatakuchanganya sana akili yako ni kudhani kwamba unaweza kumbadilisha mtu fulani tabia ili awe kama unavotaka wewe.

Nikupe taarifa tu rafiki kwamba jambo hilo linauwezekano mdogo unaokaribiana na kushindikana.
Na ikiwa utachagua kuamini kwamba haiwezekani kumbadilisha mtu tabia ili kuwa kama unavotaka wewe, niseme tu kwamba utakuwa umefanya uchaguzi wa busara sana.

Kuna watu wamekuwa wakijidanganya kwamba watawabadilisha marafiki, ndugu, au mpenzi eti ili wawe kama yeye binafsi anavotaka, rafiki unapoteza muda.

Watu wengi wamejikuta katika nyakati ngumu, kwa vipindi tofauti, na wengine hata sasa ninavyoandika hapa wanajitoa uhai kwa sababu tu waliamini kwamba wamewabadilisha watu wao wanaowapenda sana na kufikiri kwamba wataishi maisha ya raha mustarehe ndani ya dunia waliojitengenezea, Hilo ni jambo la kuchekesha na kusikitisha kwa wakati mmoja.

Kwa uzoefu wangu, na juhudi katika kujifunza kwa umakini juu ya tabia za watu wanaonizunguka, marafiki, wapenzi, na kusoma, nimebaini jambo moja zuri kuhusu mabadiliko ya mtu ya tabia.

Jambo la awali kabla ya kufikiri mara mbili unapaswa pasina shaka kujua kwamba mabadiliko ya mtu mwingine yanatoka ndani yake yeye mwenyewe. Na mtu anabadilika baada ya kukubali yeye pekeake bila shuruti kwamba inampasa kubadilika.

Lakini mpaka mtu kufikia kutaka kubadilika. Je kiu hii ya mabadiliko inaanzaje?

Nikutanabaishe tu kwamba si kwa viboko wala maneno makali. Imethibitika kwamba kwa njia hizo haiwezekani kumbadilisha mtu mzima ili kuwa bora bali kuwa mbaya zaidi.

Kuamini kwamba unaweza kuwabadilisha watu wengine ni mawazo ya gizani na ya kishetani, nilichogundua katika maandiko pia ni kwamba Mfalme wa Nuru (YHWH) hakuwahi kuthubutu kuwabadilisha watu akili zao ili wamtumikie yeye bali aliwataka wabadilike wao wenyewe ili wamgeukie.

Jambo la busara sana linaloweza si tu kukupa furaha bali pia kukufanya uishi vizuri na kuvumiliana na watu ni kujua kwamba msaada pekee unaoweza kuwapa watu katika eneo hili ni KUCHOCHEA au KUANZISHA kiu ya mabadiliko yao binafsi na baada ya hapo ukae pembeni, mabadiliko yao kamili ni jukumu lao na si lako

Moja kati ya vichocheo ambavyo dunia inavitumia sana kuanzisha kiu ya mabadiliko ndani ya watu ni KUWAVUTIA watu katika mambo fulani, kuonesha upande mmoja wa faida za mambo fulani, na kuwa wema sana kwa watu katika mambo fulani.

Jukumu la kuamua kubadilika linabaki kuwa lako, na katika hilo hakuna wa kumlaumu.

Ni ukweli kwamba mtu anauwezekano mkubwa wa kubadilika na kuwa bora zaidi au mbaya zaidi kwa sababu ya watu waliomzunguka, ni sahihi kabisa. Lakini unahitaji fikra safi kugundua kwamba mabadiliko ya mtu huyu yanatokana na yeye binafsi kuvutiwa na tabia za waliomzungua na kuchagua yeye binafsi kubadilika

Katika hilo asitokee yeyote na kusema kambadilisha mtu huyo, HAPANA, mabadiliko kamili ni hatua ya mwisho anayoipiga mtu binafsi.

Leo hii tuna mapadre, wachungaji na masheikh wengi wa hovyo ambao watu wanawaamini na kudhani eti vitabu vimewaweka katika njia nyoofu, lakini kwa isivyo bahati vitabu havijafanikiwa kuwabadili kwakuwa wao binafsi bado hawapo tayari kubadilika

Ishi humo.
 
Moja kati ya mambo ambayo yatakuchanganya sana akili yako ni kudhani kwamba unaweza kumbadilisha mtu fulani tabia ili awe kama unavotaka wewe.

Nikupe taarifa tu rafiki kwamba jambo hilo linauwezekano mdogo unaokaribiana na kushindikana.
Na ikiwa utachagua kuamini kwamba haiwezekani kumbadilisha mtu tabia ili kuwa kama unavotaka wewe, niseme tu kwamba utakuwa umefanya uchaguzi wa busara sana.

Kuna watu wamekuwa wakijidanganya kwamba watawabadilisha marafiki, ndugu, au mpenzi eti ili wawe kama yeye binafsi anavotaka, rafiki unapoteza muda.

Watu wengi wamejikuta katika nyakati ngumu, kwa vipindi tofauti, na wengine hata sasa ninavyoandika hapa wanajitoa uhai kwa sababu tu waliamini kwamba wamewabadilisha watu wao wanaowapenda sana na kufikiri kwamba wataishi maisha ya raha mustarehe ndani ya dunia waliojitengenezea, Hilo ni jambo la kuchekesha na kusikitisha kwa wakati mmoja.

Kwa uzoefu wangu, na juhudi katika kujifunza kwa umakini juu ya tabia za watu wanaonizunguka, marafiki, wapenzi, na kusoma, nimebaini jambo moja zuri kuhusu mabadiliko ya mtu ya tabia.

Jambo la awali kabla ya kufikiri mara mbili unapaswa pasina shaka kujua kwamba mabadiliko ya mtu mwingine yanatoka ndani yake yeye mwenyewe. Na mtu anabadilika baada ya kukubali yeye pekeake bila shuruti kwamba inampasa kubadilika.

Lakini mpaka mtu kufikia kutaka kubadilika. Je kiu hii ya mabadiliko inaanzaje?

Nikutanabaishe tu kwamba si kwa viboko wala maneno makali. Imethibitika kwamba kwa njia hizo haiwezekani kumbadilisha mtu mzima ili kuwa bora bali kuwa mbaya zaidi.

Kuamini kwamba unaweza kuwabadilisha watu wengine ni mawazo ya gizani na ya kishetani, nilichogundua katika maandiko pia ni kwamba Mfalme wa Nuru (YHWH) hakuwahi kuthubutu kuwabadilisha watu akili zao ili wamtumikie yeye bali aliwataka wabadilike wao wenyewe ili wamgeukie.

Jambo la busara sana linaloweza si tu kukupa furaha bali pia kukufanya uishi vizuri na kuvumiliana na watu ni kujua kwamba msaada pekee unaoweza kuwapa watu katika eneo hili ni KUCHOCHEA au KUANZISHA kiu ya mabadiliko yao binafsi na baada ya hapo ukae pembeni, mabadiliko yao kamili ni jukumu lao na si lako

Moja kati ya vichocheo ambavyo dunia inavitumia sana kuanzisha kiu ya mabadiliko ndani ya watu ni KUWAVUTIA watu katika mambo fulani, kuonesha upande mmoja wa faida za mambo fulani, na kuwa wema sana kwa watu katika mambo fulani.

Jukumu la kuamua kubadilika linabaki kuwa lako, na katika hilo hakuna wa kumlaumu.

Ni ukweli kwamba mtu anauwezekano mkubwa wa kubadilika na kuwa bora zaidi au mbaya zaidi kwa sababu ya watu waliomzunguka, ni sahihi kabisa. Lakini unahitaji fikra safi kugundua kwamba mabadiliko ya mtu huyu yanatokana na yeye binafsi kuvutiwa na tabia za waliomzungua na kuchagua yeye binafsi kubadilika

Katika hilo asitokee yeyote na kusema kambadilisha mtu huyo, HAPANA, mabadiliko kamili ni hatua ya mwisho anayoipiga mtu binafsi.

Leo hii tuna mapadre, wachungaji na masheikh wengi wa hovyo ambao watu wanawaamini na kudhani eti vitabu vimewaweka katika njia nyoofu, lakini kwa isivyo bahati vitabu havijafanikiwa kuwabadili kwakuwa wao binafsi bado hawapo tayari kubadilika

Ishi humo.
Uzi mzuri sana nashangaa nyuzi fikirishi kama hizi zinaakosa wachangiaji
 
Ni Kweli kabisa kumbadili tabia MTU Mzima ww binafsi ni Kazi ngumu kabisa Sababu, tabia ya mtu ni mchanganyiko wa tabia mbalimbali alizozipokea tangia akiwa mdogo kwa kufundishwa,kwa kuona,kwa kurithi,na tabia za kimazingira husika ya MTU alikokulia nk.

Sasa kwa MTU Mmoja pekee,ambae ww umekutana nae ukubwani akiwa na Uzoefu wa mchanganyiko WA tabia mbalimbali ni Kazi ngumu sana,kama isiyowezekana kabisa kuifanya.

MTU mwenye tabia yake kama yéyé anakupenda WW kimapenzi,na akabaini kuwa ww huipendi tabia flani aliyonayo,atakachofanya ni kukudanganya kwa kuificha tabia hiyo akiwa na ww Ili uone kuwa amebadilika na Ili aweze kutimiza Lengo lake.

Lengo lake likishatimia ndio pale MTU analia na kusaga meno kuwa pamoja na kuishi nae miaka yote hiyo Ktk ndoa lakini Bado hakujua tabia halisi za mwenzi wake jinsi alivyo.

MAGEREZA ni Njia ngumu pekee ambayo hutumiwa Serikali nyingi duniani Ili kubadili tabia za watu.kwa Njia Moja MAGEREZA huwa inafanikiwa n'a wakati mwingine huwa inazidisha tatizo zaidi kuliko hapo awali kwa baadhi ya watu.

UPENDO pia ni aina ya Njia inayopendekezwa Zaidi Ktk kumbadili MTU kutoka tabia fulani inayopendeza or isiyopendeza kwenda Tabia nyingine.Lakini nayo kama ilivyo Njia ya MAGEREZA hufanya kazi kwa baadhi ya watu lakini kwa wengine haifanyi KAZI.

Hivyo kwa kuhitimisha kwa mtazamo wangu,hakuna Njia Maalum ya kuitumia kuweza kumbadili MTU kutoka tabia Moja kwenda nyingine,kama ambavyo Kila MTU amekulia Mazingira tofauti,itikadi tofauti,Imani tofauti,Malezi tofauti n'a Marafiki tofauti tofauti.
 
Moja kati ya mambo ambayo yatakuchanganya sana akili yako ni kudhani kwamba unaweza kumbadilisha mtu fulani tabia ili awe kama unavotaka wewe.

Nikupe taarifa tu rafiki kwamba jambo hilo linauwezekano mdogo unaokaribiana na kushindikana.
Na ikiwa utachagua kuamini kwamba haiwezekani kumbadilisha mtu tabia ili kuwa kama unavotaka wewe, niseme tu kwamba utakuwa umefanya uchaguzi wa busara sana.

Kuna watu wamekuwa wakijidanganya kwamba watawabadilisha marafiki, ndugu, au mpenzi eti ili wawe kama yeye binafsi anavotaka, rafiki unapoteza muda.

Watu wengi wamejikuta katika nyakati ngumu, kwa vipindi tofauti, na wengine hata sasa ninavyoandika hapa wanajitoa uhai kwa sababu tu waliamini kwamba wamewabadilisha watu wao wanaowapenda sana na kufikiri kwamba wataishi maisha ya raha mustarehe ndani ya dunia waliojitengenezea, Hilo ni jambo la kuchekesha na kusikitisha kwa wakati mmoja.

Kwa uzoefu wangu, na juhudi katika kujifunza kwa umakini juu ya tabia za watu wanaonizunguka, marafiki, wapenzi, na kusoma, nimebaini jambo moja zuri kuhusu mabadiliko ya mtu ya tabia.

Jambo la awali kabla ya kufikiri mara mbili unapaswa pasina shaka kujua kwamba mabadiliko ya mtu mwingine yanatoka ndani yake yeye mwenyewe. Na mtu anabadilika baada ya kukubali yeye pekeake bila shuruti kwamba inampasa kubadilika.

Lakini mpaka mtu kufikia kutaka kubadilika. Je kiu hii ya mabadiliko inaanzaje?

Nikutanabaishe tu kwamba si kwa viboko wala maneno makali. Imethibitika kwamba kwa njia hizo haiwezekani kumbadilisha mtu mzima ili kuwa bora bali kuwa mbaya zaidi.

Kuamini kwamba unaweza kuwabadilisha watu wengine ni mawazo ya gizani na ya kishetani, nilichogundua katika maandiko pia ni kwamba Mfalme wa Nuru (YHWH) hakuwahi kuthubutu kuwabadilisha watu akili zao ili wamtumikie yeye bali aliwataka wabadilike wao wenyewe ili wamgeukie.

Jambo la busara sana linaloweza si tu kukupa furaha bali pia kukufanya uishi vizuri na kuvumiliana na watu ni kujua kwamba msaada pekee unaoweza kuwapa watu katika eneo hili ni KUCHOCHEA au KUANZISHA kiu ya mabadiliko yao binafsi na baada ya hapo ukae pembeni, mabadiliko yao kamili ni jukumu lao na si lako

Moja kati ya vichocheo ambavyo dunia inavitumia sana kuanzisha kiu ya mabadiliko ndani ya watu ni KUWAVUTIA watu katika mambo fulani, kuonesha upande mmoja wa faida za mambo fulani, na kuwa wema sana kwa watu katika mambo fulani.

Jukumu la kuamua kubadilika linabaki kuwa lako, na katika hilo hakuna wa kumlaumu.

Ni ukweli kwamba mtu anauwezekano mkubwa wa kubadilika na kuwa bora zaidi au mbaya zaidi kwa sababu ya watu waliomzunguka, ni sahihi kabisa. Lakini unahitaji fikra safi kugundua kwamba mabadiliko ya mtu huyu yanatokana na yeye binafsi kuvutiwa na tabia za waliomzungua na kuchagua yeye binafsi kubadilika

Katika hilo asitokee yeyote na kusema kambadilisha mtu huyo, HAPANA, mabadiliko kamili ni hatua ya mwisho anayoipiga mtu binafsi.

Leo hii tuna mapadre, wachungaji na masheikh wengi wa hovyo ambao watu wanawaamini na kudhani eti vitabu vimewaweka katika njia nyoofu, lakini kwa isivyo bahati vitabu havijafanikiwa kuwabadili kwakuwa wao binafsi bado hawapo tayari kubadilika

Ishi humo.
Hili jambo ni gumu tena ukizingatia mtu mmekutana ukubwani kila mtu Yuko na malezi yake na akili za alikokulia inatutesa mno kikubwa mheshimiane kunaweza mbadilisha mtu taratibu
 
Kumbadili mtu tabia unaanza na kumbadili mtu uwelewa wake wa jambo au mambo husika, ili mtu aweze kubadili uwelewa wake wa mambo, yafaa awe tayari kujifunza, ili mtu aweze kujifunza kuna mambo kadhaa
1. Mtu anaweza kujifunza kwa uzoefu ( experience) mfano aliwahi ambiwa usile ukiwa umelala akawa hajasikia, siku akala hindi amelala akapaliwa nusu kufa, hapo atajifunza kwa lazima.
2. Kijifunza kwa kuelekezwa, hapa inategemea na mambo yafuatayo:-

1. Utayari wa kujifunza
2. Kuwe na matokeo baada ya kujifuza.
3. Pia inategema na uwezo wa akili wa mhusika.

Utayari wa kujifunza unaweza ukaathiliwa na
1. Uhusiano kati ya anaejifunza na anaeelekeza au anaetaka ajifunze
2. Uzoefu wa anaejifunza
3. Imani/ mzimamo wa mhusika
4. Njia inayotumika kumfunza. Let say mtu mkubwa unamfunza kwa kumkejeli nk.

Kifupi pene nia pana njia, akiwa tayari kujifunza akapata uwelewa anaweza kubadilika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom