Je unakumbuka nini miaka ya 80’s na 90’s.

Je unakumbuka nini miaka ya 80’s na 90’s.

duh, long nakumbuka kipindi cha mashairi rtd saa nane, ndo mida ya kutoka shule, njaa inakongoli, jua linawaka na chini umetia chachacha, ni full mateso.
 
mi nakumbuka tulikuwa tunaenda mtoni kuoga then tunasugua miguu kwenye jiwe na kuosha ndala halafu tunazishika mkononi huku tukitembea peku wakati tukirudi nyumbani ili zisichafuke.
 
Zama za 80's sukari shida! Kimbo ilikuwa nadra kuliona kopo wacha kuipikia! Halafu crimpline ndiyo nguo hi class, fundi anaambiwa bana kiuno halafu chini achia (pecos)
 
Kweli kipinde kile raha sana. Nakumbuka katika tarafa vijijini, moja akiwa nalo kijiji kizima kitasoma.

Kulikuwa na mchezaji wa bush stars ansitwa kobelo. Hadithi tsmu ya maji mzito mtunzi marehemu m.m bawji
 
duh, long nakumbuka kipindi cha mashairi rtd saa nane, ndo mida ya kutoka shule, njaa inakongoli, jua linawaka na chini umetia chachacha, ni full mateso.

Nakumbuka kipindi cha majira ndio natoka kwenda shule ufigio na kidumu cha maji cha mafuta ya oki
 
me nakumbuka kipindi hcho nlikuwa napenda kusikiza rtd kipind cha majira sa 3ucku. bas ikifka mida hyo dady alikuwa ananiita kuckiliza. nlikuwa namsikiza mtangazaj m1 wa iringa alikuwa aitwa monika lyampawe,yan nkimsikiza tu roho yangu ilikuwa inasuuzka ndo naingia kulala!
 
OLANDA bwaaaaaaana...yaan m2 akiniletea hayo mafuta leo naammpa hela za kotosha...yananukiaaaa mpaka kesho kutwa!!!
 
kipindi cha mama na mwana RTD kama ckosei j1 saa8 untoi pembeni ya redio sauti juu kuckiliza hadithi,walikuwa wanatangaza kwa hisia zile hadith za kutisha hadi nlikuwa naogopa.
 
Kipindi cha michezo rtd wanasubili mpaka mwisho ndio wanatangaza matokeo ya mechi ambazo watu tunasubili yanga au simba mikoani wakichelewa kupata matokeo mpaka kesho majira
 
Nakumbuka siku za sikuku kama Christmas, Idd, Pasaka. Kuchinjwa Ngombe, Mbuzi & kuku ilikuwa kawaida. Tofauti na sasa, Kweli hapo zamani mambo yalikuwa shwari.
 
Nakumbuka miaka ya 90 mwshn nililia sana kupelekwa shule kuanza darasa la kwnz.
 
Jamani wengne tumezaliwa 1990, sasa tukumbuke nn? Mbna mwatutenga
 
Nakumbuka enzi za RATION CARD yaani maduka ya ugawaji,kila kaya ilikuwa inapata chakula kwa card haijalishi familia za kishua au duni wote tulienda sawa!!!
 
mi kaka nakumbuka kulikua na noti ya mia mbili ina picha ya samaki kipindi hiyo nanilii bado anaombakuja angalia tv kwetu ile back na white si nanii bhana huyu yuko sirikalini siku hizi ah nanni huyu basi nimemsahau tu
 
mi nakumbuka wadhamin wa matangazo ya rtd kama oko,sabuni kodrai,revola,halaf kipind cha ijue IDM Mzumbe,posta na cm.
 
Viatu vinaitwa-DH
CHUPI ZA V.I.P KWA MALES
CHUPI ZA TAIWAN 4 FEMALES
MAGAGULO,Mabalongo,KANIKI,SABUN YA MBUNJU,FOMA,KIPINDI CHA MAMA NA MWANA, BAISKEL ZA SWALA,MADUKA YA RTC,MAFUTA YA RAYS,ASHANTI,NDALA ZA UMOJA,SKY WAY,KITO,

dah skyway...nami nimeziona kwa kakaangu akiwa shule mwaka 92
 
Mie nimeyamiss sana mafuta ya Rays,vilabu vya pombe za kienyeji kama vile komoni,mbege ,mnazi vilikuwa vikijitegea tofauti na bar maana cku hz kuna pub nyingi after 2 days zinafungwa
 
Back
Top Bottom