ShesRise_1
JF-Expert Member
- Aug 21, 2025
- 17,238
- 40,773
Kikawaida kwenye maisha watu tunategemeana
Iwe kwenye afya au ugonjwa, kuna muda kila mmoja wetu huhitaji watu. Kuna msemo unasema watu ni mtaji
Lakini utakuta wengine wanasema, Mimi nipo kivyangu, sijui cha ndugu wala marafiki
Wengine huamini ukipata pesa watu watajitokeza wenyewe, kana kwamba pesa ni sumaku inayovuta kila kitu pesa subuni ya roho
Ukweli ni kwamba, watu tunahitajiana kwa namna nyingi sana
Unaweza kuwa umefungua mradi wako, lakini ili ufikie malengo lazima uwe na team ya watu wa kushirikiana nao
Kuna wakati unaweza kuumwa mpaka ushindwe hata kujisogeza hapo utahitaji watu wakusaidie
Ukiwa mahabusu, utahitaji mtu wa kukutolea dhamana
Ukiandaa sherehe, ili ifane na iwe na furaha lazima watu wajitokeze kulingana na mialiko uliyoitoa
Maana yake ni kwamba, watu tunahitajiana
Swali ni je, wewe una watu?
Una watu ambao ukiwaita wanaweza kuja?
Ukipata matatizo unaamini watakuwa pembeni yako, au ni watu wa misimu leo wapo, kesho hawapo?
Na moja ya watu tunaowazungumzia hapa ni ndugu
Ndugu zako ukiwaita watakuja? Au ni wewe ndiye unayewakimbilia kila wakati? ndugu vichomi
Hivi una mtu anayoweza kukukimbilia maji yakizidi unga?
Au upo kwenye kisiwa chako mwenyewe, lonely 🙁
ShesRise_1
Iwe kwenye afya au ugonjwa, kuna muda kila mmoja wetu huhitaji watu. Kuna msemo unasema watu ni mtaji
Lakini utakuta wengine wanasema, Mimi nipo kivyangu, sijui cha ndugu wala marafiki
Wengine huamini ukipata pesa watu watajitokeza wenyewe, kana kwamba pesa ni sumaku inayovuta kila kitu pesa subuni ya roho
Ukweli ni kwamba, watu tunahitajiana kwa namna nyingi sana
Unaweza kuwa umefungua mradi wako, lakini ili ufikie malengo lazima uwe na team ya watu wa kushirikiana nao
Kuna wakati unaweza kuumwa mpaka ushindwe hata kujisogeza hapo utahitaji watu wakusaidie
Ukiwa mahabusu, utahitaji mtu wa kukutolea dhamana
Ukiandaa sherehe, ili ifane na iwe na furaha lazima watu wajitokeze kulingana na mialiko uliyoitoa
Maana yake ni kwamba, watu tunahitajiana
Swali ni je, wewe una watu?
Una watu ambao ukiwaita wanaweza kuja?
Ukipata matatizo unaamini watakuwa pembeni yako, au ni watu wa misimu leo wapo, kesho hawapo?
Na moja ya watu tunaowazungumzia hapa ni ndugu
Ndugu zako ukiwaita watakuja? Au ni wewe ndiye unayewakimbilia kila wakati? ndugu vichomi
Hivi una mtu anayoweza kukukimbilia maji yakizidi unga?
Au upo kwenye kisiwa chako mwenyewe, lonely 🙁
ShesRise_1