TANESCO ifutwe tu tuanzwe upya na biashara ya umeme

Zemanda

JF-Expert Member
Jan 10, 2021
5,707
11,956
Kiukweli shirika takataka lisilo na faida kwasasa tukiachana na TTCL basi ni Tanesco. Hakuna na wala binafsi sioni faida ya hili shirika ambalo linaendeshwa kipigaji kuendelea kuwapo huku likisababisha hasara na usumbufu kwa watanzania as if tunapewa umeme bure.

Hivi inafaida gani kwa miezi 5 mfululizo kuwa na mgao usiokwisha kwa kisingizio cha matengenezo yasiyoeleweka na yasiyoisha.

Hatukatai kwamba maswala ya umeme huhitaji marekebisho ya mara kwa mara ili kuboresha huduma ya usambazaji wa umeme ila kwa kinachoendelea sidhani kama ni ajenda ya matengenezo bali ni uhujumu uchumi.


Kama tunakubali kucheka na huu uendeshaji wa kimasihara wa shirika nyeti la nishati ya umeme, uendeshaji wa masihara wa uingizwaji wa nishati ya mafuta, then tujiandae kama taifa kushuka kiuchumi kadiri siku zikienda.

Kwann TANESCO wasiwekwe benchi tu ili wabia wengine wa nishati waingie tupate umeme kwa bei ya chini na umeme wa uhakika kuliko hivi sasa umeme unakatwa kila dakika bila hoja za msingi wala ratiba ya kueleweka, halafu tunacheka nao.

Aiseee hii kitu inakera sana. Pale Tabata umeme kila siku kuanzia majira ya asubuhi huwa haueleweki unakatwa kwasababu gani. Na ukikatwa hiyo asubuhi basi unarejeshwa kama sio kuanzia saa moja jioni basi saa mbili hadi saa tatu ya usiku.

Sasa hayo ni maisha gani aisee.

TANESCO ifutwe haina maana kwasasa, ifutwe tenda wapewe watu binafsi.
 
Tanesco ingekuwa ishabinfsishwa kitambo.kuna vikwazo vinaendelea ndani Kwa ndani ikiwemo waajiriwa wake.

Na mi nahisi Kuna mtu anafanya mchezo kuongeza joto la ubinafsishaji Kwa maslahi yake
Mtu mkubwa sana govt
 
Yaani hadi saa hii tokea asubuhi hatuelewi umeme upo wapi. Wanawasha na kuzima ng'ombe hawa.
 
Tatizo ni Rais wako, kwani kuna kitu amefanikiwa hadi sasa? Kitu kidogo tu kama kuendesha mradi wa mwendokasi serikali yake imefeli itakuwa mambo makubwa kama umeme na huduma nyingine muhimu.
 
Kiukweli shirika takataka lisilo na faida kwasasa tukiachana na TTCL basi ni Tanesco. Hakuna na wala binafsi sioni faida ya hili shirika ambalo linaendeshwa kipigaji kuendelea kuwapo huku likisababisha hasara na usumbufu kwa watanzania as if tunapewa umeme bure.

Hivi inafaida gani kwa miezi 5 mfululizo kuwa na mgao usiokwisha kwa kisingizio cha matengenezo yasiyoeleweka na yasiyoisha.

Hatukatai kwamba maswala ya umeme huhitaji marekebisho ya mara kwa mara ili kuboresha huduma ya usambazaji wa umeme ila kwa kinachoendelea sidhani kama ni ajenda ya matengenezo bali ni uhujumu uchumi.


Kama tunakubali kucheka na huu uendeshaji wa kimasihara wa shirika nyeti la nishati ya umeme, uendeshaji wa masihara wa uingizwaji wa nishati ya mafuta, then tujiandae kama taifa kushuka kiuchumi kadiri siku zikienda.

Kwann TANESCO wasiwekwe benchi tu ili wabia wengine wa nishati waingie tupate umeme kwa bei ya chini na umeme wa uhakika kuliko hivi sasa umeme unakatwa kila dakika bila hoja za msingi wala ratiba ya kueleweka, halafu tunacheka nao.

Aiseee hii kitu inakera sana. Pale Tabata umeme kila siku kuanzia majira ya asubuhi huwa haueleweki unakatwa kwasababu gani. Na ukikatwa hiyo asubuhi basi unarejeshwa kama sio kuanzia saa moja jioni basi saa mbili hadi saa tatu ya usiku.

Sasa hayo ni maisha gani aisee.

TANESCO ifutwe haina maana kwasasa, ifutwe tenda wapewe watu binafsi.
Broo Umeandika kitu ambacho mimi mwenyewe binafsi nashindwa kuelewa kwa nini UMEME HAKUNA. Huwa najiuliza sisi wa Tanzania ni Punda wa dobii na vile huwa najiuliza tena wa Tanzania ni wehuu tunashindwa kuandamana mpaka kwa Waziri kumuuliza kwa nini hakuna umemee na maji ,sijui sisi ni ma caward ,haki yetu tunashindwa kuidai au sisi ni ignorance peoples ktk dunia hii any way mashirika binafsi ya umeme yaruhusiwe tu kama mashirika ya simu Topo Karne ya 22 umeme mpk leo bado kabisaa halafu unataka wawekezaji waje hapa kuekeza .
Solution
Jenga kinu cha umeme wa Nuclear .Utawauzia Kenya ,Uganda Rwanda ,Malawi mpk Zambia .
 
Naunga. mkono hoja. Eti kuna nguzo niliona wanabadikisho kutoka ya mti kuwwka ya zege, wakati ile ya mti ina uwezo wa kukaa miaka 50 . Sasa huu kama sio uhujumu uchumi ni nii hiki.
 
Back
Top Bottom