mpaka sasa hakuna hata mtu ambaye amefanya kama niliyoagiza hapo juu!! hii inaonesha kuwa hakuna mtu ambaye yupo tayari kujua siku yake ya kufa( siku ambayo mtu atakutana na Mungu).
licha ya kuwa kila mtu anafahamu kuwa maisha ni mafupi na ipo siku ambayo atakufa(utakutana na Mungu wako)lakini binadamu hatuachi yale ambayo tumekatazwa katika vitabu vyetu ambavyo tunaamini( kwa wale wenye kuamini). kila siku watu wanazini, wanaiba, wanadhulumu, wanaroga, wanaua na mambo mengine mabaya. wakuu hizi pumzi tunazozivuta zisitudanganye tukawa wenye kujisahau hapa ulimwenguni! Mungu yupo na ipo siku utakutana nae. Tujitahidi kuishi kama tulivyoagizwa kwenye vitabu vyetu tunavyoviamini.
Kwa ufupi hakuna mtu ambaye anaweza kujua siku yake ya kufa na ndio maana tunatakiwa kila wakati tujiandae kwa hilo kwa kufanya yake ambayo ni mema.
Mbarikiwe na jumapili njema wote.