Munaraha sana munao sifia baba zenu.
Wengine hatukuwahi kupata mapenzi ya Baba,Mzee alikuwa Kitombi balaa,Majukumu yote ya nyumbani alimuachia mama(Bahati nzuri mama alikuwa muhangaikaji).Tulikuwa tunasikia tu sifa za mzee wetu huko nje anavyo nufaisha Wanawake wengine na watoto wao.
Tulisoma kwa Tabu na ndugu yangu,Mama alikanyaga sana charahani kuhakikisha watoto wake tunafikia ndoto zetu(Ahsante Mungu tumefika si Haba).
Mbaya zaidi mzee alifanya umalaya na hakutujali lakini alikuwa MTU wakumrudisha Nyuma mama yetu,Yaaani akiwa amefulia alikuja kumuhadaa Mama na anaondoka na akiba ndogo ya pesa ambayo mama alijitunzia(Mama alimpenda sana mzee).
Hii hali ilitufanya Mimi na ndugu yangu kuanza maisha yakuhangaika na biashara tukiwa wadogo sana,nakumbuka miaka ya 90,Mama alikuwa fundi cherehani,basi alikuwa akishona vi chupi vya watoto vya mikojo,Akimaliza tunagawana njia,yeye kaskazini Mimi na ndugu yangu kusini kwenda kutembeza(kuuza),kisha tunarudi ndio tunapata chakula cha siku hiyo.
Kipindi chote sikuwa mzembe na shule,na Mungu alinibariki haswa darasani,Japo sikwenda na viatu shule nilivaa ndala,na pia sikuwahi kutumia bag wakati wote nikisoma primary na hata secondary mwanzoni,lakini nilibidiika na masomo.
Baada ya dhiki zote na kusoma kwa shida,Mama alipata tenda yakushona sare za kwaya kanisani,hapo ndipo mwanzo wa mafanikio ya familia yangu ulianzia,
Mama alitusua,namimi nilifaulu kote nilipopita,kuanzia primary, secondary na kisha chuokikuu.
Mzee alianza kuwa mpole nakujirudi baada yakuona mafanikio ya mama na walau watoto wanakuwa.
Sasa tunamtunza mzee wetu japo yeye hakufanya hivyo,lakini ni Baba yetu ni Damu yetu,tunampenda na tunafarijika walau tunaye Baba,Naamini anamajuto moyoni na amekwisha kutubu.
Wakati mwingine maisha hutokea hivyo ili kukupa msingi bora wa maisha,Mana Ile biashara yakutembeza nguo mtaani ilinijenga sana kiakili,sikuwaza kuajiriwa ktk maisha yangu hata baada ya masomo ya vyuo vikuu,Mimi ni Biashara na Biashara.
Nampenda Baba lakini kwasababu ya jina lake sio kwa Malezi kama wengine mulivyofaidi kwa Baba zenu.
Sent using
Jamii Forums mobile app