Je, una tabia ya kuongea na wewe mwenyewe?

Je, una tabia ya kuongea na wewe mwenyewe?

Je, una tabia ya kujiongelesha mwenyewe?

Mfano kujipa maoni binafsi au kujiambia: Hiki ninachofanya si sahihi sitaki tena Kuna wakati kujisemesha mwenyewe ni muhimu sana ukweli ni kwamba hakuna anayekujua zaidi ya unavyojijua wewe mwenyewe.

Kuna tabia zipo ndani yetu ambazo si rahisi mtu wa nje kuziona au hata akiziona asikuambie moja kwa moja Wengine wanaamini wewe ni mtu mzima unajitambua hivyo wanakuacha bila ushauri

Lakini ukweli ni huu tabia mbaya (wengine huiita dhambi) huanza kidogo kidogo, halafu zinakutafuna taratibu mpaka siku unakuja kushtuka tayari umechelewa Mfano wa tabia ambayo unaweza kuanza kuijirekebisha mwenyewe

1. Umalaya kwa jinsia zote
Hii ni tabia ya kuwa na wapenzi wengi bila utulivu wa kuchagua mmoja huu ni ufsika🤨

Tabia hii huleta madhara mengi
Kukosa amani ya moyo
Kuishi kwa hofu mda wote macho jujuu unahisi kufumaniwa au kuumbuka mda wowote

Hatari za kiafya
Kupoteza heshima binafsi
Ni muhimu kujithamini mwili wako
Mbali na hapo Azuma ni deilee
Badala ya kuishi maisha ya mchanganyiko usio na mwelekeo tafuta mwenza anayekufaa na utulie nae hakuna mkamilifu, lakini kuna mtu ambaye mapungufu yake unaweza kuvumilia tulia nae

Kwa wanaume pia tabia hii huathiri nguvu muda na hata uchumi wako Unajikuta unatawanya nguvu na kipato chako bila mwelekeo
Mwanaume unataka kushindana k utaweza ?

Wewe mwanamke una haribu kiungo hicho mwisho kiwe kama sikio la tembo 🙌

Jiambie leo
Nataka kubadilika Sitaki tena hii tabia

Je, wewe unajiongelesha mwenyewe ili kubadilika?
Ni tabia gani ungependa kuacha?
Karibuni
Tabia zingine nitazitaja kwenye comment 😊

It's me again ShesRise_1 🖐
Kabisa.Mimi huwa najionya na kujikumbusha mara nyingi kwamba nisiwe serious sana na malimwengu.Yatapita na yote ni ubatili mtupu!
 
Kabisa.Mimi huwa najionya na kujikumbusha mara nyingi kwamba nisiwe serious sana na malimwengu.Yatapita na yote ni ubatili mtupu!
MashaAllah
Maisha yamegawanyika katika nyakati
Kuna season ya furaha
Kuna season ya huzuni
Lakini tuna uwezekano wa kuchagua season nzuri ikawa permanent
Japo hii haizuii kua nyakati ngumu
Zitatutembelea & zinatutembelea
 
Kujilaumu kuna kuja kwenye makosa ambayo umeshafanya na hayarekebishiki kw wakati huo
Nimekuelewa na hapa ndio mtu huseme laiti ningejua lakin inakua haina maana tena
Lakini uzuri ni kwamba umejifunza na huwezi kurudia kosa hilo kamwe
Muhimu hilo kosa halijakuua bado nafasi ya kurekebisha kufanya mambo kwa usahihi bila kukosea inawesekana

Saivi acha kujilaumu chukulia kipindi kile ulikua mjinga usie jua chochote
Na ufurahie maisha 😊

Jisemeshe vitu positive vya kukujenga
Acha kujilaumu hiyo sauti ya lawama achana nayo 🤝
 
Nimekuelewa na hapa ndio mtu huseme laiti ningejua lakin inakua haina maana tena
Lakini uzuri ni kwamba umejifunza na huwezi kurudia kosa hilo kamwe
Muhimu hilo kosa halijakuua bado nafasi ya kurekebisha kufanya mambo kwa usahihi bila kukosea inawesekana

Saivi acha kujilaumu chukulia kipindi kile ulikua mjinga usie jua chochote
Na ufurahie maisha 😊

Jisemeshe vitu positive vya kukujenga
Acha kujilaumu hiyo sauti ya lawama achana nayo 🤝
Mtaji ni afya mkuu as long bado tuna afya bado nafasi ya kusahihisha ipo
 
Kiufupi hizo zote ulizizitaja kama tabia ni roho chafu zinazofuatilia mtu na kumtumikisha zipendavyo ili kuharibu ukuu wa mtu ambao aliumbwa nao.
 
Kiufupi hizo zote ulizizitaja kama tabia ni roho chafu zinazofuatilia mtu na kumtumikisha zipendavyo ili kuharibu ukuu wa mtu ambao aliumbwa nao.
Kwa unyenyekevu mkubwa hebu naomba ufafanue tuweze kujifunza🙏
 
Kwa unyenyekevu mkubwa hebu naomba ufafanue tuweze kujifunza🙏
Katika kila tendo /maisha ya mwanadamu kuna roho inayomwongoza kufanya jambo fulani yamkini ni roho chafu ambayo husimamia matendo machafu kama wizi, zinaa,ulevi ama husuda na Roho safi ambayo husimamiwa na Roho Mtakatifu mwenyewe.
Bila Shaka umeshawahi kutaka kufanya jambo ama kusikia mtu alifanya/kughairisha jambo na mabaya yakatokea:
Mfano: Unaweza ukawa unataka kusafiri unakuta kuna sauti/fikra inakuzuia na ukitii kuna matokeo utaona, ama ukifanya kuna matokeo utaona mara nyingi matokeo hasi.
Sasa basi, hakuna tendo linafanyika mwilini bila kuwa na roho.
Kama ilivyo utajiri, umasikini, uzinzi, ulevi, wizi nk zote hizo ni roho, hizo ndizo zinaamua mtu aweje na zinatoka ndani ya mtu.
Na roho hizi huenda kizazi hata kizazi; Tuchukue mfano mdogo wa Baba yetu wa Imani Ibrahimu alikuwa na roho ya utasa, alimzaa Isaka kupitia kwa Sara katika hali ya uzee kadhalika Isaka nae baada ya kumuoa Rebeka akawa hapati watoto, ikabidi aingie magotini.
Mwanzo 25:21
“Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mkewe, maana alikuwa tasa; Bwana akamkubali, Rebeka akapata mimba.”
Mtoto wa Isaka ambaye ni Yakobo aliyezaliwa pacha na Essau nae alikutana na utasa kupitia kwa mkewe Rahel ambae alimlilia mmewe kwamba nipe mtoto la sivyo nitakufa mimi.
Mwanzo 30: 1

Mwanzo 29:31
“Bwana akaona Lea amechukiwa, akamfungua tumbo lake; lakini Raheli alikuwa tasa.”

Huo ni mfano mmoja tu, ila katika familia zetu kuna roho zinazofuatilia familia ama koo, Mfano roho za magonjwa, mauti ya aina fulani kama ajali, kutoolewa, kuzalia nyumbani nk (hawa wanakuwa wamepandiwa rohonya aibu)
kujidhuru, nk.
Kikitokea watu ndo hukumbuka aaah na babu yake alikufa kwa mtindo huu ila kwakua hawana maarifa wanapuuza hadi lije litokee tena.

Hili somo ni refu sana, bahati mbaya sijajiandaa kulifundisha naomba niishie hapa, nimechukua hatua sababu umeniomba.
Naamini kuna mwanga fulani umepatikana.
Maana kuna namna ya kujitenga nazo nalo ni somo refu tu.
 
Back
Top Bottom