​:shock:
jamani kuna huu mchakato wa vazi la taifa unaoendelea , nimejaribu kutafuta umuhimu wake kwa sasa sikuweza kuuona . wizara ita tumia helanyingi kwenye hi shuhuli lakini itamsaidiaje mtanzania wakawaida ? hivi na wenzetu kama Nigeria walifanya hivyo kupata vazi lao?
ok pamoja na maswali nilio nayo bado nimegundua hata wano endesha hishuhuli hawana utaifa kabisa na sithani hata kama ilo vazi litakua na utafa.
Tuangalie mfano mmoja. kwenye Matangazo ya Television wana sisitiza hilo vazi lazima liwe na rangi za bendera ta taifa lakini wao wenyewe kwenye tangazo lao halina rangi ya bendera ya taifa sijui kwanii , baada yakusikia na kuona hilo tangazo nikajipa moyo nikasema labda ni kwasababu ni tangazo lamunda tu na mwisho wake ni baada ya mchakato .
Kwenye hayo matangazo ya TV kuna Tovuti wana toa kwaajili ya kujiandikisha ama kujiunga kama wataka kushiriki ,nikaamua kuifuatilia ile Tovuti na hiki ndicho kinachonijulisha kua Vazi lataifa linatafutwa na watu wasio na utaifa.
Nimaranyingisana tumesikia mamlaka ya mawasiliaano ina himiza watanzania tutumie domin ya tanzania kwenye Tovuti ya kitanzania yaani Tovuti ziwe
www.tovuti.co.tz ilikuonyesha utaifa zaidi kua tunajali vya kwetu. kilichonishangaza nikukuta Tovuti ya vazi lataifa ni
www.vazilataifa.com yaani haijatokana na domain yenye uwakilishi wa Tanzania yaani
www.vazilataifa.co.tz sasa hapo kuna utaifa kweli ? mi nafikiri mambo kama haya yangeanza kwa waandaji kua na utaifa kwanza kabla ya kuleta kwetu.
ok nilipo ona hilo nikafikikiri wamejisahau nikajipa moyo ninga access Tovuti yenyewe
www.vazilataifa.comkusema kweli imenikatisha tamaa na kugundua huumchakato umeshakua sawasawa na ule mchakato wa kupata katiba mpya yaani tumeshaanza na mguu mbaya. iweje wana sisitiza kua vazi lataifa linatakiwa liwe na rangi ya bendera ya taifa lakini rangi zilizopo kwenye Tovuti yenyewe hazina uhusiana na bendera ya taifa na kwenye Title bar ya hiyo Tovuti inasomeka my business ina maana hi Tovuti ni kwaajili ya business yao ?ama walikua wana maanisha nini ? ina maana hawapo serious na wanachofanya ama nikupuuzia?
niulize wadau inachukua mudangani kutengeneza Tovuti? sikutegemea hata sikumoja kama kutengeneza Tovuti inaweza chukua mwezi mima ? siamini kama walishindwa kuitengeneza ndani ya wiki moja kama inashindikana basi msiitangaze ama mwiifunge kabisa ili hicho kinacho waonyesha kua hamjajipanga kisionekane .
lingine ni hili la matumizi ya luga kwenye hii Tovuti, Lugayetu kuu inayo waounganisha watanzania wote ni kiswahili lakini kwenye hii Tovuti kunamchanganyiko wa kiswahili na kiingereza.
pamoja na matangazo yoote wanayofanya iliwashindaje kuweka maelezo yote kwenye hi Tovuti hata kuweka ile kamati imewashinda ama kuwenka hivyo vigezo wana vyo tangaza kwenye TV imewashinda ?
mimi naishauri hii kamati ifanye mambo kwenye uhalisia na ijarubu kuelimisha watu hili Vazi la taifa lina maana gani na litatusaidiaje . Nina wasiwasi mkubwa kua tulio wengi hatujui maana ya hili vazi na litatusaidiaje nilishangaa kusikia watu wana bisha na nakusema hili vazi litakua uniform yaani watu hawatatakiwa kuvaa nguonyingine , wengine wakasema hilivazi litakua ndo vazikuu lasherehe na matukio makubwa ama kama watu wanasafiri kwenda nje ndo watalivaa.
pia nilisha wahi sikia watu wanajiuliza je hilivazi litakuaje je kutakuana na lakike na lakiume? je kutakua na hijabu yataifa ama wapenda hijabu watavaanini wakati wakitaka kuvaavazi lataifa na je wale wamasai wa arusha wata tupa vazilao nakujiunga na vazi lataifa na wale wazee wetu wa pwani wavaao misuli watawekachini misuli na kuvaa vazi la taifa?
hayo na mengineyo mengi nimaswali ambayo yapo vichwani mwa watu na hawana majibu ilikuhakikisha kua hilivazi linaletamaana kabla yakuli tengeneza nivyema watu wakajua maana na umuhimuwake na faida zake na litatumika wakati gani na kwamuda gani
kamati ijipange tena kwani inaonekana inataka kuanza na mguu mbaya na mwishowe tutakua tumetumihe helanyingi bila maana yeyote kwan hakutakua na wanao jua maana yake na umuhimu wake , kwani litaishia kuwemwa kabatini na lisiwe namaana yeyote kama ilivyo kusudiwa. kamati haijachelewa nivyema ikaaza sasa