Je, umeme unokatwa nchini na Tanesco wajumuisha ofisi zote nyeti, balozi na sehemu zingine kama Oysterbay? Au ni kwa watanzania wa hali ya chini tu?

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Kero ya kukatwa umeme na Tanesco imekuwa kubwa na sasa umeme wakatwa nchi nzima katika mikoa mbalimbali.

Lakini ningependa kufahamu kama umeme huu wakatwa katika sehemu zote nyeti, ofisi za kibalozi, viwandani, maeneo ya uzunguni na katika makazi ya watu muhimu katika nchi hii?

Je, umeme huo hukatwa katika sekta binafsi hususan katika kumbi za starehe, maduka makubwa na maeneo yote ambayo ni lazima yawe na umeme?

Hivi karibuni nikiwa katika safari zangu huko ugahibuni nikakutana na habari kwamba umeme huenda ukawa wakatwa nyakati za mchana tu ambapo watumiaji wa majumbani huwa ni wachache kwa kuwa huenda makazini na majumbani hakuna mtu.

Sababu ya umeme kukatwa huko Ughaibuni ni mgogoro wa Ukraine na Urusi ambao umesababisha kupanda kwa bei ya gesi ambayo ndo hutumika kuleta umeme katika nchi nyingi za Ulaya. na hiyo ni kwasababu Urusi wameamua kupunguza kiasi cha gesi wanoiuza kwenda barani Ulaya.

Lakini tatizo hilo (la kukata umeme) lilikuwa ni la wiki chache sana na baada ya hapo wananchi wa Ughaibuni hawajawahi kukosa umeme. Ukisikia Ughaibuni kuna tatizo la umeme basi fahamu ni kutokana na kutokea kwa gharika, au janga la mvua kali na upepo ambao huweza kuathiri njia za umeme na vituo vya kufulia umeme huo.

Serikali za Ulaya zinatambua kuwa umeme ukikatwa bila maelezo ya kutosha na bila miongozo wala sababu za kueleweka basi serikali hizo huingia matatizo makubwa ikiwemo wananchi kutishia mstakabali wa serikali iliyopo.

Sasa bila kuchosha sana na mada hii lengo ni kutaka kufahamu kwamba pale Tanesco wanapoukata umeme nchini je, umeme huo unokatwa ni ule uendao katika maeneo fulani tu nchini khasa makazi ya watu wa kawaida yaani wale hohehahe au pia huathiri maeneo yote niloyataja hapo juu, na kwa kuongezea maeneo ya jeshi, magereza na mashuleni?

Siwezi kusema umeme ukatwe katika mahospitali lakini angalau sehemu hizo zingine nazo zipate mgao wa masaa machache ili nao watambue kuwa kuna tatizo la umeme nchini.

Au ndo mradi wa Tanesco na wafanyabiashara wa majenereta umeshika kasi?

Ukisema ni majenereta wazungumzia suala zima la mazingira na tabia nchi ambapo moshi huathiri hali ya hewa na uoto wa asili.

Sasa waziri aneshughulikia mazingira nae ameona hili suala la majenereta kuwa ndo chanzo kikuu cha umeme na si malengo ya makusudi ya kuathiri watanzania kiafya kwa kuvuta hewa chafu ya moshi na gesi?

Hayati John Magufuli alisema kuwa kulikuwa na mtindo wa kufunga maji ili kuweka level ndogo na kila mtu alielewa hili kuwa ni hujuma.

Kwa nini Serikali yachukulia hujuma hii ni ya kawaida?

Masuali ni mengi lakini ndo hayo.
 
Kuna Prime areas ni nadra sana umeme kukatika, na ukikata wahusika wanaweza wasijue maana kuna Back up power.

Unajua maana ya back up power kijana?
 
Lakini ningependa kufahamu kama umeme huu wakatwa katika sehemu zote nyeti, ofisi za kibalozi, viwandani, maeneo ya uzunguni na katika makazi ya watu muhimu katika nchi hii?

Je, umeme huo hukatwa katika sekta binafsi hususan katika kumbi za starehe, maduka makubwa na maeneo yote ambayo ni lazima yawe na umeme?
Kuna maeneo umeme haukatwi na hakuna hata ubalozi wala wa nyumba 10
 
Kuna Prime areas ni nadra sana umeme kukatika, na ukikata wahusika wanaweza wasijue maana kuna Back up power.

Unajua maana ya back up power kijana?
Naelewa uzuri sana maana ya "back up power".

Hio ni pale tatizo la umeme ni linapokuwa "critical" na ni sehemu ya hatua za dharura zinazowekwa "standby" endapo umeme utakatika ghafla.

Lakini suali langu halihusu unachouliza, bali lahusu tatizo la ukataji umeme wa mara kwa mara unoifanywa na Tanesco miaka nenda rudi..
 
Naelewa uzuri sana maana ya "back up power".

Hio ni pale tatizo la umeme ni linapokuwa "critical" na ni sehemu ya hatua za dharura zinazowekwa "standby" endapo umeme utakatika ghafla.

Lakini suali langu halihusu unachouliza, bali lahusu tatizo la ukataji umeme wa mara kwa mara unoifanywa na Tanesco miaka nenda rudi..
Ushawahi kufuatilia kwa kina kwanini wanakata umeme?
 
Ameuliza hajasema anafurahi, Mabalozi huenda hata hawajui kama kuna migao chronic ya umeme.
Cha kushangaza huu mgao ambao ni chronic ulikuwepo hadi 2015.

Tokea 2015 hadi 2022 kukawa hakuna tatizo.

Kuanzia 2021 hado sasa tatizo ambalo ni "chronic" limerudi tena kwa kasi kubwa.

Kwanini Tanesco wasifanye umeme usikatike tena kama ilivyokuwa kati ya 2015-2022?
 
WhatsApp Image 2023-09-17 at 2.10.59 PM.jpeg
 
Ninapoishi ni line moja na Hosp ya Rufaa zonal, ni nadra sana pengine sijawai shuhudia umeme ukikatika.
 
Kero ya kukatwa umeme na Tanesco imekuwa kubwa na sasa umeme wakatwa nchi nzima katika mikoa mbalimbali.

Lakini ningependa kufahamu kama umeme huu wakatwa katika sehemu zote nyeti, ofisi za kibalozi, viwandani, maeneo ya uzunguni na katika makazi ya watu muhimu katika nchi hii?

Je, umeme huo hukatwa katika sekta binafsi hususan katika kumbi za starehe, maduka makubwa na maeneo yote ambayo ni lazima yawe na umeme?

Hivi karibuni nikiwa katika safari zangu huko ugahibuni nikakutana na habari kwamba umeme huenda ukawa wakatwa nyakati za mchana tu ambapo watumiaji wa majumbani huwa ni wachache kwa kuwa huenda makazini na majumbani hakuna mtu.

Sababu ya umeme kukatwa huko Ughaibuni ni mgogoro wa Ukraine na Urusi ambao umesababisha kupanda kwa bei ya gesi ambayo ndo hutumika kuleta umeme katika nchi nyingi za Ulaya. na hiyo ni kwasababu Urusi wameamua kupunguza kiasi cha gesi wanoiuza kwenda barani Ulaya.

Lakini tatizo hilo (la kukata umeme) lilikuwa ni la wiki chache sana na baada ya hapo wananchi wa Ughaibuni hawajawahi kukosa umeme. Ukisikia Ughaibuni kuna tatizo la umeme basi fahamu ni kutokana na kutokea kwa gharika, au janga la mvua kali na upepo ambao huweza kuathiri njia za umeme na vituo vya kufulia umeme huo.

Serikali za Ulaya zinatambua kuwa umeme ukikatwa bila maelezo ya kutosha na bila miongozo wala sababu za kueleweka basi serikali hizo huingia matatizo makubwa ikiwemo wananchi kutishia mstakabali wa serikali iliyopo.

Sasa bila kuchosha sana na mada hii lengo ni kutaka kufahamu kwamba pale Tanesco wanapoukata umeme nchini je, umeme huo unokatwa ni ule uendao katika maeneo fulani tu nchini khasa makazi ya watu wa kawaida yaani wale hohehahe au pia huathiri maeneo yote niloyataja hapo juu, na kwa kuongezea maeneo ya jeshi, magereza na mashuleni?

Siwezi kusema umeme ukatwe katika mahospitali lakini angalau sehemu hizo zingine nazo zipate mgao wa masaa machache ili nao watambue kuwa kuna tatizo la umeme nchini.

Au ndo mradi wa Tanesco na wafanyabiashara wa majenereta umeshika kasi?

Ukisema ni majenereta wazungumzia suala zima la mazingira na tabia nchi ambapo moshi huathiri hali ya hewa na uoto wa asili.

Sasa waziri aneshughulikia mazingira nae ameona hili suala la majenereta kuwa ndo chanzo kikuu cha umeme na si malengo ya makusudi ya kuathiri watanzania kiafya kwa kuvuta hewa chafu ya moshi na gesi?

Hayati John Magufuli alisema kuwa kulikuwa na mtindo wa kufunga maji ili kuweka level ndogo na kila mtu alielewa hili kuwa ni hujuma.

Kwa nini Serikali yachukulia hujuma hii ni ya kawaida?

Masuali ni mengi lakini ndo hayo.
WAPIGIE UWAULIZE. NAMBA YA CUSTOMER CARE NI

0748 550 000, 0784768586, 0715 768 586, 0715 768 587, 068 400 1066,​

 
Naona naanza kuhojiwa na walewale.

Mkuu, nawe ni mwananchi wa jamhuri ya wapigaji au?
Sasa unatakaje umeme usikatwe wakati hujui sababu za umeme kukatwa mara kwa mara?

Is your head receiving waves from one direction only?
 
Sasa unatakaje umeme usikatwe wakati hujui sababu za umeme kukatwa mara kwa mara?

Is your receiving waves from one direction only?
Fikiri kwanza kabla ya kuandika kingereza maana hii lugha kwako weye wahitaji kujipanga.

NIlikuwa na mashaka kwamba weye ni raia wa Jamhuri ya Wapigaji sasa nimeelewa.

Jamhuri ya Wapigaji ni taifa dogo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Fikiri kwanza kabla ya kuandika kingereza maana hii lugha kwako weye wahitaji kujipanga.

NIlikuwa na mashaka kwamba weye ni raia wa Jamhuri ya Wapigaji sasa nimeelewa.

Jamhuri ya Wapigaji ni taifa dogo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mpaka aibu kabisa,ivi wakenya hawapo humu? Maana wanavyojua kutucheka!
 
Back
Top Bottom